العقيدة الصحيحة وما يضادها
تكلم المؤلف في هذا الكتيب الصغير عن العقيدة الصحيحة التي تتلخص في: الإيمان بالله، وملائكته، وكتبه، ورسله، واليوم الآخر، وبالقدر خيره وشره، فهذه الأمور الستة هي أصول العقيدة الصحيحة عند أهل السنة والجماعة. وقد شرح الشيخ في الكتاب هذه الأصول الستة مستدلًا بالكتاب والسنة وما عليه سلف هذه الأمة، ثم تكلم عن مسألة الإيمان وقرر أنه قول وعمل يزيد بالطاعة وينقص بالمعصية. ثم ذكر مسألة الولاء والبراء وواجب المسلم تجاه أخيه في الدين. ثم شرع في ذكر المنحرفين عن هذه العقيدة الصحيحة مع ذكر أصنافهم، وذكر شبهة المعاصرين وأنها هي نفس شبهة الأولين، وذكر بعض العقائد الكفرية وما زاده المشركون المتأخرون على الأولين. وأكد الشيخ أن النصر لا يأتي إلا بإخلاص العبادة لوجه الله تعالى وحده لا شريك له، ثم ختم هذا الكتيب بذكر نواقض الإسلام.
Itikadi sahihi na mambo yanayopingana nayo.
Mtunzi
Mheshimiwa, sheikh Abdul aziz ibnu Abdillahi ibnu Baaz.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.
Utangulizi
Kila sifa njema ni zake Mwenyezi Mungu peke yake, na rehema na amani ziwe juu ya yule ambaye hakuna nabii atakayekuja baada yake, na ziwe juu ya watu wa familia yake na maswahaba wake.
Ama baada ya kusema hayo: Na kwa namna ilivyokuwa itikadi sahihi ndiyo asili ya dini ya Uislamu na msingi wa mila, nimeona iwe ndiyo maudhui ya muhadhara. Na inavyofahamika kwa ushahidi wa kisheria utokanao na Qur'ani na hadithi ni kuwa matendo na maneno yanakuwa sahihi na kukubaliwa ikiwa yatatokana na itikadi iliyo sahihi. Hivyo basi, ikiwa itikadi siyo sahihi, hubatilika kila kinachotokana na hiyo itikadi miongoni mwa matendo na maneno kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Leo hii mmehalalishiwa kila kilicho kizuri ,na chakula cha wale waliopewa kitabu ni halali kwenu, na chakula chenu ni halali kwao. Na mmehalalishiwa kuwaoa wanawake wema wa Kiislamu na wanawake wema katika wale waliopewa kitabu kabla yenu. Ni halali kwenu kuwaowa mtakapowapa mahari yao mkafunga nao ndoa bila ya kufanya uzinzi wala kuwaweka wanawake kinyumba. Na anayekufuru imani, bila shaka matendo yake mema yamepotea na yeye katika akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara}. [Suratul-Maidah aya ya 5] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Kwa hakika uliletewa wahyi wewe, ewe Mtume, na Mitume waliokuwa kabla yako kwamba lau ungelimshirikisha Mwenyezi Mungu na asiyekuwa Yeye, basi bila shaka matendo yako yangalibatilika na ungalikuwa ni miongoni mwa waliopata hasara}. [Surat Zumar aya ya 65] Na aya zenye maana hii ni nyingi, na kwa hakika kitabu cha Mwenyezi Mungu kilicho wazi na sunna za Mtume wake muaminifu, ziwe juu yake kutoka kwa Mola wake Mlezi rehema na amani bora zaidi, vimeweka wazi kuwa itikadi sahihi kwa muhutasari ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na Siku ya Mwisho, na kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu ya heri yake na ya shari yake. Hivyo basi, haya mambo sita ndiyo msingi wa itikadi iliyo sahihi ambayo Kitabu kitukufu cha Mwenyezi Mungu kiliteremka nayo, na Mwenyezi Mungu akamtuma Mtume wake Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake - nayo. Na kinatokana na misingi hii, kila kinachopasa kuaminiwa katika mambo yasiyoonekana, na kila kitu ambacho Mwenyezi Mungu na Mtume wake - rehema na amani ziwe juu yake - walijulisha juu yake. Na ushahidi wa hii misingi sita katika Qur'ani na Hadithi ni mingi sana. Miongoni mwa mwake ni maneno ya Mwenyezi Mungu aliyetakasika: {Sio wema tu peke yake kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi katika kusali, bali wema hasa ni wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii}. [Al-Baqara: 177]. Hadi mwisho wa Aya, na maneno yake aliyetakasika: {Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake Mlezi, na Waumini vile vile. Wote wamemuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake na Mitume wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume wake}. [Al-Baqara: 285] Na kauli yake Mtukufu: {Enyi mlioamini! Muaminini Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake, na Kitabu alichokiteremsha kabla yake. Na anayemkataa Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na Siku ya Mwisho, basi huyo amekwishapotea kupotea kwa mbali}. [An-Nisaa: 136] Na kauli yake Mtukufu: {Je, hujui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliomo mbinguni na katika ardhi? Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi}. [Al-Hajj: 70] Ama Hadithi zilizo sahihi zenye kufahamisha hii misingi ni nyingi sana. Miongoni mwake ni hadithi sahihi na maarufu aliyoipokea imamu Muslimu katika sahihi yake kutoka katika hadithi ya kiongozi wa Waumini Omar ibni Khatwab - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kuwa: Jibriil, amani iwe juu yake, alimuuliza Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - kuhusu imani. Akamwambia: "Ni kumuamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na siku ya Mwisho, na kuamini mipango ya Mwenyezi Mungu, ya kheri yake na ya shari yake." [1] Hadi mwisho wa hadithi. Na hadithi hiyo wameipokea masheikh wawili (Bukhari na Muslim) kutoka kwa Abuu Huraira. Na hii misingi sita kinatokana nayo kila kitu kilicho lazima kwa Muislamu kukiamini katika kuhusiana na Mwenyezi Mungu Mtukufu na katika jambo la kurudishwa kwa Mwenyezi Mungu, na mengineyo katika mambo yasiyoonekana. (1) Ameipokea Muslim katika Kitabu cha Imani (8), Tirmidhiy katika Kitabu cha Imani (2610), An-Nasaai katika Kitabu cha Imani na Ufafanuzi wake (4990), Sunna ya Abii Daaudi (4695), Utangulizi wa ibnu Maajah (63), Ahmad (1/27).
Kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu
Ni kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Mungu wa kweli anayestahiki kuabudiwa mbali na kila kisichokuwa yeye.
Na miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu mtukufu, ni kuwa na imani ya kuwa yeye Mwenyezi Mungu ndiye Mungu wa kweli anayestahiki kuabudiwa mbali na kila kisichokuwa yeye, kwa kuwa yeye ndiye Muumba wa waja, Mwenye kuwatendea wema, Mwenye kusimamia riziki zao, Mwenye kujua mambo yao ya siri na ya wazi, Mwenye uwezo wa kumlipa thawabu mtiifu wao na kumuadhibu mwenye kuasi miongoni mwao. Mwenyezi Mungu aliumba majini na wanadamu kwa ajili ya ibada hii na akawaamrisha kuifanya kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na sikuwaumba majini na wanadamu ila waniabubu}. [Dhariyat: 56]. {Sitaki kutoka kwao riziki wala sitaki wanilishe}. [Dhariyat: 57]. {Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti}. [Dhariyat: 58]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi aliyewaumba nyinyi na wale wa kabla yenu, ili mpate kuwa wachamungu}. [Al-Baqara: 21]. {(Mwenyezi Mungu) ambaye amewafanyia hii ardhi kuwa kama tandiko, na mbingu kama paa, na akateremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo akatoa matunda yawe riziki zenu. Basi msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua}. [Al-Baqara: 22]. Na kwa hakika Mwenyezi Mungu aliwatuma Mitume na akateremsha Vitabu kwa ajili ya kubainisha haki na kuilingania, na kutahadharisha yote yanayopingana nayo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu aliyetakasika, Mtukufu: {Na kwa hakika, kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Twaghuut (Shetani na vyote vinavyoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu}. [An-Nahli: 36]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipokuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu}. [Al-Anbiya: 25]. Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Alif Lam Raa. Hiki ni kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi kisha zikapambanuliwa vizuri, kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye hekima, Mwenye habari za kila kitu}. {Imefanywa hivyo) ili msiabudu isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi kwenu ni mwonyaji na mbashiri nitokae kwake}. [Huud: 1-2] Na uhakika wa ibada hii ni katika kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa mambo yote wanayotumia waja kuabudia miongoni mwa dua, khofu, kutaraji, kuswali, kufunga, kuchinja wanyama, kuweka nadhiri na mengineyo miongoni mwa ibada zinazofanywa kwa kumnyenyekea yeye, kumpenda na kumwogopa pamoja na kumpenda kikamilifu yeye aliyetakasika, kujishusha chini mbele ya ukuu wake. Na sehemu nyingi za Qur'ani tukufu ziliteremka kuhusiana na misingi hii mitukufu, kama ilivyo katika maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Basi mwabudu Mwenyezi Mungu hali ya kumtakasia dini}. {Hakika Dini Safi ni ya Mwenyezi Mungu tu}. [Az-Zumar: 3-2] Na kauli yake Mtukufu: {Na amekwishahukumu Mola wako Mlezi ya kuwa msimuabudu yoyote ila yeye tu}. [Al-Israai: 23] Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Basi, muombeni Mwenyezi Mungu peke yake mumfanyie ibada yeye peke yake hata kama makafiri watachukia} [Ghaafir: 14] Na katika sahihi mbili imepokewa kutoka kwa Muaadh - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - alisema: ((Haki ya Mwenyezi Mungu juu ya waja wake, ni wamuabudu yeye na wala wasimshirikishe na kitu chochote)). (2) Bukhari katika mlango wa Jihadi na vita mbalimbali (2701), Muslim katika Kitabu cha Imani (30), At-Tirmidhiy katika mlango wa Imani (2443), Ibnu Maajah katika mlango wa Kuipa dunia mgongo.
Kuamini mambo yote aliyoyawajibisha kwa waja wake kama vile nguzo tano za Uislamu zilizo wazi.
Na vilevile miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu ni kuamini kila jambo alilolifanya kuwa ni wajibu kwa waja waje, kama vile nguzo tano za Uislamu zilizo wazi, nazo ni: Kushuhudia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, na kuwa Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na kusimamisha swala, kutoa zaka, kufunguga mwezi wa Ramadhani, na kuhiji nyumba tukufu kwa yule awezae njia ya kuiendea, na yasiyokuwa hayo miongoni mwa mambo ya lazima ambayo yaliletwa na sheria iliyo safi.
Na nguzo kubwa na muhimu zaidi katika hizi, ni kushuhudia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Hivyo, kushuhudia kuwa hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake kunamhitaji mtu kuitakasa ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, na kupinga kila chenye kuabudiwa asiyekuwa yeye. Hii ndiyo maana ya laa ilaha illa llahu. Kwani, maana yake ni kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake. Kwa hivyo, kila chenye kuabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu katika wanadamu, Malaika, majini au visivyokuwa hao, vyote hivyo ni viabudiwa batili, na mwenye kuabudiwa kwa haki ni Mwenyezi Mungu peke yake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ndiye wa haki, na kwamba kila wanachokiabudu kinyume na yeye ni batili}. [Surat Al-Hajj: 62]. Na kwa hakika imekwishawekwa wazi kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwaumba majini na watu kwa ajili ya msingi huu wa asili na akawaamrisha kuufuata, na akawatuma kwa ajili hiyo Mitume wake na akateremsha kwa ajili hiyo Vitabu vyake. Hivyo basi fikiria hilo vizuri na uzingatie sana ili iwe wazi kwako namna gani Waislamu wengi walivyotumbukia kwenye wimbi la ujinga mkubwa wa kutokujuwa msingi huu wa asili mpaka wakafikia kumuabudu Mwenyezi Mungu pamoja na asiyekuwa yeye, na wakailekeza haki yake ya pekee kwa asiyekuwa yeye. Basi Mwenyezi Mungu tu ndiye anayetakwa msaada.
Kuamini ya kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa ulimwengu, Mwenye kupanga mambo yao na Mwenye kuwaendesha kwa elimu yake na uwezo wake.
Na miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kuamini kuwa yeye ndiye Muumba wa ulimwengu, Mwenye kupanga mambo yao na Mwenye kuwaendesha kwa elimu yake na uwezo wake kama anavyotaka Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kwamba yeye ndiye Mmiliki wa dunia na akhera, na ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote, hakuna muumba asiyekuwa yeye wala hakuna mola mlezi asiyekuwan yeye. Na kwamba yeye alituma Mitume na akateremsha Vitabu ili kuwafanya waja kuwa wema na kuwalingania kwenye mambo yenye wokovu wao na kutengenea kwao duniani na akhera. Na kwamba yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu hana mshirika yeyote katika hayo yote, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Mwenyezi Mungu aliyetukuka ndiye Muumba wa vitu vyote, naye ndiye Mlinzi wa kila kitu}. [Az-Zumar: 62]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akainuka juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zilizotiishwa kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba ni kwake, na amri (ni yake). Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote}. [Al-A'araf: 54]
Kuyaamini majina yake mazuri na sifa zake za hali ya juu pasina kuzibadailisha wala kuzipinga wala kujifanya kujuwa namna zilivyo hasa wala kuzifanisha
Na vilevile, miongoni mwa kumuamini Mwenyezi Mungu, ni kuyaamini majina yake mazuri na sifa zake za hali ya juu zilizokuja katika Kitabu chake kitukufu, na zilizothibiti kutoka kwa Mtume wake muaminifu pasina kubadilisha wala kupinga wala kujifanya kujuwa zilivyo hasa wala kuzifananisha. Bali ni wajibu kuzipitisha tu kama zilivyokuja pasina kujifanya kujua namna zilivyo hasa pamoja na kuamini maana kubwa ambazo ziliashiria, ambazo ni sifa za Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu. Ni wajibu kumsifu kwazo kwa namna inayoendana naye, pasina kumfananisha na viumbe vyake kwa chochote katika sifa zake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona}. [Ash-Shura: 11]. Na amesema Mwenye nguvu na utukufu: {Basi msimpigie Mwenyezi Mungu mifano. Kwa hakika yeye anajuwa, na nyinyi hamjui kitu chochote}. [An-Nahli: 74]. Na hii ndiyo itikadi sahihi ya Ahlusanna waljamaa miongoni mwa maswahaba wa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - na wale waliowafuata baada yao kwa wema, na ndiyo itikadi aliyoinukuu katika kitabu chake imamu Abul Hasani Al-ash-ariy Mwenyezi Mungu amrehemu, kitabu kiitwacho "Makala kuhusu watu wa hadithi na wa sunna" na pia waliyanukuu wengineo miongoni mwa watu wenye elimu na imani.
Amesema Al-Awzaaiy - Mwenyezi Mungu amrehemu -: siku moja aliulizwa Zuhriy na Mak-huul kuhusu aya zenye sifa za Mwenyezi Mungu. Wakasema: Zipitisheni tu kama zilivyokuja. Naye Al-Walidu bin Muslim - Mwenyezi Mungu amrehemu -alisema: Aliulizwa Malik, Al-Awzaiy, Laithy bin Sa'ad na Sufyan Ath-thawry kuhusu aya zenye sifa za Mwenyezi Mungu. Wote wakasema: Zipitisheni tu kama zilivyokuja bila ya kufanya kujua namna zilivyo hasa. Na amesema Awzaaiy, Mwenyezi Mungu amrehemu: Tulikuwa sisi na mataabiy (waliokuja baada ya maswahaba) kwa uwingi wetu tukisema: Hakika Mwenyezi Mungu aliyetakasika yupo juu ya Kiti chake cha Enzi, na na tunaamini yote yaliyokuja katika Hadithi miongoni mwa sifa za Mwenyezi Mungu. Na alipoulizwa Rabii'a ibn Abdurahmani, sheikh wa imamu Maalik, Mwenyezi Mungu amrehemu yeye na sheikh wake, kuhusu kuwa juu kwa Mwenyezi Mungu, akasema: Kuwa juu kunafahamika, na namna yake hasa haifahamiki, na ujumbe hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na niwajibu wa Mtume kufikisha kwa wazi na ni wajibu kwetu sisi kukusadiki. Na alipoulizwa imamu Maalik, Mwenyezi Mungu amrehemu, kuhusu hilo, alisema: "Kuinuka juu kunajulikana, na namna yake hasa haijulikani, na kuamini hilo ni wajibu na kuuliza kuhusu namna yake hasa ni uzushi." Kisha akasema kumwambia muulizaji: "Na sikuoni wewe isipokuwa ni mwanamume mbaya." Kisha akaamrisha, na akatolewa nje.
Na maana hii pia imepokewa kutoka kwa mama wa Waumini, Ummu Salama - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake. Naye imamu Abuu Abdurahman ibn Mubaarak, rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alisema: (Tunamjuwa Mola wetu Mlezi kuwa yeye yupo juu ya Kiti chake cha Enzi, amejitenga mbali na viumbe vyake). Na maneno ya maulamaa kwenye mlango huu ni mengi sana hatuwezi kuyanukuu yote katika muhadhara huu, na mwenye kutaka kulifuatilia hilo zaidi, basi ayarejelee yaliyoandikwa na maulamaa wa sunna katika mlango huu, mfano kitabu kiitwacho "As-Sunnah" cha mtunzi aitwaye Abdullah ibn imamu Ahmad, na pia kitabu kiitwacho "At-Tawhiid" cha mtunzi aitwaye Al-imamu al-jaliil Muhammad ibn Khuzaimata, na kitabu kiitwacho "As-Sunna" cha mtunzi aitwaye Abulqaasim Al-lalkaaiy At-twabariy, na kitabu kiitwacho "As-Sunna" cha mtunzi aitwaye Abuubakar ibn Aaswim, na majibu ya sheikhul-islaam ibn Taimiyat kujibu watu wa Hamaat, nalo ni jibu zuri lenye faida kubwa. Ameweka wazi humo -Mwenyezi Mungu amrehemu - itikadi ya Ahlusunnah, na akanukuu humo mengi ya maneno yao, na ushahidi wa kisheria na kiakili juu usahihi wa yale waliyoyasema Ahlusunnah, na ubatili wa yale waliyoyasema wagomvi wao. Na vilele ujumbe wake Ibnu Taimiyat iliyopewa jina la Tadmuuriyat. Hakika amekunjuwa masuala haya ndani yake na akabainisha humo itikadi ya Ahlusunnah kwa kutumia ushahidi wake wa kimaandiko na kiakili, na kuwajibu wenye kupinga kwa yale yenye kuiweka wazi haki na kuitokomeza batili kwa kila mwenye kuitazama miongoni mwa watu wenye elimu kwa lengo zuri la kutaka kuijuwa haki. Na kila aliyekwenda kinyume na Ahlusunnah katika yale wanayoitakidi katika mlango wa majina na sifa za Mwenyezi Mungu, kwa hakika huyo bila shaka ataangukia kwenye kuhalifu ushahidi wa kimaandiko na kiakili pamoja na mgongano wa wazi na kila anachothibitisha na kukanusha.
Ama Ahlussunna waljamaa, wao wamemthibitishia Mwenyezi Mungu Mtukufu yale aliyoyathibitisha mwenyewe katika Kitabu chake kitukufu, au aliyomthibitishia Mtume wake Muhammad -rehema na amani ziwe juu yake - katika Hadithi zake zilizo sahihi, kuthibitisha panisa kufananisha. Pia walimtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu kutokana na kufanana na viumbe vyake, utakaso ambao umeepukana na kukanushia sifa hizo, kwa hivyo wakafaulu kwa kusalimika kutokana na makinzano, na wakaufanyia kazi ushahidi wote. Hii ndiyo desturi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusiana na mwenye kushikamana na haki ambayo amewatuma kwayo Mitume wake na akatoa muda wake kwa ajili ya hilo, na akaitafuta haki kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, kwamba Mwenyezi Mungu humuwezesha kuipata haki na kuzipa ushindi hoja zake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Bali (tulifanyalo ni hili) tunaitupa kweli juu ya batili; ikaivunjilia mbali, na mara ikatoweka}. [Al-Anbiyaa: 18]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Wala hawatakuletea mfano wowote, ila na Sisi tutakuletea (jawabu) kwa haki, na tafsiri iliyo bora}. [Al-Furqan: 33] Na kwa hakika ametaja ibnu Kathiir - Mwenyezi Mungu amrehemu - katika Tafsiri yake inayofahamika kwa wengi, alipozungumzia kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu - ((Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu ambaye aliziumba mbingu saba na ardhi kwa siku sita kisha akawa juu ya Kiti chake cha Enzi)). [Al-A'araf: 54] Alisema maneno mazuri katika mlango huu, yapendeza kuyanukuu hapa kutokana na faida zake kubwa. Amesema Ibnu Taimiyat, Mwenyezi Mungu amrehemu, na maneno yake hasa ni haya: ((Watu katika suala hili wana maneno mengi sana, na hapa siyo mahala pake pa kuyafafanua kwa kina. Bali kwa hakika katika suala hili tunafuata madhehebu ya wema waliotangulia: Maalik, Al-Wzaaiy, Aththawriy, Al-laithiy ibnu Saad, Shaafiiy, Ahmad, Is-haqa ibnu Rahaawaihi na wengineo miongoni mwa maimamu wa Waislamu wazamani na wa sasa. Nalo ni kuzipitisha (sifa na majina ya Mwenyezi Mungu) kama zilivyokuja pasina kutaka kujua namna zilivyo hasa, wala kuzifananisha, wala kuzipinga. Na maana ya dhahiri inayotekea kwenye akili za wenye kuzifananisha inakataliwa na haiendani na Mwenyezi Mungu. Kwani hakika Mwenyezi Mungu hafanani na chochote katika viumbe vyake, na hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona. Bali uhakika wa jambo hili ni kama walivyosema Maimamu, miongoni mwao akiwa ni Nuaimu ibnu Hammad Al-khuzaaiy, sheikh wa Imamu Bukhariy. Alisema: Yeyote atakayemfananisha Mwenyezi Mungu na viumbe vyake, basi amekufuru. Na atakayepinga chochote ambacho Mwenyezi Mungu amejielezea kwacho mwenyewe, basi amekufuru. Na hakuna kufananisha katika yale ambayo Mwenyezi Mungu alijielezea kwayo wala alichomwelezea kwacho Mtume wake. Kwa hivyo atakayemthibitishia Mwenyezi Mungu Mtukufu katika yale ziliyokuja nayo aya zilizo waziwazi, na habari zilizo sahihi kwa namna ambayo inaendana na utukufu wa Mwenyezi Mungu, na kumkanushia Mwenyezi Mungu mapungufu, basi atakuwa ameifuata njia ya uongofu)).
Kuamini Malaika
Ama kuwaamini Malaika, hilo linajumuisha kuamini uwepo wao kwa ujumla na kwa uchanganuzi. Kwa hivyo, Muislamu anapaswa kuamini kuwa Mwenyezi Mungu anao Malaika amewaumba ili wamtii na akawaelezea kuwa ni waja waliotukuzwa. Hawamtangulii kwa kauli, na wao wanatekeleza mambo kulingana na amri yake. {Mwenyezi Mungu anayajuwa yaliyo mbele yao (hao Malaika) na yaliyo nyuma yao (hao Malaika) wala hawamuombei yeyote ila yule anayemridhia Mwenyezi Mungu, nao kwa sababu ya kumuogopa wananyeyekea}. [Al-Anbiya: 28]. Na wao wapo aina nyingi. Miongoni mwao wamo waliopewa jukumu la kukibeba Kiti cha Enzi, na miongoni mwa kuna walinzi wa Pepo na Moto, na miongoni mwao kuna waliopewa jukumu la kuhifadhi matendo ya waja. Na tunaamini kwa njia ya uchanganuzi kuhusiana na yule ambaye Mwenyezi Mungu na Mtume wake walimtaja jina lake miongoni mwao kama vile Jibril, Miikail, Malik, mlinzi wa Moto, na Israafiil aliyejukumishwa kupuliza parapanda. Huyu ametajwa katika hadithi sahihi. Pia imethibiti kutoka katika vitabu sahihi kutoka kwa Aisha - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake - alisema: ((Malaika wameumbwa kutokana na nuru, na majini wameumbwa kutokana na moto wa asili usio na moshi, na amemuumba Adam kutokana na kile mlichoelezewa)). (3) Imepokelewa hadithi hii na imamu Muslim katika Sahihi yake. (3) Muslim, Kuipa dunia mgongo na mambo ya kulainisha moyo (2996), Ahmad (6/153).
Kuamini Vitabu
Na hivyo hivyo kuamini Vitabu ni wajibu kuviamini kwa ujumla, ya kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu aliteremsha Vitabu kwa Manabii wake na Mitume wake ili kuiweka wazi haki na kuilingania, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Kwa hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa hoja za waziwazi, na tukateremsha Kitabu pamoja nao na Mizani, ili watu wasimamie uadilifu}. [Al-Hadid: 25]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: ((Watu wote walikuwa ni umma mmoja. Basi Mwenyezi Mungu akatuma Manabii wabashiri na waonyaji. Na pamoja nao akateremsha Kitabu kwa Haki, ili kihukumu baina ya watu katika yale waliyokhitalifiana. Na wala hawakukhitalifiana ndani yake ila wale waliopewa Kitabu hicho...)) [Al-Baqara: 213].
Na tunaamini kwa upambanuzi vile ambavyo Mwenyezi Mungu alivyovitaja jina miongoni mwake, kama vile: Taurati, Injili, Zabuuri na Qur'an, nacho ndicho kitabu bora zaidi kuliko vyote na cha mwisho chake. Nacho ni chenye kuvihukumia vitabu vyote vilivyopita na kuvisadikisha. Nacho ndicho kitabu ambacho yapasa umma wote kukifuata na kuhukumiana kwacho pamoja na kufuata sunna sahihi kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake. Kwa sababu, Mwenyezi Mungu Mtukufu alimtuma Mtume wake Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake - hali ya kuwa ni Mtume aliyetumwa kwa majini na wanadamu wote, na akamteremshia Qur'ani hii ili ahukumu kwayo, na akaifanya hiyo Qur'ani kuwa ni ponya kwa yaliyo vifuani, ubainisho wa kila kitu, muongozo na rehema kwa Waumini, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na hiki ni Kitabu tulichokiteremsha, kilicho barikiwa. Basi kifuateni, na mchenimngu, ili mrehemewe}. [Al-An'aam: 155]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na tumekuteremshia kitabu hiki kielezacho kila kitu na ambacho ni uongofu na rehema na habari za furaha kwa Waislamu}. [An-Nahli: 89]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Sema: Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume kwenu nyinyi nyote, niliyetumwa na Mwenyezi Mungu Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Hapana mungu ila Yeye anayehuisha na anayefisha. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake asiyejua kusoma na kuandika, ambaye anamuamini Mwenyezi Mungu na maneno yake. Na mfuateni yeye ili mpate kuongoka}. [Al-A'araf: 158] Aya zenye maana hii zipo nyingi.
Kuamini Mitume
Na vilevile ni wajibu kuwaamini Mitume wote kwa jumla na mmojammoja. Hivyo tunaamini kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu alituma kwa waja wake Mitume miongoni mwao, waliokuwa ni wenye kuleta bishara njema na waonyaji na wenye kulingania kwenye haki. Basi yeyote aliyewakubali, alipata furaha. Na yeyote aliyekwenda kinyume nao, aliambulia hasara na majuto. Na wa mwisho wao ni Muhammad ibnu Abdillahi - rehema na amani ziwe juu yake - kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kwa hakika, kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Twaghuut (Shetani na vyote vinavyoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu)}. [An-Nahl: 36]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Mitume hao ni wabashiri na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kuletewa Mitume}. [An-Nisaa: 165] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa Manabii}. [Al-Ahzab: 40]. Na kila Mtume ambaye Mwenyezi Mungu alimuita kwa jina lake au imethibiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kumuita kwa jina lake, wote hao tunawaamini kwa ujumla na mmojammoja kama vile Nabii Nuuh, Huud, Swaleh, Ibrahiim na wengineo, ziwe juu yao na juu ya Mtume wetu rehema bora zaidi na amani safi mno.
Kuamini Siku ya Mwisho
Ama kuamini Siku ya Mwisho:
Inangia ndani yake kuamini kila kitu ambacho Mwenyezi Mungu na Mtume wake - rehema na amani ziwe juu yake - walijulisha juu yake amacho kitatokea baada ya kufa, kama vile mtihani wa kaburini na adhabu na neema zake, na yatakayokuwa siku ya Kiyama miongoni mwa mambo ya kutisha na ya shida, na uwepo wa Njia (Swiraat), mizani, kuhesabiwa, kulipwa na kusambazwa daftari la matendo kati ya watu. Basi kutakuwa na mwenye kukichukuwa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia na mwenye kukichukuwa kwa mkono wake wa kushoto au kwa nyuma ya mgongo wake. Na huingia vilevile katika imani hiyo, kuamini uwepo hodhi ya Mtume wetu Muhammad, ambalo watu watakwenda kunywa maji kutoka humo, na kuamni uwepo wa Pepo, Moto, Waumini kumuona Mola wao Mlezi Mtukufu na kuwasemesha wao na mengineyo yaliyokuja katika Qur'ani na hadithi sahihi kutoka kwa Mtume - rehema amani ziwe juu yake. Ni wajibu kuamini hayo yote na kuyasadikisha kwa namna alivyoweka wazi Mwenyezi Mungu na Mtume wake - rehema na mani ziwe juu yake.
Kuamini Qadari
Ama kuamini Qadari, inaingia ndani yake kuamini mambo manne:
Jambo la kwanza: Kwamba Mwenyezi Mungu alikwishajuwa yaliyokuwa na yatakayokuwa, na alikwishajuwa hali za waja wake, na akajuwa kuhusu riziki zao, mwisho wa muda wa maisha yao, matendo yao na mengineyo katika mambo yao, hakuna linalofichikana kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika hayo, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika Mwenyezi Mungu juu ya kila kitu ni mjuzi}. [Al-Baqara: 231]. Na amesema - Mwenye Nguvu na utukufu: {Ili mpate kujuwa kuwa Mwenyezi Mungu ni Muweza wa ila kitu, na kuwa Mwenyezi Mungu elimu na ujuzi wake umekizunguka kila kitu}. [At-Twalaq: 12].
Jambo la pili : Kuandika kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kila alichokikadiria na kukipanga, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinachopunguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinachohifadhi yote}. [Qaaf: 4]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha}. [Yaasin: 12] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Je, hujui kwamba Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo mbinguni na katika ardhi? Hakika hayo yamo Kitabuni. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi}. [Al-Hajj: 70]
Jambo la tatu: Kuamini matashi yake yanayotekelezeka. Kwani anachotaka kiwe, basi kinakuwa. Na kile asichotaka kiwe, hakiwezi kuwa, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika mwenyezi hufanya alitakalo}. [Al-Hajj: 18]. Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Hakika amri yake anapotaka kitu kiwe, ni kukiambia, "Kuwa!" Na kikawa}. [Yasin: 82]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye elimu, Mwenye hekima}. [Al-Insan: 30]
Jambo la Nne: Kuamini uumbaji wake Mwenyezi Mungu Mtukufu wa vyote vilivyopo, hakuna muumba mwingine asiyekuwa Yeye na hakuna mola mlezi asiyekuwa Yeye, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu, na Yeye ndiye Mlinzi juu ya kila kitu}. [Az-Zumar: 62] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Enyi watu, kumbukeni neema za Mwenyezi Mungu juu yenu. Ati yupo muumba mwengine asiyekuwa Mwenyezi Mungu anayekupeni riziki kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Hapana mungu ila Yeye tu. Basi wapi mnakogeuzwa?} [Faatir: 3] Hivyo basi, kuamini Qadari kunaingia ndani yake kuamini haya mambo manne kulingana na msimamo wa ahlusunna waljamaa, tofauti na wale waliopinga baadhi ya hayo miongoni mwa watu wa uzushi.
Imani ya kweli inakuwa kwa kauli na vitendo, inazidi kwa kutii na hupungua kwa kufanya maovu.
Na huingia katika imani ya kumuamini Mwenyezi Mungu, kuwa na itikadi kwamba Imani ni kauli na vitendo, inazidi imani kwa kumtii Mwenyezi Mungu na hupungua kwa kumuasi Mwenyezi Mungu, na kwamba haifai kumkufurisha yeyote miongoni mwa Waislamu kwa kufanya maasi yasiyokuwa ushirikina na kukufuru, kama vile kufanya zinaa, uwizi, kula riba, kutumia vilevi, kutowatendea wema wazazi wawili na maasia mengine ambayo ni katika madhambi makubwa ikiwa mwenye kuyafanya (hayo maasi) hakuyahahalisha, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa, na husamehe madhambi yasiyokuwa shirki kwa amtakaye}. [Al-Nisaa: 48] Na kwa sababu ya yale yaliothibiti kwa wingi kutoka katika hadithi za Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - kwamba Mwenyezi Mungu atamtowa Motoni kila mtu ambaye moyoni mwake kuna chembe ndogo ya imani kiasi cha uzito wa punje ya haradali.
Kupenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na kuchukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kuungana na kusaidia na Waislamu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuwachukia makafiri kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Na katika kumuamini Mwenyezi Mungu, ni kupenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuchukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kuungana na kusaidia ajili ya Mwenyezi Mungu, na kufanya uadui kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Muislamu anafaa kuwapenda Waislamu wenzake na kuungana na ksaidiana nao. Na awachukie makafiri na kuwafanya kuwa ni maadui. Na wale walio juu zaidi katika Waislamu katika umma huu ni maswahaba wa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake. Kwa hivyo, Ahlusunnat waljamaa wanawapenda na wanawafanya kuwa ni vipenzi vyao, na wanaitikadi kuwa wao ndio watu bora baada ya Manabii, kwa maneno yake Mtume -rehema na amani ziwe juu yake: "Karne iliyo bora zaidi ni karne yangu, kisha karne ya waliofuta, kisha waliofuta." [4] Wanachuoni wamekubaliana kwamba hadithi hii ni sahihi. Na wanaitakidi kuwa mbora wa hao maswahaba ni Abu Bakr As-Swiddiq, kisha Umar al-Faaruuq, kisha Uthman Dhunnurain, kisha Ali Al-murtadhwa - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote. Kisha wanafuatisha baada yao waliosalia miongoni mwa wale kumi waliobashiriwa Pepo, kisha maswahaba wote - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao. Wananyamazia ugomvi uliokuwa kati ya maswahaba, na wanaitakidi kuwa wao katika ugomvi huo walikuwa ni wenye kujitahidi. Yeyote aliyefikiwa usahihi, atapata ujira mara mbili. Naye aliyekosea, basi atapata ujira mmoja. Na wanawapenda watu wa nyumba ya Mtume wa Mwenyezi Mungu - rehema na amani ziwe juu yake - wale wenye kumuamini, wanawafanya kuwa vipenzi na wanawapenda wake za Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - Mama za Waumini na wanawaombea radhi wote. Na wanajiweka mbali na njia za Mashia ambao wanawachukia maswahaba wa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - wanawatukana, na wanapindukia mipaka katika kuwasifia watu wa nyumba ya Mtume, na huwainua zaidi ya alipowaweka Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mtukufu. Kama ambavyo wanajiweka mbali na An-Nawaasibu, ambao ni kundi ambalo linaudhi watu wa nyumba ya Mtume kwa maneno na vitendo. [4] Al-Bukhariy, Ushahidi mbalimbali (2509), Muslim, Ubora wa Maswahaba (2533), At-Tirmidhiy, Al-manaaqib (3859), Ibnu Maajah, Hukumu mbalimbali (2362), Ahmad (1/434).
Na yote tuliyoyataja katika maneno haya mafupi yanaingia ndani ya itikadi sahihi ambayo Mwenyezi Mungu alimtuma nayo Mtume wake Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake - nayo ndiyo itikadi ya kundi lililofaulu, nalo ni kundi la ahlusunnat wal-jamaa, kundi ambalo amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake - kulihusu kwamba: "Halitowacha kundi moja katika umma wangu kuwa kwenye haki huku ni lenye kuinusuriwa. Halitadhuriwa na yeyote atakayewaangusha mpaka ije amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu." [5] Naye Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alisema pia: "Wamegawanyika Mayahudi katika makundi sabini na moja, na wamegawanyika Wakristo katika makundi sabini na mbili, na utagawanyika umma huu katika makundi sabini na tatu. Yote yataingia Motoni isipokuwa moja." Tukasema: 'Ni la akina nani ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?' Akasema: "Yeyote atakayekuwa katika mfano wa yale niliyo nayo mimi na maswahaba zangu." [6] Na hiyo ndiyo itikadi ambayo inapasa kushikamana nayo na kunyooka juu yake, na kujihadhari na itikadi zenye kupingana nayo. [5] Muslim, Al-imarat (1920), At-Tirmidhiy, Al-fitan (2229), Abuu Daudi, Al-Fitan wal-malaahim (4252), Ibnu Maajah, Al-Fitan (3952), Ahmad (5/279). (6) Ibnu Maajah, Al-Fitan (3992).
Kuwataja wenye kuipinga itikadi hii na wenye kwenda kinyume nayo
Aina zao
Na ama wenye kupotoka mbali na itikadi hii na wenye kwenda kinyume nayo, wao ni makundi mengi. Miongoni mwao kuna wale wenye kuabudu masanamu, Malaika, Mawalii (watu wema), majini, miti, mawe na vinginevyo. Hawa wote hawakukubali wito wa Mitume bali waliwapinga na hawakaidi, kama vile Makuraishi na makundi ya Waarabu walivyomfanyia Mtume wetu Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake. Walikuwa wakiwaomba miungu wao wawatekelezee haja zao na kuwaponya wagonjwa na kuwalinda dhidi ya maadui. Na walikuwa wakichinja kwa ajili yao na kuwawekea nadhiri. Pindi Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - alipowakataza hayo na akawaamrisha kumtakasia ibada Mwenyezi Mungu peke yake, walishangazwa na hilo, wakampinga na wakasema: {Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu}. [Swad: 5] Hakuwacha Mtume - rehema na amni ziwe juu yake - kuwalingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, kuwatahadharisha na ushirikina, kuwafafanulia uhakika wa miungu wanaowaomba; mpaka Mwenyezi Mungu alipowaongoza wale alioongoza miongoni mwao, kisha baada ya hapo wakaingia katika dini ya Mwenyezi Mungu makundi kwa makundi. Basi dini ya Mwenyezi Mungu ikapata ushindi dhidi ya dini zingine baada ya ulinganiaji wa kuendeleva, na jihadi ya muda mrefu iliyoongozwa na Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - na maswahaba zake, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, na wale waliowafuata maswahaba kwa wema. Kisha hali ikabadilika na ujinga ukawaenea watu wengi mpaka wengi wakarudi kwenye dini za zama za ujinga, kwa kuvuka mipaka kuhusiana na Manabii na mawalii, kwa kuwaomba na kuwataka msaada na maengineyo miongoni mwa aina za ushirikina, na wala hawakujuwa maana ya Laailaha illallahu kama walivyojuwa maana yake makafiri wa Kiarabu. Basi Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuombwa msaada.
Na wala haijaacha kuenea shirki hii kwa watu mpaka katika zama zetu hizi; kwa sababu ya ujinga mwingi na kuwa mbali na zama za utume.
Dhana potofu na utata wa washirikina wa sasa ndiyo dhana potofu na utata wa washirikina wa mwanzo, na kutaja baadhi ya itikadi za kikafiri.
Dhana potofu na utata wa hawa washirikina wa sasa, ndiyo Dhana potofu na utata wa washirikina wa mwanzo, na Dhana potofu hiyo ni kauli yao waliposema: 'Hawa ni waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu. Sisi hatuwaabudu wao isipokuwa watuweke karibu na Mwenyezi Mungu.' Na kwa hakika Mwenyezi Mungu alibatilisha dhana hii potofu, na akaweka wazi kuwa yeyote atakayemuabudu asiyekuwa Yeye, sawa awe ni nani, basi hakika atakuwa amemshirikisha naye na amekufuru, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Nao, badala ya Mwenyezi Mungu, wanaabudu wasiowadhuru wala kuwanufaisha, na wanasema: 'Hawa ndio waombezi wetu kwa Mwenyezi Mungu!} [Yunus: 18]. Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu akawajibu kwa maneno yake: {Sema: 'Je, mnamwambia Mwenyezi Mungu asiyoyajua yaliyoko katika mbingu wala katika ardhi? Sub-hanahu wa Taa'la (ametakasika na ametukuka) mbali na hao wanaomshirikisha naye'}. [Yunus: 18] Basi Mwenyezi Mungu Mtukufu akaweka wazi katika aya hii kuwa kumuabudu asiyekuwa Yeye miongoni mwa Manabii na Mawalii au wengineo ni ushirikina ulio mkubwa hata wakiuita wenye kufanya hivyo kwa jina lingine. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na wale wanaowafanya wengine kuwa ni waungu badala yake na wakisema: 'Sisi hatuwaabudu isipokuwa ili wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu.'} [Az-Zumar: 3]. Kwa hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu akawajibu kwa maneno yake: {Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika yale wanayohitalafiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamuongoi aliye muongo kafiri}. [Az-Zumar: 3]. Basi Mwenyezi Mungu Mtukufu akaweka wazi kwa hayo kuwa kumuabudu kwao asiyekuwa Yeye kwa kuomba, kukhofu, kutaraji na mfano wa hayo ni kumkufuru Mwenyezi Mungu Mtukufu, na akaweka wazi kuwa kauli yao ni ya uongo waliposema kwamba miungu yao inawaweka karibu zaidi na Mwenyezi Mungu.
Na miongoni mwa itikadi za kikafiri ambazo zinapingana na itikadi iliyo sahihi, na zenye kwenda kinyume na waliyokuja nayo Mitume - rehema na amani ziwe juu yao - ni kile wanachoitakidi wenye kupinga uwepo wa Muumba wanaoisha katika zama hizi miongoni mwa wafuasi wa Marx, Lenin na wasiokuwa hao miongoni mwa walinganizi wa kutokuwepo kwa Muumba na walinganiao ukafiri. Ni sawa waliite hilo kwa jina la Ujamaa au Ukomunsti au Uamsho au yasiyokuwa hayo miongoni mwa majina mengine, hakuna tofauti; kwani msingi mkuu wa hawa wanaopinga uwepo wa Mwenyezi Mungu ni kuwa hakuna mungu na kuwa maisha yalipatikana kwa nyenzo tu. Na miongoni mwa misingi yao ni kupinga kufufuliwa baada ya kufa, na kupinga uwepo wa Pepo na Moto na kupinga dini zote. Na atakayetazama kwenye vitabu vyao na kayasoma waliyokuwa nayo, atayafahamu hao kwa yakini, na hapana shaka kuwa hizi itikadi zinapingana na dini zote za mbinguni, huwafikisha watu wake kwenye mwisho mbaya hapa duniani na akhera.
Na miongoni mwa itikadi zinazopingana na haki, ni itikadi ya baadhi ya Shia (Baatwiniya) na baadhi ya Masufi wanaoitikadi kuwa baadhi ya wanaowaita Mawalii (vipenzi) wanashirikiana na Mwenyezi Mungu katika kupitisha na kuendesha mambo ya ulimwengu, na wanawaita 'Aqtwaab (nguzo), Awtaad (vigingi), Aghwaath (watoa msaada)', na majina mengine yasiyokuwa hayo ambayo wamewazulia waungu wao. Na hili ni katika shirki mbaya zaidi, na yenye shari kuliko shirki ya Waarabu iliyokuwepo enzi za ujinga. Kwa sababu makafiri wa Kiarabu hawakumshirikisha katika umola, bali walimshirikisha katika ibada tu, na shirki yao ilikuwa wakati wa raha peke yake. Ama wakati wa matatizo, walikuwa wakimtakasia ibada Mwenyezi Mungu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na wanapopanda makafiri kwenye majahazi baharini, na wakaogopa kuzama, wanampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtakasia dua wakati wa shida yao. Na Anapowaokoa akawafikisha kwenye nchi kavu, na shida ikawaondokea, wanarudi kwenye ushirikina wao}. [Al-Ankabut: 65]. Ama kuhusu umola, walikuwa wakikubali kwamba umola ni wake Yeye peke yake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na ukiwauliza ni nani aliyewaumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu!} [Az-Zukhruf: 87] Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Sema: Ni nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Au ni nani anayemiliki kusikia na kuona? Na ni nani amtoaye hai kutoka kwenye maiti, na akamtoa maiti kutoka kwa aliye hai? Na ni nani anayeyaendesha mambo yote? Watasema: Allah (Mwenyezi Mungu). Basi sema: Je, hamumchi?} [Yunus: 31]. Na aya zenye maana hii ni nyingi sana.
Waliyoyazidisha washirikina wa sasa zaidi ya wale wa mwanzo.
Ama washirikina wa sasa wamezidisha shirki zaidi ya washirikina wa mwanzo katika sehemu mbili: Sehemu ya kwanza ni ushirikina wa baadhi yao katika umola, na sehemu ya pili ni ushirikina wao wakati wa raha na shida, kama linavyofahamika hilo kwa aliyeishi nao na akawafutalia hali zao, na akaoyaona wanayoyafanya kwenye kaburi la Hussein na Badawiy na wengineo katika nchi ya Misri, na kwenye kaburi la 'Aidaruus huko Aden, na Al-Haadiy katika nchi ya Yemen, na Ibnu 'Arabiy huko Sham, na sheikh Abdulqadir Al-Jailaaniy katika nchi ya Iraq, na makaburi mengine yaliyo mashuhuri ambayo wanayatukuza wengi miongoni mwa watu, na wakayaelekezea haki nyingi za Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu. Hata hivyo, ni mara chache sana upata wenye kuwakataza hayo na kuwabainishia ukweli wa Tauhiid ambayo Mwenyezi Mungu alimtuma nayo Mtume wake, rehema na amani ziwe juu yake, na Mitume waliokuwa kabla yake - juu yao iwe amani. Basi hakika (huo ni msiba na) sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu na kwake Yeye sote tutarejea. Na tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu awarudishe kwenye uwongofu wao, na awazidishie walinganizi waongofu miongoni mwao, na awawezeshe viongozi wa Waislamu na wanachuoni wao kuipiga vita shirki hii kuimaliza pamoja na njia zake. Hakika Yeye ni Msikivu aliye karibu mno.
Na miongoni mwa itikadi potofu zinazopingana na itikadi sahihi katika mlango wa majina na sifa za Mwenyezi Mungu ni itikadi ya wazushi miongoni mwa kundi liitwalo Jahmiayyah na Muutazila na wenye kufuata njia zao katika kupinga sifa za Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu, na kuzikataa sifa zake Mwenyezi Mungu Mtukufu zenye ukamilifu, na badala yake wakamsifia na sifa za vitu visivyokuwepo, na visivyokuwa na uhai na visivyowezekana. Ametakasika Mwenyezi Mungu kuwa na sifa wanazomsifia utakasifu mkubwa wa hali ya juu. Na anaingia katika itikadi potofu kila mwenye kupinga baadhi ya sifa na kukataa baadhi yake, kama vile kundi la Ashaaira. Kwa hakika, inawalazimu katika baadhi ya sifa walizozikubali waende sambamba na zile sifa ambazo walizikimbia na kuzikataa na wakabadilisha maana zake na wakawa ni wenye kwenda kinyume na ushahidi wa kisheria na wa kiakili, na wakajitia katika mgongano ulio wazi kabisa kwenye suala hilo. Ama Ahlusunna waljamaa, wao kwa hakika walimthibitishia Mwenyezi Mungu kile alichojithibitishia mwenyewe au kile alichomthibitishia Mtume wake Muhammad - rehema na amani ziwe juu yake - miongoni mwa majina na sifa kwa njia ya ukamilifu, na wakamweka mbali na kumtakasa kwa kutomfananisha na viumbe wake, utakaso ambao uko mbali na uchafu wa kukataa kwamba Mwenyezi Mungu ana majina na sifa, na wakaufanyia kazi ushahidi wote na hawakuubadilisha wala kuukataa, na wakasalimika kutokana na mgongano ambao ulitokea kwa wengine - kama ilivyotangulia kuwekwa wazi jambo hilo. Na hii ndiyo njia ya mafanikio, na maisha mazuri duniani na akhera, na ndiyo njia iliyonyooka waliyoifuata watu wema waliotangulia katika umma huu na viongizi wake, na wala hawawezi kuwa wema watu wa mwisho wa umma huu, isipokuwa kwa kufuata kile kilichowafanya wa mwanzo wao kuwa wema, nacho ni kufuata Kitabu na Sunna, na kuwacha kila kinachokwenda tofauti na Kitabu na Sunna.
Uwajibu wa kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na sababu za kuwashinda maadui wa Mwenyezi Mungu.
Hakika wajibu muhimu kwa aliyebaleghe mwenye akili, na jambo la lazima kwake ni amuabudu Mola wake Mlezi, Mtukufu, Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na Mola Mlezi wa Arshi tukufu, mwenye kusema katika kitabu chake kitukufu: {Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akainuka juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zilizotiishwa kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba ni kwake, na amri (ni yake). Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote}. [Al-A'araf: 54] Na ameeleza Mwenyezi Mungu Mtukufu katika sehemu nyingine katika Kitabu chake kuwa yeye amewaumba majini na wanadamu ili wamuabudu yeye. Alisema Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu: {Na sikuwaumba majini na wanadamu ila waniabubu}. [Dhariyat: 56]. Na hii ibada ambayo Mwenyezi Mungu amewaumba majini na watu kwa ajili yake, ni kumpwekesha yeye kwa aina mbalimbali za ibada miongoni mwa ibada hizo ni Swala, Funga, Zaka, Hija, Kurukuu, Kusujudu, kufanya Tawafu, kuchinja, kutia nadhiri, kuwa na khofu, kutaraji, kuomba msaaada na ulinzi, kuomba kinga na aina zote za Dua. Pia huingia katika ibada kumtii yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu katika yote aliyoyamrisha na kuwacha yote aliyoyakataza kwa namna kilivyofahamisha Kitabu na Sunna za Mtume wake muaminifu, rehema na amani ziwe juu yake kutoka kwa Mola wake Mlezi. Na kwa hakika, Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaamrisha majini na wanadamu wote kufanya ibada hii ambayo wameumbwa kwa ajili yake, na akawatuma Mitume wote na akateremsha Vitabu ili kuiweka wazi ibada hii, kuifafanuwa, kuilingania na kuamrisha ifanywe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi aliyewaumba nyinyi na wale wa kabla yenu, ili mpate kuwa wachamungu}. [Al-Baqara: 21] Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu}. [Al-Israai: 23] Na maana ya neno "Qadhwaa" katika aya hii ni kwamba ameamrisha na ameusia. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti}. [Al-Bayyina: 5]. Na Aya zenye maana kama hii katika kitabu cha Mwenyezi Mungu ni nyingi. Na amesema Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu: {Na anachokupeni Mtume, chukueni. Na anachokukatazeni, jiepusheni nacho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu}. [Al-Hashr 7]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Enyi mlioamini! Mtiini Mwenyezi Mungu, na mtiini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo, basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema}. [An-Nisaa: 59] Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Mwenye kumtii Mtume, basi atakuwa amemtii Mwenyezi Mungu}. [An-Nisaai: 80]
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kwa hakika, kwa kila umma tuliutumia Mtume ya kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Twaghuut (Shetani na vyote vinavyoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu}. [An-Nahl: 36]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipokuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu}. [Al-Anbiya: 25], Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Alif Lam Raa. Hiki ni kitabu ambacho Aya zake zimewekwa wazi kisha zikapambanuliwa vizuri, kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye hekima, Mwenye habari za kila kitu}. Imefanywa hivyo) ili msiabudu isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi kwenu ni mwonyaji na mbashiri nitokae kwake}. [Huud: 1-2].
Hivyo basi, aya hizi zenye maana wazi na zisizo badilika, na zile zilizokuja na maana yake kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu, zote zinaashiria uwajibu wa kufanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake, na kwamba hiyo ndiyo asili ya dini na msingi wa mila, kama vile zinavyoashiria kuwa hilo ndilo hekima ya kuumbwa majini na watu na kutumwa Mitume na kuteremshwa Vitabu. Basi ni wajibu kwa wote wanaojukumishwa na sheria, ni kutilia umuhimu jambo hili na kujifunza, na kujihadhari na yale waliyoangukia ndani yake wengi wa wale wanaojinasibisha na Uislamu la kuvuka mipaka kuhusiana na Manabii na watu wema, kuyajengea makaburi yao, kujenga misikiti na makuba juu yake, kuwaomba hao wema na kuwataka msaada, kuwakimbilia wao kwa kuwaomba wawatekelezee haja zao na wawaondolee matatizo yao, na wawaponyee wagonjwa wao na wawalinde kutokana na maadui na mambo mengine miongoni mwa aina za shirki kubwa. Na hakika imekuja habari sahihi kutoka kwa Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - habari ambayo inawafikiana na yale yaliyokuja katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu na utukufu. Imekuja katika sahihi mbili kutoka kwa Muaadh -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, amemwambia: "Hivi unajuwa ni ipi haki ya Mwenyezi Mungu kwa waja wake na haki za waja kwa Mwenyezi Mungu?" Akasema Muadh: Nikasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanajuwa zaidi. Akasema Mtume - rehema na amani ziwe juu yake -: Haki za Mwenyezi Mungu kwa waja ni wamuabudu yeye na wala wasimshirikishe na chochote. Na haki za waja kwa Mwenyezi Mungu ni kutomuadhibu yeyote yule ambaye hakumshirikisha na chochote." 7} Hadi mwisho wa hadithi. Na katika sahihi ya Bukhari imepokelewa kutoka kwa Ibnu Masud - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba Mtume - rehema na mani ziwe juu yake - amesema: "Yeyote atakayekufa huku anamuomba mwenza pamoja na Mwenyezi Mungu, ataingia Motoni."{8} Na amepokea Imamu Muslim katika sahihi yake kutoka kwa Jaabir - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake - kwamba: Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amesema: "Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali ya kuwa hamshirikishi na chochote, ataingia Peponi. Na atakayekutananaye hali ya kuwa anamshirikisha na chochote, ataingia Motoni."{9} Na hadithi zenye maana hii zipo njingi. Na masuala haya ni katika masuala muhimu na makubwa. Na hakika Mwenyezi Mungu alimtuma Mtume wake Muhammad -rehema na amani ziwe juu yake - kulingania Tauhiid na kukataza shirki. Hivyo, akafanya kazi Mtume - rehema na amani ziwe juu yake - ya kufikisha yale aliyotumwa nayo na Mwenyezi Mungu kwa ukamilifu, na akaudhiwa maudhi makubwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu lakini alisubiri kwa hayo maudhi, na wakasubiri pamoja naye maswahaba zake - radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao - juu ya kufikisha wito wa Kiislamu mpaka Mwenyezi Mungu akatoa katika Bara Arabu masanamu na vyote viabudiwavyo visivyokuwa Mwenyezi Mungu. Basi watu wakaingia katika dini makundi makundi, na yakavunjwa masanamu yalikuwepo pembeni mwa Al-Kaaba na ndani ya Al-Kaaba na yaliangamizwa Laata, Uzza na Manata na yakavunjwa masanamu yote ambayo yalikuwa ni ya makabila ya Waarabu, na vikavunjwa vyote walivyokuwa wakiviabudu visivyokuwa Mwenyezi Mungu, na neno la Mwenyezi Mungu likawa juu, na ukaenea Uislamu katika Bara Arabu. Kisha Waislamu wakaelekea kwa ajili ya ulinganiaji nje ya Bara Arabu, na Mwenyezi Mungu akawaongoa kupitia wao waliotangulia kuandikiwa maisha ya furaha katika waja, na Mwenyezi Mungu akaieneza haki na uadilifu kupitia wao katika sehemu kubwa ya miji iliyoendelea, na wakawa kwa ulinganizi huo ni waongozi wa uongofu na viongozi wa haki na walinganizi wa uadilifu na kufanya mambo kutengenea. Kisha wakafuata njia yao waliokuja baada yao na wale waliowafuta nyuma yao kwa wema, wakawa ni waongozi wa uongofu na walinganizi wa haki wakiieneza dini ya Mwenyezi Mungu, na wanawalingania watu kwenye kumtakasia ibada Mwenyezi Mungu na wanapigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa nafsi zao, mali zao na wala hawaogopi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu lawama za wenye kulaumu. Basi Mwenyezi Mungu akawasaidia na akawapa ushindi dhidi ya maadui zao, na akawapa alichowaahidi katika kauli yake Mtukufu: {Enyi mlioamini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na ataiimarisha miguu yenu}. [Muhammad :7]. Na amesema Mwenye nguvu, Mtukufu: {Na bila ya shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anayemsaidia Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mtukufu. Wale ambao tukiwapa madaraka katika nchi, husimamisha Swala, na wakatoa Zaka, na wakaamrisha mema, na wakakataza mabaya. Na kwa Mwenyezi Mungu ndiko marejeo ya mambo yote}. [Al-Hajj 41-42]. Kisha baada ya hapo, watu wakabadilika, wakagawanyika na wakaregea kuhusiana na jambo la kupigana Jihadi, na wakapendelea maisha mazuri ya furaha na wakafuata matamanio, na yakaenea kati yao maovu isipokuwa yule aliyelindwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu. Basi Mwenyezi Mungu akawabadilishia na kuwatawalishia maadui kuwa viongozi wao ikiwa ni malipo kwa yale waliyoyafanya, na Mola wako Mlezi siku zote siyo mwenye kuwadhulumu waja. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Hayo (ya kuwafika balaa) ni kwa sababu Mwenyezi Mungu habadilishi kabisa neema alizowaneemesha watu, mpaka wao wabadilishe yaliyomo ndani ya nafsi zao}. [Al-Anfaal: 53]. Hivyo basi, ni wajibu kwa Waislamu wote na kwa serekali na mataifa kurudi kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kufanya ibada kwa ajili yake peke yake, na kutubia kwake kutokana na mapungufu na makosa yao yaliyopita, na kufanya haraka kutekeleza yale aliyowawajibishia Mwenyezi Mungu katika mambo ya lazima na kujiweka mbali na aliyowaharamishia, na kuusiana kati yao kufanya hayo na kusaidiana juu yake. [7] Al-Bukhariy, Kuomba ruhusa (5912), Muslim, Iman (30), At-Tirmidhi, Imani (2643), Ibnu Maajah, Kuipa dunia mgongo (4296), Ahmad (5/238). [8] Al-Bukhariy, Tafsiri ya Qur'ani (4227), Muslima, Imani (92), Ahmad, (1/374). [9] Al-Bukhariy, Elimu (129), Muslim, Imani (32), Ahmad,(3/157).
Na miongoni mwa mambo muhimu katika hayo, ni kutekeleza hukumu ya kisheria, na kuhukumu kwa sheria kati ya watu katika kila kitu, na kutafuta hukumu kutoka kwayo, na kuziwacha kanuni zilizowekwa na watu zilizo kinyume na sheria za Mwenyezi Mungu, na kuwacha kuhukumiana kwazo na kuyalazimisha mataifa yote kufuata hukumu ya Sheria (ya Mwenyezi Mungu), kama inavyo wajibu kwa maulamaa kuwafahamisha watu dini yao na kueneza mawaidha ya Kiislamu kati yao, na kuusiana kutenda haki na kusubiri juu yake, na kuamrisha mema na kukataza maovu, na kuwahamasisha viongozi (wa Kiislamu) kufanya hayo. Kama ambavyo ni lazima kupiga vita misingi yenye kuangamiza miongoni mwa hiyo misingi ni Usoshalisti (ujamaa), Uamsho na kutetea vikali Uraia na mingineyo miongoni mwamisingi na madhebu yenye kwenda kinyume na Sheria, na wakifanya hayo, Mwenyezi Mungu atawatengenezea Waislamu yale yaliyoharibika na atawarudishia yaliyoondoka, na atawarudishia heshima yao iliyokuwepo mwanzo, na atawanusu dhidi ya maadui zao na atawapa utulivu katika ardhi kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu naye ndiye msema kweli zaidi ya wote: {Na ni wajibu juu yetu kuwanusuru waumini}. [Ar-Rum: 47]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walioamini miongoni mwenu na wakatenda mema, ya kwamba atawafanya wasimamizi katika ardhi kama alivyowafanya wazimamizi wale wa kabla yao, na kwa yakini atawasimamishia Dini yao aliyowapendelea, na atawabadilishia amani baada ya hofu yao. Wawe wananiabudu Mimi, wala wasinishirikishe na chochote. Na watakaokufuru baada ya hayo, basi hao ndio wavukao mipaka}. [An- Nuur: 55]. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Hakika bila ya shaka Sisi tunawanusuru Mitume wetu na wale walioamini katika uhai wa duniani na siku watakaposimama Mashahidi}. [Suratul Ghaafir :51]. {Siku ambayo hautawafaa madhalimu udhuru wao, nao watapata laana, na watapata makazi mabaya kabisa}. [Ghaafir: 52]
Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ndiye aombwaye kuwaboresha viongozi wa Waislamu na watu wote, na kwamba awape ufahamu wa dini, na kulikusanya jambo lao kwenye uchamungu, na awaongoze wote katika njia yake iliyonyooka, na ainusuru haki kwa na kuididimiza batili kupitia wao, na awawezeshe wote wasaidiane kwenye wema na uchamungu, na kuusiana kuifuata haki na kuwa na subira juu yake. Hakika yeye ndiye msimamizi na Muweza wa hilo. Na rehema za Mwenyezi Mungu na amani ziwe juu ya mja wake na Mtume wake aliye mbora kwake katika viumbe vyake ambaye ni Nabii wetu, kiongozi wetu na bwana wetu Muhammad ibnu Abdillah, amani iwe juu ya watu wake, Maswahaba zake na mwenye kufuata muongozo wake. Na amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yenu na rehema zake na baraka zake.