المختصر في صفة الحج

المختصر في صفة الحج

Muhtasari wa namna ya kufanya Hija Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote, na rehema na amani ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad, na aali zake na Maswahaba zake wote.

Language: lang_sw
Prepared by: Kamati ya kisayansi ya jumuia ya huduma ya maudhui za kiislamu kwa lugha mbalimbali.
Version: 3.0
Translations 44
Amharic Assamese Azerbaijani Bambara +40
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

Muhtasari wa namna ya kufanya Hija Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote, na rehema na amani ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad, na aali zake na Maswahaba zake wote.

Ama baada ya hayo:

Hii ni Makala fupi katika namna ya kufanya Hija, tumefanya hima kubwa katika kubainisha mambo mengi ya msingi anayoyahitaji Mwenye kuhiji.

Na Mwenyezi Mungu pekee ndiye ninayemuomba aifanya kazi hii iwe ni kwa ajili ya uso wake mtukufu, na awanufaishe kwayo Waislmu wote.

Kamati ya kisayansi ya jumuia ya huduma ya maudhui za kiislamu kwa lugha mbalimbali.

Utangulizi

Kwanza: Sharti za kukubalika kwa ibada:

Ibada haikubaliki mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu isipokuwa kwa sharti mbili:

Ikhlas: Nayo ni mtu akusudie kwa ibada yake uso wa Mwenyezi Mungu peke yake, na nyumba ya Akhera. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu."[1] [Al-Bayyina: 5] Yaani: Wamuelekee Yeye tu na wamuabudu Yeye tu, na wajiepushe na kila kisichokuwa Yeye. Tafsiri ya As-Sa'adi (uk. 538)

Na amesema Mtume, rehehma na amani zimshukie: "Hakika matendo yote huzingatiwa nia, na hakika kila mtu atalipwa kwa lile alichokinuia." [2] Kaipokea Bukhari, kwa nambari 1, na Muslim, kwa nambari 1907.

Kumfuata Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, ndani yake kwa kauli na vitendo. Amesema Mtume, rehema na amani ziwe juu yake: "Yeyote atakayezua katika jambo letu hili kitu ambacho hakimo, basi hicho kitakataliwa." Kaipokea Bukhari (2697) na Muslim (1718), na katika riwaya nyingine ya Muslim (1718): "Mwenye kufanya tendo ambalo hatukuliamrisha, basi tendo hilo litakataliwa." [3] Kaipokea Bukhari, kwa nambari 2697, na Muslim, kwa nambari 1718. [4] Kaipokea Muslim, kwa nambari 1718.

***

Kwanza: Hukumu za vituo vya kuhirimia:

Vituo vya kuhirimia: Ni sehemu alizozianisha Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, ili ahirimie hapo mwenye kutaka kufanya Hija au Umra.

Kwa hivyo, yeyote anayepita katika mojawapo ya hizo huku akiwa amekusudia kuhiji au kufanya Umra, basi ni lazima ahirimie huko, na wala hataruhusiwa kuzipita bila ya kuhirimia.

Na yeyote aliye karibu na Makka katika wakazi wa vituo hivi, basi kituo chake ni mahali anapoishi. Basi atahirimia papo hapo Hija na Umra.

Na ama watu wa Makka na wakazi wake, wao watahirimia Hija kutokea Makka. Na ama Umra, hiyo watatoka waende katika eneo lisilo takatifu (al-hill) na watahirimia hutokea huko, kama vile Taniim na mfano wake.

Na yeyote atakayekuwa ndani ya ndege, yeye atahirimia atakapofika usawa wa Miqat. Hivyo basi, anafaa kujiandaa na kuvaa nguo za ihram kabla ya kufika usawa wa Miqat. Atakapofikia usawa wake, basi papo hapo atahirimia, na wala haruhusiwi kuichelewesha mpaka atakapotua kwenye uwanja wa ndege. Pia anaweza kuchukua hadhari kabla ya kuifika, akafanya Talbiya (kuhirimia) kabla ya kuifikia Miqat kwa kuhofia asijepita mahali pa kuhirimia kwa sababu ya kasi kubwa ya ndege.

Ya pili: Aina za Hija na hukumu zake:

Hija ina aina tatu: Kujistarehesha kwa Hija na Umra, Hija pekee, kuunganisha Hija na Umra bila kujistarehesha.

Na kujistarehesha ndio bora kuliko zote kwa yule ambaye hakuleta mnyama wa kuchinja. Aina hii ya Hija huwa ambapo mtu anahirimia Umra ndani ya miezi ya Hija, na akatufu na akatembea Swafa na Marwa (saiyi), kisha akamaliza kwa kunyoa (Tahalluli), kisha akahirimia kuingia katika Hija ndani ya mwaka huo huo.

Hija pekee: Ni mtu kuhirimia Hija pekee. Basi akifika Makka, ni sunna kwake kutufu tawafu ya mtu aliyewasili (Twawaful-Quduum), kisha atakwenda kutembea kati ya Swafa na Marwa kwa ajili ya Hija, wala hatonyoa wala kupunguza nywele, na wala hatojivua katika ihiramu yake. Bali atabaki katika ihiram, na atajivua baada ya kutupa vijiwe kwenye Jamaratul-Akaba siku ya Idi. Na ikiwa atachelewesha Sayi (kutembea kati ya Swafa na Marwa) mpaka baada ya kutufu kwa ajili ya Hija, basi hakuna ubaya.

Na kuunganisha: Ni mtu kuhirimia Umra na Hija kwa pamoja, kwa kusema: "Labbaika llaahumma Umratan wa Hajjan (Nimekuitikia ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Umra na Hija)."

Na matendo ya muunganishaji kati ya Umra na Hija yako sawa na matendo ya anayefanya Hija pekee, isipokuwa anayeunganisha atatakiwa kutoa mnyama (dhabihu), ilhali mwenye kufanya Hija pekee hatotoa mnyama.

Ya tatu: Namna ya kuhirimia na hukumu zake:

Ni sheria kwa mwenye kutaka kuhirimia kufanya yafuatayo:

Kuoga, nayo ni sunna iliyotiwa mkazo, upande wa wanaume na wanawake, mpaka mwenye hedhi na nifasi (damu ya baada ya kuzaa).

Kupaka manukato mazuri zaidi atakayopata, kama vile mafuta ya udi au kinginecho kichwani kwake na ndevu zake, na wala haimdhuru lolote kubakia kwa harufu baada ya kuhirimia. Na ama mwanamke, yeye haruhusiwi kujitia marashi yenye harufu kali; ili wanaume wa kando wasiyanuse.

Kuvaa nguo za Ihram, ambazo ni kikoi na shuka. Sunna ni kwamba ziwe nyeupe na safi au mpya. Mwanamke anaweza kuvaa nguo zozote anazotaka bila ya kuonyesha mapambo yake, isipokuwa anapaswa kujiepusha na kuvaa nikabu na glovu. Atafunika uso wake na mikono yake kwa kitu kingine.

Inaruhusiwa kuhirimia baada ya swala, sawa iwe ni swala ya faradhi au ya sunna, lakini si lazima kwamba mtu ahirimie baada ya swala.

Atasema: "Labbaika llaahumma Umra (Nimekuitikia ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Umra).", ikiwa anataka kufanya Umra, au "Labbaika llaahumma Hajjan (Nimekuitikia ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Hija).", ikiwa anafanya Hija pekee, au "Labbaika llaahumma Umratan wa Hajjan (Nimekuitikia ewe Mwenyezi Mungu kwa ajili ya Hija na Umra)." ikiwa anazikusanya zote mbili kwa wakati mmoja.

Na iwapo mtu anayetaka kuhirimia Hija au Umra anahofia kizuizi kitakachomzuia kukamilisha ibada yake, basi inafaa kwake aweke sharti anapoingia katika Ihram. Basi atasema: “...na ikiwa nitazuiliwa na kizuizi chochote, basi mahali pangu pa kutoka katika ihramu ni pale kitakaponizuilia." Kwa hivyo, pindi atakapoweka sharti hili na akapatwa na cha kumzuia kukamilisha ibada yake ya Umra, basi atatoka katika ihramu na wala hakutakuwa na chochote juu yake.

Kisha atarudia kutoa Talbiya mara kwa mara: (Nimekutikia, ewe Mwenyezi Mungu, nimekuitikia. Nimekuitikia, huna mshirika, nimekuitikia. Hakika sifa njema, neema zote na ufalme ni vyako, huna mshirika). [4] Mwanamume atainua juu sauti yake kwa hili, na mwanamke pia; Isipokuwa ikiwa mwanamke atakuwa kati ya wanaume wasiokuwa maharimu wake. Mtu huyu aliyehirimia Hija au Umra anafaa kurudia Talbiya mara kwa mara, hasa pale hali na nyakati zinapobadilika, kama vile anapopanda mahali pa mwinuko, au anaposhuka chini, au unapoingia usiku au mchana. Maana ya mtu kusema: “Labbaika” ni nimekuitikia ewe Mola Mlezi mara baada ya mara. Hili linamaanisha kwamba mtu amemuitikia Mola wake Mlezi na akadumu katika kumtii. Innalhamda wanni'imata laka walmulk. Tafsiri: Alhamdu ni kumsifu anayesifiwa kwa ukamilifu pamoja na upendo na taadhima. Na: Anni'imat (neema) ni yale ambayo Mwenyezi Mungu huwapa waja wake kutokana na fadhila zake kwa kuwawezesha kupata kile wanachokitafuta na kuwazuilia wanachokichukia. Na kauli yake 'almulk' inamaanisha kwamba ufalme ni wako. Kwa hivyo Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka ndiye Mwenye kumiliki peke yake. Na kauli yake 'laa shariika lak' inamaanisha kwamba hakuna anayeshiriki nawe katika kile ambacho ni mahususi kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika sifa zake kamili, ikiwa ni pamoja na upekee wake katika ufalme wake, kuumba, kuendesha mambo na uungu. (Maj-muu'ul-fataawaa warasaailul-'Uthaimiin (22/96)) kwa muhtasari.

Talbiya ni sheria katika Umra kwanzia katika ihiramu mpaka atakapoanza kutufu. Na katika Hija, ni kwanzia mtu anapohiramia mpaka atakapoanza kutupa vijiwe kwenye Jamaratul-Akaba siku ya Idi.

Mtu aliyehirimia Hija au Umra analazimika kutahadhari asije akaangukia katika makatazo yoyote ya ihramu mpaka atakapotoka katika ihramu yake.

Ya nne: Makatazo ya ihiramu

Makatazo ya ihiramu ni:

Kunyoa nywele au kuzipunguza au kuzing'oa kutoka sehemu yoyote ile ya mwili.

Kukata kucha zote au baadhi yake kwenye miguu au mikono.

Kufunika kichwa kwa kitu kinachoshikamana nacho, kama vile kofia, kitambaa na kilemba, au kuweka shuka juu ya kichwa, au kuweka leso za mikononi, blanketi, boksi au kitu kingine chochote kinachoweza kutumika katika kufunika kichwa. Haya ni maalumu kwa wanaume, sio kwa wanawake.

Kuvaa mavazi ya kawaida yaliyoshonwa ili kuvaliwa kwenye mwili mzima, kwa njia ya kawaida, kama vile: Nguo iliyoshonwa, suruali, shati, soksi na glovu. Haya ni maalumu kwa wanaume tu, sio kwa wanawake. Ama wanawake, wao wanakatazwa tu:

Kuvaa nikabu, au burka', au pazia linalofanana na nikabu, lakini itamlazimu kufunika uso wake mbele ya wanaume wasiokuwa maharimu wake kwa kitu kinachotumika kwa kawaida katika kufunika uso; Hata kama kifuniko hicho kitaugusa uso wake, lakini haruhusiwi kutumia kizuizi au kitu kama hicho kwenye kichwa chake ili kuzuia kifuniko hicho kuugusa uso wake; Kwa sababu hakuna ushahidi wa kuruhusiwa kwa hilo.

Kuvaa glovu mikononi mwake, na itamlazimu kufunika mikono yake mbele ya wanaume wasio maharimu wake kwa kuiweka ndani ya abaya (buibui) yake.

Kujipaka manukato mwilini au katika nguo za ihramu.

Kuua viwindwa vya mwituni, au kuwawinda hata kama hatawauwa.

Kuposa au kumposea mtu mwingine.

Kufunga ndoa.

Kumpapasa mwanamke katika sehemu zisizokuwa tupu; kama vile kumbusu na kumgusa kwa matamanio.

Kujamiiana kwenye uke.

***

Ya tano: Namna ya kuzunguka Al-kaaba

Mtu aliyehirimia Hija au Umra atakapoingia kwenye Msikiti Mtukufu, ni sunna kwake autangulize mguu wake wa kulia na aseme dua ya kuingia Msikitini. Miongoni mwa mambo yaliyo sahihi kabisa kuhusiana na hilo ni aseme: “Ewe Mwenyezi Mungu, nifungulie milango ya rehema zako.” Dua hii ataisema wakati wa kuingia msikiti wowote, na sio maalumu kwa Msikiti Mtukufu.

Anapotaka kuanza kuzunguka Al-Ka'aba, atavaa lubega. Na namna ya kuvaa lubega ni kuweka katikati ya upande wa juu wa shuka yake chini ya kwapa lake la kulia na ncha zake mbili za juu kwenye bega lake la kushoto. Atakapomaliza kuzunguka Al-Ka'aba, atalirudisha shuka lake katika hali yake ya kabla ya kuzunguka Al-Ka'aba. Kwa sababu kuvaa lubega mahali pake ni katika kutufu peke yake.

Kisha ataliendea Jiwe jeusi na kuligusa kwa mkono wake wa kulia na kulibusu. Ikiwa hataweza kulibusu, ataligusa kwa mkono wake kisha aubusu mkono wake. Na ikiwa hataweza kuligusa kwa mkono wake, ataligusa kwa kitu alichonacho, kama vile fimbo au kitu kama hicho kisha akibusu. Na ikiwa hataweza kufanya hivyo, basi atalielekea Jiwe hilo na aliashirie kwa mkono wake lakini asiubusu. Kilicho bora zaidi ni kwamba asiwaudhi watu kwa kuleta msongamano.

Atakapoligusa Jiwe hilo au kuliashiria, atasema: "Allahu Akbaru ( Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)."

Kisha atakwenda upande wa kulia na aiweke Al-Ka'aba upande wake wa kushoto. Atakapoifikia kona inayoelekea upande wa Yemeni, ataigusa bila kuibusu. Na ikiwa hilo halitawezekana, basi asilete msongamano hapo wala asiiashirie.

Atasema baina ya kona ya Yemen na Jiwe Jeusi: "Mola wetu Mlezi, tupe duniani mema, na Akhera mema, na utulinde kutokana na adhabu ya Moto!"

Kila mara atakapolipita lile Jiwe Jeusi, ataliashiria kwa mkono wake na kusema: “Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.”

Na mizunguko yake iliyosalia, atasema chochote anachopenda mingoni mwa dhikri, dua na kusoma Qur’ani.

Sunna ni kwamba afanye "Arramalu" kukimbia mtiti katika mizunguko mitatu ya kwanza peke yake. Arramalu ni kutembea kwa kasi lakini kwa hatua fupi fupi. Na ama mizunguko minne iliyosalia, hiyo haina Arramalu. Atatembea kama kawaida.

Akikamilisha mizunguko, ataelekea katika mahali aliposimama Ibrahim (Maqamu Ibrahim) na asome: "Na mfanye mahali pa kisimamo cha Ibrahim kuwa mahali pa kuswalia", kisha ataswali rakaa mbili nyuma yake ikiwezekana, na isipowezekana ataziswali mahali popote msikitini, atasoma katika rakaa ya kwanza baada ya suratul-Fatiha: "Qul-Yaa ayyuhal-kaafiruun (Sema: Enyi makafiri!)" na atasoma katika rakaa ya tatu baada ya Faatiha: "Qul-huwallaahu Ahad (Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee)." (...Na alipokuwa akisimama Ibrahim pafanyeni pawe pa kuswalia...) [Al-Baqarah: 125] Kisha ataswali rakaa mbili nyuma yake ikiwezekana. Vinginevyo, ataswalia mahala popote pale Msikitini. Katika rakaa ya kwanza baada ya Fatiha, atasoma: "Qul-yaa ayyuhal-kaafiruun (Sema: Enyi makafiri)." [Suratul-Kaafiruun: 1] Na katika rakaa ya pili, baada ya Al-Fatihah, atasoma: "Qul-huwallaahu Ahad" Yaani, "Sema: Yeye ndiye Mwenyezi Mungu aliyepwekeka." [Al-Ikhlaas: 1]

Ya sita: Namna ya kufanya sa'yi

Atakapomaliza kutufu na rakaa zake mbili, basi atatoka kuelekea Masaa (sehemu ya kukimbia) na akikaribia Swafa, atasoma: "Hakika Swafa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu." kisha atasema: "Ninaaanza na kile alichoanza nacho Mwenyezi Mungu." "Innas-swafaa wal-marwata min sha’aa-irillah.” Yaani, “Hakika vilima vya Safaa na Marwa ni katika alama (za ibada) za Mwenyezi Mungu." Kisha aseme: "Abda-u bimaa bada-allaahu bihi" Yaani, "Ninaanza kwa kile alichoanza kwacho Mwenyezi Mungu."[6] [6] Kaipokea Muslim, kwa nambari 1218.

Kisha atapanda juu ya Swafa mpaka aweze kuiona Al-Ka'aba au muelekeo wake. Atampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtukuza kwa kusema: “Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye ni Muweza wa kila kitu. Hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu peke yake, aliitekeleza ahadi yake, na akamnusuru mja wake, na akayashinda makundi (ya maadui) peke yake." Atayarudia haya mara tatu, na ataomba dua kati yake. "Laa ilaaha illa llaahu wahdahuu laa shariika lahuu, lahul-mulku walahul-hamdu wahuwa alaa kulli shay-in Qadiir. Laa ilaaha illa llaahu, wahdahuu, anjaza wa'dahuu, wanaswara abdahuu, wa hazamal-ahzaaba wahdahuu", Yaani: Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye ni Muweza wa kila kitu. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, Yeye pekee. Alitimiza ahadi yake, na akamnusuru mja wake, na akayashinda makundi ya maadui peke yake." Kisha ataomba kati ya dua hiyo. Na atasema namna hii mara tatu.[7] [7] Kaipokea Muslim, kwa nambari 1218.

Kisha atashuka kutoka Swafa na aende hadi Marwa kwa miguu. Atakapoifikia alama (taa) ya rangi ya kijani kibichi, atatembea haraka. Na atakapoifikia alama (taa) ya rangi ya kijani kibichi ya pili, atatembea kama kawaida. Wanawake hawaruhusiwi kuharakisha mwendo katika kutembea wakati wa kufanya sa'yi.

Atakapofika Marwa, anaruhusiwa kufanya yale aliyoyafanya kwenye Swafa (tazama kifungu cha 2).

Kisha atashuka kutoka kwenye Marwa kwenda Swafa kwa kutembea kwa miguu. Atakapofika kwenye alama ya kijani, atatembea haraka. Na atakapoifikia alama (taa) ya rangi ya kijani kibichi ya pili, atatembea kama kawaida.

Ataendelea hivi hadi amalize mizunguko saba. Kutoka Swafa hadi Marwa ni mzunguko mmoja, na kurudi kutoka Marwa hadi Swafa ni mzunguko mwingine.

Na atasema katika sa'yi yake chochote anachopenda miongoni mwa dhikri, dua na kusoma Qur'ani.

Ya saba: Namna ya kunyoa na kupunguza nywele

Mwenye kufanya Umra atakapomaliza kuzunguka Al-Ka'ba na kufanya sa’yi, itamlazimu anyoe kichwa chake au azipunguze ikiwa ni mwanaume. Sunna ni kunyoa au kupunguza kichwa chote.

Kunyoa nywele ni bora kuliko kupunguza, isipokuwa ikiwa wakati wa Hija umekaribia kiasi kwamba hakuna wakati wa kutosha wa kuota nywele za kichwa. Basi kilicho bora ni kuzipunguza tu.

Ama mwanamke, yeye atapunguza kwenye ncha za nywele zake kiasi cha ncha ya kidole au chini ya hivyo.

Na ama aliyehirimia kwa ajaili ya Hija sawa iwe ni Hija pekee au kaambatanisha Hija na Umra basi asipunguze chochote katika nywele zake isipokuwa siku ya Idi baada ya kurusha vijiwe katika Jamaratul-Akaba.

Na kufikia hapa mtu atakuwa kakamilisha Umra yake, na vile vile Hujaji aliyetia nia ya kujistarehesha katika Umra yake.

Namna ya kufanya Hija

Kwanza: Ni kuhirimia (kutia nia) ya kuingia katika Hija:

Sunna kwa mwenye kutaka kuhiji ni ahirimie asubuhi ya siku ya Tarwiya. Yaani: Tarehe nane ya mwezi wa Dhul-hijja, kwanzia mahali alipo, alipokusudia Hija akiwa hapo, endapo atakuwa Makka au eneo lililo ndani ya mipaka ya Mikati (Kituo). Na kama hatokuwa Makka, basi atatakiwa kufika kwenye Miqati yoyote itakayokuwa katika njia yake.

Na atafanya wakati wa kuhirimia kwake Hija yale aliyoyafanya wakati wa kuhirimia kwake Umra; kama kuoga, kupaka marashi na kuswali. Hapo atahirimia Hija na atatoa talbiya. Namna ya kufanya talbiya katika Hija ni kama namna tu ya talbiya katika Umra isipokuwa hapa atasema: "Labbaika Hajjan (Nimekuitikia kwa ajili ya Hija)", badala ya kusema: "Labbaika Umratan (Nimekuitikia kwa ajili ya Umra)."

Na iwapo mtu anayetaka kuhirimia Umra anahofia kizuizi kitakachomzuia kukamilisha ibada yake, basi inafaa kwake aweke sharti anapoingia katika Ihram, kwa kusema: “...Na ikiwa nitazuiliwa na kizuizi chochote, basi mahali pangu pa kutoka katika ihramu ni pale kitakaponizuilia." Basi pindi atakapoweka sharti hili na akapatwa na cha kumzuia kukamilisha ibada yake ya Umra, basi atatoka katika ihramu na wala hakutakuwa na chochote juu yake.

Kisha atarudia kutoa Talbiya mara kwa mara: "Nimekuitikia, ewe Mola, nimekuitikia. Nimekuitikia, huna mshirika, nimekuitikia. Hakika sifa na neema zote ni zako, na ufalme, huna mshirika."[4] Mwanamume atainua juu sauti yake kwa hili, na mwanamke pia; Isipokuwa ikiwa mwanamke atakuwa kati ya wanaume wasiokuwa maharimu wake. Mtu huyu aliyehirimia Umra au Hija anafaa kurudia Talbiya mara kwa mara, hasa pale hali na nyakati zinapobadilika, kama vile anapopanda mahali pa juu, au anaposhuka chini, au unapoingia usiku au mchana.

Na talbiya ni sheria kuanzia kuhirimia mpaka atakapotupa vijiwe vya Jamaraati siku ya idi.

Mtu aliyehirimia Hija au Umra analazimika kutahadhari asije akaanguka katika makatazo yoyote ya ihramu mpaka atakapotoka katika ihramu yake.

***

Pili: Kulala Mina usiku

Kisha ni sunna kwake atoke kwenda Mina katika siku ya nane; na ataswali hapo Adhuhuri, Lasiri, Magharibi, Ishaa na Alfajiri. Ataziswali kwa kuzipunguza pasina kuziunganisha; kwa sababu Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alikuwa akipunguza swala anapokuwa Mina na wala haziunganishi.

Ya tatu: Ni kusimama Arafa na kulala Muzdalifa usiku

Likichomoza jua katika siku ya tisa ambayo ni siku ya Arafa atatembea kutoka Mina kuelekea Arafa. Atashuka Namira na atakaa hapo mpaka jua litakapopinduka, ikiwa hilo litakuwa jepesi kwake. Na akishindwa, basi hakuna ubaya pia; kwa sababu kushuka Namira ni sunna wala sio lazima.

Jua likishapinduka, basi ataswali Adhuhuri na Lasiri rakaa mbili mbili. Atazikusanya kwa kuzitanguliza, kama alivyofanya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake.

Kisha atajitenga baada ya swala kwa ajili ya kumtaja Mwenyezi Mungu, na kuomba dua na kujinyenyekeza kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Na hapo ataomba dua yoyote aipendayo huku akiwa kanyanyua mikono yake na akiwa kaelekea kibla.

Na ilikuwa mara nyingi zaidi dua ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, katika mahali hapo patukufu ni: "Laa ilaaha illa llaahu wahdahu laa shariika lahu, lahul-mulku walahul-hamdu, wahuwa a'laa kulli shai-in qadiir." Yaani: Hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake asiye na mshirika. Ufalme ni wake na sifa njema, naye ni Muweza wa kila kitu.

Na ikichoka na akataka kupumzika kwa kuzungumza na jamaa zake kwa mazungumzo yenye manufaa au kusoma vitabu vyenye faida atakavyoweza kuvipata, hasa hasa vile vinavyohusu ukarimu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na vipawa vyake; ili matumaini yake katika siku hiyo yapate nguvu, basi hilo litakuwa ni zuri zaidi. Kisha atarejea tena kumnyenyekea Mwenyezi Mungu na kumuomba, na atapupia sana kufaidika na fursa ya mwisho wa mchana kwa dua. Kwani bila shaka dua bora ni dua ya siku ya Arafa.

Jua likizama katika siku ya Arafa, basi ataondoka kuelekea Muzdalifa.

Basi akifika hapo, ataswali Magharibi rakaa tatu, na Ishaa rakaa mbili kwa kuzikusanya swala hizo.

Na ikiwa atahofia kufika Muzdalifa baada ya nusu ya usiku, basi ataswali hata kama hajafika Muzdalifa, na wala haifai kuichelewesha swala mpaka baada ya nusu ya usiku.

Na atalala Muzdalifa, na pindi itakapompambazukia Alfajiri, ataswali Alfajiri mapema, kwa Adhana na Ikama.

Kisha ataelekea sehemu tukufu, na hapo atampwekesha Mwenyezi Mungu na kumtukuza na kuomba dua yoyote aipendayo mpaka mwanga uwe wa njano sana. Na asipoweza kwenda sehemu tukufu (Mash'ari), basi ataomba dua akiwa hapo hapo alipo; kwa mujibu wa kauli ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake: "Nimesimama hapa na Jam'u (yaani Muzdalifa) yote ni mahali pa kusimama." Atakaelekea kibla wakati anafanya dhikiri na kuomba dua huku kainua juu mikono yake. "Nimesimama hapa, na Jam'u (yaani Muzdalifa) yote ni mahali pa kusimama."[8] Na wakati wa dua, anatakiwa kuelekea kibla huku kanyanyua mikono yake. [8] Kaipokea Abuu Daudi, kwa Nambari 1936.

Ya nne: Matendo ya siku ya Idi

Mawingu yatakapokuwa ya njano sana, ataondoka kutoka Muzdalifa - kabla jua halijachomoza - na kwenda Mina, na atakwenda haraka akifika katika Bonde la Muhassir.

Akifika Mina, atarusha vijiwe katika Jamaratul-Akaba, na ndio kituo cha mwisho kilicho karibu na Makka. Atarusha vijiwe saba kwa mfululizo, kimoja baada ya kingine. Kila kimoja kiwe na usawa wa kokwa la tende takribani, na atatoa takbira kwa kila kijiwe anachorusha.

Kisha atachinja mnyama wake likiwezekana hilo.

Kisha atanyoa kichwa chake au kupunguza akiwa ni mwanaume, na kunyoa ndio bora zaidi. Ama mwanamke, yeye anaruhusiwa katika sheria kupunguza tu bila kunyoa.

Akitupa vijiwe na akanyoa, basi atakuwa kajivua kwa mara ya kwanza kutoka katika ibada yake, na hapo kila kitu kitakuwa halali kwake isipokuwa wanawake.

Kisha atashuka Makka, na atazunguka Kaaba twawafu ya Hija (TwawafuI Ifadha) kisha atakwenda kutembea kati ya Swafa na Marwa (Sa'yi) kwa ajili ya Hija yake ikiwa ni katika wale waliofanya Hija ya akujistarehesha, au kama alifanya Hija pekee yake au ikiwa aliziunganisha zote kwa pamoja, na akawa hakutembea kati ya Swafa na Marwa baada ya mzunguko wake wa kuwasili Makka (Tawaful-Qudum). Na anaruhusiwa kuchelewesha tawafu na sa'yi mpaka usiku au katika siku ya pili, kulingana na jinsi itakavyokuwa rahisi kwake.

Ya tano: Matendo ya siku za Tashriiq

Atakaporusha vijiwe na akanyoa na akafanya sa'yi, basi hapo atakuwa kajivua jumla jumla kutoka katika ibada yake, na hapo kila kitu kitakuwa halali kwake hata wanawake.

Atarejea Mina na atalala huko usiku wa tarehe kumi na moja, kumi na mbili na kumi na tatu ikiwa atachelewa (kutoka siku ya kumi na mbili).

Na atazirushia vijiwe Jamaraati tatu zote mchana jua litakapopinduka.

Atairushia vijiwe Jamarati ya kwanza katika siku ya kumi na moja. Na ndiyo Jamaraati iliyo mbali zaidi kutokea upande wa Makka, lakini iko karibu mno na Msikiti wa Khaif. Atairushia vijiwe saba vyenye kufuatana mfululizo, kimoja baada ya kingine, na atatoa takbira (Allaahu Akbaru) kwa kila kijiwe. Kisha atasongea mbele kidogo na ataomba dua ndefu kwa chochote akipendacho. Ikiwa atapata tabu kusimama kwa muda mrefu na kuomba dua, basi ataomba dua yoyote nyepesi kwake hata kama itakuwa fupi, ilimradi tu aipate sunna.

Kisha atairushia vijiwe Jamaraati ya katikati hivyo hivyo, na ataomba pia baada yake.

Kisha atairushia Jamaratil Akaba vile vile, isipokuwa hii ataondoka pasina kuomba dua baada yake.

Kisha atazirushia Jamaraati zote tena katika siku ya kumi na mbili kama alivyofanya katika siku ya kumi na moja. Akikamilisha kurusha vijiwe, akitaka anaweza kufanya haraka na akatoka Mina.

Na akitaka, anaweza kuchelewa na akalala hapo usiku wa kuamkia tarehe kumi na tatu, na kuzirushia Jamarat hizo vijiwe baada ya kupinduka jua kama ilivyotangulia. Kuchelewa kutoka Mina ndio bora zaidi.

Na si wajibu kuchelewa Mina mpaka siku ya kumi na tatu isipokuwa kama jua litazama katika siku ya kumi na mbili akiwa bado yuko Mina; basi atalazimika kusalia huko mpaka arushe vijiwe katika zile Jamaraati tatu baada ya jua kupinduka.

Na ikiwa jua litazama akiwa bado yuko Mina katika siku ya kumi na tatu pasina kupenda kwake, mfano kama aliondoka na akapanda kipando chake lakini akachelewa kwa sababu ya msongamano wa magari na mfano wake, basi halazimiki kusalia huko. Kwa sababu, kuchelewa kwake huko mpaka kuzama jua, kulikuwa nje ya uwezo wake.

Ya sita: Tawafu ya kuaga

Atakapotaka kutoka Makka kwenda katika mji wake, basi hataondoka mpaka atufu tawafu ya kuaga.

Isipokuwa mwenye hedhi na mwenye damu ya uzazi (nifasi), wao hawalazimiki kuaga, na wala haitakiwi wakae katika mlango wa Msikiti Mtukufu kwa ajili ya kuaga; kwa sababu hilo halikunukuliwa kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake.

Na ataifanya tawafu ya kuaga ndio agano la mwisho na nyumba tukufu atakapotaka kuondoka kwa ajili ya safari.

Na ikiwa atabakia baada ya kuaga, kwa ajili ya kuwasubiri marafiki zake au kubeba mabegi yake, au akanunua haja yoyote njiani, basi hakuna ubaya juu yake. Hatorudia tawafu isipokuwa kama atanuia kuahirisha safari yake, mfano kama akitaka kusafiri mwanzo wa mchana kisha akatufu tawafu ya kuaga, kisha akaahirisha safari mpaka mwisho wa mchana kwa mfano, basi hapo atalazimika kurudia tawafu ili kiwe kitu chake cha mwisho hapo Makka ni kuizunguka Nyumba tukufu.

***