الإمام محمد بن عبد الوهاب دعوته وسيرته
كتاب "الإمام محمد بن عبد الوهاب: دعوته وسيرته" للشيخ عبد العزيز بن باز يستعرض الكتاب حياة الشيخ محمد بن عبد الوهاب ودعوته الإصلاحية في القرن الثاني عشر الهجري.
Imamu Muhammad Bin Abdul Wahaab ulinganizi wake na Historia yake.
Utunzi wa Shekh Abdul Aziz Bin Abdillahi Bin Baaz
Sifa zote njema anastahiki ALLAH Mola wa viumbe wote, sala na salam na baraka ziwe juu ya mja wake na Mtume wake mbora wa viumbe bwana wetu na kiongozi wetu Muhammad bin Abdillahi, na watu wake na Swahaba zake na wenye kufuata nyayo zao.
Ama baada ya hayo: Enyi ndugu zangu watukufu, Enyi wanangu watukufu, muhadhara huu mfupi nauleta mbele yenu ili kuzinawirisha fikra, pamoja na kuweka wazi uhakika wa mambo, na kuwanasihi waja kwa ajili ya ALLAH, na kutekeleza baadhi ya mambo yanayo niwajibikia miongoni mwa haki, na muhadhara huu anuwani yake ni: Shekh Imamu Muhammad bin Abdul Wahaab, ulinganizi wake na historia yake.
Kwa sababu mazungumzo kuhusu watu wenye kufanya islahi (wenye kuweka mambo sawa katika jamii), na walinganizi wahuishaji wenye kujitahidi, na kukumbusha kuhusu hali zao, na mambo yao yenye kusifiwa, na matendo yao mazuri, na kufafanua historia yao inayo onyesha ikhlasi yao, na ukweli wao katika kulingania kwao, na kurekebisha kwao, kwasababu kuwazungumzia hao ambao ni watengenezaji (katika ardhi) wenye kuigwa kimandhari, tabia, matendo na mwenendo wao, ni katika mambo ambayo nafsi nzuri zina shauku kuyajua, na nyoyo zinastarehe kwayo, na atapenda kuyasikia kila mwenye ari juu ya dini, na kila mwenye pupa ya kuweka sawa mambo, na (kila mwenye kupenda) kulingania katika njia ya haki, (kwahiyo) nimependelea kuwaelezea kuhusiana na mtu mkubwa na mtengenezaji mkubwa na mlinganiaji mwenye ari, naye ni Sheikh Imamu Mhuishaji wa Uislamu katika bara la Arabuni katika karne ya kumi na mbili baada ya kuhama kwa Mtume Amani ya ALLAH iwe juu yake. Ambaye ni Imamu Muhammad bin Abdul Wahaaab bin Sulaiman bin Ally Attamimiy Alhambaliy.
Watu wamemfahamu Imamu huyu na hasa hasa wanazuoni wao na viongozi wao na wakubwa wao na wasaidizi wao katika bara la Arabuni na nje yake. Na watu wameandika kumhusu vitabu vingi vifupi na virefu. Na hakika watu wengi wamemuandika peke yake kwa maandishi, mpaka waandishi wajihusishao na masuala ya mashariki ya kati wamemuandika kwa maandishi mengi, Na wengine wamemuandika juu ya watu warekebishaji wa jamii, na katika kuandika kwao (waemuweka) katika historia. Wamemsifia waandishi kuwa yeye ni mrekebishaji (mtengenezaji) mkubwa, na kwamba yeye ni muhuishaji wa uislamu, na kwamba yupo katika muongozo na nuru kutoka kwa Mola wake na maelezo yao yamewatikisa wengi.
Miongoni mwa (walioandika juu ya Imamu huyu) ni muandishi mkubwa naye ni Abubakar Sheikh Hussein bin Ghannam Al Ihsaaiy. Amemuandika sheikh huyu, amemueleza vizuri na amefaidisha wengi na akataja historia yake, na ametaja vita alizopigana, na akaelezea kwa urefu kuhusu hayo, na akaandika risala zake nyingi pamoja na kutoa (ushahidi wa maeleo yake) katika kitabu cha Allah Mtukufu, na miongoni mwao pia ni Sheikh Uthman bin Bashar, katika kitabu chake Un'waanul Majid, naye vilevile ameandika kuhusu sheikh huyu, kuhusu kulingania kwake, na kuhusu historia yake, na ameandika juu ya historia ya maisha yake, na kuhusu vita alizopigana na jihad, na (Mashekh wengine waliomuandika) wanatoka nje ya bara la Arabuni, miongoni mwao ni Dr. Ahmad Amiin katika kitabu chake Zuamaaul Isw'laah, hakika amemuandika na akawa muadilifu. Na miongoni mwao ni Sheikh Mkubwa Masuud Annadawiy, amemuandika na kumuita mtengenezaji aliedhulumiwa na ameandika kuhusu historia yake na akaeleza vema katika hilo, Na wengine pia wameandika kuhusu yeye, miongoni mwao ni Sheikh mkubwa Amiir Muhammad bin Ismail Asswanaaniy, Kwani yeye alikuwa katika zama zake na alikuwa katika ulinganiaji wake, na mara baada ya kumfikia ulinganiaji wa Sheikh basi aliufurahia na akamhimidi Allah (akamshukuru) kwa hilo.
Na vile vile alimuandika mwanazuoni mkubwa Sheikh Muhammad bin Alliy Shaukaani mwenye kitabu kiitwacho "Naylul Awtwaar" na akamuelezea kwa sifa kubwa. Na wamemuandika watu wengi wasiokuwa hawa wanawajua wasomaji na wanazuoni na kwa sababu ya wingi wa watu huenda imefichika kwao hali ya imamu huyu na historia yake na ulinganiaji wake, kwahiyo nimeonelea nishiriki katika kuweka wazi hali ya mtu huyu, na aliyokuwa akiyafanya na historia yake nzuri, na ulinganiaji wake mwema, na jihadi ya kweli, na nitafafanua machache katika mambo ninayoyajua kumhusu Imamu huyu ili watu wajue kuhusu habari yake kwa mwenye kuwa na chochote katika lililofichika, au mwenye shaka katika hali ya Imamu huyu na ulinganiaji wake na aliyokuwa akiyafanya. Kuzaliwa kwake na kukua kwake Imamu huyu amezaliwa mwaka 1115h, mwaka huo ndio mashuhuri kuhusu kuzaliwa kwake Allah Amrehemu, na inasemekana amezaliwa mwaka 1111h, na unaojulikana sana ni kwamba yeye amezaliwa mwaka 1115h, baada ya kuhama Mtume rehma za ALLAH ziwe juu yake na ukamilifu wa maamkuzi.
Na kasoma kwa baba yake katika mji wa Uyaina, na mji huu ndio mahala alipozaliwa -ALLAH amrehemu- nacho ni kijiji maarufu kiko Yamama Najidi, Kaskazini magharibi mwa mji wa Riyadh, kati yake na mji wa Riyadh ni mwendo wa kilo mita sabini (70 km), alizaliwa hapo -ALLAH amrehemu-, na akakua makuzi mema, na alisoma Qur'ani mapema na akafanya juhudi katika masomo na akachukua elimu ya sheria kwa baba yake Sheikh Abdul Wahhab Suleiman na alikuwa mwanasheria mkubwa, na alikuwa mwanachuoni mwenye heshima, na alikuwa hakimu katika mahakama ya mji wa Uyaina. Kisha baada ya kufikia ujana alihiji na akaenda katika nyumba ya ALLAH tukufu, na akachukua elimu kutoka kwa baadhi ya wanachuoni wa Msikiti mtukufu. Kisha akaelekea katika mji wa Madina kwa mkazi wake ziwe juu yake sala na salamu bora, akaungana na wanachuoni wake, na akaishi huko muda mrefu, na akachukua elimu kutoka kwa wanachuoni wawili wakubwa na maarufu katika mji wa Madini kwa wakati huo. Nao ni Sheikh Abdallah bin Ibrahim bin Seif Al Najdi, asili yake anatokea Mji wa Majma'a, na ndiye mzazi wake na sheikh Ibrahim bin Abdallah Mtunzi wa kitabu cha (Al Adhbul faaidh fii ilmil Faraaidh), Na akachukua elimu pia kutoka kwa Sheikh mkubwa Muhammadi Hayat Al Sanadiy katika mji wa Madina. Hawa wanachuoni wawili ni katika mashekhe ambao wamekuwa maarufu sana kuwa sheikh alichukua elimu kutoka kwao katika mji wa Madina, na huenda alichukua pia kwa wanachuoni wengine zaidi ya hao katika wale tusiowafahamu.
Na Sheikh akaenda Iraq kwa ajili ya kutafuta elimu, alielekea Basra na akakaa na wanachuoni wake, na akachukua kutoka kwao kiasi alichotaka ALLAH akichukue katika elimu, na akatangaza kulingania katika Tauhidi akiwa huko, na akawaita watu katika sunna, na akawadhihirishia watu kuwa jambo la wajibu kwa waislamu wote nikuwa wanatakiwa kuchukua dini yao kutoka katika kitabu cha ALLAH, na mafundisho ya Mtume wa ALLAH-Sala na Amani ziwe juu yake-, na akafanya mijadala na akakumbusha katika hilo, na akafanya midahalo na wakazi wa huko miongoni mwa wanachuoni, akajulikana katika mashekhe wake shekhe mmoja aitwaye Sheikh Muhammadi Al Majmui, na walimchukia baadhi ya wanachuoni waovu wa mji wa Basra, na yakampata baadhi ya maudhi yeye na shekhe wake aliyetajwa, akatoka kwa sababu ya hilo, na ilikuwa nia yake aelekee Sham (Siria), akawa hakuweza kufanya hivyo kwa kutokuwa na matumizi ya kutosha, akatoka Basra akaenda Zubair, na akaelekea kutoka Zubairi mpaka Ahsaa, na akakaa na wanachuoni wa huko na akawakumbusha mambo mengi katika mambo ya msingi katika dini, Kisha akaelekea katika mji wa Harimla na hiyo ilikuwa (Allah ndiye mjuzi zaidi) katika miaka ya hamsini katika umri wake, karne ya kumi na mbili, kwa sababu baba yake alikuwa hakimu katika mji wa Uyaina na kukatokea sintofahamu kati yake na kiongozi wake mkuu, akahama akaelekea Harimla mwaka 1139 H, Sheikh Muhammadi akaelekea kwa baba yake katika mji wa Harimla baada ya baba yake kuhamia huko mwaka 1139 Hijiria, Hivyo inakuwa kufika kwake katika mji wa Harimla ni mwaka 1140 Hijiria au baada yake, na akabakia huko, na akawa bado anaendelea kujishughulisha na kusoma na kusomesha na kulingania watu katika mji wa Harimla mpaka alipofariki mzazi wake mwaka 1153 Hijiria, ikatokea shari kati yake na watu wa Harimla, na wakapania baadhi ya wajinga kumdhuru, na inasemekana kuna baadhi yao waliwahi kuruka ukuta wakamvamia, akapiga kelele kuwajulisha watu wakakimbia, na baada ya hapo sheikh aliondoka kuelekea Uyaina - ALLAH amrehemu.
Na sababu za kumchukia hao wajinga ni kwakuwa alikuwa akiamrisha mema na kukataza maovu, na alikuwa akiwahimiza viongozi kuwafedhehesha waovu, wanaofanya uadui kwa watu kwa wizi uporaji na maudhi mbali mbali, hawa wajinga ambao wanaitwa kwa jina la watumwa huko, na walipojua kuwa sheikh yuko dhidi yao, na kuwa yeye hafurahishwi na vitendo vyao, na kwamba yeye anawahimiza viongozi kuwaadhibu, na kuwasimamishia sheria kwa vitendo vyao, walimchukia na wakapanga kumvamia, Mwenyezi Mungu akamlinda na akamuhifadhi, kisha akahamia katika mji wa Uyaina na kiongozi mkuu wakati huo alikuwa ni Othman bin Nasiri bin Ma'mar, akaenda kwake na kiongozi akamkaribisha, na akasema: Simamia swala la kuwalingania watu kwa ALLAH, na sisi tuko pamoja nawe na tutakutetea, na akamuonyesha mambo mazuri, na mapenzi na kumuunga mkono juu ya hilo analolifanya.
Akajishughulisha sheikh na kufundisha na kuelekeza na kulingania watu katika njia ya ALLAH-Aliyetakasika na kutukuka-, na kuwaelekeza watu katika kheri, na kupendana kwa ajili ya ALLAH wanaume kwa wanawake, na kazi yake ikawa mashuhuri katika mji wa Uyaina, na nguvu yake ikawa kubwa, na watu wakaanza kuja kwake kutoka katika vijiji jirani, na siku katika masiku sheikh alimwambia kiongozi Othman: Tunaomba uturuhusu tubomoe kuba lililoko katika kaburi la Zaidi bin Khattwab -Radhi za ALLAH ziwe juu yake- kwani limewekwa kinyume na uongofu, nakuwa ALLAH Mtukufu haridhii jambo hili, na Mtume -Sala na Amani ziwe juu yake- amekataza kujenga juu ya makaburi, na kufanya misikiti juu yake, na kuba hili limewafitinisha watu na limebadilisha itikadi sahihi, na limesababisha kutokea kwa shirki hivyo ni lazima kulibomoa, kiongozi akasema: Hakuna tatizo katika hilo, Sheikh akasema: Mimi nahofia huenda wakakasirika watu wa Jubaila, na Jubaila ni kijiji kiko huko karibu na kaburi, akatoka Othman akiwa na jeshi linalofikia wapiganaji mia sita (600) kwa ajili ya kubomoa kuba. Na akiwa pamoja nao Sheikh-ALLAH-amrehemu- walipolikaribia kuba walitoka watu wa Jubaila waliposikia hilo kwa ajili ya kulinusuru na kulihami. Walipomuona kiongozi Othman na pamoja na wale waliopamoja naye wakasitisha kwenda na wakarudi. Sheikh akashiriki kulibomoa na kuliondoa, ALLAH Mtukufu akaliondoa kupitia mikono yake ALLAH amrehemu. Hebu tutaje dondoo za hali ya Najidi kabla ya sheikh kuisimamia -ALLAH amrehemu-, na sababu za kuisimamia, na ulinganizi wake.
Walikuwa watu wa Najidi kabla ya da'wa ya sheikh katika hali ambayo hakuna muumini anairidhia, shirki kubwa Ilikuwa kubwa na imeenea, mpaka wakaanza kuabudu makuba (vijumba vinavyojengwa juu ya makaburi) na wakaabudu miti, na mawe, na wakaabudu Ghayaran (mti unaofanana na zaituni) Na wakaabudu waliodai kuwa ni mawalii, hali yakuwa ni katika wapungufu wa akili, na wakaabudu kinyume na ALLAH watu waliodai kuwa watukufu, hali yakuwa ni wendawazimu waliorukwa na akili, na wakawa mashuhuri wachawi na makuhani katika mji wa Najidi, Na kuulizwa kwao mambo ya ghaibu na kuaminika kwao, na hakuna mtu wa kukemea isipokuwa yule aliyemtaka ALLAH, na watu wakaelemewa na kuipupia dunia na matamanio yake, na wakawa wachache wenye kusimama kwa ajili ya ALLAH na kunusuru dini ya ALLAH, Na hali ni hiyo hiyo katika misikiti miwili mitukufu, na Yemen pia ulienea ushirikina, na kujenga makuba juu ya makaburi, na kuwaomba mawalii na kutaka msaada kwao, na Yemen wakati huo kulikuwa na mambo mengi, na katika miji ya Najidi wakati huo kulikuwa na mambo mfano wa hayo yasiyokuwa na idadi, kati ya kaburi au pango, na mti na baina ya mwenye kuombwa, na mwenda wazimu mwenye kuombwa kinyume na ALLAH na akiombwa msaada pamoja na ALLAH , na miongoni mwa mambo yaliyojulikana Najidi na yakawa mashuhuri ni kuwaomba majini na kutaka msaada kwao, na kuwachinjia vichinjwa, na kuviweka katika kona za nyumba kwa kutaraji mazuri yao, na kuogopa shari zao. Alipoona sheikh na Imamu ushirikina huu na kudhihiri kwake kwa watu, na kutopatikana mkemeaji wa hayo, na mwenye kusimamia kuwalingania watu kwa ALLAH katika hayo, alikunja goti la juhudi (aliongeza juhudi), na akasubiri juu ya kufikisha ujumbe, na akajua kuwa ni lazima afanye mapambano, na subira na kuvumilia maudhi, akaongeza juhudi katika kufundisha na kuelekeza na kutoa muongozo akiwa katika mji wa Uyaina, na huku akiwaandikia barua mbali mbali viongozi juu ya hilo, na kujadiliana nao akitarajia wanaweza kusimama pamoja naye katika kuinusuru dini ya ALLAH, na kupambana na ushirikina huu na mambo haya ya hovyo, wakaipokea da'wa yake wengi katika wanachuoni wa Najidi na wanachuoni wa misikiti miwili mitukufu, na wanachuoni wa Yemen, na wengineo, na wakamuandikia barua za kukubali, na wengine wakapinga na wakakosoa anayoyalingania na wakamtukana, na wakaachana naye nao wakiwa kati ya mambo mawili, ima mtu ni mjinga ni mtu anayefuata mambo ya hovyo haijui dini ya ALLAH na wala haijui Tauhidi ya ALLAH, bali anajua waliyokuwa nayo baba zake na babu zake katika ujinga na upotovu na ushirikina, na uzushi, na mambo ya hovyo, kama alivyosema ALLAH aliyetakasika na kutukuka kuhusu mfano wa watu kama hao: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wakiwa kwenye tamaduni na hakika sisi juu ya athari zao ni wenye kufuata. [Azzukhruf: 23], Na kundi jingine miongoni mwa watu wanaojinasibisha na elimu walimshambulia kwa ukorofi na husuda, ili watu wa kawaida wasijekusema: Mna nini mbona nyinyi hamkutukemea jambo hili? Kwanini amekuja huyu bin Abdil wahhab na akawa yuko katika haki, hali yakuwa na nyinyi ni wanachuoni na hamkukemea batili hii?. Wakamuhusudu na wakawafanya watu wa kawaida wamuogope, na wakadhihirisha wazi ukaidi wa kupinga haki, na wakathamini masilahi ya dunia kuliko ya akhera, na wakawaiga mayahudi kwa kuithamini dunia zaidi kuliko akhera, Tunamuomba Allah atupe afya na salama.
Ama Sheikh alivuta subra na akafanya juhudi kubwa katika kufikisha ujumbe, na akahamasishwa na miongoni mwa watu waliomuhamasisha katika wanachuoni na watu wengine ndani ya kisiwa, na nje yake, akadhamiria juu ya hilo na akataka msaada kwa Mola wake Aliyetakasika na kutukuka, na akakaa kabla ya hapo katika kitabu cha ALLAH, na alikuwa na mkono mrefu katika kutafsiri kitabu cha ALLAH(Alikuwa mahiri), na kuchambua hukumu kutoka katika kitabu cha Allah, na akasimama katika historia ya Mtume -Sala na Amani ziwe juu yake- na maswahaba zake, na akafanya juhudi kubwa katika hilo na akaelimika ipasavyo, mpaka akapata katika hilo yale yanayoweza kumsaidia na kumuimarisha katika haki, akakaza mkono wa juhudi, na akadhamiria kufikisha ujumbe na kueneza elimu kwa watu, na alikuwa akiwaandikia ujumbe viongozi pamoja na wanachuoni katika hilo, na hakujali, lolote litakalokuwa na liwe!
ALLAH akamtimizia malengo mazuri, na akaeneza ujumbe kupitia yeye, na akampa nguvu ya kuwa katika haki, na ALLAH akamuandalia watu wa kumtetea na wa kumsaidia na wa kumuunga mkono pia, mpaka ikadhihiri dini ya ALLAH , na neno la ALLAH(Laa ilaaha illa llaahu -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa ALLAH) likawa juu, sheikh akaendelea kufikisha ujumbe katika mji wa Uyaina kwa kufundisha na kuelekeza, kisha akaongeza nguvu ya kutekeleza na kuondoa athari za ushirikina kwa vitendo, alipoona da'wa haijazaa matunda, alianza kufanya da'wa kwa vitendo kuyaondoa kwa mkono wake yale yaliyowezekana, na yale yaliyoyamkinika katika athari za ushirikina, alisema sheikh kumwambia kiongozi Othman bin Ma'mar: Ni lazima kubomoa kuba hili ambalo liko juu ya kaburi la Zaidi. Na huyu Zaidi bin Khattwab -Radhi za ALLAH ziwe juu yake- ndiye ndugu yake na Omari bin khattwab kiongozi wa waumini -Radhi za ALLAH ziwe juu yao wote. Na alikuwa ni miongoni mwa mashahidi waliokufa katika vita vya kupambana na muongo Musaila mwaka wa 12 Hijiria, akawa ni miongoni mwa waliouawa huko, na likajengwa kuba juu ya kaburi lake kwa namna inavyoelezwa, na linawezekana likawa ni kaburi la mtu mwingine, lakini kwa jinsi wanavyoeleza ni kuwa hilo ni kaburi lake, Othman akaafiki hilo kama tulivyoeleza awali, na Alhamdulillah kuba likabomolewa, na ikatoweka athari yake mpaka leo, neema na kila sifa njema zinamstahiki ALLAH, alilifisha ALLAH Mtukufu lilipobomolewa kwa nia njema, na kusudio lililonyooka na kwa ajili ya kuitetea haki, lakini pia kuna makaburi mengine, miongoni mwake kuna kaburi linalosemekana kuwa ni kaburi la Dhurar bin Auzi, juu yake lilikuwa na kuba likabomolewa pia, lakini pia kuna sehemu zingine ALLAH Mtukufu aliziondoa, na kulikuwa na Ghayarani (mti unaofana na mti wa zaituni) na miti mingine iliyokuwa ikiabudiwa kinyume na ALLAH Aliyetakasika na kutukuka, ikaondolewa na ikateketezwa na watu wakatahadharishwa juu ya hilo.
Na makusudio yake nikuwa Sheikh -ALLAH amrehemu- aliendelea na kufikisha ujumbe, kwa kauli na vitendo kama ilivyotangulia, kisha sheikh alijiwa na mwanamke, na akakiri kuwa kafanya zinaa zaidi ya mara moja, akaulizi kuhusu akili yake akaambiwa kuwa akili yake iko sawa wala hakuna tatizo, alipozidi kukiri, na wala hakurudi nyuma katika kukiri kwake, na wala hakudai kuwa kulazimishwa wala utata katika hilo, na alikuwa kaolewa, sheikh ALLAH amrehemu aliamrisha apigwe mawe, akapigwa mawe yule mama kwa amri yake, wakati akiwa ni hakimu wa mji wa Uyaina, baada ya hapo swala lake likawa maarufu kwa kubomoa kuba, na kupigwa mawe yule mama, na kwa da'wa tukufu ya kulingania watu kwa ALLAH, na watu kuanza kuhamia katika mji wa Uyaina.
Na zikamfikia taarifa kiongozi wa mji wa Ahsaa na pembezoni yake katika bani Khalidi Suleiman bin Ariri Al Khalidi kuhusu jambo la sheikh,na kwamba yeye analingania katika njia ya ALLAH, nakuwa yeye anabomoa makuba (vijumba vinavyojengwa juu ya makaburi) nakuwa yeye anasimamisha sheria, hili jambo likakuzwa kwa huyu bwana wa kijijini, kwa sababu katika tamaduni za watu wa vijijini -Ila wachache walioongozwa na Allah- ni kujitosa katika dhulma, na kumwaga damu, na kupora mali, na kuvunja sheria, akahofia kuwa huyu sheikh huenda msimamo wake ukapata nguvu, na ukaondoa utawala wa kiongozi huyu wa kijijini, akaandika barua ya vitisho kwenda kwa Othman akimuamrisha amuuwe huyu mtu anayejitolea katika mji wake wa Uyaina, na akasema: Hakika huyo bwana anayejitolea huko kwenu zimetufikia taarifa zake kuwa ni kadhaa wa kadhaa!! Ima umuue, au ima tukate kodi yako ambayo iko kwetu!! Na kiongozi Othman alikuwa na kodi ya dhahabu kwao, likamshughulisha Othman swala la kiongozi huyu, na akahofia akipingana naye atamkatia kodi yake, au atampiga vita, Sheikh akasema: Hakika kiongozi katuandikia ujumbe kadha wa kadhaa, na hakika sisi haitupendezi kukua, na sisi tunamuogopa kiongozi huyu na wala hatuwezi kupigana naye vita, kama utaona inafaa basi ni bora kutoka hapa itakuwa vizuri, sheikh akasema: Hakika ninachokilingania ni dini ya ALLAH, na kulithibitisha neno la Laa ilaaha illa llaahu -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa ALLAH- na kuthibitisha kushuhudia kuwa Muhammadi ni Mjumbe wa ALLAH, atakayeshikamana na dini hii na akawa mkweli katika hilo basi ALLAH atamnusuru na atampa nguvu na atampa utawa juu ya miji ya maadui zake, ikiwa utasubiri na ukawa na msimamo, na ukaikubali kheri hii basi kuwa na matumaini,ALLAH atakunusuru na atakulinda dhini ya mtu huyu wa shamba na wengineo, na ALLAH atakutawalisha mji wake na watu wake. Akasema: Sheikh sikiliza, sisi hatuwezi kupigana naye, na wala hatuwezi kuvumilia kumpinga. Basi wakati huo Sheikh akatoka na akahama kutoka Uyaina akaelekea miji ya Dariya, alikwenda kwa kutembea kwa miguu inavyosemekana, mpaka akaingia nyakati za mwisho wa mchana (jioni), na alitoka Uyaina asubuhi akitembea kwa miguu, othman hakumsindikiza, akaingia kwa mtu mmoja katika waheshimiwa wa hapo maeneo ya juu ya mji, bwana huyo akiitwa Muhammadi bin Suwailim Al Arini, akafikia kwake, na inasemekana huyu bwana aliogopa sheikh kufikia nyumbani kwake, na akawa katika wasi wasi mkubwa, na akamhofia kiongozi wa Daria Muhammadi bin Saud, sheikh akamtoa hofu akamwambia: kuwa na matarajio mazuri, hiki ninachowaitia watu kwake ni dini ya ALLAH, na ALLAH ataidhihirisha. Taarifa zikamfikia Muhammadi bin Saudi za sheikh Muhammadi, na inasemekana alielezwa na mke wake, walikwenda kwake baadhi ya watu wema na wakamwambia mama huyo: Mpe taarifa Muhammadi kuhusu ujio wa bwana huyu, na umuhamasishe juu ya kukubali ujumbe wake, na umtie hamasa ya kumtetea na kumsaidia, na huyu mwanamke alikuwa ni mwanamke mwema na mzuri wa tabia, alipoingia kwake Muhammadi bin Saudi kiongozi wa Dar'ia na kanda zake, huyu mama akasema kumwambia: Nakupa habari njema ya bahati nzuri kubwa! Hii ni bahati kubwa kaileta ALLAH kwako, mtu mmoja mfikishaji wa ujumbe anayewaita watu katika dini ya ALLAH, analingania katika kitabu cha ALLAH, analingania katika mafundisho ya Mtume -Sala na Amani ziwe juu yake- ni bahati kubwa ilioje hii!. Fanya haraka sana kumkubali na fanya haraka sana kumtetea, na katu usisite katika hilo, kiongozi akakubali ushauri wake, kisha akapata shaka, je amfuate au amuite aje kwake?! Akashauriwa, na inasemekana pia mwanamke ndiye aliyemshauri pamoja na watu wengine katika wema, wakamwambia: Haitakiwi umuite kwako, bali inatakiwa umfuate kwake na umfuate wewe mwenyewe, na uiheshimu elimu na mwalimu wake pia anayefundisha watu katika kheri, akalikubali hilo pale ambapo ALLAH alipomuandikia kupata furaha na kheri -ALLAH amrehemu-, na akamkirimu mgeni wake, akaenda kwa sheikh akiwa katika nyumba ya Muhammadi bi Suwailim akamfuata akamsalimia na akazungumza naye, na akasema kumwambia: Ewe Sheikh Muhammadi, nakupa habari njema ya kupata utetezi na amani na msaada, sheikh akasema kumwambia: Nawe pia kuwa na habari njema ya kupata nguvu na mwisho mwema, hii ni dini ya ALLAH atakayeinusuru ALLAH atamnusuru, na atakayeitetea ALLAH atamtetea, na utapata matokeo ya hilo haraka, Akasema: Ewe sheikh nitakuunga mkono katika dini ya ALLAH na Mtume wake, na kupigana katika njia ya ALLAH, lakini mimi nahofia ikiwa tutakuunga mkono na kukutetea na ALLAH akakupa ushindi dhidi ya maadui wa uislamu huenda ukatafuta mahala pengine pasipokuwa hapa, na ukatuhama ukaenda katika ardhi nyingine, Akasema: Hapana; Nakupa ahadi juu ya hili, nakupa ahadi kuwa damu yangu ni damu yako, na kuumia kwako ni kuumia kwangu, sitotoka milele katika mji wako, akampa ahadi ya kumtetea, na kubakia katika mji, nakwamba atabakia kwa kiongozi akimsaidia, na akipambana pamoja naye katika njia ya ALLAH, mpaka dini ya ALLAH idhihiri, Na makubaliano yakakamilika juu ya hilo. Na watu wakaanza kufunga safari kwenda katika mji wa Dar'ia kila kona, kutoka Uyaina, Araqa, na Manfuuha, na Riyadh na miji mingineyo iliyoko jirani, ikawa bado Dar'ia inaendelea kuwa ni mji wa watu kuhamia huko kutoka kila mahali, na watu wakawa wanaelezana kuhusu habari za sheikh, na masomo yake katika mji wa Dar'ia, na da'wa yake kwa ALLAH na kuelekeza kwake, wakaanza kuja makundi kwa makundi na mtu mmoja mmoja, sheikh akaishi katika mji wa Dar'ia akiwa ni muheshimiwa mwenye kuungwa mkono mwenye kupendeka na kutetewa, na akapangilia masomo ya itikadi (Aqida) katika mji wa Dar'ia, na katika Qur'ani tukufu, na katika tafsiri,na fiq-hi (kuitambua sheria), na hadithi na Mustwalaha zake (kanuni zake) na fani za lugha ya kiarabu, na historia, na masomo mengineyo katika elimu zenye manufaa.
Na watu wakakusanyika kwake kutoka kila mahali, na vijana na wengineo wakajifunza kutoka kwake akiwa Dar'ia, na akawapangia watu masomo mengi, kwa ajili ya watu wote na watu maalumu, na akaeneza elimu katika mji wa Dar'ia, akaendelea katika kufikisha ujumbe kisha akaanza kupambana, na akawaandikia ujumbe watu wa kuingia katika viwanja hivi, na kuondoa ushirikina ulioko katika miji yao, na akaanza na watu wa Najidi, na akawaandikia barua viongozi wake na wanachuoni wake, na akawaandikia wanachuoni wa mji wa Riyadh na wanachuoni wa miji ya kusini na mji wa Kasiim, Haili, na Washim, na Sadiri, na miji mingineyo. Na akaendelea kuwatumia ujumbe wao na wanachuoni wao, na hivyo hivyo wanachuoni wa Ahsaa na wanachuoni wa Misikiti miwili mitukufu (Makka na Madina), na pia wanachuoni wa nje katika nchi ya Misri, na Sham na Iraq, na India, na Yemen, na miji mingineyo, akawa bado anaendelea kuwaandikia ujumbe watu na akisimamisha hoja, na akiwakumbusha watu yale ambayo viumbe wengi waliyaangukia miongoni mwa ushirikina na uzushi, na hii haimaanishi kuwa huko katika miji mingine hapakuwa na watu wa kuitetea dini, bali walikuwepo watetezi, na ALLAH aliyetakasika na kutukuka alichukua dhamana kuwa ni lazima kuwe na watetezi wa dini hii, na bado halitoacha kuendelea kuwepo katika haki kundi katika umma huu lenye kunusuriwa, kama alivyosema -Sala na Amani ziwe juu yake-, kuna watetezi wa haki katika nchi nyingi, lakini mazungumzo yetu kwa wakati huu tunazungumzia Najidi, kulikuwa na shari na uharibifu na ushirikina na mambo ya hovyo ambayo hakuna ayajuaye idadi yake isipokuwa Allah aliyetakasika na kutukuka, pamoja nakuwa kulikuwa na wanachuoni ambao ni watu wa kheri, lakini hawakuweza kupata nguvu ya kulingania na kusimama kama ipasavyo.
Na pia huko Yemen na kwingineko kuna walinganiaji wa haki, na watetezi waliokuwa wanaujua ushirikina huu na mambo haya ya hovyo, lakini ALLAH hakukadiria da'wa yao kuwa na mafanikio kwa kiwango alichomkadiria sheikh Muhammadi kwa sababu nyingi, miongoni mwazo: kutopata wepesi wa kupata wasaidizi, na miongoni mwake pia: Walinganiaji wengi kukosa subira, na kuvumilia maudhi katika njia ya ALLAH.
Na miongoni mwake: Ni uchache wa elimu ya baadhi ya walinganiaji ambayo wanaweza kuitumia kupambana na watu kwa njia inayotakiwa, na ibara zinazofaa, na hekima na mawaidha mazuri. Na miongoni mwake: Ni sababu zingine zisizokuwa hizi, na kwa sababu hii ndio maana aliandika barua nyingi na akapambana, swala la sheikh lilipata umaarufu, na ujumbe pia ukadhihiri, na ujumbe wake ukaungana pamoja na wanachuoni walioko ndani ya kisiwa na nje yake, na wakaathirika na ujumbe wake kundi kubwa la watu, India na Indonesia na Afghanistani na Afrika na Moroco na Misri, na Sham (syria, Jordan, Palestina) na Iraq, lakini pia kulikuwa na walinganiaji wengi, waliokuwa na elimu ya kuitambua haki na kuilingania pindi ilipowafikia da'wa ya sheikh basi ikawaongezea uchangamfu na ikawaongezea nguvu, na wakawa maarufu kwa kufikisha ujumbe, na ikaendelea kuenea da'wa ya sheikh na kudhihiri katika ulimwengu wa kiislamu na kwingineko, Kisha katika zama hizi za mwisho vikachapishwa vitabu vyake, na jumbe zake, na vitabu vya watoto wake na wajukuu zake, na watetezi wake, na wasaidizi wake miongoni mwa wanachuoni wa waislamu katika kisiwa na nje yake, na pia vilichapishwa vitabu vilivyokuwa vikielezea da'wa yake, na historia yake, na hali za watetezi wake, mpaka akawa maarufu kwa watu katika miji na nchi nyingi, na inavyofahamika kuwa kila neema haikosi hasidi, na kuwa kila mlinganiaji ana maadui wengi, kama alivyosema ALLAH Mtukufu: Na hivyo tumejalia kwa kila nabii kuwa na maadui wenye sifa ya ushetani miongoni mwa watu na majini wakishushiana ufunuo wao kwa wao uwongo wa maneno hali ya kuwa ni udanganyifu na kama angetaka MOLA wako wasinge fanya hilo basi chukua tahadhari nao na yale wanayo yazusha. [Al An'am: 112], Alipopata umaarufu sheikh kwa kulingania, na akaandika jumbe nyingi, na akatunga vitabu mathubuti, na akavisambaza kwa watu, na wanachuoni wakamuandikia ujumbe pia, walijitokeza kundi kubwa la mahasidi wake na wenye kumpinga, na wakadhihiri pia maadui wengine.
Na maadui zake na wagomvi wake wakwa katika makundi mawili: Kuna kundi lilimfanyia uadui kwa kupitia jina la elimu na dini, na kundi jingine: Lilimfanyia uadui kwa jina la siasa japo walijificha kwenye kivuli cha elimu, na wakajificha katika jina la dini, na wakatumia fursa ya uadui wa wale waliompiga vita miongoni mwa wasomi, wale waliodhihirisha uadui wao na wakasema kuwa hayuko katika haki, na wakasema kuwa yuko hivi na vile, na sheikh ALLAH amrehemu akiendelea kufundisha na kuondoa utata, na akiweka wazi ushahidi, na akiwaelekeza watu katika uhalisia wa yale yalioko katika kitabu cha ALLAH na mafundisho ya Mtume -Sala na Amani ziwe juu yake- Na mara nyingine wanasema: Huyu ni katika makhawariji (Siasa kali), na wakati mwingine wanasema: Anaharibu makubaliano ya wanachuoni na anadi kuwa anafanya jitihada za moja kwa moja, na wala hajali waliokuwa kabla yake katika wanachuoni na wasomi wa sheria, na wakati mwingine wanamsingizia vitu vingine, na haya ni kwa sababu ya uchache wa elimu kwa kundi kubwa miongoni mwao. Na kundi jingine likawaiga kundi jingine, na likawategemea, na kundi jingine likaogopa kupoteza nafasi yake likamfanyia uadui upande wa siasa, na likajificha chini ya kivuli ya uislamu na dini, na likategemea zaidi kauli za waliopinda na waliopotea.
Na wagomvi kuihalisia walikuwa sehemu tatu: Wanachuoni wa hovyo wanaoiona haki ni batili na batili ni haki, na wanaamini kuwa kujenga juu ya makaburi, na kufanya misikiti juu yake, na kuyaomba kinyume na ALLAH na kuyataka msaada na mfano wa hayo hiyo ndiyo dini na ndiyo uongofu, na wanaamini kuwa mwenye kupinga hilo atakuwa kawachukia watu wema, na kawachukia mawalii, na mtu huyu ni adui ni lazima kupigana naye jihadi.
Na sehemu nyingine: Ni katika wale wanaonasibishwa kuwa wamesoma, hawakujua uhalisia wa huyu mtu, na wala hawakuijua haki anayoilingania, bali waliwaiga wengine, na wakayaamini yaliyosemwa kumuhusu yeye na watu wa hovyo na waliopotea, na wakadhani kuwa wao wako katika uongofu katika yale waliomnasibishia kama kuwachukia mawali na Manabii, na miongoni mwa kawaida yake ni kupinga karama zao. Wakamtukana sheikh, na wakaitia doa da'wa yake na wakamchukia.
Na sehemu nyingine: Walihofia vyeo vyao na daraja zao, wakamfanyia uadui ili wanaoiunga mkono da'wa ya kiislamu isijekupata nguvu, ikawaondoa katika ngazi zao, na ikateka miji yao, na vikaendelea vita baridi (vya maneno) na mijadala na kujiona na kujifaharisha kati ya sheikh na wagomvi wake, wakijibizana, wanamtumia ujumbe naye anawatumia ujumbe, na wanamjadili na anawajibu na wao wanamjibu, na hivyo ndivyo ilivyoendelea hata kati ya watoto wake na wajukuu zake, na watetezi wake, na kati ya wagomvi wa da'wa yake, mpaka zikakusanywa kwa sababu ya hilo risala nyingi, na majibu mengi pia. Na zimekusanywa risala hizi na majibu na fatwa na majibu haya zikafikia vitabu vingi, na vingi vimekwisha chapishwa Alhamdulillah, na akaendelea sheikh katika da'wa na kupambana, na akasaidiwa na kiongozi Muhammadi bin Saudi kiongozi wa mji wa Dar'ia, na familia ya Saudia ikafanya juhudi kubwa juu ya hilo; na ikanyanyua bendera ya jihadi, na jihadi ikaanza mnamo mwaka: 1158H sawa na mwaka: 1737G, vikaanza vita kwa upanga na kwa maneno, na kwa hoja na ushahidi, kisha da'wa na jihadi kwa upanga vikaendelea, na inafahamika kuwa mwenye kulingania katika njia ya ALLAH anapokuwa hana nguvu ya kuitetea haki na kuiweka wazi basi ni haraka sana da'wa yake hufifia na huzimika umaarufu wake, kisha wanapungua watetezi wake, na inafahamika kuwa silaha hazina athari yoyote kubwa katika kueneza ujumbe, na kuwazimisha wapinzani, na kuitetea haki na kuzimisha batili, na bila shaka amesema kweli ALLAH Mtukufu katika kauli yake, naye ni mkweli aliyetakasika katika yote anayoyasema: Hakika tumetuma mitume wetu kwa uwazi na tumeteremsha pamoja nao kitabu na mizani ili wasimame watu kwa uwadilifu na tukateremsha chuma ndani yake kuna silaha na manufaa kwa watu na ili apate kujua ALLAH na atakye mnusuru yeye na mtume wake bila kumuona hakika ALLAH ni mwenye nguvu mtukufu. [Al Hadidi: 25] Akabainisha aliyetakasika na kutukuka yakuwa yeye alituma Mitume kwa uongofu, nao ni hoja na ushahidi wenye kung'aa, ambao ALLAH anautumia kuibainisha haki, na kuizuia batili, na akateremsha vitabu pamoja na Mtume ambavyo ndani yake kuna ubainifu, na uongofu na uwazi, na akateremsha mizani pamoja nao, nao ni uadilifu ambao wanautumia kutenda haki kati ya mdhulumu na mdhulumiwa, na isimamishwe haki kwa misingi hiyo pamoja na uongofu, na watu waamiliane kwa haki na uadilifu, na akateremsha chuma chenye nguvu kubwa, na akakemea na akakaripia kwa mwenye kwenda kinyume na haki, chuma kitamfaa ambaye hoja hazitosaidia kitu kwake, na mazingira yakawa hayajamuathiri, basi hicho ndicho kitakachokata mzizi wa ujeuri.
Na alisema vizuri aliyesema maneno katika mazingira mfano wa haya:
Na hakuna kingine isipokuwa ni wahyi au makali yaliyonolewa* Yanayoondoa ukungu wake na kunyoosha kila kilichopinda.
Hii ndiyo dawa ya ugonjwa kwa kila mjinga * Na hii ndiyo dawa ya kila ugonjwa kwa kila muadilifu.
Mwenye akili ni yule mwenye uelewa salama, mwenye kunufaika na ubainifu, na akaikubali haki kwa dalili zake, na ama dhalimu mwenye kufuata matamanio yake huyu hakuna kinachoweza kumkemea zaidi ya panga, hivyo akafanya juhudi sheikh katika da'wa na Jihadi, na wakamsaidia watetezi wake katika familia ya Saudi ALLAH azing'arisha athari zao katika hilo, na wakaendelea katika jihadi na da'wa tangu mwaka: 1158H mpaka alipofariki sheikh mwaka 1206H Jihadi na da'wa ikaendelea takribani miaka hamsini (50), ni Jihadi, da'wa, na kujihami, na mijadala katika haki, na kuyaweka wazi yale aliyoyasema ALLAH na Mtume wake, na kulingania katika dini ya ALLAH, na kuelekeza katika sheria za Mtume wa ALLAH-Sala na Amani ziwe juu yake- mpaka watu wakashikamana na utiifu, na wakaingia katika dini ya ALLAH, na wakayabomoa makuba waliyokuwa nayo, na wakayaondoa yote waliyokuwanayo miongoni mwa misikiti iliyojengwa juu ya makaburi, na wakahukumu kwa sheria za ALLAH, na wakazitumia katika maisha yao, na wakaachana na yale waliyokuwa nayo miongoni mwa kuhukumu kupitia yaliyopita kutoka kwa baba zao na babu zao, na kanuni zao, na wakarudi katika haki, na misikiti ikaimarishwa kwa ibada za swala, na vikao vya kielimu na zaka ikatekelezwa, na watu wakafunga ramadhani kama alivyoelekeza ALLAH aliyetakasika na kutukuka, na watu wakaamrisha mema na wakakataza mabaya, na amani ikatawala katika miji na vijiji na njia na mabonde, na vijiji vikakaa katika mipaka yake, na wakaingia katika dini ya ALLAH na wakaikubali haki, na sheikh akaieneza kwao da'wa, na sheikh akawatumia walimu, na walinganiaji kwenda majangwani na mabondeni, kama alivyotuma waelekezaji pia, na mahakimu katika miji na vijiji, na kheri hii kubwa ikaenea, na uongofu wa wazi katika Najidi yote, na haki ikaenea, na ikadhihiri ndani yake dini ya ALLAH aliyetakasika na kutukuka.
Kisha baada ya kufariki sheikh -ALLAH amrehemu- wakaendelea watoto wake na wajukuu zake, na wanafunzi wake, na watetezi wake katika da'wa na jihadi, na wakiongozwa na watoto wa sheikh, Imamu Abdallah bin Muhammadi, na sheikh Husein bin Muhammadi, na sheikh Ally bin Muhammadi, na sheikh Ibrahim bin Muhammadi, na miongoni mwa wajukuu zake, ni sheikh Abdul rahman bin Husein, na sheikh Ally bin Husein na sheikh Suleiman bin Abdallah bin Muhammadi, na kundi la watu wengine, Na miongoni mwa wanafunzi wake pia ni sheikh Hamdi bin Nassor bin Ma'mar, na kundi kubwa la wanachuoni wa Dar'ia, na wengineo waliendelea katika da'wa na jihadi na wakaieneza dini ya ALLAH Mtukufu, na kuandika risala na kutunga vitabu mbali mbali, na kuwapiga vita maadui wa dini, na hapakuwa na lolote kati ya hawa walinganiaji na mahasimu wao isipokuwa nikuwa hawa walilingania katika kumpwekesha ALLAH na kuzitakasa ibada kwa ajili ya ALLAH aliyetakasika na kutukuka, na kuwa na msimamo katika hilo, na kubomoa misikiti na makuba yaliyojengwa juu ya makaburi, na wakalingania juu ya kuhukumu kwa sheria za ALLAH na kuwa na msimamo juu yake, na wakalingania juu ya kuamrisha mema na kukataza maovu, na kutekeleza adhabu ya mipaka ya kisheria, hii ndiyo ikawa sababu ya ugomvi kati yao na watu wengine. Na muhutasari: Nikuwa wao walielekeza katika tauhidi -kumpwekesha ALLAH-, na wakawaamrisha katika hilo, na wakawatahadharisha watu kutokana na kumshirikisha ALLAH na kitu kingine, na njia zake na mianya yake, na wakawalazimisha watu kufuata sheria ya kiislamu, na anayekataa na akaendelea na ushirikina baada ya kufikiwa na ujumbe na ubainifu, na uwazi na hoja, walimpiga vita kwa ajili ya ALLAH Mtukufu, na walimfuata mpaka katika mji wake mpaka anyenyekee aikubali haki, na atubie, au walikuwa wakimlazimisha kwa nguvu na upanga mpaka asalimu amri yeye na watu wa mji wake katika hilo, na vile vile waliwatahadharisha watu kutokana na uzushi na mambo ya hovyo, ambayoALLAH hakuyateremshia maelekezo, kama kujenga juu ya makaburi na kuweka makuba juu yake, na kuhukumiana kwa sheria zisizokuwa za ALLAH, na kuwauliza wachawi na makuhani, na kuwasadikisha kwao na mengineyo, yote hayo ALLAH akayaondoa kupitia mkono wa Sheikh na watetezi wake Sala za ALLAH ziwe juu yao wote.
Na misikiti ikaimarishwa kwa masomo ya kitabu kitukufu na sunna safi, na vitabu mbali mbali vya kiislamu, na elimu za kiarabu zenye manufaa, na watu wakawa wakisomeshana, sayansi, na uongofu, na da'wa, na kuelekeza, na wengine wakashughulika na maswala yanayohusu dunia yao kama kilimo, na ufundi na mengineyo, elimu, na kazi, na da'wa, na kuelekeza, na dunia na dini, mtu akawa anajifunza na anarejea alichojifunza, lakini pamoja na hivyo bado anafanya kazi katika shamba lake la kilimo, au katika ufundi wake, au biashara na kazi zinginezo, wakati mwingine anakuwa katika maswala ya dini yake na wakati mwingine anakuwa katika dunia yake, na walinganiaji katika njia ya Mwenyezi Mungu na waelekezaji katika njia hiyo, lakini pamoja na hivyo wanajishughulisha na shughuli za kiuchumi katika miji yao, na wanachuma kwa shughuli hizo kipato kinachowawezesha kutohitaji kutoka katika miji mingine. Baada ya kumaliza shughuli ya da'wa waliganiaji pamoja na familia ya Saudi katika mji wa Najidi, basi da'wa yao ilienea katika miji miwili mitukufu (Makka na Madina), na kusini mwa kisiwa, na wakawaandikia ujumbe wanachuoni wa Misikit miwili wa zamani na wa baadaye, walipoona ujumbe haujazaa matunda na wakaendelea watu wa haramaini na yale waliyonayo miongoni mwa kuyatukuza makuba, na kuyajenga juu ya makaburi, na kupatikana kwa ushirikina hapo, na kuiomba miungu, alielekea Imamu Muhammadi bin Saudi bin Abdil Azizi kwa miaka kumi na moja akielekeza nguvu huko hijazi baada ya kifo cha sheikh akaanza na watu wa Twaif kisha akaelekea kwa watu wa Makka, na watu wa Makka alikuwa tayari amekwisha kuwafuata kabla ya imamu Saudi kiongozi Othman bin Abdil Rahman Al Mudhwaifi, na alishuka kwa nguvu kubwa aliyoituma kwake Imamu Saudi bin Abdul Azizi bin Muhammadi kiongozi wa Dari'a akiwa na nguvu kubwa kutoka kwa watu wa Najidi na wengineo, na wakamsaidia mpaka akaitawala Twaif, na akatoa wanachuoni watukufu, na akaidhihirisha da'wa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na akaelekeza katika haki, na akakataza shirki na kumuabudu bin Abbas na wengineo miongoni mwa wale waliokuwa wakiwaabudu watu wajinga huko, na wapumbavu miongoni mwa watu wa Twaif. Kisha akaelekea kiongozi Saudi kwa amri ya baba yake Abdul Azizi upande wa Hijazi, na yakakusanywa majeshi pembezoni mwa Makka.
Alipojua kiongozi wake kuwa hapa ni lazima kufanya moja kati ya mambo mawili, ima kujisalimisha au kukimbia basi alikimbilia Jiddah, na Saudi akaingia yeye pamoja na wale alionao miongoni mwa waislamu bila mapigano, na wakaitawala Makkah katika nyakati za Alfajiri siku ya juma mosi tarehe nane mwezi Muharram mwaka 1218H, na wakatangaza da'wa katika njia ya Mwenyezi Mungu na wakayabomoa yote yaliyomo miongoni mwa makuba yaliyokuwa yamejengwa katika kaburi la Bi Khadija na wengineo, wakayaondoa makuba yote, na wakatangaza ujumbe wa kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na wakachagua walimu wataokaa kufundisha, na waelekezaji, na viongozi, na mahakimu watakao hukumu kwa sheria ya Mwenyezi Mungu, kisha baada ya muda mchache ukafunguliwa mji wa Madina, Na wakautawala familia ya Saudi (Al Saudi) mji wa Madina mwaka 1220H baada ya mji wa Makka kwa takriban miaka miwili, na ikaendelea miji miwili mitukufu kuwa chini ya utawala wa familia ya Saudi, na wakachagua viongozi na waelekezaji, na wakaeneza uadilifu katika miji yote na kuhukumu kwa sheria, na kuwafanyia wema wakazi wake, na hasa hasa masikini na wenye uhitaji wakawafanyia wema kwa kuwapa mali, na wakawaliwaza na wakawafundisha kitabu cha ALLAH, na wakawaelekeza katika mambo ya kheri, na wakawapa heshima wanachuoni na wakawahamasisha juu ya kufundisha na kutoa maelekezo, bado misikiti miwili ikaendelea kuwa chini ya utawala wa Al Saud mpaka mwaka 1226H, Kisha majeshi ya Misri na Uturuki yakaanza kuelekea katika miji ya Hijazi, kwa ajili ya kuwapiga vita Al Saudi na kuwatoa katika misikiti miwili mitukufu (Makka na Madina) kwa sababu nyingi na baadhi yake zimetangulia hapo awali, Na sababu hizi nikuwa maadui zao, na mahasidi wao, na wenye kufuata mambo ya hovyo wasiokuwa na elimu, na baadhi ya wanasiasa waliotaka kuizimisha da'wa hii na wakahofia huenda wakapoteza nafasi zao, na huenda ikakatisha tamaa zao, wakamsingizia sheikh pamoja na wafuasi wake na watetezi wake, na wakasema: Hawa wanamchukia Mtume Sala na Amani ziwe juu yake-, nakuwa wanawachukia mawalii, na wanapinga karama zao na wakasema pia kuwa wao wanasema kadhaa wa kadhaa, miongoni mwa mambo ambayo wanadai kuwa nikushusha heshima ya Manabii Amani iwe juu yao, na wakayaamini maneno haya baadhi ya wajinga, na baadhi ya wapingaji, na wakafanya hiyo kuwa ndio ngazi ya kuweza kuwafikia na kuwapiga vita, na wakahamasishana waturuki na wamisri juu ya kuwapiga vita, yakatokea yaliyotokea miongoni mwa fitina na mapigano, na yakawa mapigano ni katika misri kusini na Uturuki na wale waliopamoja nao, na kati ya Al Saudi katika mji wa Najidi, na Hijazi, yakatembea mapigano hayo muda mrefu tangu mwaka 1226H sawa na 1805G, mpaka mwaka 1233H sawa na mwaka 1812G, miaka saba yote ni mapigano na mashambulizi kati ya nguvu ya haki na nguvu ya batili.
Na kwa muhutasari huyu ndiye sheikh Muhammadi bin Abdul Wahhab -ALLAH amrehemu, hakika alisimama kuitangaza dini ya ALLAH, na kuwaelekeza watu katika tauhidi ya ALLAH, na kuyakemea yale waliyoyaingiza watu ndani yake miongoni mwa mambo ya uzushi na mambo ya hovyo, na akasimamia pia kuwalazimisha watu kufuata haki, na akawakemea juu ya batili, na akwaamrisha mema, na akakataza maovu.
Huu ndio muhutasari wa da'wa yake -ALLAH amrehemu-naye katika maswala ya itikadi yuko katika njia ya wema waliotangulia, anamuamini ALLAH na majina yake na sifa zake, na anawaamini Malaika wake na Mitume wake, na vitabu vyake, na siku ya mwisho, na makadirio kheri yake na shari yake, kupitia njia ya maimamu wa uislamu katika kumpwekesha Mwenyezi Mungu, na kutakasa ibada kwa ajili yake Mtukufu, na katika kuamini majina ya ALLAH na sifa zake katika njia inayoendana na ALLAH Mtukufu, haziharibu sifa za ALLAH na wala hamfananishi ALLAH na viumbe wake,na katika kuamini kufufuliwa na kuhudhurishwa mbele ya ALLAH, na kulipwa na kuhesabiwa, na pepo na moto, na mengineyo, na anasema katika maswala kiimani yale waliyoyasema wema waliotangulia kuwa imani ni kauli na matendo inazidi na inapungua, inazidi kuwa kumtii ALLAH, na inapungua kwa maasi. Yote haya ni katika itikadi yake ALLAH amrehemu, yeye yuko katika njia yao na yuko katika itikadi yao, kwa kauli na matendo, na wala hakuwahi kutoka katika njia yao hio katu, na wala hana madhehebu yake maalumu katika hayo, na wala mfumo maalumu, bali yeye yuko katika njia ya wema waliotangulia katika maswahaba na waliowafuata kwa wema ALLAH awaridhie wote.
Bali alilidhihirisha hilo katika mji wa Najidi na miji ya pembezoni mwake, na akalingania katika hilo, kisha akapigana jihadi juu ya hilo kwa aliyelikataa, na akakaidi, na akawapiga vita, mpaka ikadhihiri dini ya ALLAH na haki ikapata ushindi, na vile vile yeye yuko pamoja na yale wanayoyalingania waislamu wengine kwenye da'wa katika njia ya ALLAH, na kupinga batili, na kuamrisha mema na kukataza maovu, lakinii sheikh na wafuasi wake walikuwa wakiwalingania watu katika haki, na wakiwalazimisha kuifuata, na wakiwakataza batili, na wakiwakemea juu yake, mpaka waiache, na vile vile alifanya juhudi kubwa katika kukemea uzushi na mambo ya hovyo mpaka ALLAH Mtukufu akayaondoa kwa sababu ya da'wa yake, sababu hizi tatu zilizotangulia hivi punde ndizo sababu za uadui na ugomvi kati yake na watu wengine, nazo ni:
Ya kwanza: Kupinga ushirikina na kuwaita watu katika kumpwekesha ALLAH halisi, Ya pili: Kupinga uzushi, na mambo ya hovyo, kama kujenga juu ya makaburi na kuweka misikiti juu yake na mfano wa hayo kama sherehe za maulidi na mambo ya twarika yaliyozushwa na makundi ya kisufi. Ya tatu: Hakika yeye alikuwa akiamrisha mema, na akiwalazimisha kuyafuata kwa nguvu, mwenye kukataa mema aliyowajibishiwa na ALLAH alikuwa akilazimishwa na akifedheheshwa akiyaacha, na alikuwa akiwakataza watu maovu na akiwakemea, na akisimamisha sheria zake, na akiwalazimisha watu kuifuata haki, na akiwakemea batili, na kwa sababu hii haki ilidhihiri na ikapata ushindi, na batili ikaanguka na ikakatika, na watu wakawa katika mwenendo mzuri, na mfumo ulionyooka katika masoko yao, na katika misikiti yao, na katika hali zao zote.
Uzushi ukawa haujulikani kwao, na wala ushirikina ukawa haupatikani katika miji yao, na wala maovu hayaonekani wazi baina yao. Bali ikawa mtu yeyote mwenye kuitazama miji yao na akatazama hali zao na yale wanayoyafanya anakumbuka hali za wema waliotangulia zama za Mtume Sala na Amani ziwe juu yake-, na zama za Maswahaba zake, na zama za wafuasi wao kwa wema katika karne bora -ALLAH awarehemu-. Watu wote walikwenda katika mwenendo wao. Na wakapita katika njia yao, na wakavumilia juu ya hilo, na wakafanya juhudi katika hilo, na kupambana, na yalipotokea baadhi ya mabadiliko katika zama za mwisho baada ya kufariki kwa sheikh Muhammadi kwa muda mrefu, na kufariki kwa watoto wake wengi -Sala za ALLAH ziwe juu yao- na watetezi wake wengi, yalitokea baadhi ya mabadiliko, likaja balaa na ukaja mtihani kupitia Dola ya Uturuki na Dola ya Misri, Na hii ni kusadikisha kauli yake aliyetakasika na kutukuka: Hakika ALLAH habadilishi hali waliyonayo watu mpaka wabadilishe yale yaliyomo nafsini mwao. [Al Ra'di: 11] Na tunamuomba ALLAH aliyetakasika na kutukuka ayafanye yale yaliyowafika kuwa ni sababu ya kufutiwa madhambi na kutakaswa na makosa, na iwe ni sababu ya kunyanyuliwa na iwe ni shahada kwa waliouawa miongoni mwao -ALLAH awaridhie na awarehemu-. Na bado da'wa yao Alhamdulillah inaendelea na imezagaa mpaka leo hii, hii baada yakuwa majeshi ya Misri yameuumiza mji wa Najidi, na yakawaua wale yaliyoweza kuwaua, na yakawatoa baadhi ya watu, haikupita miaka mingi baada ya tukio hilo kisha da'wa ikasimama na ikaendelea na ikaenea, na akaibuka kwa kufikisha ujumbe baada ya tukio hilo kwa miaka mitano Imamu Turki bin Abdallah bin Muhammadi bin Saudi -ALLAH amrehemu- akaieneza da'wa katika mji wa Najidi na miji ya pembezoni mwake-, na akawafurusha waturuki waliokuwa huko, na wamisri, aliwafukuza kutoka katika mji wa Najidi na vijiji vyake, na miji yake, na da'wa ikaenea baada ya hapo katika mji wa Najidi mwaka 1240H.
Na tukio la kuuharibu mji wa Dar'ia na kuimaliza dola ya Al Saudi lilikuwa katika mwaka wa 1233H. Wakawa wanaishi katika vurugu katika miji ya Najidi, na mapigano, na fitina kubwa takribani miaka mitano, tangu mwaka wa 1234 mpaka mwaka 1239H, kisha katika mwaka wa Elfu moja na mia mbili na arobaini (1240H), ilikusanyika nguvu ya waislamu katika mji wa Najidi kwa Imamu Turki bin Abdallah bin Saudi, na haki ikapata ushindi, na wanachuoni wakaandika barua mbali mbali, kwenda katika vijiji na miji, na wakawahamasisha watu na wakawaita katika dini ya ALLAH na mapigano yakamalizika yaliyokuwa baina yao baada ya vita vya muda mrefu ambavyo vilitokea mikononi mwa wamisri na wasaidizi wao, Hivi ndivyo vilivyozimika vita na fitina zilizotokea baina yao baada ya vita vile na moto ukapoa, na dini ya ALLAH ikapata nguvu, na baada ya hapo watu wakashughulika na kufundisha na kuelekeza, na kufikisha ujumbe, na kutoa muongozo, mpaka maji yakarudi katika mkondo wake, na watu wakarudi katika hali zao, na yale waliyokuwa nayo zama za sheikh, na wakatulizana wanafunzi wake, na watoto wake, na watetezi wake, ALLAH awaridhie wote, na kazi ya kufikisha ujumbe ikaendelea kuanzia mwaka 1240H mpaka leo hii, kwa msaada wa ALLAH(Alhamdulillah), wakaendelea kurithishana familia ya Sauidi (Al Saudi) baadhi yao kwa baadhi, na familia ya sheikh na wanachuoni wa Najidi baadhi yao kwa baadhi, Al Saudi (Familia ya Saudi) wakawa wanarithishana katika uongozi na usimamizi wa kufikisha ujumbe katika njia ya ALLAH na jihadi katika njia ya ALLAH.
Na hivi ndivyo wanachuoni wanavyorithishana baadhi yao kwa baadhi katika da'wa ya ALLAH na kuelekeza katika da'wa hiyo, na kuelekeza katika haki. Isipokuwa Misikiti miwili mitukufu (Makka na Madina) ilibakia kuwa imetengwa katika dola ya Saudia kwa miaka mingi, kisha ikarudi mikononi mwao mwaka 1343H na akaitawala misikiti hii miwili mitukufu Imamu Muhammadi bin Abdul Azizi bin Faisal bin Turki bin Abdallah bin Saudi ALLAH amrehemu, na bado kwa msaada wa ALLAH iko chini ya utawala wa dola hiyo mpaka leo hii.
Kila sifa njema zinamstahiki ALLAH, na tunamuomba ALLAH aliyetakasika na kutukuka awarekebisha kizazi kilichobakia cha Al Saudi, na katika familia ya sheikh, na kwa wanachuoni wa waislamu kwa ujumla katika miji hii na mingineyo na awawezeshe wote kuyafikia yale anayoyaridhia, na awaongoze wanachuoni wa waislamu mahala popote watakapokuwa, na ainusuru haki kwa wote, na aididimize batili, na awape taufiki walinganiaji wa uongofu popote walipo ya kuyasimamia yale aliyowawajibishia ALLAH juu yao, na atuongoze sisi pamoja nao katika njia iliyonyooka, na aiimarishe misikiti miwili mitukufu, na vyote vyenye kuambatana nayo, na miji yote ya waislamu kwa uongofu, na kwa dini ya haki, na kwa kukitukuza kitabu cha ALLAH, na mafundisho ya Nabii wake Amani na rehema ziwe juu yake, na awaneemeshe watu wote kwa elimu ya kuitambua sheria, na kushikamana nayo, na kuvumilia juu ya hilo, na kudumu katika hilo, na kuhukumia kwa sheria hizo, mpaka watakapokutana na Mola wao aliyetakasika na kutukuka, kwani yeye juu ya kila kitu ni muweza, na kujibu kwake ndio bora zaidi. Na hapa ndio mwisho wa yale ambayo tumeweza kuyaweka wazi, na kuyabainisha, katika hali za sheikh, na da'wa yake na watetezi wake, na yote yanayomuhusu yeye, na Allah ndiye wakutakwa msaada, na kwake ndiko kwa kuegemea, na hakuna ujanja wala nguvu isipokuwa kwa ALLAH aliye juu na Mtukufu, Tunakuomba ALLAH umpe salamu na amani na umbariki mja wako na Mtume wako, Nabii wetu na Imamu wetu Muhammadi bin Abdillah, na juu ya familia yake, na yeyote atakayepita katika njia yao na akaongoka kwa muongozo wao, na kila sifa nje zinamsitahiki ALLAH Mola mlezi wa walimwengu wote.