3 : 72
وَقَالَت طَّآئِفَةٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ ءَامِنُواْ بِٱلَّذِيٓ أُنزِلَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَجۡهَ ٱلنَّهَارِ وَٱكۡفُرُوٓاْ ءَاخِرَهُۥ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ
Na kikundi katika Watu wa Kitabu walisema: Yaaminini yale waliyo teremshiwa wenye kuamini mwanzo wa mchana, na yakataeni mwisho wake; huenda wakarejea.
Explanation & meanings · 1
- Katika mtindo wao wa kutaka kuwapotoa Waumini, hawa Watu wa Kitabu wakiwaambia wenzao: Jitieni kuiamini Qur'ani aliyo teremshiwa Muhammad asubuhi, na ikifika jioni ikataeni. Huenda kwa hivyo mkawafitini hawa kwa kuwaingiza shaka katika nyoyo zao, wakaiacha dini yao.