الأذكار التي تقال صباحًا ومساءً

الأذكار التي تقال صباحًا ومساءً

الأذكار التي تقال صباحًا ومساءً كتبها بخط يده فضيلة الشيخ العلامة محمد بن صالح العثيمين من صحيح الأذكار الثابتة عن النبي -صلى الله عليه وسلم-

Language: lang_sw
Prepared by:
Version: 2.0
Translations 56
Amharic Assamese Azerbaijani Bengali +52
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma mwenye kurehemu adhkaari ambazo husemwa Asubuhi na Jioni.

Mwenyezi Mungu hakuna mola isipokuwa Yeye,(na) ndiye Mwenye uhai wa maisha, Msimamia kila jambo, Kusinzia hakumshiki wala kulala. Ni Vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo katika ardhi, Na nani huyo awezaye kuombea mbele Yake (Mungu) bila idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao, hawalijui lolote katika elimu Yake (Mwenyezi Mungu) isipokuwa kwa alipendalo (Mwenyezi Mungu).Kiti chake cha Enzi kimeenea mbingu na na ardhi, wala kuvilinda hivyo hakumshindi, na Yeye (peke yake) ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu" Ayatul Kursiy 255 Al Baqarah.

Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake, na Waislamu, (pia wameamini hivyo) wote wamemwamini Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na vitabu vyake, na Mitume wake hatutofautishi baina ya yeyote katika Mitume wake, na husema tumesikia na tumetii (Tunakuomba msamaha Mola wetu na marejeo ni kwako* Mwenyezi Mungu hailazimishi nafsi yoyote isipokuwa yaliyo sawa na uweza wake. (Faida ya) yale iliyochuma (nafsi hiyo) ni yake na hasara ya yale iliyochuma ni juu yake. (Husema); Mola wetu usitutese kama tukisahau au tukikosa, Mola wetu na usitubebeshe mzigo kama uliowabebesha wale waliokuwa kabla yetu. Mola wetu usitutwike tusiyoyaweza na utusamehe na utufutie na uturehemu, Wewe ndiye Mlinzi wetu. Basi tusaidie juu ya watu makafiri. Aya 285-286.Al Baqarah

Sema ni Yeye Mwenyezi Mungu Mmoja) Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko) Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu) Zitasomwa sura zote tatu kwa ukamilifu mara tatu tatu.

Ninajikinga kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyo timia kutokana na shari alizo ziumba. Mara tatu.

Kwa jina la Mwenyezi Mungu ambaye hakidhuru kitu chochote (kwa kutaja) pamoja na jina lake (Mwenyezi Mungu) katika ardhi wala katika mbingu na Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye ujuzi. Mara tatu.

Nimeridhia kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Mola Mlezi na uislamu ndio dini ya kweli na Muhammadi-Rehema na amani ziwe juu yake ni Nabii. Mara tatu.

Tumeingia asubuhi na ufalme wa asubuhi umethibiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kila sifa njema ni zake Mwenyezi Mungu hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, Ufalme ni wake na sifa ni zake na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza,Ewe Mola Mlezi ninakuomba heri zinazo patikana ndani ya siku hii na heri za baada ya siku hii, na ninajikinga kwako kutokana na shari za siku hii na shari za baada ya siku hii,Ewe Mola Mlezi ninajikinga kwako kutokana na uvivu na uzee (ukongwe) na utu uzima mbaya, na ninajikinga kwako kutokana na adhabu ya moto na adhabu ya kaburi. Na jioni atasema: Tumeingia jioni na ufalme wajioni umethibiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Na atasema: Ewe Mola Mlezi ninakuomba heri za usiku huu. Mpaka mwisho, badala ya: (tumeingia asubuhi na umethibiti) na kuhusu (siku hii).

Ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili yako tumeingia asubuhi na kwa ajili yako tumeingia usiku na kwa ajili yako tunapata uhai na kwa ajili yako tunakufa na kwako ndiko kuna kukusanywa Na jioni atasema: Ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili yako tumeingia jioni na kwa ajili yako tumeingia asubuhi na kwa ajili yako tunakufa na kwa ajili yako tunapata uhai na kwako ndiko kuna kukusanywa.

Ewe Mwenyezi Mungu haijapambazuka kwangu au kwa yeyote katika viumbe wako neema yoyote, isipokuwa inatoka kwako peke yako hauna mshirika, basi sifa njema na shukurani ni zako Na jioni atasema: Kila kilicho fikiwa na jioni kwangu.

Mara tatu

Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba afya duniani na akhera, Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba msamaha na afya katika dini yangu na dunia yangu na watu wangu na mali zangu, Ewe Mwenyezi Mungu sitiri aibu zangu na unipe amani kutokana na uoga wangu, Ewe Mwenyezi Mungu nihifadhi mimi mbele yangu na nyuma yangu na kuliani kwangu na kushotoni kwangu na juu yangu, na ninajikinga kwa utukufu wako nisishambuliwe chini yangu.

Ewe Mwenyezi Mungu wewe ndiye Mola Mlezi hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, umeniumba na mimi ni mja wako na mimi nipo juu ya ahadi yako na maonyo yako kwa kiasi niwezavyo, ninataka hifadhi kwako kutokana na shari niliyo ifanya, ninakiri kwa neema zako zilizo juu yangu, na ninakiri kwa madhambi yangu, basi nisamehe mimi, kwani hakuna afutae madhambi isipokuwa wewe.

Ewe Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi, mjuzi wa yaliyofichikana na yenye kuonekana, Mola Mlezi wa kila kitu na mmiliki wake, ninakubali ya kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, ninajikinga kwako kutokana na shari za nafsi yangu na kutokana na shari za shetani namitego yake, na ninajikinga kwako kuto fanya juu ya nafsi yangu ubaya au nikaupeleka kwa muislamu.

Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimepambazukiwa na asubuhi, ninakufanya Wewe kuwa shahidi na ninawashuhudisha Malaika wabebao Arshi yako na Malaika wako kwa ujumla na Manabii wako na viumbe wako wote kuwa wewe ni Allah, hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe na kuwa MuhammadI ni mja wako na Mtume wako. Na jioni Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi nimeingia jioni... Mpaka mwisho (mara nne)

Hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake asiye na mshirika, Mwenye ufalme na Mwenye sifa na yeye juu ya kila kitu ni Muweza. (mara mia moja) asubuhi na jioni.

Ananitosha Allah hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye na Yeye ni Mmiliki wa Arshi (kiti cha enzi) kitukufu. (mara saba).

Utakasifu ni wa Allah na Sifa njema ni zake (mara mia moja) Asubuhi na jioni. Au nyakati zote kwa pamoja.

Ninamtaka Mwenyezi Mungu msamaha na ninatubia kwake. (mara mia moja).

Haya ndiyo yaliyo wezekana kuyaandika, nina muomba Allah Mtukufu anufaishe kwayo umma.

Ameandika Muhammad Swalehe Al-Uthaymini Tarehe: 20-1-1418 H