مقدمة وغلاف المنتقى من موسوعة الأحاديث النبوية

مقدمة وغلاف المنتقى من موسوعة الأحاديث النبوية

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

Language: lang_sw
Prepared by:
Version: 1.0
Translations 63
Akan Amharic Assamese Azerbaijani +59
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

Utangulizi

Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, na rehema na amani zimfikie Nabii Muhammadi, na watu wake na Maswahaba zake wote, na wote watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya malipo, ama baada ya hayo:

Hakika katika mambo anayotakiwa kuyapa kipaumbele muislamu ni kusoma kwa umakini na kuzingatia, nakutafuta elimu na kuifanyia kazi -hii iwe baada kujifunza kitabu cha Mwenyezi Mungu- yafuate mafundisho ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake, Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake "Nimeacha kwenu nyinyi enyi watu, mambo ambayo ikiwa mtashikamana nayo, kamwe hamtopotea: Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na mafundisho ya Nabii wake". Hadithi hii kaipokea Imam Malik, Na alisema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na yale aliyo kuleteeni Mtume basi yachukueni na yale aliyo kukatazeni yaepukeni" [Suratul-Hashri: 7] Na kwa sababu hii jumuia ya kuhudumia maudhui za Uislamu kwa lugha mbalimbali, na Jumuia ya kufikisha ujumbe na kuwahudumia wageni ya Rabwa zimefanya hima ya kuandaa Ensaiklopidia ya hadithi za Mtume na kuzitafsiri kwa lugha kadhaa.

Na Mwenyezi Mungu ametia wepesi wa kuchagua orodha kadhaa ya Ensaiklopidia hii (ya hadithi) anazozihitajia muislamu katika dini yake na dunia yake, ikiwa ni pamoja na kubainisha muhtasari wake, na kufafanua maana yake na muongozo wake, na baadhi yake, na kuziandika katika kitabu hiki kinachoitwa: "Kuchagua kutoka katika Ensaiklopidia ya Hadithi za Mtume" Na kazi ya kutafsiri kwenda katika lugha zote hai ulimwenguni bado inaendelea, ili faida iwafikie watu wote kwa maudhui zake zote, na kuweza kuwafikishia mafundisho ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa viumbe kwa lugha zao.

Na tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu aitakabali amali hii, na aifanye kuwa ni amali yenye baraka, iliyotakaswa kwa kutaka radhi zake tukufu, na amlipe kila atakayesaidia katika kuiandaa na kuitafsiri na kuisambaza.

Na mwisho tunaomba rehema na amani zimfikie Nabii Muhammadi

Dondoo za muhtasari

Hadithi za Mtume ndiyo msingi wa pili katika misingi ya Sheria, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na wala haongei kwa matamanio ya nafsi yake (3) Haikuwa maneno yake ila ni ufunuo anaofunuliwa" [An najmu: 3-4]

Na uchaguzi huu wa Ensaiklopidia ya hadithi unakusanya orodha ya hadithi zinazokusanya maudhui muhimu, zile anazohitajia muislamu katika dini yake na dunia yake, ikiwa ni pamoja na kubainisha muhtasari wake, na kuweka wazi maana yake, na baadhi ya faida zake zikiwa zimefasiriwa kwa idadi kadhaa ya lugha hai za ulimwengu, ili faida ienee kwa watu wote kupitia maudhui zake, na kuweza kuyafikisha mafundisho ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa watu kupitia lugha zao.