أنا مسلم

أنا مسلم

MIMI NI MUISLAMU

Language: lang_sw
Prepared by: Kamati ya kielimu ya usimamizi wa mambo ya dini katika Msikiti wa Makkah na Msikiti wa Mtume
Version: 1.0
Translations 30
Amharic German English Spanish +26
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

MIMI NI MUISLAMU

Kamati ya Kielimu ya usimamizi wa mambo ya Dini ya Msikiti Mtukufu wa Makkah na Madinah

Mimi ni Muislamu, kuwa hivyo anakusudia kuwa dini yangu ni Dini ya Uislamu,

Na Uislamu ni neno Tukufu lililotukuka walilo lirithi Manabii-Amani iwe juu yao- Toka wa mwanzo wao na wamwisho wao,

Na neno hili linabeba maana iliyo Nzuri iliyo simama madhubuti iliyo na heshima,

Neno hilo linakusudia kujisalimisha, na kujielekeza na kumtii Muumbaji,

Na neno hili linakusudia,Amani,Kujisalimisha,Utukufu,Salama,Furaha kwa mtu mmoja na kwa jamii.

Kwa ajili hii yamekuwa maneno ya Amani na Uislamu ni zaidi ya wingi wa Maneno kwa kupokelewa ndani ya Sheria ya Kiislamu,

Basi neno Salamu ni Jina miongoni mwa majina ya Allah,

Na Maamkizi ya Waislamu baina yao ni Amani,

Na Mamkizi ya watu wa Peponi ni(Amani),

Muislamu wa kweli ni yule ambae wamesalimika Waislamu kutokana na Ulimi wake na Mkono wake,

Basi Uislamu ni dini ya kheri kwa watu wote, Uislamu unawatosha, nao ndiyo njia ya Utukufu wao Duniani na Akhera,

Kwa ajili hiyo umekuja Uislamu ukiwa umekusanya umeenea ukiwa wazi umefunguliwa kwa kila mmoja asiye pambanua kati ya msingi na msingi,wala kati ya rangi na rangi,isipokuwa anawatazama watu kwa mtazamo wa pamoja,

Na wala hatofautishwi yeyote na kufanywa kuwa bora kuliko wengine ndani ya Uislamu isipokuwa kwa kiasi alicho kichukua kwa kujifunza kwake.

Kwa ajili hii Nafsi zote zinaukubali,kwa kuwa unaendana na Maumbile,

Basi kila Mtu anazaliwa akiwa ameumbwa kwa Kheri,na Uadilifu,Uhuru,Mwenye kumpenda Mola wake,Mwenye kumkubali kuwa yeye(Allah) ndiye muabudiwa mwenye kustahiki kuabudiwa peke yake kinyume na asiye kuwa yeye,

Na hakuna yeyote anaweza kujitoa kwenye maumbile haya isipokuwa kwa chenye kumtoa kinambadilisha kwenye maumbile,

Na Dini hii Allah ameichagua kwa ajili ya Watu,Muumbaji wa Watu,na Mola wao,na muabudiwa wao.

Na Dini yangu ya Uislamu inanifundisha kuwa mimi nitaishi ndani ya Dunia hii,na baada ya kufa kwangu nitaelekea kwenye nyumba ya Akhera,nayo ndiyo nyumba ya kubakia ambayo inakuwa muelekeo wa watu kwenda Peponi au Motoni.

Na Dini yangu ya Uislamu inaniamrisha mimi kwa Maamrisho na Inanikataza kunako makatazo,

Basi nitakapo tekeleza yale Maamrisho, na nikajiepusha na makatazo nitapata Utukufu Duniani na Akhera,

Na nitakapochupa mipaka ndani ya makatazo Itapatikana Ususuwavu Duniani na Akhera kwa kiasi cha kuchupa kwangu mipaka na mapungufu yangu.

Na jambo kubwa ambalo Uislamu umeniamrisha ni Kumpwekesha Allah (Tauhiid),

Basi mimi ninakubali,na ninaitakidi kuitakidi kwa ukweli kuwa Allah ndiye Muumbaji wangu,na ndiye muabudiwa wangu,

Basi simuabudu asiye kuwa Allah,hali ya kumpenda,na hali ya kuogopa adhabu zake,na kutarajia malipo yake,na kumtegemea.

Na upwekeshaji huo unawakilisha kumkubali Allah kwa upweke wake, na Mtume wake Muhammad kwa ujumbe (aliotumwa nao kutoka kwa Allah),

Na Muhammad ndiye Nabii wa mwisho,Allah alimtuma akiwa ni Rehema kwa walimwengu,na Allah akaukamilisha Utume kwa kumtuma Mtume Muhammad na Ujumbe,hakuna Nabii baada yake,

Na alikuja kwa Dini inayo faa kwa kila zama,na sehemu,na umma.

Na Dini yangu inaniamrisha maamrisho ya ukweli kuwaamini malaika,na Mitume wote,na mwanzo wao ni Nuhu,Ibrahimu,Musa,Issa na Muhammad-Amani ziwe juu yao-

Na unaniamrisha kuamini Vitabu vya mbinguni ambavyo vilivyo teremshwa kwa Mitume,na kumfuata wa mwisho wao,na mtimilifu wao,na mtukufu wao ni (qur'anI tukufu)

Na Dini yangu inaniamrisha mimi kuamini siku ya kiyama,ambayo watalipwa watu kwa matendo yao,

Na Dini yangu imeniamrisha kuamini makadirio,na kuridhia kwa yale yanayo tokea kwangu kwenye maisha kutokana na kheri au shari,na kufanya haraka kuchukua sababu za kufaulu.

Na kuamini makadirio kunaniongezea Raha, na utulivu, na kusubiri, na kuacha kujutia kwa yale yaliyo pita,

Kwakuwa mimi nina fahamu ufahamu wa yakini kuwa yale yaliyo nipata hayakuwa ni yenye kunikosa,na yale yaliyo nikosa hayakuwa ni yenye kunipata,

Kila kitu kilicho kadiriwa na kuandikwa kutoka kwa Allah na haikuwa kwangu mimi isipokuwa kwa kuchukuwa sababu,na kuridhika kwa yale yanayo kuwa baada ya hayo.

Na Uislamu unaniamrisha kwa yale yenye kuitakasa Roho yangu kwa matendo Mazuri,na Tabia njema ambazo anazo ziridhia Mola wangu,na zinatakasa Nafsi yangu,na zinatukuza Moyo wangu,na zinakunjua Kifua changu,na zinang'arisha Njia yangu,na zinaniweka kuwa ni kiungo chenye manufaa kwenye Jamii.

Na Jambo muhimu ya matendo hayo:ni kumpwekesha Allah,na kusimamisha Swala tano usiku na mchana,na kutoa Zaka ya mali,na Funga ya Mwezi kila mwaka,nao ni Mwezi wa Ramadhani,na kwenda kutembelea Nyumba ya Allah katika mji wa Makka kwa mwenye kuweza kuhiji.

Na miongoni mwa mambo muhimu Dini yangu imenielekeza kutokana na mambo ambayo kifua changu kinakunjuka ni wingi wa kuisoma Qur'ani ambayo ni maneno ya Allah,na mazungumzo ya kweli,na maneno yaliyo Mazuri na Matukufu yake,na ndiyo jambo kubwa lililokusanya Elimu za watu wa mwanzo na wa mwisho.

Kuisoma Qu'ani au kuisikiliza unaingiza Utulivu na Raha na Utukufu ndani ya Moyo,hata kama atakuwa Msomaji au Msikilizaji hatambui vizuri kiarabu au asiye kuwa Muislamu.

Na miongoni mwa mambo yanayo kunjua Kifua ni wingi wa kumuomba Allah,na kuelekea kwake,na kumuomba kila Dogo na Kubwa,

Basi Allah ni mwenye kumjibu kila anaye Muomba na akaitakasa ibada kwa ajili yake (Allah)

Na miongoni mwa mambo Mazuri yanayo kunjua Kifua ni kumtaja sana Allah -aliye Tukuka na Kutakasika-

Na hakika ameniongoza Nabii wangu-Sala na Amani ziwe juu yake-namna ya kumtaja Allah,na akaifundisha Mambo yaliyo Bora kumtaja kwayo Allah,

Na miongoni mwa hayo ni: Maneno Manne ambayo ndiyo Maneno Bora baada ya Qur'ani, nayo ni: (Sub-haana llahi, Wal-hamdulillah, Walaa ilaaha illa llah, Wallahu Akbaru) Utakasifu ni wake Allah, na Sifa njema ni zake Allah, na Hapana Mola apasaye kuabdiwa kwa haki isipokuwa Allah.

Na vile vile (Astaghfiru llah, Walaa Haula Walaa Quwwata illaa billaah) ninamtaka msamaha Allah, na hapana Ujanja wala Nguvu isipokuwa kwa Allah.

Basi kwa kusema maneno haya kunapatikana Athari ya ajabu katika kukunjuka Kifua,na kuteremka Utulivu ndani ya Moyo.

Na Uislamu unaniamrisha niwe kwenye kiwango cha juu niwe mbali na yote yanayo poromosha Utu na Utukufu.

Na nitumiE Akili yangu na Viungo vyangu kwa yale niliyo umbiwa kwayo kutokana na kutenda Matendo yenye Manufaa kwenye Dini yangu na Dunia yangu.

Na Uislamu unaniamrisha upole,na Tabia Njema,na mufungamano Mazuri,na kuwafanyia Viumbe Wema kwa kiasi niwezavyo kwa Kauli na Matendo.

Na miongoni mwa mambo makubwa niliyo amrishwa kwayo ni kutokana na haki za Viumbe na haki za Wazazi Wawili,Dini yangu inaniamrisha kuwafanyia wao Wema,na kuwapendelea Kheri wao,na kupupia kuwasaidia,na kuwatangulizia wao Wema,hasa hasa wanapo fikia Uzeeni.

Na ajili hiyo utamuona Mama na Baba kwenye Jamii ya Kiislamu Wapo kwenye Daraja la juu kutokana na kuwaheshimu na kuwatukuza,na kwa Huduma zitokazo Upande wa Watoto Wao,

Kila Wazazi Wawili wanapo fikia Miaka ya Utu Uzima,wanapatwa na Maradhi,au kushindwa basi Watoto wanazidisha kwa wao Wema.

Dini yangu imenifundisha kuwa Wwanamke ana Utukufu wa juu,na anazo Haki Tukufu,

Basi Wanawake katika Uislamu ni Ndugu wa wanaume, na mtu bora kuliko wote ni yule mbora wao kwa mke wake,

Mwanamke wa Kiislamu katika Utoto wake anayo Haki ya kunyonya,na Malezi,na kumfanyie Wema wa kimalezi,na yeye katika wakati ule ni kitulizo cha jicho,na Nitunda la Moyo kwa Wazazi Wake na kwa Ndugu zake.

Na anapo kuwa Mkubwa anakuwa Mwenye kutukuzwa Mwenye kuheshimiwa,ambaye msimamizi wake anakuwa na Wivu juu yake,na anamuhifadhi kwa Malezi yake.

Haridhii anyooshewe Mikono kwa Ubaya,na Ndimi kwa Udhia,wala jicho la hiyana.

Na anapo Olewa linakuwa jambo hilo kwa neno la Allah,na kwa ahadi zake zilizo kuwa Nzito,

Na anakuwa Nyumbani kwa Mume kwa Ujirani ulio Mzuri,

Na ni Wajibu kwa Mume wake kumkirimu,na kumfanyia Wema,na kuto mfanyia Udhia,

Na anapokuwa Mama unakuwa Wema wake umekutanishwa kwa Haki ya Allah-Mtukufu-na kuto mtii na kumfanyia Udhia kumekutanishwa na kumshirikisha Allah,na niuharibifu katika Ardhi.

Na akiwa Dada basi yeye ndiye ambae Muislamu ameamrishwa kumuungia udugu,na kumkirimu,na kumuonea Wivu,

Na akiwa ni Mama Mdogo au mkubwa basi anakuwa ni Daraja la Mama katika kumfanyia Wema na kumuungia Udugu.

Na akiwa ni Bibi au mkubwa kiumri inaongezeka Heshima yake kwa Watoto wake,na Wajukuu zake,na kwa ndugu wote wa karibu,basi Ombi lake si lenye kurejeshwa,na Mtazamo wake si Wenye kupuuzwa.

Na anapokuwa yupo Mbali na Watu wa karibu hawamsogelei au majirani, basi Uislamu unayo haki ya kumuondoshea Udhia, na kuinamisha Macho na mfano wa hayo.

Na haita acha kuwa Jamii ya Kiislamu ikichunga Haki hizi Ukweli wa kuzichunga,kutokana na mambo ambayo yamemfanya Mwanamke kuwa ni Mwenye Thamani na Mazingatio,haipatikani haki hizo kwenye jamii isipokuwa kwa Mwanamke wa Kiislamu.

Kisha Hakika Mwanamke katika Uislamu anayo Haki ya Kumiliki,na Kuajiri,Kuuza,Kununua,na Baki ya Makubaliano,anayo Haki ya Kujifunza,na Kufundisha,Kufanya Kazi,kwa Mambo ambayo hayaendi kinyume na Dini yake,

Isipokuwa kuna Miongoni mwa Elimu ipo ambayo ni Lazima na anapata Madhambi yule Mwenye kuicha awe Mwanamume au Mwanamke.

Na Hakika anayo Mwanamke yale waliyo nayo Wanamume isipokuwa kwa yale aliyo husishwa kwayo kinyume na Wanamume,au kwa yale wanayohusika nayo Wanamume kinyume na Mwanamke kutokana na Haki na Hukumu ambazo zinazo Mkamilisha kila Mmoja kwa Upande ambao ulio bainishwa katika Sehemu zake.

Na Dini yangu yaniamrisha kuwapenda Ndugu Zangu wa Kiume,na Wakike,na Shangazi zangu,na Wajomba zangu.na Mama zangu Wadogo,na jumla ya Ndugu zangu wakaribu,na inaniamrisha kusimamia Haki za Mke wangu,na Watoto Wangu,na Jirani zangu.

Na Dini yangu inaniamrisha kujifunza,na inanihimiza kila kinacho ipanuwa Akili yangu,na Tabia zangu,na kufikiri kwangu.

Na Dini yangu yaniamrisha kuwa na Haya,Upole,Ukarimu,Ushujaa,Hekima,Utulivu,Subira,Uwaminifu,Unyenyekevu,Kujizuia,Kujitakasa,Kutekeleza,na Kuwapendea Kheri Watu,na kufanya Haraka katika kutafuta Riziki,kuwafanyia Upole Masikini,kutembelea Wagonjwa,na kutekeleza Ahadi,na Maneno Mazuri,na kuwapokea Watu kwa Uchangamfuu,na Kupupia kuwasaidia kwa kile Niwezacho.

Na upande mwingine Dini yangu yanitahadharisha kutokana na Ujinga,na inanikataza kunako Ukafiri,kuikataa Haki,na Uwovu,na Machafu,na uZinifu,na kwenda kinyume na Usawa,na Kiburi,Husda,na Kinyongo,na Dhana mbaya,na kujipa Mikosi,na kuhuzunika,na Uwongo,na Kukata Tamaa,na Ubakhili,na Uvivu,na Uwoga,na kuishi bila ya Kazi,na Kukasirika,na Kuharibika Kitabia,na kuwa Mjinga,na kuwakosea Watu,na Maneno Mengi bila Faida,na kutoa Siri,na Hiyana,na kuto Tekeleza Ahadi,na kuto watii Wazazi Wawili,na kukata Udugu,na kuwapuuza Watoto,na kumuudhi Jirani na Viumbe wote kwa Ujumla.

Na Uislamu unanikataza -vile vile- kuto kunywa Vilevi, na kutotumia Mihadarati, na kutocheza Kamari, na Wizi, na udanganyifu na utapeli, na kuwapumbaza Watu, na kuwapeleleza, na kufuatilia Aibu zao.

Na Dini yangu ya Uislamu inahifadhi Mali,na kaitka hilo kuna kueneza Salama na Amani,kwa ajili hii Uislamu umehimiza Uwaminifu,na ukawasifia Waaminifu,na ukawaahidi kuwa na Maisha Mazuri,na kuingia kwenye mabustani Siku ya Mwisho,na ukaharamisha Wizi,na ukamuahidi Mwenye kufanya Vitendo vya Wizi atakuwa na Adhabu Duniani na Siku ya Mwisho.

Na Dini yangu inazihifadhi Nafsi,na kwa hili Uislamu umeharamisha kua Nafsi bila ya Haki,na kuchupa Mipaka kwa Wengine kwa aina yeyote ya kuchupa Mipaka hata kama itakuwa ni Tamshi.

Na Uislamu umeharamisha Mtu kuchupa Mipaka hata kwa Nafsi yake Mwenyewe,Uislamu haukumpa Nafasi Mtu kuiharibu Akili yake,au Aingamize Afya yake,au aiue Nafsi yake.

Na Dini yangu ya Uislamu inadhamini Uhuru,na umedhibiti.

Mtu ndani ya Uislamu yupo Huru katika kufikiria kwake, na katika Kuuza kwake, na katika Kununua kwake, na katika Biashara zake, na katika harakati zake, na yuko Huru katika Kustarehe kwa Vitu Vizuri vya Kimaisha miongoni mwa Vyakula na Vinywaji, na Mavazi, na vya kusikiliza, kwa Muda ambao hajafanya jambo la Haramu madhara yakarudi kwake au kwa Mwingine.

Na Dini yangu imedhibiti Uhuru,Uislamu hauruhusu yeyote kuvuka mipaka kwa mungine,au Mtu aende kwenye starehe za Haramu ambazo zinamaliza Mali zake,na Utukufu wake ,au Utu wake.

Na kama utaangalia kwa wale ambao waliojipa Uhuru wa kila kitu,na wakazipa Nafsi zao kila kinachopendwa na Nafsi kutokana na Matamanio bila ya kuwahofisha Upande wa Dini,au Akili,utawaona kuwa wao wanaishi Chini ya Mashimo ya Ususuavu na Dhiki,na utawaona Baadhi yao wanapenda kujiangamiza,hali ya kutaka kujiondoa kutokana na Msongo wa Mawazo.

Na Dini yangu inanifundisha Tabia Njema katika Kula na Kunywa,na Kulala,na Kuchanganyika na Watu.

Na Dini yangu inanifundisha Ukarimu kwenye Kuuza na Kununua,na kutafuta Haki,

Na inanifundisha Ukarimu kwa wanao kwenda kinyume na Dini,nisiwafanyie Dhulma,na wala nisiwafanyie Makosa,isipokuwa niwafanyie Wema,na nitamani Kheri iwafikie.

Na Historia ya Waislamu inatoa Ushahidi kwa Ukarimu kwa wanao kwenda kinyume na Dini,Ukarimu haukujulikana Kwa Watu walio kuwa kabla Yao.

Hakika waliishi Waislamu na Watu walio kuwa na Dini Tofauti,na wakaingia Chini ya Utawala wa Waislamu,na wakawa Waislamu-pamoja nao-na Miamala Mizuri inayo hitajika kwa Viumbe.

Kwa ujumla Hakika Uislamu umenifundisha kuwa na Adabu,na Miamala Mizuri,na Tabia Njema ambazo zinazo ng'arisha Maisha yangu na kutimia kwa Furaha yangu,

Na Uislamu umenikataza kunako kila kinacho kuwa ni kikwazo katika Maisha yangu,na kueleta Madhara kwenye Muonekano wa Kijamii,au Nafsi,au Akili,au Mali,au Utukufu,au Heshima.

Na kwa kiasi cha kuchukuwa Mafunzo yale basi Utukufu wangu unakuwa Mkubwa,

Na kwa kiasi cha kuchupa kwangu Mipaka na kupunguza kitu katika yale niliyo fundishwa inapunguza Utukufu wangu kwa kiasi cha kupungua yale Mafundisho.

Na wala hakusudii kuwa yale yaliyo pita kuwa Mimi nimehifadhika sikosei,na wala sipunguzi,Dini yangu inachunga Mwenendo wangu wa Kiutu,na Udhaifu kwa baadhi ya Nyakati,basi inapatikana kwangu Makosa,na Mapungufu,na kupunguza,kwa Ajili hii Uislamu ukanifungulia Mlango wa Kutubia,na Kuomba Msamaha,na Kurejea kwa Allah,na Kutubia Kunafuta Mabaki ya Mapungufu yangu,na kunanyanyua Nafasi yangu mbele ya Mola wangu.

Na kila Mafundisho ya Dini ya Kiislamu kutokana na Itikadi,na Tabia,na Adabu,Miamala,Vyanzo vyake ni Qur'ani Tukufu na Suna zilizo Safi.

Na Mwisho ninasema kwa kutilia Mkazo: Laiti Kama kila mwanadamu angelitazama katika kila Sehemu yoyote ndani ya Dunia juu ya uhalisia wa Dini ya Kiislamu kwa jicho la Uadilifu na Upembuzi isinge muwezekania isipokuwa angeukubali Uislamu, na Tatizo ni kuwa Dini ya Uislamu inachafuliwa na walinganizi waongo, au Matendo ya baaadhi ya wale wanaojinasibisha na Uislamu Miongoni mwa wale ambao Uislamu unachukuliwa kupitia wao.

Na kama yeyote angelitazama Uhakika wa Uislamu kama ulivyo,au Hali za Waislamu walio Simama kwa Ukweli basi asingelitatizika katika Kuukubali Uislamu,na Kuingia Ndani ya Uislamu,

Na itambainikia kuwa Uislamu unawataka Watu kwenye Utukufu wa KibinaADAM,na kuunganisha Salama na Amani,na kueneza Uwadilifu na Wema.

Na kwenda kinyume na Uislamu kwa baadhi ya Wale wanao jinasibisha na Uislamu-kwa uchache au wingi-haifai kwa namna yeyote idhaniwe kuwa ndio Dini,au Dini ikaabishwa,isipokuwa Uislamu Upo Mbali na hayo,

Na kinacho Fuatia kwa wale wanaokwenda kinyume na Uislamu kinarudi kwa wao wenyewe,kwani Uislamu haujamrisha hayo,isipokuwa Uislamu umewakataza na umewakemea kuto kwenda kinyume na yote yaliyo kuja na Uislamu.

Kisha ahakika Uadilifu unatakikana kwa kutazama hali za wale walio Simama Madhubuti kwa Dini Ukweli wa Kusimama,na wale wanao tekeleza Maamrisho yake na Hukumu zake wao Wenyewe na kwa wengine,Hakika kwa hilo Nyoyo zinajaa Utukufu na Utulivu kwa Dini hii na Watu wake,

Na Uislamu haukuacha Dogo wala Kubwa katika Maelekezo na Kuadabisha isipokuwa umehimiza hayo, na Hakuna Udhalili wala uharibifu isipokuwa Umekemea, na ukazuia Njia zake.

Na kwa Ajili hiyo wakawa wale Wenye kuheshimu Jambo la Uislamu,wenye Kusimamisha Alama za Uislamu ni Watu Watukufu,na wapo Tabaka la Juu kutokana na Adabu za Nafsi,na kuzilea katika Malezi Mazuri yenye Kuheshimika,na Tabia Nzuri,Mambo hayo yanaonekana kwa aliye Mbali na alie Karibu,na Mwenye kukubali na Asie kubali.

Ama kwa kiasi cha kutazama Hali za Waislamu walio punguza Haki za Dini yao,walio jitoa katika Njia iliyo ya Sawa-Hakuna chochote katika Uwadilifu,isipokuwa ni Dhulma ya Wazi.