صفة العمرة لابن باز
NAMNA YA KUFANYA UMRAH
NAMNA YA KUFANYA UMRAH
Mtunzi
Abdulaziz bin Abdillah bin Baaz
Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu peke yake, na baada ya hayo:
Huu ni muhtasari mfupi wa matendo ya ibada za Umrah. Na kwa msomaji, maelezo ya hayo ndiyo haya:
Mwenye kufanya Umrah atakapofika kwenye Miqat (sehemu za kunuia Hija au Umrah), inapendekezwa aoge na kujisafisha. Mwanamke pia atafanya hivyo hata kama atakuwa katika hedhi au katika damu ya baada ya kuzaa, isipokuwa hataruhusiwa kuzunguka Ka'aba mpaka atwaharike kutokana na damu na aoge.
Mwanamume anatakiwa kujipaka manukato kwenye mwili wake kabla ya kuvaa nguo zake za ihram. Ikiwa haitawezekana kuogea kwenye Miqat, basi hakuna ubaya ikiwa ataoga anapofika Makka kabla ya kuzunguka Ka'aba ikiwa hilo litawezekana.
Mwanamume atavua nguo zote za kawaida zilizoshonwa na kuvaa kikoi na shuka, na inapendekezwa ziwe nyeupe na safi.
Ama mwanamke, yeye atahirimia katika nguo zake za kawaida (isipokuwa hatavaa nikabu, barakoa na glovu. Hivyo atavivua na aufunike uso wake na mikono yake kutokana na wanaume wasio mahram wake kwa nguo nyinginezo) ambazo hazina mapambo wala si za umaarufu.
Kisha ataweka nia ya kuingia katika ibada (ya Umra) moyoni mwake na kuitamka kwa ulimi wake akisema: “Labbayka umrah (Nimekuitikia kwa kufanya Umra).” au “Allahummma labbayka umrah (Ewe Mwenyezi Mungu, nimekuitikia kwa kufanya Umra).” Iwapo aliyehirimia Umrah atachelea kuwa hataweza kutekeleza ibada zake kwa sababu ni mgonjwa au anaogopa adui au mfano wa hayo, basi anaruhusiwa kuweka sharti anapohirimia kwa kusema: "Ikiwa nitazuiliwa na kizuizi, basi mahali pangu pa kutoka katika ihram ni pale kitakaponizuilia." Haya ni kwa mujibu wa Hadithi ya Dhwuba’ah bint Az-Zubayr, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi. [1] As-Sunan Al-Kubra, cha Al-Bayhaqi, nambari 10117.
Kisha atafanya mwitikio (Talbiyah) ya Mtume,rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, ambayo ni: “Labbaykallaahumma labbayka. Labbayka laa shariika laka labbayka. Innalhamda wanni'imata laka walmulk laa shariika laka (NimekuitikIa ewe Mwenyezi Mungu nimekuitikia! Nimekuitikia hauna mshirika nimekuitikia. Hakika sifa njema na neema na ufalme ni vyako, nimekuitikia huna mshirika)!" "Labbaika llaahumma labbaika. Labbaika laa shariika laka labbaika. Innalhamda wanni'imata laka walmulk laa shariika laka (Nimekuitikia ewe Mwenyezi Mungu nimekuitikia! Nimekuitikia hauna mshirika nimekuitikia. Hakika sifa njema na neema na ufalme ni vyako, nimekuitikia huna mshirika)!" Na ataendelea kurudia mwitikio (talbiya) huu mara nyingi pamoja na kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu hadi afike katika Al-Kaaba.
Wanaume wanaruhusiwa kupaza sauti zao, nao wanawake watashusha chini sauti zao kama walivyokuwa wakifanya Maswahaba, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao.
Anapofika kwenye Nyumba ambayo ni Al-Kaaba, aache kufanya mwitikio (Talbiyah), kisha aende kwenye Jiwe Jeusi, alielekee, kisha aliguse kwa mkono wake wa kulia na kulibusu kama hilo litawezekana. Lakini asiwaudhi watu kwa kuleta msongamano. Aseme wakati anapoligusa: “Bismillaahi, Allaahu akbar” yaani, “Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa." Kama itakuwa vigumu kulibusu, ataligusa kwa mkono au kwa fimbo au kwa mfano wake, kisha akibusu kile alicholigusa kwacho. Na kama itakuwa vigumu kuligusa, basi ataliashiria na aseme: “Allaahu akbar” yaani, “Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa” na asibusu kile alichoashiria kwacho.
Ili tawafu iwe sahihi, ni sharti kwamba mwenye kutufu awe safi kutokana na hadathi ndogo na kubwa. Kwa sababu, tawafu ni kama swala, isipokuwa iliruhusiwa kuzungumza ndani yake.
Ataiweka Al-Kaaba upande wake wa kushoto na aizunguke mara saba. Kila anapofika kwenye kona ya Yemeni, ataigusa kwa mkono wake wa kulia ikiwezekana na kusema: “Bismillaahi, Allaahu akbar” yaani, “Kwa jina la Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa,” lakini asiibusu. Ikiwa itakuwa vigumu kwake kuigusa, ataiacha na kuendelea na tawafu yake, na asiiashirie wala asiseme: "Allaahu akbar” yaani, “Mwenyezi Mungu ni Mkubwa.” Kwa sababu hilo halikusimuliwa kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake.
Ama Jiwe Jeusi, kila anapokuwa sawa nalo, ataligusa na kulibusu kama tulivyotaja hapo awali. Vinginevyo, ataliashiria tu na kusema: "Allaahu akbar” yaani, "Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa." Inapendekezwa kutembea kwa hatua za haraka fupi fupi katika mizunguko mitatu ya kwanza ya Tawafu ya kufika Makka (Twawaf al-Quduum), kwa wanaume tu. Inapendekezwa kutembea kwa kasi, kwa hatua fupi, wakati wa mizunguko mitatu ya kwanza ya Tawaf al-Qudum, na hili ni mahususi kwa wanaume.
Pia inapendekezwa kwa mwanamume kuvaa lubega (Idhtwibaa) katika Tawaf al-Quduum (Tawafu ya kuingia Makka) katika mizunguko yote. Idhtwibaa inamaanisha kuweka sehemu ya katikati ya upande wa juu wa shuka yake chini ya bega lake la kulia na ncha zake mbili za juu kwenye bega lake la kushoto. Idhtwibaa: Inamaanisha kuweka sehemu ya katikati ya juu ya shuka yake chini ya bega lake la kulia na ncha zake mbili za juu kwenye bega lake la kushoto.
Na ni sunna pia kufanya dhikri na kuomba dua kwa wingi, kiasi iwezekanavyo katika mizunguko yote.
Hakuna dua wala dhikri mahususi katika tawafu. Bali mtu ataomba na kumjata Mwenyezi Mungu kwa dua na utajo wowote anaoweza. Na atasema kati ya pembe mbili za Al-Ka'aba: "Rabbanaa aatina fid-dun-yaa hasana, wafil-aakhirati hasana, waqinaa ‘adhaaban-naar.” Yaani, “Mola wetu Mlezi, tupe Duniani mema, na khera mema, na utulinde kutokana na adhabu ya Moto)!" (Suratul-Baqara: 201) Surah Al-Baqarah: 201 katika kila mzunguko. Kwa sababu, hili lilithibiti kutoka kwa Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.
Ataumaliza mzunguko wa saba kwa kuligusa Jiwe Jeusi na kulibusu ikiwezekana, au kuliashiria huku akisema “Allaahu Akbar (Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa.” kulingana na maelezo yaliyotajwa kabla ya muda mfupi. Baada ya kukamilisha mzunguko huu, atavaa shuka lake kwa kuliweka juu ya mabega yake na kona zake mbili za juu kwenye kifua chake.
Kisha ataswali rakaa mbili nyuma ya Maqam Ibrahim ikiwa itakuwa rahisi kufanya hivyo. Lakini kama hataweza kufanya hivyo, basi ataswalia mahali popote Msikitini. Baada ya kusoma surat Al-Fatihah, atasoma ndani yake: “Qul yaa ayyuhal kaafiruun” yaani, “Sema, ‘Enyi makafiri,’” (Surat Al-Kafiruun) katika rakaa ya kwanza, na “Qul huwallahu ahad”, yaani, “Sema, ‘Yeye Mwenyezi Mungu ni wa Pekee.'” (Surat Al-Ikhlaas) katika rakaa ya pili. Hilo ndilo bora zaidi, lakini akisoma kitu kingine, basi hakuna tatizo. Kisha, baada ya kumaliza rakaa mbili hizi, ataelekea kwenye Jiwe Jeusi, ikiwa hilo litawezekana. "Qul-yaa ayyuhal-kaafiruun (Sema: Enyi makafiri)." [Suratul-Kaafiruun: 1] katika rakaa ya kwanza, na: "Qul-huwallaahu Ahad" Yaani, "Sema: Yeye ndiye Mwenyezi Mungu aliyepwekeka." [Surat Al-Ikhlaas: 1] katika rakaa ya pili. Hili ndilo bora zaidi, lakini ikiwa atasoma sura nyinginezo zozote badala yake, basi hakuna ubaya wowote. Kisha, baada ya kutoa salamu ya kumaliza swala baada ya rakaa ya pili, ataliendea jiwe jeusi (Al-Hajarul-Aswad) na kuligusa kwa mkono wake wa kulia ikiwa hilo litakuwa rahisi. Inapendekezwa kunywa maji ya Zamzam baada ya kuswali rakaa mbili za baada ya Twawafu, ikiwezekana.
Kisha atatoka aende kwenye Safaa na apande juu yake au asimame hapo karibu. Kupanda juu yake ndiyo bora zaidi ikiwezekana. Kisha atasoma maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Innas-swafaa wal-marwata min sha’aa-irrllah.” Yaani, “Hakika vilima vya Safaa na Marwa ni katika alama za Mwenyezi Mungu." (Suratul-Baqarah: 158)
Na inapendekezwa kwamba aelekee Kiblah, amsifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu. Atasema: “Laa ilaaha illallaahu wallaahu akbaru, laa ilaaha illallaahu wahdahuu laa shariika lahu, lahulmulku, walahulhamdu, wahuwa ‘alaa kulli shay-in qadiir, laa ilaaha illallaahu wahdahuu anjaza wa’adahuu wanaswara ‘abdahuu wahazamal ahzaaba wahdahu (Hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mkubwa. Hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye ni Muweza mno wa kila kitu. Hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu peke yake, alitekeleza ahadi yake, na alimnusuru mja wake, na aliyashinda makundi (ya maadui) peke yake).” Kisha ataomba awezacho huku ameinua juu mikono, na atairudia dhikri hii na dua hii mara tatu. Allaahu akbaru, Allaahu akbaru. Laa ilaaha illallaahu allaahu akbaru, Allaahu akbaru walillaahilhamdu. Laa ilaaha illallaahu wahdahuu laa shariika lahu, lahulmulku, walahulhamdu, wahuwa ‘alaa kulli shay-in qadiir. Laa ilaaha illallaahu wahdahuu anjaza wa’adahuu wanaswara ‘abdahuu wahazamal ahzaaba wahdahu (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa. Hakuna mungu apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, Mwenyezi Mungu ni Mkubwa, na sifa njema zote ni zake. Hakuna mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu asiye na mshirika. Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, naye ni Muweza wa kila kitu. Hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu peke yake, aliitekeleza ahadi yake, na akamnusuru mja wake, na akayashinda makundi (ya maadui) peke yake)."[2] Ataomba kwa dua yoyote anayoweza, kisha atarudia dhikri hii na dua mara tatu. Hii ndiyo Sunnah aliyoifanya Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, huku ameelekea kibla. Kisha atashuka na atembee akienda Marwah mpaka afikie alama (taa ya rangi ya kijani kibichi) ya kwanza, na hapo mwanamume ataharakisha mwendo wa kutembea mpaka afikie alama ya pili. [2] Imepokelewa na Muslim, nambari 1218.
Ama mwanamke, yeye haruhusiwi kuharakisha mwendo katika kutembea. Kwa sababu yeye ni uchi. Kisha atatembea na kupanda juu ya Marwah au kusimama hapo karibu. Kupanda juu yake ndiyo bora zaidi ikiwezekana. Kisha atasema na kufanya juu ya Marwah aliyoyasema na kuyafanya juu ya Safaa. Kisha atateremka chini na kutembea katika sehemu aliyotembea na kuongeza kasi katika sehemu ambayo aliongeza kasi mpaka afike Safaa. Atafanya hivyo mara saba. Kwenda kwake ni raundi, na kurudi kwake ni raundi pia. Ikiwa atafanya Sa'yi huku amepanda, basi hakuna ubaya, hasa inapobidi. Hakuna ubaya kwa mtu anayefanya Sa’yi akiwa amepanda, hasa pale kunapokuwa na haja. Inapendekezwa kwamba aongeze kufanya dhikri na dua wakati wa Say’i yake, kiasi awezavyo, na awe safi kutokana na uchafu mkubwa na mdogo wa kiibada.
Inapendekezwa kwamba afanye dhikri na kuomba dua kwa wingi katika Sa'yi yake awezavyo. Pia inapendekezwa kwamba awe safi kutokana na hadathi kubwa na ndogo. Hata hivyo, ikiwa ataifanya bila twahara, basi hilo litamtosheleza.
Anapomaliza Sa’yi, mwanamume atanyoa nywele za kichwa chake au atazifupisha. Kuzinyoa ndiyo bora. Lakini ikiwa kuwasili kwake Makka ni karibu na wakati wa Hija, basi kuzifupisha ndiyo bora kwake ili aweze kunyoa sehemu ya kichwa chake iliyosalia wakati wa Hija. Ama mwanamke, yeye atakusanya nywele zake na kuzipunguza kiasi cha ncha ya kidole au chini ya hapo. Mtu aliyehirimia Umrah atakapofanya kile kilichotajwa, basi Umrah yake itakuwa imekamilika, na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu. Hapo, kila alichoharamishiwa kwa sababu ya ihram, sasa kitakuwa halali kwake. Mtume, rehema na amani za Mwenyezi Mungu zimshukie, hakuswali rakaa mbili baada ya kumaliza Umra, na anayempenda na afanye mfano wake. "Hakika nyinyi mnacho kiigizo chema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa anayemtaraji Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho, na akamtaja Mwenyezi Mungu sana." [Al-Ahzab: 21].
Mwenyezi Mungu atuwezeshe sisi na ndugu zetu Waislamu wote katika kuifahamu dini yake na tuwe imara ndani yake, na aikubali kutoka kwa kila mtu. Yeye aliyetakasika ndiye Mpaji, Mkarimu.
Na rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya mja wake na Mtume wake, Nabii wetu Muhammad, na aali zake, maswahaba zake, na wafuasi wake waliomfuata kwa wema mpaka Siku ya Malipo.
Muhtasari Mfupi wa matendo ya ibada za Umrah. Ulitolewa na Ofisi ya mheshimiwa, mtunzi wake, tarehe 13/2/1416 Hijria (Mkusanyiko wa Fatwa na Makala ya Sheikh, Ibn Baaz 17/425).