آداب المشي إلى الصلاة

آداب المشي إلى الصلاة

يتناول الكتاب آداب وسنن المشي إلى الصلاة، وكيفية الاستعداد لها بطهارة وخشوع، والتصرفات المستحبة عند دخول المسجد والخروج منه. يشمل الكتاب تعليمات حول التوجه إلى الصلاة بالسكينة والوقار، والدعاء بالأدعية المأثورة، والتأكيد على أداء ركعتي تحية المسجد عند الدخول. الكتاب يعكس اهتمام الشيخ محمد بن عبد الوهاب بتفاصيل السلوكيات اليومية للمسلم وتعليم الآداب الإسلامية المرتبطة بالصلاة.

Language: lang_sw
Prepared by:
Version: 1.0
Translations 10
Bengali English French Hindi +6
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

(Kitabu cha Adabu za kwenda katika Swala)

Mtunzi: Sheikh Al- islaam na alama miongoni mwa alama, kiongozi aliyerudisha upya elimu ya dini, Sheikh Muhammad bin Abdulwahhab Allah Mtukufu amrehemu.

Wamefanya kazi ya kusahihisha na kulinganisha Nakala iliyoandikwa kwa mkono katika Maktaba ya Saudia kwa namba 269/86 na nakala nyingine nyingi zimechapishwa na masheikh wafuatao: Abdul karim bin Muhammad Al-laahim. Naasir bin Abdillahi Al- Twariim, Suud bin Muhammad Al- bashar.

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu:

(Mlango wa adabu za kwenda katika Swala)

Ni Sunna kutoka kuiendea swala hali ya kuwa umejitwaharisha ukiwa ni mnyenyekevu, kwa kauli yake Mtume- Rehema na Amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: "Ikiwa atatawadha mmoja wenu na akafanya vizuri katika kutawadha kwake, kisha akatoka akikusudia kwenda msikitini basi na asifungamanishe kati ya vidole vyake kwani yeye kwa hakika yuko katika swala " Na aseme wakati anapotoka nyumbani -hata kama kutoka kwake si kwa ajili ya swala- (Kwa jina la Mwenyezi Mungu ,nimejishikiza kwa Mwenyezi Mungu, nimetegemea kwa Mwenyezi Mungu na hakuna hila (namna ) wala nguvu isipokuwa kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, Ewe Mola wangu wa haki hakika mimi najikinga kwako ili nisipotee au kupotezwa au kuteleza na kufanyakosa au kutelezeshwa na kufanya makosa au kudhulumu au kudhulumiwa au kudanganya au kudanganywa mimi) Na Sunna kutoka kuiendea swala hali ya kuwa umejitwaharisha ukiwa ni mnyenyekevu, kwa kauli yake Mtume- Rehema na Amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: (Na mkisikia Ikama basi nendeni na mlazimiane na utulivu na kile mtakachokikuta katika rakaa basi swalini na kile kitakachowapita katika rakaa basi lipeni) Na ni katika Sunna kupiga hatua ndogo ndogo na aseme: (Ewe Mola wangu wa haki hakika mimi ninakuomba kwa haki ya wenye kuomba -yaani kujibiwa- na haki ya kutembea kwangu huku -kwa ajili ya utiifu- kwa hakika mimi sijatoka kwa kukusudia shari wala kwa kiburi, wala kujionyesha au kutaka kusikika, bali nimetoka kwa kuogopa hasira zako na kutafuta radhi zako, ninakuomba uniepushe na moto na unisamehe madhambi yangu yote kwani hakuna awezaye kusamehe madhambi isipokuwa wewe). Na aseme: (Ewe Mola wangu wa haki naomba uweke katika moyo wangu nuru na katika ulimi wangu nuru na uiweke nuru katika macho yangu na masikio yangu na mbele yangu na nyuma yangu kuliani kwangu kushotoni kwangu na juu yangu na chini yangu, ewe Mola wangu nipe nuru) Na akiingia msikitini inapendeza na ni Sunna kutanguliza mguu wake wa kulia na atasema: (Kwa jina la Mwenyezi Mungu, najilinda kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kwa uso wake Mtukufu na utawala wake wa tangu na tangu (najilinda) kutokana na shetani aliyefukuzwa kutoka katika rehema za Mwenyezi Mungu, Ewe Mola wangu wa haki teremsha rehema kwa Muhammad na unisamehe madhambi yangu na unifungulie milango ya rehema zako) Na wakati wa kutoka kwake Msikitini atatanguliza mguu wake wa kushoto na atasema: (Na unifungulie milango ya Fadhila zako) Na akiingia msikitini basi asikae mpaka aswali rakaa mbili, kwa kauli yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: (Akiingia mmoja wenu msikitini basi asikae mpaka aswali rakaa mbili) Na ashughulike na kumtaja Mwenyezi Mungu na akae kimya na wala asiingie kwenye mazungumzo ya kidunia ,ikiwa atadumu katika hali hiyo atahesabika yuko katika swala na Malaika wanakuwa wanamuombea msamaha ikiwa hatoleta maudhi au kuongea.

Mlango wa namna ya kuswali:

Ni Sunna na inapendeza asimame kwa ajili ya swala pale muadhini atakaposema :-Qad Qaamati swalaaa- Hakika imesimama swala, kama ikiwa Imamu yupo msikitini, na kama hayupo atasimama atakapomuona, aliambiwa imamu Ahmad kabla ya Takbiira ya kuhirimia unasema kitu chochote? akasema: Hapana, kwa kuwa haikupokelewa kutoka kwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: wala kwa yeyote katika maswahaba wake, kisha imamu atazisawazisha safu kwa kulinganisha mabega na fundo za miguu.

Na ni Sunna kukamilisha safu ya Kwanza kisha inayofuata na kushikana maamuma kwa pamoja na kuziba mianya kwenye safu, na kila safu ya upande wa kulia ndiyo bora, na ya karibu na imamu ndiyo bora zaidi kwa kauli yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Na wafuatie nyuma yangu waliobaleghe miongoni mwenu na wenye akili" "Na safu iliyobora ya wanaume ni safu ya kwanza, na safu yenye shari ni ya nyuma, na safu bora ya wanawake ni safu ya mwisho na yenye shari ni safu ya mwanzo" Kisha atasema akiwa amesimama kama atakuwa na uwezo wa kusimama "Allahu Ak-bar" na halimtoshelezi neno lolote lisilokuwa hili. Na hekima ya kufungua swala kwa takbira ni ili kuuhudhurisha utukufu wa mwenye kusimama mbele yake na hivyo humfanya kuwa mnyenyekevu, kwani kuivuta herufi Hamza (A) katika neno Allah au neno 'Ak-baru' au akasema; Ik-baaru, haitafungika swala, na Bubu ataleta Takbira ya kuhirimia moyoni mwake na wala hatoutikisa ulimi wake na hivyo hivyo ndiyo hukumu ya kusoma Qur'ani na Tas-biihi na adh-kari nyingine zisizokuwa hizi mbili.

Na ni Sunna kwa Imamu kudhihirisha sauti kwa kuleta Takbira, kwa kauli yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Atakapo leta Takbira Imamu basi nanyinyi leteni Takbira" "Na ni sunna kusema imamu kwa sauti Samiallahu limani hamida" kwa kauli yake Mtume: Na akisema Imamu 'samiallahu liman hamidahu' Yaani: -amemsikia Mwenyezi Mungu mtu mwenye kumuhimidi- basi semeni:" Rabbana walakal Hamdu" Yaani: -Ewe Mola wetu sifa njema ni zako-

Na maamuma husema kwa siri na pia mtu mmoja mmoja, na atainua mikono yake miwili kwa kunyoosha vidole vya mikono yake miwili ikiwa imeshikanishwa na ataelekeza matumbo ya mikono yake kibla kwa usawa wa mabega yake mawili, ama ikiwa hana udhuru, na ataiinuwa mikono yake hali yakuwa ni ishara ya kufunua pazia lililopo kati yake na Mola wake, kama vile ambavyo kidole cha shahada kina ashiria upekee wa Mwenyezi Mungu, kisha anakishika kiganja chake cha mkono wa kushoto kwa kutumia mkono wa kulia na kuiweka chini ya kitovu chake, na maana yake ni kujidhalilisha mbele ya Mola wake Mtukufu. Na ni Sunna na inapendeza kutazama sehemu anaposujudia katika hali zote za swala isipokuwa kwenye Tahiyyatu ataangalia kidole chake cha shahada. Kisha atafungua swala yake kwa siri kwa kusema: (Sub-haanakallahumma wa bihamdika)- maana yake: ninakutakasa wewe utakaso unaoenda na wewe ewe Mola wangu, maana ya (wabihamdika) nakusanya pamoja kwa ajili yako utakaso na shukurani (Wa Tabaaraka smuka) yaani: Baraka hupatikana kwa kukutaja wewe (Wataala Jadduka) yaani: umetakasika utukufu wako (Walaa ilaha ghairuka ) yaani: hakuna aabudiwaye hapa ardhini wala mbinguni kwa haki isipokuwa wewe ewe Mwenyezi Mungu, na yafaa kuifungua swala kwa kila dua ambayo imethibiti kuwa imepokelewa, Kisha atajikinga na shetani kwa siri kwa kusema: (Audhubillahi mina shaitwani rajiim) na vyovyote atakavyojikinga na kinga zilizothibiti basi ni vizuri, kisha ataleta Bismillahi kwa siri, na hiyo Bismillahi si Aya katika Suratil Faatiha wala sura nyingine, bali ni Aya katika Qur'ani iliyoko kabla ya Suratil Faatiha na kati ya kila sura mbili isipokuwa surat Baraa'at na An-faal, Na ni sunna kuiandika Suratul Faatiha mwanzo wa vitabu kama alivyoiandika Nabii suleimani -juu yake na amani- na kama vile ambavyo alikuwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: Alikuwa akifanya na akitamka mwanzo wa vitendo vyote na hiyo Bismillahi inamfukuza shetani Amesema Imamu Ahmad: Bismillahi haiandikwi mbele ya shairi wala pamoja na mashairi. Kisha atasoma suratil Faatiha kwa mpangilio na kwa kuifuatanisha, na Al-fatiha ni nguzo katika kila rakaa kama ilivyokuja katika hadithi "Hakuna swala kwa yeyote ambaye hakusoma sura kifunguzi cha kitabu (suratul faatiha)" Na huitwa mama wa Qur'ani kwa sababu ndani yake kumetajwa Uungu na siku ya ahadi na utume na kuthibitisha Qadar, na Aya mbili za mwanzo zinajulisha juu ya Uungu na {Mwenye kumiliki siku ya mwisho} inajulisha ahadi. "Wewe tu tunakuabudu na ni wewe tunakuomba msaada" Na suratul Faatiha inajulisha kuamrisha mema na kukataza mabaya na kutegemea na kuyafanya yote hayo kwa ikhlaas, yaani: kwa ajili ya Allah, na ndani yake kunakuzindushwa juu ya kufuata haki na watu wa haki, na kuna tahadhari ya kutofuata njia ya upotofu na upotevu, na inapendeza kusimama katika kila

Aya, kwa mujibu wa kisomo chake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- na ni sura Tukufu katika Qur'ani, na Aya tukufu zaidi ndani ya Qur'ani ni Ayatul Kursiyyu, ndani yake kuna Shadda (kusoma kwa kukaza) mara kumi na moja, na ni machukizo kukaza mpaka kupitiliza, au kufanya uzembe katika kukaza, na ikiwa atamaliza atasema: Aamiin baada ya kunyamaza kidogo ili ijulikane kuwa hiyo Aamin si katika Qur'ani, na maana ya Aamin: Ewe Mola wangu tukubalie, na ataisema kwa sauti imamu na maamuma katika swala zinasomwa kwa sauti, Na ni sunna kunyamaza imamu baada ya kuisoma katika swala zinazo swaliwa kwa sauti, kwa ushahidi wa hadithi ya Samrat, na ni lazima kwa asiyeijua ajifunze na ikiwa hatojifunza hali yakuwa ana uwezo basi swala yake haitokubaliwa, na yule asiyeweza kusoma chochote katika suratil faatiha wala chochote katika Qur'ani itamlazimu aseme :" Sub-hanallah Wal-hamdulillah Walaahaula walaaquwwata illa Billah" kwa maneno yake Mtume-Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Ikiwa unayo Qur'ani basi isome na ikiwa hauna Basi Muhimidi Mola wako na ulete Tah-liil (Laailaha illa llah) na ulete Takbira, kisha urukuu" Ameipokea hadithi hii Abuu Daudi na Tirmidhiiy, kisha atasoma Bismillah kwa siri, kisha atasoma sura kamili, na inamtosha kusoma Aya moja, isipokuwa imamu Ahmad amependekeza kuwa Aya hiyo iwe ndefu, na kama itakuwa nje ya swala ikiwa atataka atadhihirisha Bismillah na ikiwa atataka ataisoma kwa siri, Na huwa sura inayosomwa katika swala ya Alfajiri ni katika sura ndefu zilizo gawanywa, na sura ndefu huanzia surat Qaaf kwa maneno ya swahaba Ausi aliposema: "Niliwauliza masahaba wa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: vipi mwaigawanya Qur'ani? Wakasema: tunaigawa kwa namna tatu na tano na saba na kumi na moja na mgawanyo uliochambuliwa mmoja, na ni karaha kusoma sura fupi katika swala ya Alfajiri pasina kuwa na udhuru, kama safari, ugonjwa na mfano wake. Na atasoma katika swala ya magharibi sura fupi na atasoma katika swala hiyo baadhi ya nyakati sura ndefu kwa sababu Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: aliwahi kusoma katika swala ya magharibi suratil Aaraaf, na husoma katika rakaa zilizobakia sura za katikati kama hapatakuwa na dharura, na kama kutakuwa na dharura atasoma sura fupi, na wala si vibaya kwa mwanamke kusoma kwa sauti kama ikiwa hatosikiwa na mtu asiyekuwa maharimu yake, na mwenye kusali sunna za usiku anatakiwa kuchunga maslahi, ikiwa kuna mtu yuko karibu na anaudhika kwa kutoa kwake sauti basi ataswali bila kutoa sauti, kama itakuwa kuna mwenye kumsikiliza basi atasoma kwa sauti, na ikiwa atasoma kwa siri katika swala ya kusoma kwa sauti na akasoma kwa sauti katika swala ya kusoma kwa siri atasoma kwa namna inavyotakiwa kusoma, na kufuatanisha Aya ni wajibu kwa sababu jambo hilo limethibiti kwa dalili,na kupangilia sura ni jitihada.

Na haikuthibiti upangiliaji wa sura kwa dalili katika kauli ya jopo la maulamaa, hivyo basi yafaa kusoma sura hizi kabla ya zingine, na kwa namna hiyo ndiyo maana misahafu ya maswahaba ikawa ya aina tofauti tofauti katika uandishi wake, na anaona Imamu Ahmad kuwa ni karaha kusoma kisomo cha Hamza na Kisaaiy, na Id-ghaam kubwa ya Abii Amru, (Rejea vitabu vya tajiwidi na visomo) kisha atainua mikono yake miwili kama alivyonyanyua mara ya kwanza baada ya kumaliza kusoma na baada ya kusimama vizuri, mpaka atulizane, na wala asiunganishe kisomo chake na takbira ya kurukuu, Na ataleta Takbira na kuweka mikono yake hali ya kutawanya vidole vyake juu ya magoti yake hali ya kila mkono kushika goti na ataunyoosha mgongo wake na kuulinganisha sawa na na kukiweka kichwa kiwe sawa asikinyanyue wala kukishusha, kwa mujibu wa hadithi ya Aisha, na huweka kando ya mbavu zake mikono yake miwili, kwa hadihi ya Abii Humaid, na atasema: katika kurukuu kwake: "Sub-hana rabiyal adhwiim" kwa hadithi ya Hudhaifa ameipoke Muslim na uchache wa ukamilifu ni mara tatu na zaidi yake kwa imamu ni mara kumi, na hivyo hivyo hukumu ya 'Sub-hanarabbiyal Aa'la katika kusujudu", Na wala asisome kwenye kurukuu na kusujudu kwa makatazo yake bwana Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani, kisha atainua kichwa chake na mikono yake mfano wa kunyanyua kwake mara ya kwanza, na huku akisema imamu na mwenye kuswali peke yake, "Samia llahu liman hamidah" Na ni wajibu, na maana ya (Samia) amejibu na akishamaliza kusimama atasema; "Rabbana walakal hamdu, mil as samaawaati wal ardhwi wamil'a maaashiita min shain Baad" Na akipenda atazidisha: 'Ahluth'thanaa walmajda ahaqqu maaqaalal abdu wakulluna laka Abdu, laa maania limaa aa'twaita walaa muutwiya limaa manaata, walaa yanfau dhaljaddi minkal jaddu' Yaani: Ewe Mstahiki wa shukurani nyingi na utukufu, yana haki zaidi (maneno) aliyoyasema mja, na sisi sote kwako ni waja, hakuna wa kuyazuia uliyoyatoa, na wala wa kuyatoa uliyoyazuia, na utukufu wowote hauwezi kunufaisha zaidi kuliko utukufu wako" Na ni ruhusa kwake kuleta adhkaar (Nyiradi) zingine zisizokuwa hizi katika zile zilizopokelewa. Na ikiwa atapenda atasema: Allahumma rabbanaa lakal hamdu " bila ya wau kwa kupokelewa hilo kutoka katika hadithi ya Abii Saidil khuduriyy na wengine, na ikiwa atamkuta maamuma imamu katika rukuu hii basi atakuwa amekuta rakaa, kisha ataletaTakbira na ataporomoka kwenda kusujudu na wala asiinue mikono yake na ataanza kuweka magoti yake mawili kisha mikono yake miwili kisha uso wake na atamakinisha (kuegemeza) uso wake na pua yake kwenye Ardhi anakuwa juu ya ncha za vidole vyake na kuelekeza ncha za vidole vyake upande wa Qibla, na kusujudu kwa viungo hivi saba ni nguzo, na ni sunnah mwenye kuswali kuweka moja kwa moja matumbo ya viganja vyake na kuvikusanya vidole vya mikono yake miwili na akivielekeza qibla na awe mwenye kuinua fundo zake za mikono pasina kuishikanisha.

Na ni karaha kuswali katika sehemu yenye joto kali au baridi kali, kwani hali hiyo huondosha unyenyekevu, na ni sunnah kwa mwenye kusujudu aweke mbali viwiko vyake na asishikanishe na mbavu zake na aweke mbali tumbo lake na mapaja yake na atenganishe na miundi yake na aweke mikono yake usawa wa mabega yake na ataachanisha kati ya magoti yake na miguu yake. Kisha atainua kichwa chake na kuleta Takbira na atakaa akiwa ameukunjua mguu wake wa kushoto na kuukalia, na atausimamisha mguu wa kulia na kuutoa chini yake na ataweka matumbo ya vidole vyake ardhini ili iwe ncha za vidole vyake vikielekea Qibla, kwa hadithi ya Abuu Humaidi katika sifa za swala ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani, akiwa katika hali ya kukunjua mikono yake juu ya mapaja yake akiwa ameshikanisha vidole na akisema "Rabbighfir lii" na hakuna ubaya kama atazidisha kwa maneno ya bin Abbas kuwa alikuwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani akisoma kati ya sijida mbili: "Rabbighfirliiy war-hamniiy wahdiniiy warzuquniiy waafiniiy" (Ewe Mola wangu nisamehe mimi na unihurumie na uniongoze na uniruzuku na unisamehe) Imepokelewa na Abuu Daud, Kisha atasujudu mara ya pili kama vile ya mwanzo na akitaka ataomba katika sijida hiyo, kwa mujibu wa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Na ama kwenye kusujudu zidisheni humo dua kwa kuwa kuna uhakika wa kujibiwa maombi yenu" Ameipokea Imamu Muslim Na imepokelewa pia katika Sahihi Muslim, kutoka kwa Abuu Huraira kuwa; Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- alikuwa akisema kwenye kusujudu kwake: (Allahummaghfir lii Dhambii kullahu diqqahuu wa jullahuu wa awwalahuu wa aakhirahuu wa a'laaniyatahuu wa sirrahuu) Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe mimi dhambi zangu, ndogo zake na kubwa zake za mwanzo wake na mwisho wake, za wazi zake na za siri zake", Kisha anainua kichwa chake huku akileta Takbira akisimama kwa vifua vya miguu yake hali ya kuegemea magoti yake, kwa hadithi ya Waail, isipokuwa itakapokuwa ni uzito kwa sababu ya utu uzima au ugonjwa au udhaifu, kisha atasali rakaa ya pili kama ya kwanza isipokuwa hatoleta takbira ya kuhirimia na ya kufungua swala hata kama hajaileta katika rakaa ya kwanza, kisha atakaa kwa ajili ya Attahiyaatu huku akikunjua miguu yake na kuweka mikono yake juu ya mapaja yake hali ya kuvitandaza vidole vyake vya mkono wa kushoto na kuvielekeza kibla, na kushikanisha vidole vya mkono wake wa kulia kidole kidogo na kinachofuatia hali ya kukutanisha kidole gumba pamoja na kidole cha katikati kisha atatoa shahada kimya kimya na akiashiria kwa kidole chake cha shahada cha kulia katika Tahiyyatu yake akiashiria kumpwekesha Mwenyezi Mungu wakati wa kuomba kwake dua katika swala na nje ya swala, kwa maneno ya bin Zubeir: Alikuwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- akiashiria kwa kidole chake anapokuwa anaomba na wala hatikisi kidole chake" ameipokea hadithi hii Abuu Daud. Na atasema: "Attahiyyaatu lillaahi, wasswalawaatu wattwayyibaatu, assalaamu a'laika ayyuhan nabiyyu, warahmatullaahi wabarakaatuh, assalaamu a'lainaa wa a'laa ibaadillaahi sswaalihiin, ash-hadu anlaa ilaaha illa llaahu, wa ash-hadu anna Muhammadan 'abduhu warasuuluhu" Tafsiri yake: Maamkizi (Amani) ni ya Mwenyezi Mungu, na swala na vile vilivyo vizuri, amani iwe juu yako ewe nabii na rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake, amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Mwenyezi Mungu, nashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na ninashuhudia kuwa Muhammadi ni mja wake na ni mjumbe wake. Na Tashashudi (Tahiyatu) yoyote atakayoisoma katika zile zilizopokelewa kutoka kwa bwana Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- inafaa, na bora zaidi ni kuileta kwa ufupi pasina kuzidisha, na hii ndiyo Attahiyyatu -Tashahudi- ya kwanza. Kisha kama itakuwa swala ni ya rakaa mbili tu atamswalia Mtume -Rehema za Mwenyezi mungu ziwe juu yake na amani- na atasema: Allahumma swalli alaa Muhammad wa a'laa aali Muhammad, kamaa swallaita alaa Ibrahiim wa a'laa aali Ibraahiim innaka hamiidun majiidun, wabaariki alaa Muhammad wa a'laa aali Muhamad kamaa baarakta alaa Ibraahiim wa a'laa aali Ibraahiim innaka hamiidun majiidun. Na inafaa amswalie Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- kama ilivyopokelewa. Wa Aalu Muhammad; wanakusudiwa watu wa nyumbani kwake, na maana ya (Attahiyyaat) yaani maamkizi yote ni ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ni haki yake na miliki yake (Wasswalawaatu) maombi (Watwayyibaatu) matendo mema kwa hivyo yeye kutakasika na machafu ni kwake huamkiwa na wala haombewi amani kwa sababu amani ni dua. Na inafaa kumswalia asiyekuwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- kipekee ikiwa halitozidishwa na kufanywa ni nembo ya baadhi ya watu au ikakusudiwa baadhi ya maswahaba na kuwaacha wengine, na ni sunna kumswalia Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- nje ya swala na hutiliwa mkazo mkubwa wakati anapotajwa. Na katika siku ya ijumaa na usiku wake, na ni sunna aseme: "Allaahumma inni a'udhubika min adhaabi jahannama, wa min adhaabil qabri, wamin fitnatil mahyaa wal mamaati, wamin sharri fitnatil masiihiddajjaali" Ewe Mola wangu hakika mimi ninajilinda kwako kutokana na adhabu za jahanamu, na fitina za uhai na za kifo, na kutokana na fitina za masihi dajali". Na ikiwa ataomba dua isiyokuwa hiyo katika dua zilizopokelewa basi ni vizuri pia, kwa maneno yake -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Kisha atachagua Dua impendezayo". Ikiwa haitokuwa uzito kwa Maamuma, na inafaa kumuombea dua mtu maalumu, kwa kufanya kwake hivyo Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- katika kuwaombea wanyonge wa Makkah, kisha atatoa salamu akiwa amekaa akianzia kuliani kwake huku akisema; Assalaamu alaikum warahmatullahi, na upande wa kushoto hivyo hivyo, na kugeuka ni sunnna, na inakuwa kugeuka kwake upande wa kushoto ni zaidi kiasi cha kuonekana shavu lake, na imamu atadhihirisha utoaji salamu wa mara ya kwanza tu na atatoa kwa siri ya pili, na ni sunna kutokuvuta sauti yake wakati wa kutoa salamu, na atanuia kutoka katika swala na atanuia vile vile salamu kwa Malaika na waliohudhuria. Na ikiwa swala ni ya zaidi ya rakaa mbili atainuka kwa vifua vya nyayo zake huku akileta takbira, na atakapokuwa ameshamaliza tashahudi ya kwanza, na ataleta kilichobakia katika swala yake kama ilivyotangulia, isipokuwa yeye hatodhihirisha wala kusoma chochote baada ya suratil faatiha, na kama atasoma si vibaya, kisha atakaa katika tashahud ya pili mkao wa Tawarruki, nao ni ataukunjua mguu wake wa kushoto na kuusimamisha mguu wa kulia, na anaitoa yote miwili upande wake wa kulia na kuweka kalio lake ardhini, na ataleta Tahiyyatu ya kwanza kisha kumswalia Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani -kisha ataleta dua kisha anatoa salamu. Na atawageukia Imamu maamuma kwa upande wake wa kulia au wa kushoto, na wala asichukue muda mrefu Imamu akielekea kibla baada ya kutoa salamu, na wala asiondoke maamuma kabla ya imamu, kwa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi mungu ziwe juu yake na amani- "Hakika mimi ni imamu wenu basi msinitangulie kwa kurukuu wala kusujudu wala kuondoka", Ikiwa wata swali pamoja na wanawake, wataondoka wanawake na watabakia wanaume kidogo ili wasiwakute walioondoka katika hao wanawake, na ni sunnah kuleta dua na nyiradi na istighfaar baada ya swala, na atasema: As-tagh-firullaha- mara tatu kisha atasema Allahumma Anta s' salaam Waminka Salaam Tabaarkta yaa dhal jalaal wali-ikraam, Laailaaha illa llahu wahdahu laa shariika lahuu, lahulmulku walahul hamdu wahuwa alaa kulli shain Qadiir, walaa haula walaa quwwata illa billaah laailaaha illa llahu walaa naabudu illa iyyaahu lahu nniimata walahulfadhwil walahuu thanaaul husna laailaaha illa llahu mukhliswiina luhuddiin walaukarihal kaafiruun: "Allahuma laa maania limaa aa'twaita walaa muutwiya limaa mana'ata walaa yanfau dhaljaddi minkal jaddu". Kisha ataleta tasbiih, tahmiid na Takbiir kila moja mara thelathini na tatu, na atasema kukamilisha mia moja: "Laa ilaaha illa llahu wah'dahu laa shirika lahu, lahul mulku walahul hamdu wahuwa a'laa kulli shain qadiir". Na atasema baada ya swala ya Alfajiri na magharibi kabla hajamsemesha mtu yeyote: "Allaumma Ajir'nii mina nnari" Yaani: Ewe Mola wangu nikinge na moto, mara saba na kuleta dua kwa siri ni bora zaidi na vilevile kuomba dua iliyopokelewa, na inakuwa ni kwa adabu na unyenyekevu na kuuhudhurisha moyo na kuwa na shauku na hofu wakati wa kuomba, kwa mujibu wa hadithi"

"Wala haijibiwi dua ya mtu aliyeghafilika moyoni mwake" Na huomba kupitia majina na sifa na kumpwekesha, na kuchagua muda wa kujibiwa, na muda huo ni pale inapofikia nusu ya mwisho wa usiku na muda kati ya Adhana na Iqama, na mwisho wa swala za faradhi na mwisho wa saa za Ijumaa, na asubirie majibu na wala asifanye haraka, na wala asiharakishe na kusema: Hakika nimeomba na kuomba na wala sikujibiwa, na wala si vibaya ikiwa atafanya kwa ajili ya nafsi yake isipokuwa katika dua ataitikia, na haipendezi kuinua sauti.

Na ni machukizo katika swala kugeuka kidogo na kuinua macho juu kuangalia picha iliyotundikwa, au kuangalia uso wa mwanadamu na kuelekea moto hata kama ni taa, na kukunjua mikono yake katika sijida na wala asiingie kwenye swala hali ya kuwa anabana haja ndogo au kubwa, au kuletwa chakula akipendacho hivyo ataichelewesha swala hata kama itampita swala ya jamaa. Na ni machukizo kugusa vijiwe na kushikamanisha vidole vyake na kuegemea mikono yake wakati wa kukaa na kushika ndevu zake na kuzifunga nywele zake na kukunja nguo, na kama atapiga miayo atazuia kwa kadiri ya uwezo wake na ikiwa kutamshinda ataweka mkono wake kwenye mdomo wake, Na huchukiwa kusambaza udongo pasina ya udhuru, na atamrudisha mwenye kupita mbele yake japo kwa kumsukuma kwake, mwanadamu anayepita au yeyote katika swala ya faradhi au ya Sunnah, ikiwa atakataa basi ni haki yake kumpiga hata kama atasogea kidogo, na ni haramu kupita baina ya mwenye kuswali na kati ya kizuizi na kupita mbele yake hata kama hajaweka kizuizi, Na ni haki yake kuwauwa nyoka na Nge na chawa na kutengeneze nguo na kilemba na kubeba kitu na kukiweka chini na ni haki yake kutoa ishara kwa mkono wake na uso wake na macho kwa ajili ya dharura, Na ni machukizo kutolea salamu mwenye kuswali na ikiwa atasalimiwa atarudisha kwa ishara na anakosa la kumkosoa imamu wake ikiwa atakosea au kuchanganya, na ikiwa kitamtokea kitu katika swala. mwanaume ataleta Tasbiih na mwanamke atapiga makofi, na yakimshinda mate au makohozi au makamasi hali yakuwa yupo msikitini basi atatema katika nguo yake na ikiwa si msikitini basi atatema upande wake wa kushoto, na ni karaha kutema mate chini ya miguu yake au upande wake wa kulia.

Na huchukiza kwa asiyekuwa imamu kuswali pasina kuweka kizuizi hata kama hachelei kuwa mpitaji kukatisha swala yake, aweke ukuta au kitu chenye kutokeza kama vile chuma au kitu kingine chochote mfano wa kiti cha kipando. Na ni sunna akikaribie kizuizi hicho, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Atakaposwali mmoja wenu basi na aswali akiwa ameweka sitara kizuizi na akikaribie kizuizi hicho" Na atakuwa nacho pembeni kidogo, kwa kitendo chake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-, na ikiwa itashindikana basi atachora msitari, na ikiwa kitapita chochote nyuma yake hakuna machukizo, na ikiwa hakutakuwa na kizuizi au akapita mwanamke kati yake na kizuizi au mbwa au punda itakuwa swala yake imebatilika.

Na ni haki yake kusoma katika msahafu na kuomba Rehema katika Aya ya rehema, na kuomba kinga katika Aya ya adhabu.

Na kusimama ni nguzo katika swala ya faradhi kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu "Na simameni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hali yakuwa mnanyenyekea" Isipokuwa asiyejiweza au aliye uchi au anaogopa au ni maamuma yuko nyuma ya imamu wa mtaa aliyeshindwa kusimama, na ikiwa atamkuta imamu katika rukuu basi ataleta kiasi cha Takbira ya kuhirimia.

Na Takbiiratul Ihraam ni nguzo na vile vile kusoma suratul Faatiha kwa Imamu na mtu mmoja mmoja na vile vile kurukuu ni nguzo: {Enyi mlioamini Rukuuni na Msujudu}. Na imepokelewa hadithi kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani kuwa mtu mmoja aliingia msikitini na akaswali kisha akaja kwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- na akamsalimia Mtume akasema Mtume: "Rudi kaswali, kwani wewe hujaswali", Alifanya hivyo mara tatu kisha akasema: Namuapa yule aliyekutuma kwa haki kuwa Nabii, sina namna nyingine ya kufanya vizuri zaidi ya hapo, basi nifundishe, akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kumwambia-: "Utakaposimama katika swala basi toa takbira, (sema Allaahu Akbaru), kisha soma kitakachokuwa chepesi kwako katika Qur'ani, kisha rukuu mpaka utulizane ukiwa umerukuu, kisha nyanyuka mpaka ulingane sawa ukiwa umesimama, kisha usujudu mpaka utulizane ukiwa umesujudu, kisha nyanyuka mpaka utulizane ukiwa umekaa, kisha fanya hivyo katika swala yako yote", Wameipokea jamaa. Hadithi ikajulisha kuwa vilivyotajwa hapa haviondoki kwa hali yoyote, laiti yasingelikuwa ni ya lazima haya ndani ya swala basi kwa huyu Bedui asiyejuwa kitu.

Na kunyenyekea katika vitendo hivi ni nguzo miongoni mwa nguzo kama ilivyotangulia. Na alimuona Hudhaifa akiwa hatimizi rukuu yake wala sijida zake, Hudhaifa akamwambia: Haukuswali na lau ungekufa ungekufa katika umbile ambalo si la Mwenyezi Mungu ambalo Mwenyezi Mungu amemuumbia nalo Muhammad -Rehema na Amani ziwe juu yake.

Na Attahiyyaatu (tashahudi) ya mwisho ni nguzo kwa kauli ya bin Mas'oud:Tulikuwa tukisema kabla ya kufaradhishiwa Attahiyyatu: Assalamu ala llahi, (Amani iwe juu ya Mwenyezi Mungu) Assalaam ala jibril wa mikaaiil (Amani iwe juu ya Jibriil na Mikail), Akasema: Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake: "Msiseme hivyo, lakini semeni: Attahiyyatu lillahi "(Maamkizi mema ni ya Mwenyezi Mungu) Ameipokea An-nasaai na wapokezi wake ni waaminifu.

Na wajibu ambao unaanguka kwa mtu kusahau ni mambo Nane: Takbira ambayo si ya kwanza, na kusema Samiallahu liman hamida, kwa Imamu na mtu anaposwali peke yake, na kusema; Rabbana walakal hamdu kwa wote, na Tas-biihi wakati wa kurukuu na kusujudu, na kusema; Rabbigh-firlii, na Tashahudi ya kwanza na kikao chake na yasiyokuwa hayo katika sunna za kauli na vitendo.

Na Sunnah za maneno ni kumi na saba: ni kuleta dua ya ufunguzi, na Audhubillaahi na Bismillah, na kusema "Aamiin" na kusoma sura katika Rakaa mbili za mwanzo na katika swala ya Alfajiri na swala ya ljumaa na Eid na Swala za Sunna zote na kudhihirisha na kusoma kwa siri na kusema Mil-a samaai wal-ardhwi mpaka mwisho na kilichozidi zaidi ya mara moja katika Tas-biihi na Rukuu na Sujudu, na kusema; Rabbighfir lii, na kuomba kinga ya mambo manne katika tashahudi ya mwisho, na kuwaswalia watu wa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake na kumuombea baraka yeye na watu wake. Na zisizokuwa hizo basi huwa ni sunna za vitendo, mfano; kushikanisha vidole na kuvikunjua kwa kuvielekeza kibla wakati wa kuhirimia na kurukuu na kutoka kwenye kurukuu, na kuvikunjua baada ya hapo, na kutumia mkono wa kulia kuushika mkono wa kushoto, na kuiweka mikono miwili chini ya kitovu, na kuangalia sehemu ya kusujudia kwake, na kuachanisha baina ya miguu yake miwili wakati wa kusimama kwake na kuipa nafasi, na kusoma kwa utaratibu, na kufupisha swala kwa imamu, na kuifanya rakaa ya kwanza kuwa ni ndefu kuliko ya pili, na kuyashika magoti yake hali ya kuvitanua vidole vyake katika kurukuu, na kuunyoosha mgongo wake mpaka kulingana sawa, na kichwa kulingana sawa, na kutanguliza magoti yake kabla ya mikono yake wakati wa kusujudu kwake na kuinua mikono yake kabla ya magoti yake wakati wa kusimama, na kumakinisha (kutuliza) paji lake la uso na pua yake ardhini na kuachanisha mikono yake na mbavu zake, na kuachanisha tumbo lake na mapaja yake, na mapaja yake kuyaachanisha na miundi yake, na kusimamisha nyayo zake, na kuweka matumbo ya miguu katika ardhi kwa kuitawanya, na kuweka mikono yake usawa wa mabega yake hali ya kuachanisha vidole anaposujudu, na kuvielekeza kibla vidole vyake vikiwa vimeshikanishwa, na aiguse moja kwa moja sehemu anayoswalia kwa mikono yake na paji lake na kusimama kwake kuelekea kwenye rakaa kuwe ni upande wa mbele ya miguu yake akiegemea kwa miguu yake mapaja yake, na kukunjua miguu wakati wa kukaa kati ya sijida mbili, na kuleta tashahudi na kuukalia mguu wa kushoto ukiwa umechomoza upande wa kulia na kuusimamisha mguu wa kulia katika rakaa ya pili, na kuweka mikono yake juu ya mapaja yake kwa kuikunjua katika hali ya kushikanisha vidole na kuvielekeza kibla akiwa kati ya sijida mbili katika tahiyyatu, na kukunja kidole kidogo na kinachofuata toka upande wa kulia na kuviringisha kidole gumba pamoja na kidole cha kati na kuashiria kwa kidole cha shahada na kugeuka kuliani na kushotoni katika salamu na kuupendelea upande wa kushoto zaidi kuliko kulia katika kugeuka.

Ama kusujudu kwa kusahau amesema imamu Ahmad anahifadhi kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake mambo matano: Alitoa salamu kwa rakaa mbili na akasujudu -sijida ya kusahahu-, na akatoa salamu kwa rakaa tatu kisha akasujudu -sijida ya kusahau- na pia alisujudu sijida ya kusahau alipozidisha au kupunguza, na akasimama kutoka katika rakaa ya pili bila kukaa Tashahudi. Amesema Alkhatwabi kuwa: kinachozingatiwa kwa wasomi ni hadithi hizi za maswahaba watano: yaani; Hadithi ya bin Masud na Abii Said na Abii Huraira na bin Buhainat na kusujudu kwa kusahau ni sheria, sawa mtu awe kazidisha au kupunguza, au kutia shaka katika swala ya faradhi au ya sunna, isipokuwa shaka ikizidi inakuwa ni wasiwasi hivyo ataachana nao. Na vile vile katika Udhu na kuoga na kuondoa Najisi, basi wakati wowote akizidisha katika swala hiyo kisimamo au kurukuu au kusujudu au kukaa kwa makusudi hubatilika swala yake, na ikiwa ni kwa kusahau basi atasujudu sijida ya kusahau kwa maneno yake Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Atakapozidisha mtu au akapunguza katika swala yake Basi na asujudu sijida mbili" Ameipokea Imamu Muslim Na atakapokumbuka atarudi katika utaratibu wa swala pasina ya kuleta Takbira, na ikiwa atazidisha rakaa moja atakatiza pale atakapokumbuka, na ataendelea na kitendo chake kile kilichokuwa kabla ya kuzidisha, na wala asilete tahiyatu ikiwa alishaileta, kisha atasujudu sijida ya kusahau na atatoa salamu, na wala asiizingatie ile rakaa iliyozidi na wala asiihesabu, ikiwa kama yeye ndiye imamu au anasali peke yake akakumbushwa na watu wawili waaminifu, kuwa hiyo rakaa imezidi itamlazimu kwake kurudi, na wala hatorudi ikiwa atakumbushwa na mtu mmoja isipokuwa atakapokuwa na yakini kuwa yuko sawa, kwani Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hakurudi kwa kauli ya dhulyadaini peke yake.

Na wala haibatiliki swala kwa kutenda kitendo kidogo, kama mfungulia mlango Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Aisha na kumbeba kwake Umama na kumweka chini, na ikiwa ataleta kauli ambayo ni sheria katika swala lakini si mahala pake, kama vile kusoma Qur'ani katika kukaa na kuleta Tashahudi katika kusimama basi kufanya hivyo hakubatilishi swala.

Na inampasa kusujudu kwa kusahau kwake, kwa ujumla wa kauli yake -Rehema na Amani ziwe juu yake: (Ikiwa atasahau mmoja wenu basi na asujudu sijida mbili za kusahau) Na ikiwa atatoa salamu kabla ya kuitimiza kwa makusudi hubatilika swala yake na ikiwa ni kwa kusahau kisha akakumbuka kwa muda mfupi ataitimiza swala yake hata kama atakuwa ametoka msikitini au akaongea jambo dogo kwa maslahi ya swala, na ikiwa ataongea kwa kusahau au akalala na akaongea au akaponyokwa na ulimi wakati wa kusoma kwake likamtoka neno lisilokuwa Qur'ani haibatiliki swala yake.

Na ikiwa atasahau nguzo isiyokuwa Takbira ya kuhirimia swala akaikumbuka wakati wa kusoma katika rakaa baada ya hiyo, itakuwa imebatilika ile aliyoiacha na inakuwa hiyo nyingine ni badala ya ile aliyoikosea, na wala harudii kuifungua swala upya, amesema maneno hayo Imamu Ahmad, na ikiwa atakumbuka kabla ya kuanza kusoma, atairudia na ataileta na ya baada yake, na ikiwa atasahau tashahudi ya kwanza na akainuka itamlazimu kurudi na kuileta ikiwa hajakamilisha kusimama, kwa mujibu wa hadithi ya Mughiirat ameipokea Abuu Daud, Na inamlazimu maamuma kumfuata imamu, na inaporomoka Tashahudi kwake na atasujudu sijida ya kusahau, na atakayetilia mashaka idadi ya rakaa alizoswali atatakiwa kujijengea uhakika, na maamuma wakati wa shaka atafuata kitendo cha imamu wake. Na hata kama atamkuta imamu amerukuu na akatia shaka kuwa je ameinua imamu kichwa chake kabla hajamkuta akiwa karukuu hiyo rakaa haitohesabika, na ikiwa atachukulia kuwa ni hakika hajamkuta imamu amerukuu atatekeleza kilichobakia na maamuma ataileta ile rakaa aliyoichelewa baada ya imamu kutoa salamu, na atasujudu sijida ya kusahau, Na siyo haki ya maamuma kuleta sijida ya kusahau isipokuwa atakapokuwa imamu wake alisahau basi atasujudu pamoja naye, hata kama hajakamilisha Tashahudi kisha atakamilisha baada ya kusujudu kwake, na aliyetanguliwa atasujudu kwa kutoa kwake salamu pamoja na imamu wake katika hali ya kusahau na kusahau akiwa pamoja naye na atakapokuwa peke yake, na sehemu ya kusujudu ni kabla ya kutoa salamu isipokuwa ikiwa atatoa salamu kwa sababu ya kupunguza rakaa moja au zaidi, kutokana na Hadithi ya Imraan na Dhulyadain, isipokuwa atakapo chukulia kuishinda dhana na akawa na uhakika, ikiwa tutasema hivyo basi inapendeza asujudu baada ya kutoa salamu, kutokana na hadithi ya Ally na bin Masoud, Na ikiwa atasahau kuleta sijida kabla ya kutoa salamu au baada yake, ataileta sijida hiyo kama ikiwa haukupita muda mrefu, na sijida ya kusahau na anachosema humo na baada ya kunyanyuka ni kama anachosema katika sijida ya swala ya kawaida.

Mlango wa Ubora wa Swala ya kujikurubisha kwa Allah.

Amesema Abul Abbas: Kujikurubisha hutumiwa kukamilisha swala ya faradhi siku ya kiyama, ikiwa atakuwa hajatimiza swala yake, na kuna hadithi iliyotegemezwa kwa Mtume na vile vile Zakkah na matendo mengine, na tendo bora la kujikurubisha kwa Allah ni Kupigana jihadi, kisha vinavyoambatana na jihadi katika kutoa matumizi na kisha kujifunza elimu na kuifundisha, Amesema Abuu Dar'daa: Mjuzi na mwenye kijifunza wana malipo sawa, na watu wengine wote waliobakia si wenye maendeleo na hawana kheri, na imepokelewa toka kwa Ahmad: Kutafuta elimu ni katika matendo bora kwa yule atakaye takasa nia yake, na akasema: kujikumbusha elimu baadhi ya nyakati za usiku kunapendeza zaidi kwangu kuliko kisimamo cha usiku wake. Na akasema: ni wajibu kwa mtu atafute elimu itakayoisimamisha dini yake, akaulizwa mfano wa jambo gani? Akasema: jambo ambalo hapaswi kutolijua, kama swala yake na funga yake, na mfano wa hayo kisha baada ya hayo ni swala, kwa hadithi: "Kuweni na msimamo na wala hamtoweza kuyatenda yote yaliyo mema, na tambueni ya kuwa amali bora katika matendo yenu ni swala" Kisha baada ya hapo kuna mambo yenye manufaa zaidi, miongoni mwake ni kumtembelea mgonjwa au kukidhi haja ya muislamu, au kusuluhisha kati ya watu, kwa kauli yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-: "Hivi nisikupeni habari ya matendo yenu yaliyo bora? na yaliyo bora kuliko hata daraja ya swaumu na swala? Nikuwasuluhisha ndugu wa karibu, kwani kuharibika ndugu wa karibu inatosha kuwa ni kinyoleo chenye kuinyoa dini". Ameisahihisha Tirmidhiy Na akasema Ahmad: Kulifuata Jeneza ni bora kuliko swala, na kila chenye manufaa kinazidiana manufaa yake, kutoa sadaka kumpa ndugu wa karibu mwenye kuhitaji ni bora kuliko kumwacha huru mtumwa, na ni bora kuliko sadaka ya kumpa asiyekuwa ndugu wa karibu, isipokuwa akiitoa wakati wa njaa na akaongezea na hijjah, na imepokelewa kutoka kwa Anas hadithi Marfu'u kutoka kwa Mtume: "Yeyote atakayetoka katika kutafuta elimu basi huyo yuko katika njia ya Mwenyezi Mungu mpaka atakaporejea". Amesema Tirmidhiy: Hadithi hii ni Hassan na ina daraja ya gharibu. Amesema Sheikh: Kujifunza Elimu na kuifundisha inaingia katika Jihadi na ni aina yake, na akasema: Kujikita katika ibada kwenye masiku kumi ya dhul-hijjah mchana na usiku ni bora kuliko Jihadi ambayo hajafa humo wala kupoteza mali yake, na imepokelewa kutoka kwa Ahmad akisema kuwa; Hakuna chenye kufanana na Hijja kutokana na tabu ipatikanayo humo, na katika viwanja hivyo vya hijja na kuna maonyesho na matukio ambayo hayana mfano wake katika uislamu. Jioni ya siku ya Arafa kuna kuchosha mwili na kutumia mali, na imepokelewa kutoka kwa Abuu Umaama kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- Ni matendo gani yaliyo bora?Akasema: "Shikamana na kufunga kwani hakuna mfano wake" Ameipokea Ahmad na wengine kwa Isnad nzuri, Na amesema sheikh: yawezekana ikawa kila ibada ni bora kwa wakati wake, kwa kufanya kwake Mtume-Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- na Makhalifa kwa kiasi cha mahitajio na maslahi, na mfano wake ni kauli ya Ahmad: Angalia lililo na maslahi zaidi na moyo wako na ulifanye. Na akaupa nguvu Ahmad ubora wa kufikiri kuliko kuswali na kutoa sadaka, huenda ikaelekeza toka kwake kuwa matendo ya moyoni yana ubora zaidi kuliko matendo ya viungo, na kuwa makusudio ya kuamiliana ni matendo ya viungo, na linaungwa mkono hilo na hadithi: "Matendo yapendezayo zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni kupenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuchukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu" Na Hadithi "Kitu cha Thamani zaidi anachokimiliki mwanadamu ni Imani"

"Na matendo ya kujikurubisha yenye nguvu zaidi ni swala ya kupatwa kwa jua, kisha swala ya witiri, kisha swala ya sunna ya Alfajiri, kisha Magharibi, kisha sunna zingine zilizobakia, na wakati wa swala ya witiri ni baada ya swala ya Ishaa mpaka kuchomoza alfajiri, na bora zaidi ni mwisho mwa usiku kwa mwenye uhakika wa kusimama wakati huo na ikiwa hawezi ataswali witiri kabla ya kulala, na uchache wake ni rakaa moja, na wingi wake ni rakaa kumi na moja, na ni bora atoe salamu katika kila rakaa mbili kisha alete witiri kwa rakaa moja, na ikiwa ataswali tofauti na hivyo kama ilivyothibiti kutoka kwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- basi ni vizuri pia, uchache wa ukamilifu ni rakaa tatu, na bora zaidi ni kutoa salamu mbili, na inafaa kutoa salamu moja, na inafaa kama swala ya Magharibi".

Na sunna zilizo katika mpangilio maalumu- ni kumi, na kuziswali nyumbani ni bora zaidi, nazo ni rakaa mbili kabla ya swala ya Adhuhuri na rakaa mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya magharibi na rakaa mbili baada ya Ishaa na rakaa mbili za Alfajiri

Na azifupishe rakaa mbili za swala ya Alfajiri na asome hapo sura mbili za Ikhlaas, (Qul huwallaahu, na kaafirun) au asome katika rakaa ya kwanza, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Semeni tumemwamini Mwenyezi Mungu na yote tuliyoteremshiwa} Aya ambazo ziko katika Suratil Baqara, na katika rakaa ya pili atasoma: {Sema Enyi mliopewa kitabu njooni katika neno lilo sawa kati yetu na nyie } Mpaka mwisho wa Aya Na anaruhusiwa kuziswali akiwa katika kipando.

Na hakuna sunna ya kabla ya ljumaa na baada yake kuna rakaa mbili au Nne, na zinatoshelezwa na sunnah ya maamkizi ya msikiti (Tahiyyatul masjid), na ni sunna kutenganisha kati ya swala ya faradhi na sunna kwa kuongea au kusimama, kwa mujibu wa Hadithi ya Muaawiya, na atakayepitwa na sunnah hizo inapendeza kwake kuzilipa na inapendeza aziswali kati ya Adhana na Iqama.

Na swala ya Tarawehe ni sunnah aliyoianzisha Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani, na kuiswali katika jamaa ni bora zaidi, na husoma imamu kwa sauti kutokana na ilivyonukuliwa kutoka kwa waliokuja baada ya wema waliopita, na kutoa salamu katika kila rakaa mbili kwa hadithi: "Swala ya usiku ni rakaa mbili mbili" Na muda wake ni baada ya swala ya Ishaa, na sunnah ziswaliwe kabla ya witiri mpaka kuchomoza Alfajiri, kisha ndio aleta witiri baada yake, na kama ataswali Tahajudi basi ataifanya witiri iwe baada ya Tahajudi, kwa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani, "Fanyeni -Swalini -mwisho wa swala zenu za usiku kuwa witiri". Na ikiwa atapenda kumfuata imamu yule mwenye kawaida ya kuswali tahajudi, atasimama pale ambapo imamu atatoa salamu, basi ataswali rakaa moja, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Yeyote atakaye simama kuswali na imamu mpaka akamaliza imamu anaandikiwa kuwa amesimama usiku kucha" Ameisahihisha Tirmidhiy

Na inapendeza kuihifadhi Qur'ani, kwa makubaliano ya wanazuoni wote, na Qur'ani ni bora kuliko adh-kari zote zilizobakia, na ni wajibu kuhifadhi kilicho wajibu katika swala, na mlezi wa mtoto ataanza kumhifadhisha Qur'ani kabla ya kujifunza elimu isipokuwa kama kutakuwa na uzito, na ni sunnah kuimaliza kila wiki mara moja na chini ya wiki wakati mwingine, na ni haramu kuchelewa kuisoma ikiwa atahofia kuisahau, na atasema Audhubillahi kabla ya kusoma na atapupia kufanya ikhlaas na kuzuia kinachokwenda kinyume na ikhlaas (kutakasa nia), na atamaliza wakati wa masika mwanzo wa usiku na wakati wa kiangazi atamaliza mwanzo wa mchana. Amesema Twalha bin Masrif: Niliwakuta watu wa kheri katika Umma huu wakipendelea hivyo, na wakisema : Akimalizia usomaji wa Qur'ani mwanzo mwa mchana Malaika wanamswalia mpaka jioni, na akimaliza mwanzo wa usiku Malaika wanamswalia mpaka asubuhi Ameipokea Al-daaramiy kutoka kwa Saa'd bin Abii Waqqaas na sanadi yake ni nzuri, Na afanye sauti yake kuwa nzuri wakati wa kusoma Qur'ani na aisome kwa utaratibu ulio mzuri. Na asome kwa huzuni na mazingatio na kumuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu katika Aya za rehema, na aombe kinga kwa Mwenyezi Mungu anapofika katika Aya za adhabu, na wala asidhihirishe sauti yake kwa wenye kuswali au waliolala akawaudhi, na hakuna ubaya ikiwa atasoma akiwa amesimama au amekaa, au yuko juu ya kipando au anatembea kwa miguu. Na wala si vibaya kusoma Qur'ani njiani na wala mtu akiwa na hadathi ndogo (akiwa katengukwa udhu), na inachukiza kuisoma maeneo machafu, na inapendeza kujikusanya kwa ajili ya kuisoma na kujiburudisha kutokana na sauti ya msomaji, na wala asiongee wakati huo maneno yasiyokuwa na faida, na anachukia Imamu Ahmad ikisomwa kwa haraka haraka, na anachukiza kusomwa kwa kunung'unika ambako kunafanana na mziki, na wala siyo karaha kuisoma kwa kurudiarudia, na atakaye sema katika Qur'ani kwa rai yake au kwa kitu asichokijua basi na ajiandalie makazi yake motoni, na amekosea hata kama atakuwa amepatia.

Na wala haifai kwa mwenye hadathi kuugusa msahafu, na yampasa kuubeba kwa kishikio na katika mkono wa nguo yake na anatakiwa kufungua kurasa zake kwa kutumia kijiti na mfano wake, na anaruhusiwa kugusa msahafu wa tafsiri na vitabu ambavyo ndani yake kuna Qur'ani na inafaa kwa asiyekuwa na udhu kuiandika pasina kuigusa na kuchukua ujira kwa kuzitoa nakala na inafaa kuuvisha hariri, na haifai kuipa Qur'ani mgongo au kuinyooshea miguu na mfano wake katika mambo yenye kupelekea kuacha kuitukuza. Na inachukiza kuupamba kwa kutumia dhahabu au fedha na kuandika makumi na majina ya sura na idadi za Aya na vinginevyo katika vitu ambavyo havikuwepo wakati wa maswahaba.

Na ni haramu kuiandika Qur'ani au kitu chochote ambacho ndani yake kuna utajo wa Allah kwa kitu ambacho si twahara. Ikiwa ataandika nacho au akaandika juu yake basi atawajibika kuosha alichokiandika, na ikiwa msahafu umeoza au umechakaa utazikwa kwa sababu Othman Radhi za Allah Ziwe juu yake aliizika misahafu baina ya kaburi na Membari.

Na inapendeza kuswali swala za sunna nyakati zote isipokuwa nyakati zilizokatazwa, na swala za usiku zimependekezwa na ni bora zaidi kuliko swala za mchana. Na baada ya kulala ni bora zaidi kwa sababu kuamka kutoka usingizini hakuwi isipokuwa baada ya kulala, na akiamka atamtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu na atasema kilichopokelewa, na miongoni mwavyo: "Laa ilaaha illa llahu wah'dahuu laa shariikalahuu, lahul mulku walahul hamdu wahuwa alaa kulli shain qadiir, Alhamdulillah wasub-haanallah walaa ilaaha illa llah wallahu akbar walaa haula walaa quwwata illa billah" Kisha ikiwa atasema: "Allahumma ghfirliy au akaomba atajibiwa, na ikiwa atatawadha na akasali, itakubaliwa swala yake kisha atasema: Alhamdulillah ladhii ah-yaaniy baada maa amaataniiy wa ilaihi nushuur, laa ilaaha illa anta wahdaka laa shariika laka, sub-haanaka astagh-firuka lidhambii waas-aluka rahmataka Allahumma zidniiy il-man walaa tuzigh qalbiiy ba'ada idh- hadaitaniiy wahab lii minladunka rahmatan innaka antal wahhaab, Alhamdulillahi lladhi radda alaiyya ruuhii waafaniiy fii jasadii adhina lii bidhikrihi, kisha atapiga mswaki na akisimama kuswali atafungua swala kwa dua ya ufunguzi iliyoandikwa na ikiwa atataka atafungua na dua nyingine yoyote kama kusema kwake: Allahumma lakal hamdu Anta nuurus samaawaati wal ardhwi waman fiihinnah walakal hamdu, Anta Qayyuumus samaawaati wal-ardhwi waman fiihinnah walakal hamdu, Anta malikus samaawaati wal ardhwi waman fiihinna walakal hamdu, Antal haqqu waliqaauka haqqu waljannatu haqqu wannaru haqqu wannabiyyuuna haqqu, was saatu haqqu, Allahuma laka as-lamtu wabika Aamantu waalaika tawakkaltu wailaika uniibu wabika Khaaswamtu wailaika haakamtu fagh-fir-lii maa qaddamtu wamaa akh-khartu wamaa as-rartu wamaa aalantu wamaa anta aalamu bii minniy, Antal muqaddim wa antal muakhir laailaha illa anta wala quwwata illa bika' Na akipenda atazidisha: "Allahumma Rabba Jibrili wa Miikaaiil wa israfiil Faatwiri samaawaati wal ardhwi Aalimul ghaibi wa shahaadah Anta tahkumu Baina ibaadika fiimaa kaanuu fiihi yakhtalifuun, Ihdiniiy limakhtulifa fiihi minal haqqi Innaka Tahdii man tashaau ilaa swirattiwil mustaqiim".

Na ni sunna afungue swala yake ya Tahajudi kwa kuswali rakaa mbili nyepesi na iwe ni swala ya kujikurubisha anayodumu nayo na ikimpita atailipa.

Na inapendeza aseme wakati wa asubuhi na jioni: yale yaliyopokelewa, vile vile wakati wa kulala na kuamka na kuingia nyumbani na kutoka na kwinginepo, na swala ya kujikurubisha kuiswalia nyumbani ni bora zaidi na kuiswali kwa siri akiwa si katika watu ambao ni sheria kwao kuiswali kwa jamaa, na hakuna ubaya kuiswali kwa jamaa ikiwa haitofanywa kuwa nikawaida na inapendeza kuleta Isti-gh-faar (kuomba msamaha) mwisho wa usiku na kuzidisha kuleta is-tigh-faar, na itakayempita swala ya tahajudi basi atailipa kabla ya sala ya Adhuhuri, wala haifai swala ya kujikurubisha kuisali kwa kulala chali.

Na ni Sunnah kuswali swala ya Dhuha, na wakati wake ni kuanzia kuondoka wakati uliokatazwa kuswali mpaka kabla kidogo ya kupinduka jua, na kuiswali pindi joto linapokuwa kali ni bora zaidi, na swala yenyewe ni rakaa mbili na akizidisha basi ni vizuri.

Na ni Sunnah kusali swala ya Isti-khaara, pindi atakapokuwa amekusudia jambo fulani, basi ataswali rakaa mbili zisizokuwa za faradhi kisha atasema: Allahumma Inniy As-takhiiruka bi ilmika, wa astaq-diruka biqud-ratika wa as-aluka min fadhw-lika al-adhwiim, fa innaka taqdiru walaa aq-diru wata'alamu walaa a'alamu wa anta allaamul ghuyuub, Allahumma inkunta ta'alamu anna haadhal amru- na atataja jambo lenyewe -Khairun lii fii diiniy wadunyaaya wamaashiiy wa aaqibatu amriy (Ajiluhuu wa Aajiluhu) Faq-dirhu lii wayassirhuu lii thumma baarik liiy fiihi, wa in kunta ta'alamu anna haadhal amru sharrun lii fii diiniy wa dun yaaya wa maashiy wa Aaqibatu Amriy Fas-rif-huu anniy was-rifniiy anhu waqdir liiyal khaira haithu kaana thummar-dhiniiy bihi" TAFSIRI YAKE: "Ewe Mwenyezi Mungu, hakika mimi ninakutaka uchaguzi kupitia elimu yako, na ninakuomba uwezo kupitia uwezo wako, na ninakuomba unipe kutoka katika fadhila zako tukufu, kwani wewe unaweza na mimi siwezi, na unajua na mimi sijui na wewe ni mjuzi wa yaliyofichikana, Ewe Mola wangu ikiwa unajua kuwa jambo hili (Anataja shida yake) ni kheri kwangu katika dini yangu na dunia yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu (iwe kwa haraka au kwa kuchelewa) basi nakuomba niwezeshe na unifanyie wepesi kwangu kisha unibariki mimi ndani ya jambo hili, Na ikiwa unajua kuwa jambo hili ni shari kwangu katika dini yangu na dunia yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu, basi liepushe nami na uniepushe nalo, kisha nipangie heri mahala popote itakapokuwa kisha niridhishe nayo". Kisha anataka ushauri kwa watu, na wala asiwe wakati wa kusali istikhaara amekwisha kuazimia kufanya au kutofanya.

Ni Sunnah kuswali Tahiyyatul masjidi, na sunna ya udhu (na kuamka usiku kati ya Ishaa na Alfajiri) na kusujudu sijida ya kisomo ni sunna iliyotiliwa mkazo na siyo wajibu, kwa mujibu wa maneno ya Omar: "Mwenye kusujudu hakika amepatia na asiyesujudu hana dhambi" Ameipokea Maaliki katika muwattwai, na ni sunna pia kwa msikilizaji. Na mpanda kipando aashirie katika kusujudu kwake kule ulipo uso wake, na mwenye kwenda kwa miguu atasujudu ardhini akielekea kibla na wala hasujudu mwenye kusikiliza, kwa ilivyopokelewa kutoka kwa maswahaba, na akasema bin Masoud kumwambia msomaji; naye ni kijana mdogo "Sujudu, kwa hakika wewe ni Imamu wetu"

Na inapendeza kusujudu kwa ajili ya kushukuru neema ya wazi inapojirudia, au jambo jipya linalomuhusu. Na aseme anapomuona aliyepewa mtihani katika mwili wake au dini yake; 'Al-hamdulillahi ladhii Afaaniiy mimmabtalaaka bihi wa fadhwwalaniiy a'laa kathiirin mimman khalaqa Taf-dhwiila'. Tafsiri yake: Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu aliyenipa afya mimi kwa hilo alilokupa mtihani wewe, na akanifanya kuwa bora kuliko wengi miongoni mwa wale aliowaumba vizuri.

Na nyakati zilizokatazwa kusali ni tano: Baada ya swala ya Al-fajiri mpaka kuchomoza jua, na baada ya kuchomoza mpaka liinuke kiasi cha mkuki, na jua litakapo kuwa limesimama katikati mpaka lipinduke, na baada ya swala ya Alasiri mpaka kukaribia kuzama na baada ya hapo mpaka kuzama, na inafaa wakati huo kulipa kadha ya swala ya faradhi, na kutekeleza nadhiri na rakaa mbili za twawafu, na kurudia kuswali swala ya jamaa kama kutaqimiwa hali yakuwa yeye yupo msikitini, na hukubalika sala ya jeneza katika nyakati mbili ndefu.

(Mlango wa Swala ya Jamaa)

uchache wa swala za faradhi ni rakaa mbili katika swala isiyokuwa ya Ijumaa, nayo ni wajibu kwa kila mtu sawa yuko safarini au nyumbani, hata katika wakati wa hofu, kwa mujibu wa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na ukiwa nao na ukawasimamishia swala } Mpaka mwisho wa Aya. Na swala ya jamaa inazidi swala ya mwenye kuswali peke yake kwa daraja Ishirini na Saba, na huswaliwa msikitini. Na kuswaliwa katika Al-kaaba ni bora zaidi, na vile vile kuswaliwa katika jamaa ya watu wengi na kuswaliwa mbali, na wala asiswalishe imamu katika msikiti ila imamu aliyepangwa maalumu isipokuwa kwa idhini yake, ila atakapochelewa si vibaya akaswalisha mtu yeyote kwa kufanya kwake Abuubakar hivyo na Abdurahmani bin Auf, Na ikishasimamishwa swala ya faradhi hairuhusiwi kuswali swala ya sunnah, na kama itasimamishwa na yeye yuko ndani ya swala basi ataitimiza kwa ufupi, na atakaye kuta rakaa moja pamoja na imamu basi atakuwa amekuta jamaa, na hupatikana rakaa kwa kurukuu pamoja na imamu, na inatosheleza Takbira ya kuhirimia badala ya Takbira ya kurukuu, kwa kitendo cha Zaid bin Thaabit na bin Omari na wala hakuna swahaba yeyote aliyewapinga, na kuzileta zote mbili-Takbira ya kuhirimia na takbira ya kurukuu ni bora zaidi ili kujiondoa kwenye utata wa mwenye kuifanya kuwa wajibu, na ikiwa atamkuta imamu baada ya rukuu basi atakuwa hajapata rakaa, na wakati huo ni wajibu kwake kumfuata imamu, na ni sunnah kuunga pamoja naye, na wala asisimame aliyechelewa isipokuwa baada ya imamu kutoa salamu ya pili, na ikiwa atamkuta katika sajida ya kusahau baada ya kutoa salamu hatounga pamoja naye, na ikiwa itampita swala ya jamaa inapendeza aswali pamoja na imamu, kwa mujibu wa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Ni nani atatoa swadaka kwa mtu huyu akaswali pamoja naye" Na wala si lazima kusoma maamuma nyuma ya imamu, kwa mujibu wa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na isomwapo Qur’ani isikilizeni, enyi watu, na mnyamaze ili muielewe kwa matarajio kwamba Mwenyezi Mungu Awarehamu kwayo". Amesema Ahmad kuwa wamekubaliana maulamaa kuwa Aya hii makusudio yake ni katika swala. Na ni Sunna kusoma pale ambapo imamu hasomi kwa sauti, wengi katika wajuzi miongoni mwa maswahaba na waliokuja baada yao wao wanaona kuwa kusoma nyuma ya imamu atakaposoma kwa siri ni kujitoa katika utata kwa yule anayewajibisha hilo, lakini tunaacha kusoma pindi anaposoma imamu kwa sauti kwa mujibu wa ushahidi, na ni sheria kusoma baada ya imamu wake pasina kupingana napo ni baada ya kumaliza imamu kusoma, na ikiwa visomo vitagongana basi ni karaha kufanya hivyo, na ni haramu kushindana na imamu kwenye kusoma, na ikiwa maamuma atasujudu au kurukuu kabla ya imamu kwa kusahau atarudi ili afanye hivyo baada ya kufanya imamu, na ikiwa hakurudi kwa makusudi na anajua kuwa kakosea basi swala yake itakuwa batili, na ikiwa atakwenda tofauti na imamu pasina yakuwa na udhuru kama kumtangulia imamu, na ikiwa kafanya hivyo kwa dharura ya kusinzia au kupitiwa au imamu alifanya haraka na akamkuta, na ikiwa atamuacha kwa rakaa moja basi atamfuata katika rakaa zilizobakia katika swala yake na atailipa ile iliyompita baada ya imamu kutoa salamu, na ni Sunna kwa imamu ikiwa litawatokea baadhi ya maamuma jambo linalowafanya kutoka ndani ya swala basi afupishe swala, na inachukiza kwenda haraka haraka itakayomzuia maamuma kufanya baadhi ya mambo ambayo ni sunnah.

Na ni Sunna kurefusha kisomo katika rakaa ya kwanza iwe ndefu kuliko rakaa ya pili, na ni Sunnah kwa imamu kumsubiri aliyechelewa ili aikute rakaa ikiwa hatowachosha maamuma.

Na imamu bora ni yule mjuzi zaidi wa kitabu cha Mwenyezi Mungu. Na kuhusu Mtume kumtanguliza Abuubakar -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- licha yakuwa wengine ni wajuzi zaidi wa kitabu cha Mwenyezi Mungu kama vile Ubaiyyah na Muadhi akajibu hilo Ahmad kuwa ni ili wafahamu kuwa yeye anatangulizwa ili awe ni kiongozi mkubwa, na akasema mwingine alipomtanguliza pamoja nakauli yake kuwa Anawaongoza watu mjuzi zaidi wa kitabu cha Mwenyezi Mungu, na ikiwa watakuwa kwenye kusoma wako sawa basi atatangulia mjuzi zaidi wa sunnah ikajulikana kuwa Abuubakar ni msomaji na mjuzi zaidi yao, kwa sababu wao walikwa hawavuki chochote katika Qur'ani mpaka wamalize kujifunza maana zake na kuifanyia kazi, kama alivyosema bin Masoud: Alikuwa mtu katika sisi akijifunza Aya kumi katika Qur'ani hazivuki mpaka amalize kujifunza maana zake zote na kuzifanyia kazi, na ameipokea Muslim kutoka kwa Abuu Masoud Al- badiriy (anairufaisha). "Anawaongoza watu yule mjuzi zaidi wa kitabu cha Mwenyezi Mungu, na ikiwa kwenye kusoma wako sawa basi atawaongoza mjuzi zaidi wa Sunna na ikiwa kwenye Sunna wako sawa basi atawaongoza yule aliyetangulia kuhama na ikiwa kuhama kwao ni sawa basi ataongoza mkubwa wao kiumri"

Na mtu asimuongoze mwenzake katika utawala wake, na wala asikae nyumbani kwake kwa ajili ya kukirimiwa isipokuwa kwa Idhini yake, na imenukuliwa kutoka katika sahihi mbili: "Anawaongozeni mkubwa wenu" Na katika baadhi ya matamshi ya bin Masoud: {basi ikiwa kwenye kuhama walihama sawa basi atatangulia wa mwanzo wao kusilimu}

Na yeyote atakaye swalisha kwa malipo hawatoswali watu nyuma yake, Amesema Abuu Daudi: Aliulizwa Ahmad kuhusu Imamu anayesema: Nitawaswalisha Ramadhani kwa kiasi hiki na hiki, akasema: Ninamuomba Mwenyezi Mungu msamaha na ni nani atakaye swali nyuma ya mtu huyu?! Na wala hakusaliwi nyuma ya Imamu ambaye hawezi kusimama isipokuwa ikiwa ndiye Imamu wa mtaa-naye ni yule Imamu wa msikiti aliyechaguliwa kwa kazi hiyo -akipata tatizo wataswali nyuma yake wakiwa wamekaa, na ikiwa ataswali Imamu hali yakuwa ametengukwa na Udhu au ana najisi na hakujua kuwa ana najisi ila baada ya kumaliza swala waliokuwa wanaswali nyuma yake hawatarudia, na imamu atarudia swala peke yake ikiwa aliswali bila yakuwa na udhu, na inachukiza kuwasalisha watu wengi ambao wana mchukia kwa haki, na ina faa kwa mtu aliyetawadha kutimiza swala nyuma ya aliye tayamamu.

Na ni Sunnah kusimama maamuma nyuma ya Imamu, kwa mujibu wa hadithi ya Jaabir na Jabbaar waliposimama kuliani kwake na kushotoni mwake aliwashika kwa mikono yake na akawasimamisha nyuma yake. Imepokelewa na Imamu Muslim Na ama swala ya bin Masoud aliwasalisha Al-qama na Al-as-wad na hali yakuwa yeye yuko katikati yao, ametoa majibu bin Sirin yakuwa sehemu ilikuwa ni finyu. Na kama ikiwa maamuma yuko peke yake basi atasimama upande wa kulia wa Imamu, na ikiwa atasimama upande wa kushoto wa Imamu atamzungusha kumleta upande wa kulia, na wala hilo halibatilishi Takbira yake ya kuhirimia na ikiwa atawasalisha mwanaume na mwanamke atasimama mwanaume upande wake wa kulia na mwanamke atasimama nyuma yake, kwa mujibu wa Hadithi ya Anas aliyoipokea Muslim, na kuwa karibu na swafu ni bora na pia kukaribiana swafu na kumuweka katikati ya swafu, kwa mujibu wa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Muwekeni kati imamu na mzibe mwanya" Na inafaa kupanga swafu na watoto wadogo, kwa maneno ya Anas; nilipanga swafu mimi na yatima na Bibi kizee akawa nyuma yetu, na ikiwa ataswali mbali peke yake haitokubalika kuwa ni jamaa, na ikiwa maamuma anamuona imamu au aliye nyuma yake swala ni sahihi hata kama swafu hazikushikana na hivyo hivyo ikiwa mmoja wao hamuoni mwenzake ikiwa atasikia Takbira ya kumuwezesha kumfuata imamu kwa kusikia takibira ni kama vile anamuona, na ikiwa kati yao kuna njia na swafu zikakatika haikubaliki, na bin Qudaama na wengine wakachagua kuwa ikiwa hivyo haizuii kumfuata imamu kwa kuwa hakuna dalili wala kukubaliana kwa wanachuoni katika hilo.

Na ni karaha Imamu kuwa juu ya Maamuma, amesema bin Masoud kumwambia Hudhaifa: Hivi hukujua kuwa wao walikuwa wakikatazwa kufanya hivyo? Akasema: Hapana, bali nilikuwa nikijua hilo. Kaipokea Imamu Shafiy kwa Isnadi ya watuTthiqa, (waaminifu) Na wala si vibaya ikiwa ni juu kidogo kama vile ngazi ya Mimbari, kwa mujibu wa Hadithi ya Sahli kwamba Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: Aliswali juu ya mimbari kisha akateremka kinyumenyume na akasujudu, Mpaka mwisho wa Hadithi. Na wala si vibaya kuwa maamuma juu kwa sababu Abu Huraira alisali juu ya msikiti kwa kufuata swala ya Imamu. Ameipokea Imamu shafi, Na ni karaha imamu kuswali swala ya sunna katika sehemu aliyosalia sala ya faradhi, kwa hadithi ya Mughiira imeinuliwa hadithi hii (Marfu'u) ameipokea Abuu daudi, lakini alisema Ahamad kuwa; siitambui hadithi kutoka kwa mtu mwingine asiyekuwa Ally, na wala asiondoke maamuma kabla ya imamu, kwa mujibu wa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Msinitangulie kwa kurukuu wala kusujudu wala kutawanyika', Na inachukiza kwa asiyekuwa imamu kutenga sehemu katika msikiti sehemu ambayo hawezi kuswali faradhi isipokuwa mahala hapo, kwa kukataza kwake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: kukita sehemu moja kama anavyokita ngamia.

Na hupewa Udhuru wa kuacha swala ya Ijumaa na Jamaa mtu mgonjwa na mwenye kuhofia kupoteza mali yake, au kinachoweza kuihifadhi mali yake: kwa sababu tabu hupatikana kwa yaliyotajwa zaidi kuliko kuloana nguo na mvua ambayo ni udhuru kwa kukubaliana wanachuoni kwa kauli ya Umar: Alikuwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: akiita muitaji wake wakati wa usiku wa baridi kali au manyunyu wakiwa safarini, swalini kwenye vipando vyenu, wameitoa hadithi hii wao wawili na wana hadithi nyingine kutoka kwa bin Abbas kuwa yeye alisema kumwambia muadhini wake siku ya Al-jumaa palipokuwa na manyunyu : "Utakaposema Ash-hadu anna muhammadan rasuulullah, basi usiseme: Hayya alas-swalaa -njooni kwenye swala- sema: swalini Majumbani mwenu" Kana kwamba watu walimpinga katika hilo akasema: Amelifanya hilo yule ambaye ni bora kuliko mimi -anakusudia Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: Na mimi nimeona ni karaha kukutoeni mje kwenye udongo na kuukanyaga, na ni karaha kuhudhuria msikitini kwa aliyekula kitunguu swaumu au kitunguu maji na hata kama atajitenga na watu bado atawaudhi Malaika kwakuja kwake msikitini.

Swala za watu wenye Dharura.

Ni wajibu kwa mgonjwa kuswali akiwa amesimama katika swala za faradhi, kwa Hadithi ya Imrani "Swali ukiwa umesimama, ikiwa hutoweza basi ukiwa umekaa, ikiwa hutoweza basi ukiwa umelalia ubavu". Imepokelewa na Al-Bukhaariy Amezidisha imamu Nasaai "Ikiwa hauwezi basi kwa kuelekea na ataashiria kwenye kurukuu kwake na kusujudu kwake kwa kichwa chake kwa kadiri ya uwezo wake, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Ninapokuamrisheni jambo fulani basi litekelezeni kadira muwezavyo"

Na inafaa kuswali swala ya faradhi kwenye kipando kikiwa kimesimama au kinatembea kwa kuogopea kero ya tope na mvua, kwa hadithi ya Yalaa bin Umaiya imeipokelewa na Tirmidhiy na kasema: Hadithi hii inafanyiwa kazi kwa maulamaa.

Na msafiri anapunguza haswa swala za rakaa Nne, na ni hiyari yake kufungua katika mchana wa Ramadhani, na ikiwa atapata utulivu yule ambaye yampasa kukamilisha basi atakamilisha, na lau kama atakaa kwa ajili ya kukidhi shida yake bila kukusudia kukaa na wala hajui ni wakati gani atamaliza haja zake, au akazuiliwa na mvua au maradhi atapunguza wakati wote, na hukumu zinazo husiana na safari ni Nne: Kupunguza, Kukusanya, Kufuta, na kufungua.

Na inafaa kukusanya kati ya Swala ya Adhuhuri na Alasiri na kati ya Swala ya Magharibi na Ishaa katika wakati wa swala moja kwa msafiri. Na kuacha kukusanya ni bora isipokuwa kukusanya kwa aina mbili, katika viwanja vya Arafa na Muzdalifa na mgonjwa ambaye akiacha kukusanya atapata madhara; kwa sababu Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: aliwahi kukusanya swala pasina kuwa na hofu yoyote wala hakuwa safarini, na imethibiti kukusanya swala kwa mwenye damu ya Ist-haadhwa nayo ni damu ya ugonjwa. Na akatoa hoja Imamu Ahmad ya kuwa tabu ya maradhi ni zaidi ya safari na akasema Kukusanya nyumbani kunakuwa kwa dharura au shughuli, na akasema; Imekubalika kwa Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: Swala ya hofu kwa namna sita au Saba zote hizo zinafaa, ama hadithi ya Sahli hilo ndiyo chaguo langu. Swala ya hofu: Kundi moja liliunga safu pamoja na Mtume na kundi lingine likawaelekea maadui, akawaswalisha wale waliokuwa pamoja naye rakaa moja kisha wakabaki wamesimama na wakikamilisha swala wao wenyewe kisha wakaondoka, na wakaunga swafu wakiwaelekea maadui,na likaja kundi jingine Mtume akawaswalisha rakaa iliyobakia katika swala yake kisha Mtume akabakia amekaa na wao wakakamilisha wenyewe kisha akawatolesha salamu. wameafikiana hadithi hii Bukhari na Muslim, na anahaki ya kuswalisha kila kundi swala nzima na kuwatolea salamu -yaani kumaliza nao pamoja- Kaipokea Ahmad na Abuu daud na Nasaai. Na inapendeza kubeba silaha katika swala ya hofu, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na wachukue silaha zao} Na kama ingekuwa ni wajibu kungekuwa na maelekezo, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na si vibaya kwenu nyinyi ikiwa mtapatwa na maudhi yatokanayo na mvua au mkiwa safarini kuziweka chini silaha zenu} Na hofu ikizidi watasali wakiwa wanatembea kwa miguu na wakiwa wamepanda vipando sawa wawe wameelekea kibla au hawajaelekea kibla, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na ikiwa mnahofu basi swalini katika hali ya kutembea kwa miguu au mkiwa kwenye kipando} Wataashiria kwa ishara kwa kadiri ya uwezo wao na kusujudu kuna kuwa chini zaidi kuliko kurukuu, na wala haifai kuswali jamaa ikiwa haiwezekani kumfuata imamu.

(Mlango wa Swala ya Ijumaa)

Na swala ya ijumaa ni faradhi ya lazima kwa kila muislamu aliyebalehe na mwenye akili, mwanaume huru na mkazi, kwa kuzingatia kuwa wote linawahusu jina moja (muislamu), na atakayehudhuria swala ya ijumaa katika wale ambao si wajibu kwao basi itakubalika, na ikiwa atakuta rakaa moja basi ataitimiza kama swala ya ijumaa, na kinyume na hapo atatakiwa kuswali adhuhuri, na ni lazima kutanguliza hotuba mbili ambazo ndani yake kuna kumshukuru Mwenyezi Mungu na kutaja shahada mbili, na kutoa usia unaogusa nyoyo, na hii ndiyo inayoitwa hotuba, na atatakiwa kuhutubia akiwa juu ya mimbari au sehemu ya muinuko, na atawasalimia maamuma anapotoka na anapowageukia, kisha atakaa mpaka adhana inapomalizika, kwa mujibu wa hadithi ya bin Omari, aliyoipokea Abudaud, Na atakaa kidogo kati ya hotuba mbili, kama ilivyo katika sahihi mbili (kitabu cha sahihi Bukhari na Muslim) kutoka katika hadithi ya Omari, na atahutubu akiwa amesimama, kwa kufanya kwake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- na aelekee mbele ya uso wake na afupishe hotuba, na swala ya Ijumaa ni rakaa mbili na husomwa kwa sauti atasoma katika rakaa ya kwanza ya swala ya Ijumaa suratil munaafiquun au Sabbihisma na suratil ghaashia, hadithi imethibiti kwa sura zote hizo, na atasoma katika sala ya Alfajiri ya siku ya Ijumaa Alif Laam Miim ya surat Sajdah na Suratil Insaan, na haipendezi kudumu kusoma hizo hizo. Na ikiwa ljumaa itaafikiana na siku ya Eid basi ljumaa itaachwa kwa yule aliyehudhuria Eid isipokuwa imamu kwakwe hawezi kuacha .

Na ni Sunna kuswali rakaa mbili au Nne baada ya swala ya ljumaa, na ljuma haina sunna ya kabla yake bali inapendeza aswali sunna atakavyo, na ni Sunnah kuoga na kupiga mswaki na kujitia manukato na kuvaa nguo nzuri, na aende mtu mapema huku akileta takbira, na ni wajibu kufanya haraka wakati wa adhana ya pili lakini kwa utulivu na unyenyekevu na kumkaribia imamu na kuzidisha dua katika siku hiyo kwa matarajio ya kupata Saa za kujibiwa dua, na muda unaotarajiwa zaidi ni Saa za mwisho baada ya Alasiri pindi atakapokuwa mtu amejitwaharisha na akawa anasubiri swala ya magharibi kwa sababu yeye huhesabika yuko katika swala, Na azidishe kumswalia Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- usiku wake na mchana wake, na inachukiza kuruka shingo za watu isipokuwa kama ataona kuna mwanya na hawezi kufika ila kwa kufanya hivyo, na wala asimsimamishe mtu akae yeye sehemu yake, hata kama ni mtumwa wake au mtoto wake, na atakae ingia na imamu ana hutubu asikae mpaka aswali rakaa mbili fupi na wala asiongee wala kufanya upuuzi na hali yakuwa imamu anahutubu, kwa mujibu wa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Na yeyote atakaye chezea kijiwe kwa hakika amefanya upuuzi" Ameisahihisha Tirmidhiy. Na atakaye sinzia atahama kutoka alipokuwa amekaa, kwa amri ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-kuamrisha hilo ameisahihisha Tirmidhiy.

Mlango wa swala za Eid mbili:

Ikiwa haitojulikana kuwa hiyo ni siku ya Eid mpaka baada ya kupinduka jua, watatoka kesho yake na ataswalisha, na ni sunna kuswali Eidil Adh-haa na kuchelewesha Eidil fitri, na ni Sunnah kula tende kwa witri kabla ya kwenda kuswali Eidui fitri, na wala asile kwenye Eidil Adh-ha mpaka amalize kuswali, Na ikiwa ataenda na njia moja atarudi na njia nyingine, na ni Sunna kuswaliwa kwenye uwanja uliokaribu na huswaliwa rakaa mbili, ataleta takbira ya kuhirimia kisha ataleta baada yake takbira sita, na katika rakaa ya pili takbira tano na atainuwa mikono yake katika kila takbira na atasoma katika rakaa zote mbili "Sabih-sma na Suratil Ghaashiyah" na akimaliza atahutubu na wala hatohama kabla yake wala baada yake baada kutoka katika sehemu yake alipokuwa, Na ni sunnah kuleta Takbira katika Eid mbili na uileta kwa sauti misikitini na njiani na kuileta wazi wazi kwa sauti kwa watu wa vijijini na mijini, na hutiliwa mkazo kuleta takbiira katika siku mbili za Eid na wakati wa kutoka kwenda kuswali, na katika Eid Al-Adh-haa Takbira zinaanza kuletwa mfululizo kuanzia katika siku kumi za Dhul hijja na huletwa kwa siku maalumu kuanzia swala ya Al-fajiri ya siku ya Arafa mpaka mwisho wa swala ya Alasiri ya siku ya mwisho mwa siku ya kutanda nyama, na ni Sunnah kujibidisha katika kutafuta elimu yenye manufaa katika siku kumi za Dhulhijjah.

(Mlango wa Swala ya Kupatwa jua)

Na muda wake ni kuanzia kukamatwa kwa jua mpaka litakapoachiwa, na Swala hiyo ni Sunnah iliyotiliwa nguvu, sawa uwe safarini au nyumbani imetiliwa nguvu kuiswali hata kwa wanawake, na Sunnah kumtaja Mwenyezi Mungu na kuomba na kuleta Istghfaar na kuwaacha huru watumwa na kutoa sadaka, na wala swala hairudiwi ikiwa imekwisha swaliwa na jua bado halikuachiwa, bali wataendelea kumtaja Mwenyezi Mungu na kumtaka msamaha mpaka liachiwe jua, na wito wake unakuwa "As-swalaat Jaamiat" yaani amkeni tuswali swala ya pamoja, na huswaliwa rakaa mbili na husomwa kwa sauti katika rakaa zote mbili, na hurefushwa kisomo na pia hurefushwa rukuu na sujudu. kila rakaa moja kuna kurukuu mara mbili, lakini rukuu mbili hizo zinakuwa katika rakaa ya pili siyo ya kwanza, kisha atatoa shahada na kutoa salamu, na hata kama jua litaachiwa ataikamilisha swala kwa ufupi, kwa maneno yake Mtume Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-: "Basi swalini na muombe mpaka liachiliwe "

(Mlango wa Swala ya kuomba mvua)

Na Swala ya kuomba Mvua ni Sunna iliyotiliwa mkazo sawa uwe safarini au nyumbani, na sifa yake ni kama sifa ya swala ya Eid, na Ni sunnah kuiswali mwanzo wa mchana, na atoke akiwa katika hali ya kunyenyekea na kujidhalilisha, Iimethibiti hilo katika Hadithi ya bin Abbas aliyoisahihisha Al-tirmidhiy, Basi atawasalisha na atahutubu hutuba moja na atakithirisha ndani yake istigh-faar na ataomba na atainua mikono yake na kukithirisha dua na atasema: Ewe Mola wetu wa haki tunyeshelezee mvua yenye msaada nzuri yenye kuridhisha, njema na yenye kubugujika, yenye kudhihiri katika mawingu yote, inamuwafaka daima na yenye manufaa, na iwe yenye kunufaisha na isiwe yenye kudhuru utunyeshelezee kwa haraka na si kwa kuchelewa, Ewe Mola wetu wa haki wanyeshelezee waja wako na wanyama wako na eneza Rehema zako na ufufue mji wako uliokufa, ewe Mola wetu wa haki tunyesheleze mvua wala usitufanye kuwa ni wenye kukata tamaa, ewe Mola wetu wa haki tunakuomba liwe nyeshelezo la Huruma na si nyeshelezo la adhabu wala la kuharibu wala kuangamiza. Ewe Mola wetu wa haki hakika waja na miji wako katika maisha ya dhiki shida kiasi ambacho hatuna pakushitakia ila kwako: "Ewe Mola wetu wa haki tuoteshee mimea, na utuzidishie maziwa na utunyeshelezee Baraka kutoka mbinguni, na uuteremshie baraka zako, Ewe Mola wetu wa haki tunakuomba msamaha kwa hakika wewe ni mwenye kusamehe, basi tuteremshie mvua kwa wingi" Na inapendekezwa kuelekea kibla wakati wa hotuba kisha kugeuza shuka yake na kuweka upande wa kulia uje kushoto na kushoto uje kulia na kinyume cha hivyo, kwa sababu Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-: Aligeuzia mgongo wake kwa watu na akaelekea kibla kisha akageuza shuka yake, wameafikiana katika hadithi Bukhari na Muslim, na ataomba kwa siri wakati wa kuelekea kwake kibla, na kama wataomba mwisho mwa swala yao au katika hotuba ya ljumaa watakuwa wamepatia Sunnah, Na inapendeza asimame mwanzo wa kuanza mvua na atoe kipando chake na nguo zake ili zipatwe na mvua, na atatoka kuelekea jangwani ikiwa maji yanatatiririka, na atatawadha na atasema atakapoiona mvua: (Ewe Mwenyezi Mungu ijaalie Mvua Hiyo kuwa ni yenye manufaa) Na Maji yakizidi na ikohofiwa wingi wa mvua ni Sunnah kusema: "Ewe Mola tuteremshie mvua na wala usituteremshie adhabu. Ewe Mola wetu ishushe mvua Milimani na juu ya miinuko na sehemu za malisho na maoteo ya miti". Na ataomba wakati wa kuteremka mvua na atasema: Tumenyeshelezewa Mvua kwa fadhila za Mwenyezi Mungu na Rehema zake, na ikiwa ataona mawingu au ukavuma upepo atamuomba Mwenyezi Mungu kheri itokanayo na upepo huo na kujilinda na shari itokanayo na upepo huo na wala haifai kuutukana upepo bali atasema: Ewe Mola wangu nakuomba kheri ya upepo huu na kheri zilizoko ndani yake na kheri iliyotumwa kwa ajili yake, na ninajilinda kwako kutokana na shari ya upepo huu na shari iliyoko ndani yake na shari iliyotumwa kwa ajili yake, Ewe Mola wetu jaalia upepo huu ni Rehema na wala usijaalie kuwa ni adhabu, Ewe Mola wetu ujaalie upepo usiwe na nguvu na wala usiujaalie kuwa na nguvu. Na akisikia sauti ya Radi na ukelele atasema: Ewe Mola wetu usituuwe kwa hasira zako, na wala usituangamize kwa adhabu zako na utusamehe kabla ya kutokea hayo, ametakasika yule ambaye Radi inamtakasa kwa kumshukuru na Malaika wanamtakasa kwa kumuogopa, na akisikia sauti ya Punda basi ajilinde kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani, na akisikia sauti ya Jogoo atamuomba Mwenyezi Mungu fadhila zake.

(Mlango wa Jeneza)

Inafaa kutumia dawa, kwa makubaliano ya wanachuoni wote na wala kutumia dawa hakupingani na kumtegemea Mwenyezi Mungu, na ni Haramu kujitibu kwa kujichoma kwa moto, na inapendeza kwa mwenye Homa kutotumia maji, na ni haramu kujitibu kwa vitu vilivyo haramu kwa kuvila au kuvinywa na kusikiliza sauti za kipuuzi, kwa mujibu wa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Msijitibu kwa dawa zilizo haramu" Na ni haramu kufunga Hirizi; Nayo ni kinga ambayo huning'inizwa, na ni Sunnah kuzidi kukumbuka kifo na kujiandaa nacho. Na kuwatembelea wagonjwa na siyo vibaya kwa mgonjwa kuelezea kinachomsumbua pasina kulalamika baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, na ni wajibu kufanya subira , na kumlalamikia Mwenyezi Mungu hakukatazwi bali ni jambo linalotakikana, na kumdhania Mwenyezi Mungu vizuri ni wajibu, na wala asitamani mauti kutokana na madhara yaliyompata, na inapendeza mwenye kumtembelea mgonjwa amuombee dua ya kuponyeshwa, na ikiwa atafikwa na mauti ni Sunna kumlakinia kwa kusema "Lailaha illa llahu" Na amuelekeze kibla na ikiwa atakufa basi na amfunge macho yake, na ndugu wa maiti wasizungumze isipokuwa kwa mambo yaliyo mazuri kwa sababu Malaika huitikia kwa yale wayasemayo, na hufunikwa maiti kwa nguo, na kufanywa haraka kumlipia Deni lake na kumuweka mbali na dhima yake kuanzia Nadhiri au Kafara, kwa kauli yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Nafsi ya Muumini huning'inizwa kwa Deni lake mpaka alipiwe" Kaifanya kuwa Hadithi Hasan Imamu Tirmidhi. Na ni Sunna kufanya haraka kumuandaa Maiti, kwa maneno yake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Na wala haifai kwa Maiti ya Muislamu kukalishwa mbele ya familia yake, (kutunzwa ndani) bali awahishwe kuzikwa" Imepokelewa na Abuu Daud, Na ni karaha kuomboleza, nako ni kupiga kelele kwa kufa kwake.

Na kumuosha na kumswalia na kumbeba na kumkafini (kumvisha sanda) na kumzika kwa kumuelekeza kibla ni faradhi ya kutoshelezana (wakilisimamia hilo wenye kutosha hawatokuwa na dhambi wengine), na ni karaha kuchukua ujira kwa ajili ya mazishi, na kumsafirisha maiti kumpeleka kwenye mji usiokuwa wake pasina kuwa na ulazima ni karaha, na ni Sunna kwa mwenye kumuosha maiti aanze na viungo vya Udhu vya upande wa kulia na amuoshe mara tatu au mara tano, na inatosheleza mara moja, na akizaliwa kichanga ambaye amefikia zaidi ya miezi minne basi ataoshwa, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: "Na kichanga (aliyeporomoka) huswaliwa na huombewa wazazi wake msamaha na Rehema" Ameisahihisha Tirmidhiiy na tamko lake "Na mtoto mdogo huswaliwa" Na atakayeshindikana kuoshwa kwa kukosekana maji au kitu kingine basi atafanyiwa Tayammam, na ni wajibu avishwe sanda na nguo yenye kumsitiri mwili mzima, na ikiwa haikupatikana nguo ya kumsitiri atasitiriwa uchi wake kisha kichwa chake na sehemu inayofuata, na atawekewa sehemu iliyobakia majani, na atasimama imamu wakati wa kumswalia mwanaume usawa na kifua chake, na atasimama katikati ikiwa anayesaliwa ni mwanamke, na Ataleta Takbira na kusoma Suratul Faatiha kisha atatoa Takbira na atamswalia Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani, kisha atatoa Takbira na atamuombea dua maiti, kisha atatoa Takbira ya Nne na atasimama baada ya takbira ya Nne kidogo kisha atatoa salamu mara moja upande wake wa kulia, na atainua mikono yake katika kila Takbira na atasimama hapo hapo mpaka maiti iondolewe, imepokelewa hivyo kutoka kwa Omari, na inapendeza kwa yule ambae hakumswalia maiti, amswalie akituliwa (akiwekwa chini) tu au baada ya kuzikwa hata kwa jamaa kwa muda wa mwezi mmoja tangu kuzikwa, Na hakuna ubaya kuzika usiku, na ni karaha kuzika wakati wa kuchomoza jua na wakati wa kuzama jua, na jua likiwa katikati, na ni Sunnah kumpeleka haraka haraka lakini siyo mwendo wa kasi, na ni karaha kukaa kwa mwenye kusindikiza jeneza mpaka liwekwe chini kwa ajili ya kuzikwa, na anatakiwa mwenye kulifuata jeneza awe mnyenyekevu na mwenye kufikiria mafikio yake, na inachukiza kutabasamu na kuzungumza mambo ya kidunia, Na inapendeza amuingize kaburini kwake kuanzia miguuni ikiwa itakuwa kuna wepesi, na ni karaha kufunikwa kaburi la mwanaume, na wala si karaha kwa mwanaume kumzika mwanamke hata kama si ndugu yake wa karibu, na kumzika katika mwanandani ndiyo bora, na ni Sunnah kumzika sehemu ndefu na kuifanya kuwa pana, na ni karaha kumzika akiwa ndani ya Sanduku, na atasema wakati wa kumuweka kaburini "kwa jina la Mwenyezi Mungu na kwa mila ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, na inapendeza kuomba dua mbele ya kaburi lake baada ya kuzikwa, kwa kusimama mbele ya kaburi, na inapendeza kwa atakaye hudhuria mazishi amwagie mchanga upande wa kichwa chake kwa michoto mitatu"

Na inapendeza na ni Sunna kuliinua kaburi kiasi cha nchi moja na inachukizwa kuinua zaidi ya hapo, kwa maneno yake Mtume - Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- akimwambia Ally (Radhi za Allah ziwe juu yake) "Usiache Sanamu yoyote isipokuwa umeivunja, wala usiliache kaburi lililozidi zaidi ya nchi moja isipokuwa uwe umelisawazisha" Ameipokea Imamu Muslim

Na hunyunyiziwa juu yake maji na huwekewa kokoto ili kuhifadhi ubichi wa udongo wa kaburi, na si vibaya kuwekewa alama kwa kuweka jiwe na mfano wake ili litambulike kuwa ni kaburi, kwa ilivyo pokelewa katika riwaya kuhusu kaburi la Othman bin Madhoon, na haifai kulisakafia kaburi na kulipiga ripu, na ni wajibu kubomoa lililojengewa, na wala haifai kuzidisha udongo ambao haukutolewa kaburini, kwa sababu ya makatazo yaliyokuja kuhusu hilo. Imepokelewa na Abuu Daud, Na wala haifai kulibusu kaburi wala kuliremba wala kulinyunyizia marashi, wala haifai kulikalia juu yake na kujisaidia haja kubwa juu yake au baina ya makaburi. Wala haifai kutaka ponyo kutokana na udongo wa kaburi, na ni haramu kuliwekea kaburi taa na kulijengea juu yake msikiti, na ni wajibu kulibomoa likiwa limejengewa, na wala haifai kutembea na viatu makaburini, kwa hadithi iliyokuja kuhusu hilo Amesema Ahmad sanadi yake ni nzuri

Na ni Sunnah kuyatembelea makaburi pasina kuyafungia safari, kwa maneno ya Mtume- Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Haifungwi safari isipokuwa kwa ajili ya misikiti mitatu" Na wala haifai kwa wanawake kutembelea makaburi, kwa maneno ya Mtume- Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- "Amewalaani Mwenyezi Mungu wanawake wenye kuzuru makaburi na wenye kuyafanya makaburi kuwa ni misikiti na kuyawashia taa" Wameipokea waandishi wa vitabu vya sunani. Na ni machukizo kujipangusia na kuswali humo na kuyatembelea kwa kukusudia kuomba makaburi, yote haya ni katika mambo maovu bali ni sehemu katika shirki, na aseme kila mwenye kuyatembelea, au mwenye kupita makaburini: "Assalamu alaikum Daara Qaumi Muuminiina, Wa innaa in sha Allahu bikum Laahiquun, Yar-hamul-mustaqdamiina minna waminkum walmustaa-ikhiriina, nas-alullaha lanaa walakumul Aafiya, Allahumma laa tah-rimna aj-rahuum walaa taf-tinnaa baadahum, waghfirlanaa walahum".

Na ni hiyari ya mtu kuileta salamu kwa dhamiri ya mtu maalumu au kwa dhamiri ya yeyote aliyekuwa hai, na kuanza kutoa salamu ni sunna na kuitikia ni wajibu na hata kama atamsalimia mtu kisha wakakutana mara ya pili au ya tatu au zaidi ya mara hizo atasalimia, na haifai kuinama wakati wa salamu na wala asimsalimie mwanamke wa kando isipokuwa kikongwe asiyekuwa na matamanio, na mtu atasalimia wakati wa kuondoka na wakati wa kuingia nyumbani kwake kwa familia yake, atasalimia kwa kusema: "Ewe Mola wangu wa Haki mimi nakuomba kheri ya kuingia na kheri ya kutoka, kwa jina Mwenyezi Mungu tumeingia na kwa jina Mwenyezi Mungu tumetoka na kwa Mola wetu tumetegemea " Na ni Sunnah kupeana mikono, kwa hadithi ya Anas, na wala haifai kupeana mikono na wanawake, na ni Sunnah kusalimia watoto, na amsalimie mdogo katika umri, na wachahe, na wenye kutembea kwa miguu, na wenye kupanda vipando, hao wote wawasalimie walio tofauti nao. Na mtu akimfikishia salamu mtu mwingine ni Sunna aseme: Alaika wa Alaihi Salaam: ziwe Juu yako na juu yake Amani.

Na ni Sunnah kwa mmoja anapokutana na mwenzake awe na pupa ya kuanza kusalimia na wala asizidishe zaidi ya kusema: Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakaatuhu, na ikiwa atapiga miayo atajizuia kwa kadiri awezavyo na ikiwa miayo itamshinda basi ataziba mdomo wake, na ikiwa atapiga chafya ataufunika uso wake na atashusha sauti yake na atamshukuru Mwenyezi Mungu kwa sauti, kiasi cha kusikia yule aliyekaa naye, na atasema aliyemsikia: Yarhamukallahu; naye atamjibu mpiga chafya kwa kusema: Yahdiikumullahu wa Yuslih Baalakum, na wala asimuombee yule ambaye hajamshukuru Mwenyezi Mungu, na kama atapiga chafya mara ya pili na ya tatu atamuombea, na baada ya hapo akipiga tena atamuombea afya njema.

Na ni wajibu kwa mtu wake wa karibu au wapembeni kubisha Hodi ya kuingia kwake, ikiwa ataruhusiwa aingie, na kama hajaruhusiwa basi na arudi, na kubisha hodi ni mara tatu, na wala asizidishe, na sifa ya kubisha Hodi ni kusema: Assalam alaikum, je niingie? Na akiingia atakaa sehemu wanapoishia watu kukaa, na wala asiwatenganishe kwa kukaa kati ya watu wawili isipokuwa kwa idhini yao.

Na ni Sunnah kumuhani aliyepatwa na msiba, na ni machukizo kukaa hapo muda mrefu, na wala hakuna maneno maalumu ambayo atayasema mwenye kuhani, bali amuhimize kufanya subra na kumuahidi malipo na amuombee maiti na aseme aliyepatwa na msiba Al-hamdulillahi Rabbil Aalamiin, Innaa Lillaahi wa innaa ilaihi Raajiuun, Allahumaa Aju-rniiy fii muswiibatiy, Wakh-luf lii khairan min-ha. Na ikiwa ataswali atakuwa ametumia kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema: {Na takeni msaada kwa kufanya subira na kuswali} basi ni vizuri, kwa kulifanya hilo bin Abbas, Na kufanya Subira ni Wajibu, na ni machukizo kumlilia maiti, na ni haramu kuomboleza. Na Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- yuko mbali na wale wenye kupiga makelele kwa ajili ya misiba na wenye kunyoa Nywele na wenye kurarua nguo, na ni haramu kuonyesha kutapatapa na kuweweseka.

Kitabu kinachohusu mambo ya Zaka:

Ni wajibu kutoa Zaka ya wanyama wafugwao, na kila chenye kutoka Ardhini na vitu vya thamani na mali iliyoandaliwa kwa ajili ya biashara kwa masharti matano, kwanza uislamu, na kuwa Huru, na kumiliki kiwango, na umiliki kuwa kamili, na kuzungukiwa na mwaka, na ni wajibu kuitolea Zaka mali ya mtoto mdogo na mwenda wazimu, imepokelewa kutoka kwa bin Omar na bin Abbas na wengine wasiokuwa hao, na wala hajulikani yeyote aliyewapinga kuhusu hilo, na ni wajibu kuitolea zaka mali iliyozidi zaidi ya kiwango isipokuwa wanyama wafugwao hawatolewi Zaka wale waliozidi wala haitolewi Zaka mali iliyotolewa kwa ajili ya Wakfu ambayo si maalum kwa ajili ya mtu fulani kama vile, misikiti, na ni wajibu kutoa Zaka kwa faida zitokanazo na Ardhi iliyotolewa Wakfu kwa kitu maalumu, na mwenye kudai deni lake kwa mtu mwenye uwezo kama vile mkopo na mahari na deni hilo likazungukiwa na mwaka kuanzia pale alipolimiliki atalitolea zaka atakapo lipokea deni hilo au chochote katika deni hilo. Na hivyo ndivyo walivyokubaliana maswahaba, na kama alichokipokea hakifikii kiwango cha kutolewa Zaka ya mtosha yeye kuitoa Zaka kabla hajapokea kiwango hicho kwa kuwepo na sababu za kuwajibisha hilo, lakini kuchelewesha kulitolea Zaka mpaka atakapokabidhiwa ni ruhusa kufanya hivyo, na kama mkononi mwake ana kiwango kilichobakia sawa ni Deni au mali potevu atatolea zaka kilichopo mkononi mwake, na ni wajibu kutoa zaka ya Deni ambalo liko kwa mtu asiyekuwa na uwezo au kwa mali iliyoporwa au iliyochukuliwa kwa nguvu pindi atakapo ipata, na imepokelewa kutoka kwa Ally na bin Abbas kwa ujumla, na ikiwa atafaidika na mali kabla ya kuzungukiwa na mwaka basi hatoitolea zaka mpaka izungukiwe na mwaka, isipokuwa zao litokanalo na wanyama wafugwao na faida ya biashara, kwa maneno ya omar "Wapigie hesabu hata watoto wa Mbuzi lakini usichukue Zaka yao" Imepokelewa na Maliki Na kwa kauli ya Ally, na wala hakuna yeyote aliyempinga katika maswahaba. Na huchanganywa faida na kilichopo mkononi mwake kwa pamoja ikiwa ni kiwango cha aina moja, au ni katika hukumu moja kama vile kuchanganya dhahabu na Fedha, na ikiwa aina ya kiwango ni tofauti basi hukumu zake zitatofautiana.

Zaka ya wanyama wafugwao.

Na haiwajibiki kutoa zaka isipokuwa kwa wanyama wafugwao tu, nao ni wanyama ambao wanachungiwa malishoni zaidi ya mwaka, na kama akiwanunua au akawachanganya na walioandaliwa kwa ajili ya kuwala basi hatowatolea Zaka, na wanyama hao wako aina tatu:

(Aina ya kwanza ) Ngamia, hawatolewi Zaka mpaka wafikie idadi ya watano, basi kwa idadi hiyo atatoa Mbuzi mmoja, na wakifikia Ngamia Kumi atatoa Mbuzi wawili na wakifikia Ngamia kumi na tano basi atatoa Mbuzi watatu, na wakifikia Ngamia Ishirini basi Atatoa Mbuzi wanne, kwa kukubaliana wanachuoni katika hilo, na ikiwa watafikia Ngamia Ishirini na tano basi atamtoa Zaka Ngamia aitwaye Bint Labuun; naye ni Ngamia mwenye miaka miwili. Ikiwa atamkosa bintu labuuni basi atamtosha Ibnu labuun, naye ni mwenye miaka miwili, na ikiwa atafikisha Ngamia thelathini na sita atatoa Bintu labuun na ikiwa atafikisha ngamia Arobaini atatoa Hiqqat; naye ni Ngamia aliyefikia miaka mitatu, na ikiwa atafikisha Ngamia sitini na moja atamtoa Jadh'aa; naye ni aliyefikisha miaka minne, na ikiwa atafikisha Ngamia Sabini na sita Atatoa Bint Labuuni wawili, na akifikisha Ngamia Tisini atatoa Hiqqataan, na ikiwa atafikisha Ngamia mia moja na ishirini na moja, atatoa Bint labuuni watatu, kisha fungu litabakia katika kila idadi ya Ngamia Arobaini atatoa Zaka ya Bint labuun mmoja, na katika kila Ngamia hamsini atatoa Hiqqah, na wakifikia Ngamia mia mbili itakuwa imewafikiana faradhi mbili akitaka atatoa Hiqqah wanne na ikiwa atataka, au atatoa bint labuun watano.

(Aina ya pili ya Wanyama) Ni Ngo'mbe: Na hawatolewi Zaka mpaka wafikie idadi ya Ng'ombe Thelathini, basi ikifika idadi hiyo atatoa Tabii'iy; au Tabii'at wote wawili hao wana umri wa mwaka mmoja, na Ng'ombe wakifika Arobaini ataoa Musinnah; naye ni ngo'mbe mwenye miaka miwili na ikiwa watafikia Ngo'mbe Sitini basi atatoa Tabii'aan; kisha katika kila thelathini atatoa Tabii'u mmoja na katika kila Ngo'mbe Arobaini atatoa Musinnat.

(Aina ya Tatu ya Wanyama) Mbuzi: na hawatolewi mpaka wafikie kiwango cha Mbuzi Arobaini, ikifikia idadi hiyo basi atatoa Zakkah ya Mbuzi mmoja mpaka kufikia mbuzi mia moja na Ishirini, na ikiwa atazidi mmoja basi atatoa mbuzi wawili mpaka kufikia mbuzi mia mbili. Na ikiwa atazidi zaidi ya mmoja basi atatoa mbuzi watatu.

Na ikiwa watafikia Mbuzi miatatu basi atatoa Mbuzi wanne kisha katika kila mia moja hutolewa mbuzi mmoja, na wala hachukuliwi Dume -beberu- wala mbuzi mkubwa wala mbuzi mwenye aibu wala hachukuliwi Mbuzi aitwaye Ribaa, naye ni yule mbuzi mwenye mtoto anamlea, wala hachukuliwi mwenye mimba wala aliyenenepa sana wala mwenye thamani ya juu zaidi, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani-: "Lakini chukueni mali zenu zenye thamani ya kati na kati, kwa hakika Mwenyezi Mungu hakukuombeni mtoe kilicho bora zaidi katika mali zenu wala hajawaamrisha kutoa mali isiyofaa- ya shari- " Imepokelewa na Abuu Daud, Na wakati wa kufuga pamoja watu wawili aina mbili za wanyama wafugwao, hupelekea kuwa ni sawa na mali ya mtu mmoja .

Zaka ya chenye kutoka Ardhini.

Ni wajibu kutoa Zaka katika kila kinachopimwa kwa kilo katika nafaka inayohifadhika katika ghala kuanzia Nafaka na vinginevyo kwa masharti mawili, sharti la kwanza: kufikia kiwango na kiwango chenyewe ni mapishi Sitini, na huchanganywa matunda ya mwaka mmoja na baadhi ya mimea huchanganywa na mimea mingine katika kukamilisha kiwango, sharti la pili: kiwe kiwango alichonacho ni miliki yake katika ule wakati wa kutoa zaka na siyo wajibu kutoa chumo la kuokota au ambalo anapewa zawadi au thamani aichukuayo ni malipo ya kuvuna kwake, na ni wajibu kutoa Ush-ru (moja ya kumi) kwa mimea. Ni wajibu kutoa moja ya kumi mazao yaliyonyeshelezwa kwa gharama, na kutoa Nusu ya na nusu ya kumi ikiwa yamenyeshelezwa kwa gharama, na robo tatu ikiwa yamenyeshelezwa kwa namna zote mbili. Na ikiwa Nafaka zilizochanganywa zinatofautiana, basi itaangaliwa Nafaka yenye Thamani zaidi, ikiwa ni pamoja na kutokujua kama kiwango kimefikia moja ya kumi, na inapasa kutoa Zaka ya nafaka iliyokuwa safi na matunda yakiwa mabichi, na wala haifai kununua mtu Zaka aliyoitoa yeye mwenyewe wala sadaka, lakini ikiwa Zaka au Sadaka imerudishwa kwake kwa njia ya kurithi basi yafaa kupokea. Na Imamu atatafuta mwenye kukadiria upimaji wa Zaka na anatosha mkadiriaji mmoja, na mkadiriaji atamwachia mtoa Zaka na Familia yake kiasi cha kumtosheleza na familia yake kilichokuwa kibichi, ikiwa mkadiriaji hajamuachia mtoa Zaka cha kumtosha, basi mwenye mali ni haki yake kuchukua, na amechukizwa Imamu Ahmad kuvuna na kukata nyakati za usiku, na wala hairudiwi Zaka ya moja ya kumi hata kama itabakia miaka, muda wakuwa tu siyo ya biashara. Hivyo itatolewa itakapofikiwa kila mwaka.

(Mlango wa Zaka ya Dhahabu na Fedha)

kiwango cha dhahabu itolewayo Zaka ni ile yenye thamani sawa na gram 85 za dhahabu na fedha sawa na gram 595, na katika kiwango hicho hutolewa robo ya kumi, 2.5% na huchanganywa moja wapo na aina nyingine katika kukamilisha kiwango, na huchanganywa thamani ya biashara katika aina zote mbili. Na hakuna Zaka katika mapambo ya halali ikiwa atayaandaa mapambo kwa ajili ya Biashara basi atayatolea mapambo hayo Zaka, na inafaa kwa mwanaume kuvaa pete ya chuma na huvaliwa katika kidole kidogo na mkono wa kushoto ni bora zaidi, na amedhoofisha Imamu Ahmad kuvaa pete mkono wa kulia. Na ni makuruhu kwa mwanaume na mwanamke kuvaa pete ya chuma na Copa iliyo andikwa juu yake, na inafaa kuitumia fedha kwa kuiweka kwenye ncha ya upanga, na kupambia Ala za mapanga kwa sababu maswahaba Radhi za Allah ziwe juu yao walitengeneza Ala zilizopambwa kwa fedha, na inafaa kwa wanawake kujipamba kwa Dhahabu na Fedha pambo ambalo ni kawaida yao kuvaa mapambo hayo, na ni Haramu mwanaume kujifananisha na mwanamke na mwanamke kujifananisha na mwanaume, na kinyume chake katika mavazi na vitu vingine.

(Mlango wa Zaka ya mali ya Biashara)

Ni wajibu kuitolea Zaka ikiwa thamani yake imefika kiwango cha kutoa Zaka kama itakuwa ni mali ya Biashara, na wala hakuna Zaka kwa kilichoandaliwa kwa ajili ya kukodisha katika viwanja au mnyama au vingine vyenye kufanana na hivyo.

(Mlango wa Zakatil Fitri)

Na Zaka hiyo humtwaharisha mfungaji kutokana na mambo ya upuuzi na machafu, na Zaka hii ni Faradhi ya lazima kwa kila muislamu itakapokuwa katika chakula chake na familia yake kuna kilichozidi kwa ajili ya siku ya Eid na usiku wake, atatoa pishi moja (kg 2.5) kwa ajili yake na kwa ajili ya wale wanao mtegemea miongoni mwa waislamu, wala si lazima kumtolea muajiriwa, na ikiwa hakupata cha kuwatosheleza wote ataanza yeye kisha ndugu wa karibu na wanaofuatia kwa ukaribu, na wala si wajibu kuitoa Zaka kwa ajili ya Mimba kwa kuafikiana wanachuoni, na yule atakayejitolea kumgharamikia muislamu mwezi mzima wa Ramadhani basi inamlazimu Zaka ya fitri yake, na inafaa kuitanguliza kabla ya Eid kwa siku moja au siku mbili, na wala haifai kuichelewesha mpaka siku ya kufungua, na akifanya hivyo hupata madhambi, Na ilivyo bora ni kuitoa siku ya Eid kabla ya Swala ya Eid, na ni wajibu kutoa pishi moja la Tende, au Ngano, au Zabibu au Shairi, au Maziwa ya Unga na ikiwa atakosa basi atatoa badala yake katika vyakula viliwavyo katika mji, na amependekeza Imamu Ahmad kutoa chakula kisafi, na amesimulia toka kwa bin Sirin na inafaa kupewa watu wengi fungu la mmoja na kumpa mmoja fungu la wengi na kinyume chake.

(Mlango wa kutoa Zaka)

Na wala haifai kuchelewesha Zaka mpaka ukatoka wakati wake wa wajibu ikiwa yawezekana kuitoa, isipokuwa atakapokuwa Kiongozi hayupo au muhusika wa kupewa hayupo, na ni wajibu wa mkusanyaji kuichelewesha na kuiacha kwa mwenyewe kutokana na udhuru wa ukame na mfano wake kama vile njaa. Ametoa Hoja juu ya hilo Imamu Ahmad kwa kitendo cha Omar.

(Mlango wa wenye kupewa Zaka)

Nao ni watu Nane na haifai kutoa kwa wasiokuwa hao kwa mujibu wa Aya:

Wa kwanza na wa pili: Ni Mafukara na Masikini. Na wala haifai kuomba, na anahaki ya kupata kinachomtosha, na siyo vibaya ikiwa ataomba maji ya kunywa kuazima kitu au kuomba mkopo, na ni wajibu kumlisha mwenye njaa na kumvisha aliyekuwa uchi na kumkomboa mateka.

Watatu: Wenye kuishughulikia Zaka kama vile waletaji na waandishi na wenye kuhesabu na kupima, na haifai kwa ndugu wa karibu, na akipenda Imamu atamtuma pasina kuingia naye mkataba, na ikiwa atataka atamtajia kiasi maalumu.

Wa nne: Wenye kuzooweshwa nyoyo zao, nao ni viongozi na wenye kuheshimika kwa watu wao katika makafiri ambao wanatarajiwa kusilimu au anatarajiwa kwa kupewa kwake kupatikana nguvu ya imani yake au kusilimu mtu wa mfano wake au kumpa nasaha au kujizuia na shari zake, na wala haifai kwa muislamu kuchukua kitu kwa ajili ya kuzuia shari zake kama vile Rushwa.

Wa tano: Watumwa; Nao ni wale ambao waliandikishana, na inafaa kumkombolea muislamu aliyetekwa akawa kwenye mikono ya makafiri kwa sababu huko ndiko kumuacha huru mtumwa, na inafaa kununua nayo mtumwa na kumwacha huru, kwa ujumla wa kauli yake {Na Mtumwa}

Wa Sita: Wenye kudaiwa; nao ni wenye madeni nao wako aina mbili, wa kwanza ni yule aliyebeba jukumu la mali kwa ajili ya kusuluhisha watu wa karibu naye, Yaani: ni yule aliyechukua mali ili kutuliza fitina na Wa pili: Ni yule aliyekopa kwa jambo lake binafsi linalofaa.

Wa Saba: waliopo kwenye njia ya Mwenyezi Mungu nao ni wapiganaji, basi hupewa kiwango kinachowatosha katika vita yao hata kama wana uwezo, na Mwenye kuhiji katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Wa Nane: Mwana wa njia: Naye ni msafiri aliyekatikiwa ambaye hana chochote cha kuweza kumfikisha anapoishi, hivyo hupewa kiasi kitakachomfikisha hata kama ana utajiri huko anakoishi, na ikiwa atadai kuwa ni fakiri yule ambaye hajulikani utajiri wake kauli yake itakubaliwa, na ikiwa ni mwenye uwezo wa kufanya kazi ngumu na likajulikana chumo lake haifai kumpa mtu huyo, na ikiwa chumo lake halijulikani atapewa lakini baada ya kupewa habari kuwa hakuna fungu la Zaka la tajiri wala mwenye uwezo wa kuchuma na ikiwa ni mtu wa kando anahitajia zaidi basi mtu wa karibu hawezi kupewa, na huzuiliwa mtu wa mbali na wala havutiwi na kujipendekeza kwa ndugu wa karibu kwa kutumia mali ya Zaka, wala haitumiki Zaka kuzuilia mabaya, wala Zaka haitumiki ili kumtumikisha yeyote, na wala asichunge mali yake kwa kutumia Zaka, na wala asiilinde mali yake kwa kutumia Zaka, na Sadaka ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu ni Sunna kutoa wakati wowote na kuitoa kwa siri ni bora zaidi, na ni bora kuitoa wakati ukiwa na afya na ukunjufu wa nafsi na kutoa kwenye Ramadhani ni bora kwa kufanya kwake Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- na katika wakati wa Haja, kwa maneno yake Allah Mtukufu aliposema: {Katika siku yenye Njaa} Na Sadaka ya Kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu ni haki kwa ndugu wa karibu, ikiwa ni sadaka na kiunganisha udugu na hasa hasa panapokuwa na uadui, kwa maneno ya Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: (Unga udugu kwa mwenye kuukata) Kisha jirani, kwa maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. {Na Jirani walio karibu na Jirani walio mbali } Na yule ambaye shida yake itakuwa ni kubwa zaidi, kwa maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu. {Au masikini asiyekuwa na kitu}. Na wala asitoe sadaka kiasi ambacho atadhurika au yule amtoleaye atadhurika, au atadhurika yule ambae inamlazimu matunzo yake, na mwenye kutaka kutoa sadaka ya mali yake yote na yeye ana familia na chumo lake linawatosha familia yake inapendeza kufanya hivyo ikiwa anajua katika nafsi yake kunakutagemea kwa Allah, yafaa hivyo kutokana na kisa cha Abuubakar Swiddiq, na ikiwa kinyume na hivyo haifai na atazuiliwa kutoa mali yake, na ni karaha kwa asiyeweza kusubiri juu ya dhiki kupunguza mwenyewe mpaka kufikia kiwango cha chini kisicho tosheleza vilivyo, na ni haramu kusimanga katika sadaka na kufanya hivyo ni katika madhambi makubwa yenye kubatilisha thawabu zake. Na yeyote atakaye toa kitu katika sadaka kisha kikamtokea kipingamizi, inapendeza kwake atekeleze, na alikuwa Amru bin- Aaswi Akishatoa chakula kumpa mwenye kuomba na hakumkuta anakitenga na anatoa kilicho kizuri, na hachukui kibaya akakitoa sadaka, na sadaka bora ni kutoa kinachobakia baada ya kutoa mahitaji ya familia, na hili hakuna anayelipinga. "Sadaka bora ni ile ambayo mtoaji wake atabakiwa na kinachomtosheleza" Makusudio ya neno -Jahdil Maqili- Baada ya mahitaji ya familia yake.

(Kitabu cha Funga)

Kufunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni moja ya nguzo za uislamu na ilifaradhishwa katika mwaka wa pili tangu kuhama Mtume Makkah, akafunga Mtume - Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani Ramadhani tisa, na inapendeza kuutafuta mwezi siku ya thelathini katika mwezi wa shabani, na ni wajibu kuufunga Mwezi wa Ramadhani kwa kuuona mwezi, na ikiwa hawakuuona na anga ni safi na hakuna mawingu basi watakamilisha siku Thelathini kisha watafunga siku inayofuata pasina kuwa na ihitilafu na akiuona mwezi atatoa takbira mara tatu na atasema: "Ewe Mola wetu wa haki uandamishe kwetu sisi kwa Amani na Imani na tuwe katika salama na uislamu na kuafikishwa kwa kila unachokipenda na kukiridhia, Mola wangu na Mola wako ni Mwenyezi Mungu, tunaomba uwe ni mwandamo wa kheri na uongofu" Na hukubaliwa kauli ya mtu mmoja muadilifu katika mwezi mwandamo, Amesimulia Tirmidhiy kutoka kwa maulamaa wengi, na ikiwa atauona mtu mmoja peke yake na ushuhuda wake ukakataliwa itamlazimu yeye peke yake kufunga na asifungue isipokuwa pamoja na watu wafungue, na ikiwa atauona mwezi mwandamo wa shawwali haruhusiwi kufungua.

Na msafiri atafungua ikiwa atakuwa amekwisha yaacha majumba ya mji wake, na bora zaidi ni kufunga ili kuondoka kwenye utata wa wanachuoni wengi, na Mwenye Mimba na mnyonyeshaji ikiwa watahofia nafsi zao au watoto wao wameruhusiwa kufungua, na ikiwa watahofia watoto wao tu, watalisha kila siku moja masikini na mgonjwa akiogopea kudhurika ni karaha kufunga kwake kwa ushahidi wa Aya, na yeyote atakaye shindwa kufunga kwa sababu ya uzee au maradhi ambayo hayatarajiwi kupona atafungua kisha atalisha kwa kila siku masikini mmoja, na ikiwa ataingia kwenye koo lake nzi au vumbi au yakaingia maji kwenye koo lake bila ya kukusudia anakuwa hajafungua.

Na wala haifai kufunga swaumu ya wajibu isipokuwa alale na nia usiku, na inakubalika funga ya Sunnah kwa kunuia kuanzia mchana kabla ya kupinduka jua na baada yake.

(Mlango kuhusu yanayo haribu Funga - swaumu-)

Yeyote atakaye kula au kunywa au akaingiza mafuta kupitia tundu za pua au kitu kingine na kikafika kwenye koo lake au akajidunga sindano au akajitapisha na akatapika au akafanya hijama au kufanyiwa basi hao swaumu zao zimeharibika, na wala haharibu swaumu yake aliyesahau akafanya jambo katika hayo yaliyotajwa, na ana haki ya kula na kunywa ikiwa atatia mashaka ya kuingia Al-fajiri, kwa maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Al-fajiri katika weusi wa usiku} Na yeyote atakaye fungua kwa kushiriki tendo la ndoa ni wajibu juu yake kutoa kafara ya Dhwihar- mtu kufananisha kiungo cha mkewe na cha mama yake- pamoja na kulipa deni, na inachukiza kupiga busu kwa mwenye kuchemkwa na matamanio, na ni wajibu kujiepusha na uongo na kusengenya na kutukana na kusengenya katika kila wakati lakini wakati wa kuwa na swaufu makatazo yake ni makubwa zaidi, na ni sunna kujiepusha na mambo yenye kuudhi, na ikiwa mtu atamtukana basi na aseme; Hakika mimi nimefunga, Na ni Sunna kuharakisha kufungua pindi patakapo kuwa kuna uhakika wa kuzama jua, na anahaki ya kufungua kwa dhana yake kuwa kubwa, na ni Sunnah kuchelewesha kula daku ikiwa haiogopewi kuwa Al-fajiri imeingia, na hupatikana fadhila za kula daku kwa kula au kunywa japo kidogo, na atafungua kwa kula tende mbichi na ikiwa hatopata basi atatumia tende kavu na ikiwa hatopata basi atakunywa maji na taomba wakati wa kufungua kwake, na atakayemfuturisha mfungaji basi ana malipo mfano wa yule aliyemfuturisha, Na ni sunna kuzidisha usomaji wa Qur'ani katika mwezi wa Ramadhani na kuleta Dhikri na kutoa swadaka, na swaumu iliyo bora ni swaumu ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu ni kufunga siku moja na kufungua siku ifuatayo, na ni Sunnah kufunga siku tatu katika kila mwezi na masiku meupe ni bora zaidi, na ni Sunnah kufunga siku ya Al-hamisi na siku ya juma tatu na siku sita za mwezi Shawwal japo kwa masiku tofauti tofauti, na kufunga siku tisa katika mwezi wa Dhulhijjah, na inayotiliwa mkazo ni siku ya tisa nayo ni siku ya Arafa.

Na kufunga mwezi wa muharram na siku bora yake ni kufunga siku ya tisa na ya kumi, na ni Sunnah kukusanya siku mbili hizo, na matendo yote yaliyotajwa katika siku ya Ashurah ukiacha funga hayana Asili bali ni uzushi, na ni makuruhu kuufunga mwezi wa Rajabu peke yake, na kila hadithi inayoelezea kuufunga mwezi wa Rajabu na kuswali katika mwezi huo ni uwongo. Na inachukiza kuitenga siku ya Ijumaa kwa ajili ya kufunga, na inachukiza kutangulia kufunga kabla ya Ramadhani kwa siku au siku mbili, na pia kufunga masiku ya kutanda nyama (katika idd kubwa) na ni makuruhu kufunga wakati wote, na usiku wa lailatul Qadri ni wenye kutukuzwa kunatarajiwa katika usiku huo kujibiwa dua, kwa mujibu wa maneno yake Mwenyezi Mungu: Usiku wa cheo na utukufu ni bora fadhila zake kuliko fadhila za miezi elfu moja isiyokuwa usiku huo. wamesema wafasiri: kusimama katika huo usiku na kufanya matendo ndani yake ni bora kuliko kusimama miezi Elfu moja iliyopita, na imeitwa lailatul Qadri kwa sababu katika usiku huo hukadiriwa mambo yatakayokuwa katika mwaka huo na usiku huo unahusishwa na siku kumi za mwisho na usiku wa witiri, na uliotiliwa mkazo zaidi ni usiku wa Ishirini na Saba, na ataomba katika usiku huo alichofundishwa Aisha na Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani: {Ewe Mola wangu wa haki hakika wewe ni msamehevu na mkarimu unapenda kusamehe basi nisamehe mimi makosa yangu} Na Mwenyezi Mungu ni mjuzi zaidi Na Rehema na Amani za Allah ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad na familia yake na Maswahaba zake.

Hukumu za Sala.

Ni Kitabu cha Sheikhul Islaam: Muhammad bin Abdul wahhab Allah amrehemu.

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu.

Sharti za swala ni tisa:

Ni uislamu, kuwa na Akili, kuwa na upambanuzi, na kuwa Twahara, na kusitiri uchi, na kujiepusha na Najisi, na kujua kuingia kwa wakati, na kuelekea kibla, na kunuia na kukusudia.

(Nguzo za Swala ni kumi na Nne)

Ni kusimama pamoja na kuwa na uwezo, na kuleta Takbira ya kuhirimia, na kusoma suratul faatiha, na kurukuu, na kuinuka kutoka katika rukuu, na kulingana sawa, na kusujudu, na kuinuka kutoka katika kusujudu, na kukaa kati ya sijida mbili, na kutulizana katika matendo yote, na kufuatanisha, na tahiyatu ya mwisho, na kukaa kwa ajili yake, na utoaji wa Salamu ya kwanza.

(Mambo yenye kubatilisha na kuharibu Swala ni mambo manane)

Kuongea kwa makusudi, na Kucheka, na Kula, na Kunywa, na Kufunua Uchi, na kuelekea upande usiokuwa upande wa Qibla, na kucheza kwingi, na kupatwa na najisi.

(Mambo yaliyo wajibu katika Swala ni mambo manane)

La kwanza: Takbira zote isipokuwaTakbira ya kuhirimia swala, La pili: kusema Samiallahul liman Hamidah kwa imamu na maamuma, La tatu: kusema Rabbana walakal hamdu, La Nne: kuleta Tas-biihi katika kurukuu, La Tano: kuleta Tas-biih wakati wa kusujudu, La Sita: ni kusema Rabbigh-firliiy kati ya sijida mbili, na wajibu ni mara moja, La Saba: kusoma Tashahudi ya Kwanza, kwa sababu yeye Mtume -Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake na amani- alifanya hivyo na alidumu katika kufanya hivyo na akadumu na kufanya hivyo na akaamrisha kufanya hivyo, na alisujudu sajida ya kusahau aliposahau kuleta Tashahudi ya kusahau pale aliposahau, Wajibu wa Nane: Ni kukaa kwa ajili ya hiyo tahiyatu.

(Mambo ya lazima katika kutawadha ni mambo Sita)

Kuosha Uso, na Kuosha mikono miwili mpaka kwenye kongo mbili, na kupaka kichwa chote maji, na kuosha miguu miwili mpaka kwenye fundo mbili, na kupangilia, na kufuatanisha.

(Masharti ya Udhu ni Matano)

Maji yaliyo twahara, na awe Muislamu mwenye kutambua, na pasiwepo na kizuizi, na kufika maji mpaka katika mwili, kuingia kwa wakati kwa mwenye Hadathi ya kudumu.

Mambo yenye Kuharibu Udhu ni manane)

Kutoka kitu katika moja ya njia mbili. Na kutoka kitu kichafu katika mwili, kuondokwa na akili kwa kulala au kwa kitu kingine, kuondokewa na Akili, kumgusa mwanamke wa kando kwa matamanio, na kuugusa uchi wa mwanadamu, na kuosha maiti, na kula nyama ya Ngamia, na kuritadi kwa kutoka katika uislamu atuepushe Mwenyezi Mungu na hilo. Na Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi.