فضل الإسلام
(فضل الإسلام) هو رسالة مختصرة من تأليف الإمام محمد بن عبد الوهاب، تهدف إلى توضيح أهمية الالتزام بالإسلام والتمسك بتعاليمه. يستعرض الشيخ في هذه الرسالة مفهوم الإسلام، وأركانه، وأهمية اتباع السنة النبوية، محذراً من الابتعاد عن الصراط المستقيم واتباع البدع والشبهات. يستشهد الإمام بالأدلة من الوحيين القرآن والسنة لتعزيز حججه، مشيراً إلى أن الإسلام هو الدين الحق الذي ارتضاه الله لعباده، وأن أي دين آخر لن يُقبل في الآخرة. الرسالة تخاطب المسلمين لتذكيرهم بضرورة العودة إلى الدين الصحيح والابتعاد عن التفرق والاختلاف الذي يؤدي إلى ضعف الأمة وضياعها.
Ubora wa uislamu
Imamu Muhammad Ibnu Abdil Wahaab.
Mlango wa Ulazima wa Kuufuata Uislamu.
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na Mwenye kutafuta dini isiyokuwa dini ya Kiislamu, ambayo ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kumpwekesha na kumfuata kwa kumtii na kumdhalilikia, na kwa Mtume wake aliye Nabii wa mwisho Muhammad, Rehema za Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa kumuamini na kumfuata na kumpenda kwa dhahiri na kwa siri, basi hiyo haitakubaliwa kwake, na yeye Akhera atakuwa ni miongoni mwa wenye kupata hasara ambao walizifanyia ubahili nafsi zao kwa kuzinyima mambo yenye kuzinufaisha". [Al-Imran: 85]. Na kauli ya Allah Mtukufu: «Na miongoni mwa mambo aliyowausia Mwenyezi Mungu ni kwamba huu Uislamu ndio njia ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, iliyolingana sawa. Basi ifuateni wala msifuate njia za upotevu zikawatawanya na kuwaepusha na njia ya Mwenyezi Mungu iliyolingana sawa. Muelekeo huo upande wa njia nyoofu, ndio Aliowausia nao Mwenyezi Mungu ili mjikinge na adhabu yake kwa kuyatekeleza maamrisho yake na kijitenga na makatazo yake.» (Al-An'am) [1]. Al Imran: 85 [2]. Al An'am: 153.
Amesema Mujaahidi: neno Al- subulu: maana yake ni Uzushi na mambo yenye kutatiza
Na imepokelewa kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake -kwamba Mtume wa Mweyezi Mungu-Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- amesema: {Yeyote atakayezua katika jambo letu hili (Dini yetu hii) jambo ambalo siyo katika dini hii basi atarejeshewa jambo hilo alilolizua} [3] Na katika Tamko lingine: "Yeyote atakaye fanya ibada ambayo hayapo katika dini yetu basi atarejeshewa" [3] Ameitoa hadithi hii Imamu Bukhaariy katika mlango wa Sulhu (2050) na Imamu Muslimu katika mlango wa Hukumu, (1718), na Abuu Daudi katika mlango wa sunnah,(4606), na Ibnu Majjah katika utangulizi, (14) na Ahmad (6/256) . (4) Ameitoa hadithi hii Imamu Bukhaariy katika mlango wa Sulhu (2050)na Imamu Muslimu katika mlango wa Hukumu, (1718), na Abuu Daudi katika mlango wa sunnah,(4606), na Ibnu Majjah katika utangulizi,(14) na Ahmad (6/256) .
Na amepokea Imamu Bukhariy kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: amesema: Mtume Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Umma wangu wote wataingia peponi isipokua atakaye kataa, akaulizwa ewe Mtume ni nani atakaye kataa? akajibu mwenye kunitii ataingia peponi na mwenye kuniasi atakuwa amekataa" [5]. (5) Imamu Bukhariy ameitoa hadithi hiyo katika kitabu kinachozungumzia kushikamana na kitabu na sunnah (6851) na Imamu muslimu katika kuzungumzia Uongozi (1835), na Ahmad,(2/361).
Na imepokelewa kutoka kwa Ibnu Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na baba yake -kwamba Mtume wa Mweyezi Mungu-Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- amesema: { Watu wanaochukiwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni watu watatu: mpagani aliyeko katika mji mtukufu wa Makkah, na mwenye kufuata na kupenda idumu katika uislamu mienendo ya kijinga (zama za ukafiri) isiyokuwa katika dini, na mwenye kutafuta damu ya muislamu pasina haki kwa lengo la kumwaga damu ya muislamu mwenzake} [6] Imepokelewa na Al-Bukhaariy Na huangukia na kuingia katika mambo ya kijaahilia (kabla ya uislamu) kwa ujumla au kwa jambo mojamoja, yaani mambo ya kijaahilia huwa kwa baadhi ya watu na wakati mwingine hayawi tu kwa baadhi ya watu, yaweza yakawa ni kutoka kwa mayahudi au kwa wenye kuabudu masanamu au kutoka kwa wasiokuwa hao waliotajwa miongoni mwa kila mwenye kwenda kinyume na mafundisho ya Mitume. Kutoka kwa Imamu Bukhariy katika kitabu cha Dia(6488)
Na katika sahihi Bukhariy imepokelewa kutoka kwa Hudhaifa -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Enyi kongamano la maulamaa na wajuzi wa kitabu na sunnah, kuweni na msimamo wa kukishika kitabu na sunna, kwa hakika mmetanguliwa katika hilo kutanguliwa kulikokuwa wazi, na ikiwa mtakwenda kinyume na amri hiyo mkapinda kulia au kushoto mkaacha msimamo uliokuwa sawa wa kushika kitabu na sunna mtakuwa mmepotea upotevu uliokuwa mbali na haki.
Na imepokelewa kutoka kwa Muhammad ibnu wadh'hi, alikuwa akiingia msikitini husimama katika halaqa ( mkusanyiko duara) na husema kwa kukumbusha na akasema: Ametupa habari ibnu Uyainah, kutoka kwa mujaalid ibnu shaabiiy, kutoka kwa masrook ,amesema abdullahi ibnu mas'uud, hautakuwa mwaka isipokuwa utakuja baada yake mwaka ambao una shari zaidi, na sisemi kuwa mwaka huu ni mzuri kimavuno kuliko mwaka mwingine, na wala kiongozi bora kuliko kiongozi mwingine, lakini nakusudia kuondoka maulamaa wenu na wabora wenu, kisha watazuka watu wanapima mambo kwa rai zao na huangamiza uislamu na kuupasua.
Mlango wa maana ya Uislamu.
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kama makafiri wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata}.((7)) (Al-imraan 20) [7]. Surat Al Imran:20
Na imepokelewa kutoka kwa Ibnu omar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na baba yake -kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu-Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- amesema: (Uislamu ni kushuhudia ya kwamba hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah Mmoja na kwamba Muhammad ni Mjumbe wa Allah, na kusimamisha Swala na kutoa Zaka, na kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhan, na kwenda kuhiji Makkah kwa mwenye uwezo) [8] [8] Ameipokea Imamu muslimu katika Mlango wa Imani (8) ,na Tarmidhiy katika kitabul Iman (2610),na Nasaai katika Mlango wa Imani na sheria zake (4990), na Abuu Daudi katika Mlango wa Sunnah (4695),na Ibnu Maajah katika muqaddimat (63),na Ahmad (1752).
Na kutoka kwa Abuu Hurayra-Radhi za Allah ziwe juu yake-katika hadithi marfu'u: (Muislamu (wa kweli) ni yule ambaye wamesalimika Waislamu kutokana na ulimi wake na mkono wake), [9]. [9] Ameipokea Imamu Tirmidhiy katika Mlango wa Iman (2627),na An'saai mlango wa Iman na sheria zake (4995) ,na Ahmad (2/379).
Na kutoka kwa Bah'zi Ibnu Hakiim kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake, yakuwa yeye alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- akasema: "Kuwa Uislamu ni kuusalimisha moyo wako kwa Mwenyezi Mungu, na kuuelekeza uso wako kwa Mwenyezi Mungu, na Kusali sala zilizofaradhishwa, na kutoa zakah iliyofaradhishwa) [10]. Imepokelewa na Ahmad [10] Na Imamu Nasaai katika mlango wa Zakah (2436), na Ahmad (5/3).
Na imepokelewa kutoka kwa Abii Qalaabat kutoka kwa Amru Ibnu Abasat kutoka kwa mtu katika watu wa Sham kutoka kwa Baba yake (yakuwa Baba yake alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Ni nini uislamu? Akasema: Uislamu ni kuusalimisha moyo wako kwa Mwenyezi Mungu, na wasalimike waislamu na ulimi wako na mikono yako, Akasema: Ni upi Uislamu bora? Akasema: Ni Imani, Akasema: Na ni nini Imani? Akasema:Imani ni kumuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na kufufuliwa baada ya kufa) [11]. [11] Ameipokea Ahmad (4/114)
Mlango Kuhusu kauli ya Mwenyezi Mungu "Na Anayetaka isiyokuwa dini ya uislamu Basi haitokubaliwa kwake, naye Akhera atakuwa katika wenye hasara"
Na kutoka kwa Abuu huraira-Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: Amesema mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake . "Yatakuja matendo siku ya kiyama, na itakuja sala na kusema: Ewe Mola wangu mimi ndio Sala, basi Mwenyezi Mungu ataijibu kwa kusema: Hakika wewe upo katika Kheri, kisha itakuja Funga na ataiambia: Hakika wewe upo katika Kheri, Kisha yatakuja matendo kwa namna hiyo na atayaambia; Hakika nyinyi mpo katika kheri, kisha utakuja uislamu na useme: Hakika wewe ni Amani na mimi ni uislamu, basi Mwenyezi Mungu atauambia: Hakika wewe upo katika kheri, kisha atasema Mwenyezi Mungu: kutoka kwako leo ninachukua na kutoka kwako ninatoa. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na anayetaka isiyokuwa dini ya uislamu Basi haitakubaliwa kwake, naye Akhera atakuwa miongoni mwa wenye hasara" [Al-Imran: 85]. Imepokelewa na Ahmad [12]. Al Imran: 85
Na katika sahihi kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake -kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: "Atakaye fanya ibada ambayo haipo katika dini yetu basi atarejeshewa" [13] Imepokelewa na Ahmad [13] Ameitoa hadithi hii Imamu Bukhariy katika mlango wa Sulhu (2050) na Imamu Muslimu katika mlango wa Hukumu, (1718), na Abuu Daudi katika mlango wa sunnah, (4606), na Ibnu Majjah katika utangulizi,(14) na Ahmad (6/256).
Mlango wa Wajibu wa kutosheka na kumfuata Mtume -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na kujiaepusha na kila yasiyokuwa mafundisho yake.
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na tumekuteremshia Kitabu hiki kinacho bainisha kila kitu}. (An Nahli 89) [14]. Al Nahli: 89.
Ameipokea Imamu Nasaai na wengine kutoka kwa Mtume -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa yeye aliona katika mkono wa Omar ibnul khattwab -Radhi za Allah ziwe juu yake- kipande cha Karatasi ya Taurat akasema: {Lau kama Nabii Mussa angelikuwa hai asingekuwa na namna yoyote isipokuwa kunifuata mimi} [15] Akasema Omar: Nimeridhia kuwa Mwenyezi Mungu ni muumba na uislamu ni dini na Muhammad ni Mtume. [15] Ameipokea Imamu Ahmad (3/387),na Al-daaramiy katika utangulizi (435)
Mlango unaohusu kutoka na kuacha kuulingania uislamu
Na kauli ya Allah Mtukufu: {Yeye Mwenyezi Mungu alikuiteni waislamu tangu katika vitabu vya zamani huko na katika Qur'an } [16] (AL- Hajj: 78) [16]. (Al Haji: 78).
Imepokelewa kutoka Al- haarith Al-ash'ariy- Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume- Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: "Ninakumrisheni mambo matano ambayo Mwenyezi Mungu ameniamrisha mimi mambo hayo, Kusikiliza na Kutii, na Kupigana Jihadi, na Kuhama, na kushikamana na umoja, kwa hakika yeyote atakaye tengana na umoja kiasi kidogo, hakika mtu huyo ameondoa kitanzi cha uislami katika shingo yake isipokuwa atakaporudi katika uislamu, na yeyote atakaye lingania mambo ya kijaahilia (kuomboleza na kupiga mashavu na kupasua pasua nguo kunusuriana kiukabila) hakika mtu huyo atakuwa miongoni mwa watakaoingia motoni, Akasema mtu mmoja: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu hata kama atasali na kufunga? Akasema: hata kama atasali na kufunga, basi muombeni Mwenyezi Mungu ambaye amekuiteni nyinyi Waislamu na Waumini kwa jina la waja wa Mwenyezi Mungu. Ameipokea hadithi hii Ahmad na Tirmidhiy,na akasema : ni Hasani na ni sahihi [17] Al-tirmidhiy katika kitabu- Al- amthaal (2863), Ahmad (4/130).
Na katika Sahihi: "Yeyote atakaye tengana na umoja kiasi kidogo, basi kifo chake kitakuwa cha kijahili (kijinga) [18] na ndani yake kuna kauli isemayo (Hivi mnalingania mambo ya kijinga hali yakuwa mimi nipo mbele yenu?) Amesema Abul Abbas: Kila kinachotoka nje ya wito wa uislamu na Qur'ani ikiwemo unasaba au utaifa au Jinsia fulani au Madhehebu fulani au njia fulani, basi hayo yote ni katika kujinasibisha na mambo ya kijinga, Bali walipogombana Muhaajir (mtu wa Makkah) na Answar (mtu wa Madinah), akasema Muhajir enyi watu wangu wa Makkah, na akasema Answaar Enyi watu wangu wa Madinah! Akasema Mtume- Rehema na amani za Allah ziwe juu yake- (Hivi mnaitana kwenye mambo ya kijinga hali yakuwa mimi nipo mbele yenu?) Na akakasirika kwa jambo hilo sana. Mwisho wa kunukuu. [18] Ameitoa Imamum Bukhari katika Mlango wa Fitna (6646), na Muslimu katika Imarat (1849), Ahmad (1/297), Al-daramiy katika Al-sairy (2519).
Mlango unaozungumzia uwajibu wa kuingia katika hukumu za Uislamu Jumla jumla, na kuacha mambo yasiyokuwa ya uislamu.
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: { Enyi mlioamini ingieni kwenye hukumu za uislamu zote } [19] (Al-baqara: 208) Na kauli ya Allah Mtukufu: { Hivi hukuwaona wale wanaodai kuwa wao wameamini yale yote yaliyoteremshwa kwako na yaliyotemshwa kwa manabii waliokuwepo kabla yako?} [20] (An-nisaa ) Aya 60. Na kauli ya Allah Mtukufu: "Siku ambayo nyuso zitakuwa nyeupe na nyuso zingine zitakuwa nyeusi". [Al-Imran: 106]. Amesema Ibnu Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- zitakuwa nyeupe nyuso za watu wa sunna na wenye kushikamana kuwa kitu kimoja, na zitakuwa nyeusi nyuso za watu wa Bid'aa na kufarakana. [19]. Al Baqara: Aya ya: 208. [20]. Al Nisaa: Aya ya: 60. [21]. (Surat Al Imran1060
Na imepokelewa kutoka kwa Abdillahi Ibnu Omar- Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: amesema: Mtume Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake:- "Wataleta Umma wangu mambo waliyoyaleta mayahudi na manaswara kidogo kidogo hatua kwa hatua, hata kama kulikuwa katika hao mayahudi na manaswara aliyemuingilia mama yake hadharani basi kutakuwa na watu katika umma wangu watakaoiga na kufanya hivyo, na kwa hakika wana wa Israail walitofautiana mpaka kufikia makundi sabini na mbili [22] Na ukamilifu wa hadithi ni maneno yake aliposema: (Na utatofautiana Umma huu mpaka utafikia makundi sabini na tatu, na makundi yote hayo yataingia motoni, isipokuwa kundi moja tu -wakasema: ni kundi gani hilo ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema: ni lile kundi ambalo ni langu mimi na maswahaba wangu ) [23] Ni uzuri ulioje wa mawaidha yanayoafikiana na maisha kutoka nyoyoni?, Ameipokea Tirmidhiy na wameipokea vilevile kutoka kwa muaawiywah kutoka kwa Ahmad na Abuu daudi na ndani yake kuna: (Hakika watatoka katika umma wangu watu ambao watatiwa matamanio ya nafsi (Uzushi) kama inavyoingia sumu ya mbwa mwenye kichaa kwa aliye ng'atwa, na haitobakia sehemu katika mwili wake wala kiungo chochote isipokuwa kitaingiliwa na sumu hiyo) Na imekwisha tangulia neno lake (Na mwenye kufuata katika uislamu mwenendo wa kijinga). [22] Ameipokea Imamu Tirmidhiy katika mlango wa Imani (2641) [23] Ameipokea Imamu Tirmidhiy katika mlango wa Imani (2641)
Mlango uliokuja kuzungumzia kuwa Uzushi (Bid'aa) ni mbaya zaidi kuliko madhambi makubwa.
Kwa maneno yake Mwenyezi Mungu aliyetukuka na Mwenye nguvu:- (Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe Madhambi ya kushirikishwa naye, na husamehe madhambi mengine yote yasiyokuwa ushirikina kwa anayemtaka) [24] (Al- nisaa :48) Na kauli ya Allah Mtukufu: "Mwisho wao utakuwa ni kuzibeba dhambi zao kamili siku ya Kiyama, hawatasamehewa chochote, na watazibeba dhambi za wale waliowadanganya ili kuwaepusha na Uislamu, bila ya kupunguziwa dhambi zao. Jueni mtanabahi, ni ubaya ulioje wa dhambi watakazozibeba!" [An Nahli:25]. [24]. Al Nisaa: Aya ya: 48. [25]. Al Nahli: 25.
Na katika Sahihi Al-bukhariy kuwa yeye Mtume- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Alisema kuhusu Khawaariji: {Popote Muwakutapo wauweni} [26]. [26] Al-bukhariy, katika kitabu cha Al-manaaqib (3415), Muslim katika mlango wa zakkah (1066,An- nasaaiy katika mlango wa kuharamisha damu (4102), Abuu Daud katika mlango wa Sunnah(4767),Ahmad,(1/131).
Na ndani yake, ni Kuwa Mtume alikataza kuwaua viongozi majeuri ikiwa watatekeleza swala.
Imepokelewa kutoka kwa Jaabir Ibnu Abdillahi kuwa mtu mmoja alitoa sadaka kisha watu wakamuiga katika utoaji wake wa sadaka basi akasema Mtume- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- (Yeyote Mwenye kufufua Sunnah katika uislamu, basi mtu huyo atapata malipo na malipo ya aliyeifanyia kazi sunnah hiyo baada yake, pasina kupunguzwa malipo yao hata kidogo, na yeyote atakaye anzisha katika uislamu mwenendo mbaya (Uzushi) Basi hubebeshwa dhambi zake na dhambi za yule aliyeufanyia kazi uzushi huo, pasina kupunguzwa katika mizigo yao hata kidogo} [27] Imepokelewa na Imamu Muslim [27] Muslim katika Mlango wa zakkah (1017), na Tarmidhiy katika mlango wa Imani (2675)An- nasaai katika mlango wa Zakkah (2554), ibnu maajah (203) na Ahmad(203). Ahmad (4/359) Al-daramiy katika mlango wa Muqddimat (514)
Na ana hadithi nyingine kutoka katika hadithi ya Abii Huraira na tamko lake ni: {Yeyote Mwenye kulingania katika uongofu- kisha akasema-Yeyote mwenye kulingani katika upotevu} [28]. [28] Muslimu katika mlango wa Elimu (2674,Al-trmidhiy) katika mlango wa Elimu (2674), Abuu daud katika mlango wa Sunnah (4609),Ahmad (2/367), Al-daaramiy katika Utangulizi (313).
Mlango uliokuja katika kuelezea kuwa Mwenyezi Mungu amezuia toba kwa mtu wa Bid'a.
Hii imepokelewa kutoka katika hadithi ya Anas kutoka katika Hadith Mursal zenye daraja la Hasan.
Na ametaja Ibnu Wadhwahi kutoka kwa Ayoub Amesema: Tulikuwa tuna mtu anaona Rai kisha akaiacha rai ile, nikamuendea Muhammad Ibnu Siiriin nikamwambia: hivi wajua kuwa fulani kaiacha rai yake? Akasema: angalia namna atakavyobadilika? Hakika Hadithi nyingine ifuatayo ni kali zaidi dhidi yao kuliko ya mwanzo: Na hadithi yenyewe ni pale Mtume aliposema {Wanachomoka katika uislamu? kisha hawarudi katika uislamu} [29] Na aliulizwa Ahmad Ibnu Hambal kuhusu maana yake akasema : kuwa maana yake hakubaliwi toba. [29] Ameipokea Imamu Bukhariy katika mlango wa Tauhid (6995), na Imamu Muslimu katika mlango wa Zakah (1064), na An-nasai katika mlango wa Zakkah (2578),Abuu daud katika mlango wa Sunnah (4764, Ahmad ) (3/68).
Mlango wa maneno ya Mwenyezi Mungu" Enyi Mliopewa kitabu kwanini mnabishana na Ibrahiim"
Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Enyi mliopewa Kitabu -mayahudi na manaswara- kwanini mnabishana na Ibrahiim} [30] [Al-Imran: 65]. Mpaka katika kauli yake: {Na hakuwa ni miongoni mwa washirikina} [31] [Al-Imran: 67]. Na kauli yake: {Hakuna yeyote anayeipa mgongo Dini ya Ibrahim, nayo ni Uislamu, isipokuwa safihi aliye mjinga. Na hakika tulimchagua Ibrahim duniani kuwa Nabii na Mtume, na kesho Akhera kuwa ni miongoni mwa watu wema ambao wana daraja za juu kabisa}. [Al Baqara: 130]. Na ndani yake kuna hadithi inayowahusu makhawaarij na imekwishatangulia, na kuna ndani yake kuwa Mtume- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: {Vipenzi vya Baba fulani siyo vipenzi vyangu, kwa hakika vipenzi vyangu ni wachamungu} [33], Na ndani yake vilevile kutoka kwa Anas yakuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Alielezwa kuwa baadhi ya maswahaba mmoja wao alisema: mimi sili nyama, na mwingine akasema: Ama mimi nitasimama na wala sitolala, na mwingine akasema: Ama mimi nitafunga na wala sitofungua, Akasema Mtume -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- {Lakini mimi Mtume ninasimama na ninalala, na ninafunga swaumu na kufungua na ninaoa wanawake, na ninakula nyama basi yeyote atakaye ichukia sunnah yangu basi mtu huyo si katika wenye kunifuata mimi } [34], Basi zingatia ikiwa baadhi ya Maswahaba walitaka kujitenga katika kufanya ibada (na kuacha mambo mengine) wakaambiwa maneno haya mazito, na kikaitwa kitendo hicho ni kuichukia sunnah, je unaonaje kwa bid'a nyingine isiyokuwa hii?!, au waonaje kama atakayefanya Bid'a kuwa ni mtu mwingine asiyekuwa swahaba? [30]. Surat Al Imran: 65. [31]. Surat Al Imran: 67 [32]. Al Baqara: Aya ya: 130. [33] Al-bukhaiy katika mlango wa Adabu (5644), Muslimu katika mlango wa Imani (215), Ahmad (4/285). [34] Al-bukhariy mlango wa Ndoa (4776) Muslimu (1401) An-nasai Ndoa (3217),Ahmad (3/285).
Mlango wa maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu "Basi elekeza uso wako katika dini takasifu"
Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Basi simamisha uso wako, ewe Mtume, wewe na waliokufuata na uendelee kwenye msimamo wa dini ambayo Mwenyezi Mungu amekuwekea, nayo ni Uislamu ambao Mwenyezi Mungu ameufanya ulingane na maumbile ya watu. Basi kuendelea kwenu kubaki kwenye Uislamu, na kushikamana kwenu nao ni kushikamana na umbile la Mwenyezi Mungu la kumuamini Mwenyezi Mungu peke yake. Hapana ugeuzaji wa uumbaji wa Mwenyezi Mungu na Dini yake, kwani hiyo ndiyo njia iliyonyooka yenye kupelekea kwenye radhi za Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe wote, na Pepo yake. Lakini wengi wa watu hawajui kuwa yale niliyokuamrisha nayo, ewe Mtume, ndiyo Dini ya haki na si nyigine}. [Ar rum: 30]. [35]. Al Ruum: 30.
Na kauli ya Allah Mtukufu: "Na Ibrāhīm na Ya’qūb waliwahimiza watoto wao kusimama imara juu ya Uislamu wakiwaambia, “Enyi watoto wetu! Mwenyezi Mungu Amewachagulia Dini hii, nayo ni Uislamu, Msiiache muda wa uhai wenu, na msifikiwe na mauti isipokuwa na nyinyi mko kwenye Dini hii.” (Al-baqara: 132) Na kauli yake Mtukufu: {Kisha tukakuletea wahyi, ewe Mtume, kwamba uifuate dini ya Uislamu kama alivyoifuata Ibrāhīm na kwamba ulingane juu yake na usiiepuke, kwani Ibrāhīm hakuwa ni miongoni mwa wale wanaowashirikisha wengine pamoja na Mwenyezi Mungu}. [An Nahli: 123]. [36]. Al Baqara: Aya ya: 132. [37]. Al Nahli: 123.
Na kutoka kwa Ibnu Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: {Hakika kila Mtume ana vipenzi katika Manabii na mimi kipenzi changu katika hao manabii ni baba yangu Ibrahim na Ibrahim ni kipenzi cha Mola wangu} [38] Kisha akasoma: {Hakika waliokaribu zaidi na Ibrāhīm na wanaohusika naye zaidi ni wale waliomuamini, wakausadiki Utume wake na wakaifuata dini yake na huyu Mtume, -rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na waliomuamini yeye. Na Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa wenye kumuamini yeye na kufuata Sheria Yake} [39]. [Al-Imran: 68]. Kaipokea Imamu Tirmidhiy [38] Ameitoa Tirmidhiy katika tafsiri ya Qur'an (2995) ,na Ahmad (1/430) [39]. Surat Al Imran: 68
Na kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- "Hakika Mwenyezi Mungu hatazami katika mili yenu wala katika sura zenu, lakini anaangalia katika nyoyo zenu na matendo yenu" [40]. [40] Muslimu katika mlango wa wema na kuunga udugu na Heshima (2564)
Na kutoka kwa Ibnu Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: {Mimi nitawatangulia kunywa katika mto Kauthar na watainuliwa na kuletwa kwangu watu miongoni mwa watu wa umma wangu mpaka nikifikia karibu ili niwanyweshe patawekwa kizuizi kati yangu na wao, Na nitasema: Ewe Mola wangu hawa ni watu wangu, na ataambiwa Hakika wewe hujui ni kitu gani walizua baada yako} [41]. [41] Kaitoa Bukhariy katika mlango wa fitina, Na muslimu katika mlango wa Fadhila (2297), na Ibnu Majah katika mlango wa Ibada (3057), na Ahmad (5/393)
Na katika Sahihi Al-Bukhari na Muslim pia kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema: {Natamani mimi kama ningeliwaona ndugu zetu, wakasema: Hivi kwani sisi si ndugu zako ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu? Akasema Mtume: Nyinyi ni Maswahaba zangu, ndugu zangu bado hawajaja, wakasema: unamjuaje ambaye bado hajazaliwa katika umma wako? Akasema: mwaonaje kama mtu angekuwa ana Farasi mwenye alama usoni na miguuni akachanganyikana na Farasi wenye alama nyeusi ya asili je asingeweza kumjua farasi wake? Wakasema: kwanini asimjue farasi wake! Akasema Mtume Hakika wao watakuja wakiwa wanag'aa paji za nyuso zao na miguu yao kwasababu ya udhu, na mimi nitawatangulia kunywa katika mto Kauthar, tambueni vyema kuwa, hakika watafukuzwa watu siku ya kiama katika mto Kauthar kama wanavyofukuzwa Ngamia waliopotea Jangwani, nitakuwa nikiwaita, Jamani, njooni!!! Basi kutasemwa: Hakika hawa walizusha na wakabadilisha baada yako, Hapo nitasema: sogeeni na kaeni mbali nami}. [42] Al-bukhariy mlango wa unywesheleaji (2238),na Muslimu katika Mlango wa twahara (249 An -nasaai (150), Abuu Daudi katika mlango wa jeneza (3237), Ibnu Maajah katika mlango wa zuhud (4306), na Ahmad (2/300), Maalik katika mlango wa Twahara (60).
Na kutoka kwa Bukhariy: {Wakati nikiwa nimesimama katika (Kauthar) mara likatokea kundi, mpaka nikalijua ni watu katika umma wangu, akatokea mtu kati yangu na wao (Malaika) akasema: kuwaambia watu hao: Njooni na fanyeni haraka, nikasema: unawaita kuwapeleka wapi huko mbali nami? na wao ni katika umma wangu? Akasema Malaika: Nawapeleka motoni, na ninamuapa Mwenyezi Mungu nitawachukua kuwapeleka motoni, Nikasema: wamefanya nini mpaka wapelekwe motoni? Akasema Malaika: Hakika wao waliritadi na wakaacha dini yao baada yako na wakarudi nyuma na wakafanya kama walivyofanya waliokuwa kabla yao, mara ghafla tena kundi lingine likatokea, Akasema Mtume: sioni kama kuna yeyote katika kundi hili atapona na kufika katika Kauthari isipokuwa atakuwa kama Ngamia aliyeachwa bila mchungaji, na ni wachache sana ambao watafika katika kauthari na kuepukana na moto} [43]. [43] Al- bukhariy Al-riqaaq (6215).
Na imepokelewa kutoka kwao wawili (Bukhari na Muslimu) kutoka katika hadithi za Ibnu Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na Baba yake- {Na nitasema kama alivyosema mja mwema: "Na nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao, na uliponikamilishia muda wangu wa kuishi, wewe ukawa mchungaji juu yao, na wewe juu ya kila kitu ni shahidi} [44] Suratul Maidah (117) [44]. Maidah, mpaka mwisho wa Aya 117.
Na kutoka kwao wawili wameipokea kutoka kwake mar'fuu "Hakuna anayezaliwa isipokuwa anazaliwa katika maumbile, basi wazazi wake ndio wanaomfanya kuwa Myahudi au Mkristo, au Mmajusi, kama anavyozalishwa mnyama mwenye ulemavu, je hua mnahisi kuwa ndani yake kunaweza kuwa na aliyekatika pua" [45] Kisha akasoma Abuu Huraira: {Ndilo umbile la Mwenyezi Mungu alilo waumbia watu} [46], [Ar rum: 30]. Wamekubaliana Bukhari na Muslim. [45] Al- bukhariy mlango wa Jeneza (1292), Muslim mlango wa Qadar (2658) Al-tirmidhiy mlango wa Qadar (2138) Abuu Daudi mlango wa sunnah (4714), Ahmad (2/315), Maalik mlango wa Jeneza (569). [46]. Al Ruum: 30.
Kutoka kwa Hudhaifa Radhi za Allah ziwe juu yake alisema: {Walikuwa watu wakimuuliza Mtume -Rehema na amani za Allah ziwe juu yake- mambo ya kheri, na mimi nilikuwa nikimuuliza mambo ya shari kwa kuhofia yasinipate, nikasema: ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, sisi tulikuwa ni watu wajinga na wenye shari, akatujia Mwenyezi Mungu na hii kheri, je baaada ya kheri hii kuna shari? Akasema ndiyo. Nikasema: je baada ya hiyo shari kuna kheri? Akasema: "Ndio, na kutakuwa na moshi, nikasema: Na ni nini huo moshi? Akasema: "watu watafuata mwenendo usiokuwa wangu na watafuata muongozo usiokuwa wangu, utawatambua lakini utakataa kama si wao", nikasema: je baada ya hiyo kheri kutakuja tena shari? Akasema: "Ndiyo, kutakuja fitina isiyoona (kumba kumba) na kutakuja walinganiaji watakaokuwa wakilingania katika milango ya kuwaingiza watu motoni, atakaye waitikia watamuingiza motoni", nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hebu tupe sifa zao, Akasema : "Ni watu wetu na wanaongea lugha yetu", nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu unaniamrisha nini ikiwa nitafikia wakati huo? Akasema Mtume: "Shikamana na umoja (jamaa) ya waislamu na kiongozi wao", Nikasema: na kama hapatakuwepo na umoja wala kiongozi? Akasema: "Basi jiepushe na hayo makundi yote, hata kama utang'ang'ania shina la mti mpaka yakufikie mauti na wewe umeng'anga'nia katika shina hilo}" [47] Hadithi hiyo wameitoa Bukhariy na Muslimu: {Kisha kinafuata kitu gani?} Akasema: Atatokea Dajjali akiwa na mto na Moto, basi atakayeangukia katika Moto wake atakuwa amepata malipo yake", Nikasema: kisha nini tena kifuatacho? Akasema: "Hapo ndiyo kusimama kiama} [48] Amesema Abuul Aaliyah : Jifunzeni uislamu na mtakapoujua basi msiuchukie, na shikamaneni na njia iliyonyooka kwani huo ndio uislamu, na wala msitetereke mkaenda kulia au kushoto na mkaiacha njia iliyonyooka, na shikamaneni na Sunna ya Mtume wenu, na jiepusheni na haya matamanio ya nafsi (Bid'a). Mwisho. [47] Al-bukhariy mlango wa Manaaqib (3411), Muslimu mlango wa Alama za kiama, (1847) ,Abuu daudi katika, mlango wa Fitna (4244), Ibnu Maajah mlango wa Fitna (3979), Ahmad (5/387). [48] Al-bukhariy mlango wa Manaaqib (3411), Muslimu mlango wa Alama za kiama, (1847), Abuu daudi katika, mlango wa Fitna (4244), Ibnu Maajah mlango wa Fitna (3979), Ahmad (5/404).
Hebu zingatia maneno haya ya Abuul -aalia namna yalivyokuwa na nguvu, na alikuwa ni mjuzi zaidi wa wakati wake ambao hutahadharishwa katika wakati huo na kufuata matamanio ambayo atakayeyafuata hakika atakuwa amekwenda kinyume na uislamu, na kuufasiri uislamu kwa sunnah na hofu yake tena kwa watu ambao ni wajuzi katika mataabiina (wanafunzi wa maswahaba) na maulamaa wao, wasijekutoka katika sunna na Qur'ani, hilo linakubainishia maana ya maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kumbuka alipoambiwa na Mola wake nyenyekea } [49] (Al-Baqara: 131) Na kauli yake: "Na Ibrāhīm na Ya’qūb waliwahimiza watoto wao kusimama imara juu ya uislamu wakiwaambia, “Enyi watoto wetu! Mwenyezi Mungu Amewachagulia Dini hii, nayo ni uislamu, Msiiache muda wa uhai wenu, na msifikiwe na mauti isipokuwa na nyinyi muko kwenye Dini hii.” (Al-Baqara: 132) Na kauli ya Allah Mtukufu: {Na nani atajitenga na mila ya Ibrahimu (akaichukia dini hii ya kiislamu ) isipokuwa anaeitia Nafsi yake katika upumbavu} [51] [Al Baqara: 130]. Na mfano wa misingi hii mikubwa ambayo ndiyo chanzo cha misingi yote ya dini lakini watu wameghafilika nayo, na kwa kuijua misingi hii inafahamika maana ya hadithi zilizopo katika mlango huu na mfano wake, na ama mtu ambaye anaisoma misingi hii na yenye kufanana akiwa katika hali ya utulivu wa moyo, kuwa hizi fitina hazitompata, na akidhani kuwa fitina hizo ni kwa watu waliojiaminisha kuwa wamesalimika na adhabu za Mwenyezi Mungu, na kwa hakika hajiaminishi kutopatwa na adhabu za Mwenyezi Mungu isipokuwa wale waliopata hasara. [49]. Al Baqara: Aya ya: 131. [50] Al Baqara: Aya ya: 132. [51]. Al Baqara: Aya ya: 130.
Kutoka kwa Ibnu Masoud- Radhi za Allah ziwe juu yake alisema: {Alituchorea mstari Mtume wa Mwenyezi Mungu - Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kisha akasema - hii ndiyo njia ya Mwenyezi Mungu. Kisha akachora mistari mingi upande wa kulia kwake na kushotoni kwake, kisha akasema: "Hizi ni njia nyingi, katika kila njia kuna Shetani Anawaita watu katika njia hiyo" Na akasoma: «Na huu Uislamu ndio njia yangu iliyolingana sawa. Basi ifuateni wala msifuate njia za upotevu zikawatawanya na kuwaepusha na njia ya Mwenyezi Mungu iliyolingana sawa" [52] (Al-anaam: 153) Ameipokea Ahmad na Al- nasaai. [52]. (Al An'am: 1153.
Mlango uliokuja kuelezea ugeni katika uislamu na fadhila za wanaoonekana wageni.
Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Basi mbona hawakuwepo watu wa mbele kabla yenu watu -wenye mabaki ya akili-wenye kukataza uharibifu katika nchi isipokuwa wachache tu miongoni mwao tuliwaokoa} [53]. (Surat Huud Aya 166) Na hadithi imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira - Mar-fuu. {Ulianza uislamu ukiwa ni mgeni na utarudi kuwa mgeni kama ulivyo anza, Basi hongera kwa wale watao onekana kuwa ni wageni} [54] Ameipokea Muslim katika mlango wa imani, na ameipokea Ahmad kutoka katika hadithi ya Ibnu Mas'uud na humo kuna: {Ni akina nani hao wageni? Akasema: "wenye kuacha ukabila, na wale wanaobakia kuwa wema watu wanapoharibika} [55]. (53) Huud: 116. [54] Muslimu katika mlango wa imani (145) Ibnu Majah Mlango wa Fitina, (3989) Ahmad (2/389). [55] Ahmad (4/74)
Na Tirmidhiy kutoka katika hadithi ya Kathiir Mtoto wa Abdillahi kutoka kwa baba yake kutoka kwa Babu yake: {Basi hongera kwa wenye kuonekana wageni, wale wanaorekebisha yale waliyoyaharibu watu katika sunna zangu (mwenendo)} (56) [56] Altirmidhiy mlango wa Imani (2630)
Na imepokelea kutoka kwa Abii Umaiya amesema: Nilimuuliza baba Thaalaba unasemaje katika Aya hii? {Enyi mlioamini lililo lazima juu yenu ni nafsi zenu hatokudhuruni aliyepotoka ikiwa mtaongoka} [57] (Al- maidah 105) Akasema: Ama kwa hakika ninaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu hakika nilimuuliza kuhusu Aya hiyo mwenye ujuzi, {Nilimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Akasema: Bali amrishaneni kufanya wema, na katazaneni kufanya uovu, mpaka mkiona ubahili ni wenye kutiiwa na matamanio ndiyo yenye kufuatwa, na watu ni wenye kupupia dunia na kuipenda na kila mtu kupenda kutanguliza rai yake kuliko dalili za kitabu na sunna basi wakati huo jitahidi kuiokoa nafsi yako na wakati huo watu watakuacha na kwa hakika nyuma yenu kutakuja siku na atakuwa mwenye Subra (kuishika dini) ni kama ameshika kaa la moto, basi atakayeishika dini na akatenda ipasavyo katika siku hizo ana malipo ya sawa na malipo ya watu hamsini ambao wanafanya mfano wa mnavyofanya matendo, tukasema: watakuwa ni miongoni mwetu au miongoni mwao? Akasema ni watu miongoni mwenu} [58] Imepokelewa na Abudaud na Tirmidhiy. [57] Maida, mpaka mwisho wa Aya 105. [58] Al-timidhiy katika tafsiri ya Qur'an (3058), Ibnu Maajah katika mlango wa fitna (4014)
Na ameipokea Ibnu Wadhwwah maana yake kutoka katika hadithi ya Ibnu Omar na Tamko lake : {Hakika baada yenu kutakuja masiku atakuwa mwenye subira katika masiku hayo na mwenyekukamatana na dini yake atakuwa kama mfano wenu leo hii, atakuwa ana malipo ya watu hamsini miongoni mwenu} [59] Kisha akasema: Ametupa habari muhammad ibnu said, ametupa habari Asad, Amesema Sufiani ibnu Uyainah :ameipokea kutoka kwa Al- baswariy kutoka kwa saidi ndugu yake Hunain anaiinua hadithi hii kasema: {Kwa hakika leo hii mpo katika uongofu wa kutoka kwa Mola wenu, Mnaamrisha mema na kukataza maovu, na mnapigana jihadi katika njia ya Mwenyezu Mungu, na wala bado havijawatokea vilevi viwili, kilevi cha ujinga na kilevi cha kupenda maisha, na mtabadilishiwa hali hiyo, Basi yule atakayeshikamana wakati huo na kitabu na sunnah atakuwa ana malipo sawa na malipo ya watu hamsini, kukasemwa ni akina nani hao?Akasema: Bali watu hao ni miongoni mwenu: } Na ana Isnadi nyingine imepokelewa kutoka kwa Al-maafiriy Amesema, Amesema Mtume rehema na Amani zimfikie: {Hongera kwa wenye kuonekana wageni ambao wanashikamana na kitabu pindi kinapokuwa kimeachwa, na wanatenda kwa mujibu wa sunna wakati inapokuwa sunna inazimwa} [60] [58] Al-tirmidhiy katika tafsiri ya Qur'an (3058), Ibnu Maajah katika mlango wa fitna (4014). [60] Ahmad (2/222)
Mlango wa kuijihadhari na Uzushi
Hadithi imepokelewa kutoka kwa I'r-baadhwi ibnu Saariyah amesema: {Alitupa mawaidha Mtume -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Mawaidha yenye kiwango cha hali ya juu, tukasema kana kwamba ni mawaidha ya kuaga basi tuusie ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, Akasema: "Ninakuusieni kumcha Mwenyezi Mungu -Mweye nguvu na utukufu- Na kusikiliza na kutii hata kama atawaamrisha mtumwa, kwa hakika atakayeishi muda mrefu miongoni mwenu basi ataona tofauti nyingi, Basi wakati huo shikamaneni na sunnah zangu na sunnah za Makhalifa waongofu walioijua haki na kuifuata, zikamateni sunnah hizo kwa magego, na jiepusheni na mambo ya uzushi, kwani kwa hakika kila uzushi ni upotevu"} [61] Amesema Al-tirmidhiy hadithi hii ni sahihi. [61] Al-tirmidhiy mlango wa elimu ( 2627), Abu daudi mlango wa Sunnah (4607), Ibnu Maajah katika utangulizi (44), Ahmad (4/126), Al-daaramiy katika utangulizi (95).
Na imepokelewa kutoka kwa Hudhaifa amesema kila ibada ambayo hawaifanyi ibada hiyo watu wa Muhammad basi msifanye ibada hiyo kwa hakika waliotangulia hawakuwaachia waliokuja baada yao makala kuhusu ibada hizo, na muogopeni Mwenyezi Mungu Enyi kongamano la wasomi- wajuzi- na chukueni na kufuata njia ya waliokuwa kabla yenu, Imepokelewa na Abudaud Na amesema Al-daaramiy: Alitupa habari Alhakam ibnu Mubaaraka. Alitupa habari Amru ibnu Yahya ,amesema: Nilimsikia baba yangu akihadithia kutoka kwa baba yake Akisema:Tulikuwa tukikaa kwenye mlango wa Abdullahi ibnu Masoud kabla ya swala ya Asubuhi, na akitoka tunakwenda naye msikitini, siku moja akatujia Abuu Mussa Al-ash'ariy Akasema: Hivi amekwisha toka Baba Abdulrahman? Tukasema: bado hajatoka, basi akakaa nasi, na alipotoka akasema: Ewe Baba Abdulrahman hakika mimi nimeona msikitini jambo ambalo ni geni, na sikuliona jambo hilo namshukuru Mwenyezi Mungu isipokuwa naona ni jambo la kheri, akasema, ni jambo gani hilo? Akasema: Ikiwa utaishi utaliona, Akasema: Nimewaona watu wamekaa duara wanangojea swala, na katika kila duara kuna mtu na katika mikono yao kuna vijiwe, na anasema: Leteni Takbira mara mia moja, na wanaleta mara mia, kisha anasema: Leteni Lailaha illa llaha mara mia moja na wanaleta mara mia, na anasema leteni Tasbiihi mara mia moja na wanaleta mara mia, akamwambia uliwaambia nini? Akasema sikuwaambia kitu nilikuwa nasubiri amri yako: Hivi hukuwaamrisha wahesabu makosa yao na ukawa umewapa dhamana ya kutopoteza chochote katika mema yao? kisha akapita katika kila duara, akasema ni vitu gani hivi? wakamwambia: Ni vijiwe tunahesabia Takbiira,Tahliil na Tasbiih, akasema hesabuni makosa yenu na mimi nawapa dhamana yakuwa hamtopoteza chochote katika mema yenu, Mna nini enyi Umma wa Muhammad? Ni kwanini mnaangamia kwa haraka hivyo?! hawa ni Maswahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu- Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- wako wamejaa tele na hizi ni nguo zake bado hazijaoza, na vyombo vyake havijavunjwa. Namuapia yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake hakika nyie mko katika mila, mila ambayo inamuongozo mzuri zaidi katika mila za Muhammad, au mnataka kufungua mlango wa upotofu? wakasema: Tunamuapia Mwenyezi Mungu ewe baba Abdurahmani hatukukusudia isipokuwa kheri, Akasema: Na ni wangapi miongoni mwa wenye kukusudia na kutaka kheri na wala hawakupatia? Hakika Mtume -Rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Ametuhadithia kuwa wao ni watu ambao wanasoma Qur'ani lakini hawapewi malipo yake wala hawaandikiwi thawabu za usomaji wa Qur'ani, na ninamuapia Mwenyezi Mungu huenda wengi wao si watu wengine isipokuwa ni nyinyi, Akasema: Amru Ibnu Salama tuliwaona wote hao wakitukashifu na kutusema vibaya siku ya vita vya Nahrawani wakiwa pamoja na Makhawaariji.