وصيتي

وصيتي

Wasia wangu

Language: lang_sw
Prepared by:
Version: 1.0
Translations 12
Bengali English Spanish Persian +8
Attachments 7
PDF
Audio
Video
+3

Wasia wangu

Kila sifa njema anazistahiki Mwenyezi Mungu, na rehema na amani ziwe juu ya Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, na baada ya hayo:

Mimi (............................................................) Mwenye namba ya kitambulisho cha uraia:

Nimetoa Wasia huu nikiwa katika hali inayozingatiwa kisheria, kwanzia kuwa na akili timamu na uwezo wa kupambanua mambo, ya kwamba mimi ninashuhudia ya kuwa, hapana mungu apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake, asiye na mshirika, na kwamba Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake, na kwamba Issa ni mja wa Mwenyezi Mungu na ni Mtume wake, na ni neno lake alilolitia kwa Mariam na ni roho kutoka kwake, na kwamba Pepo ni kweli, na Moto ni kweli, na kwamba Kiyama kinakuja wala hakina shaka ndani yake, na kwamba Mwenyezi Mungu atawafufua walioko makaburini.

Ninawausia watu wa familia yangu ya kuwa; ikiwa nitapatwa na tukio la kifo, basi wawe na subira, na waridhike na kukubaliana na mipango ya Mwenyezi Mungu.

Na ninawausia pia kutoweka matanga na sherehe maalumu kwa ajili ya maombolezo, na wapupie katika kuyafanyia kazi mafundisho ya Mtume, rehema na amani ziwe juu yake.

Na ninawausia pia kwa wasia aliowausia Ibrahim wanawe na Yakubu kwamba: "Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuchagulieni dini, basi kamwe msife, ila na nyinyi ni Waislamu."

Kama ambavyo ninawausia kumcha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kumchunga katika siri na wazi, na wachunge mipaka ya Mwenyezi Mungu, na watekeleze amri zake na wayaepuke makatazo yake, na wasiipoteze swala, kwani hiyo ndio nguzo ya dini.

Na ninawausia kutofarakana na kutotofautiana, na wahurumiane wao kwa wao, na wasikatiane udugu, na waunge jamaa zao, na watunze mali zao, na watekeleze mipaka ya Mwenyezi Mungu katika mali hizo, na wasifanye biashara isipokuwa za halali na nzuri, na wajiepushe na riba sawa iwe ndogo au kubwa, na wasaidiane wao kwa wao kwa yale yatakayofanya itengenee dini yao na dunia yao.

Kama ambavyo ninawausia pia kwa haya yafuatayo:

La kwanza: Wafanye haraka kulipa madeni yaliyo juu ya dhima yangu, kwa haraka iwezekanavyo, kwani: (Nafsi ya Muumini hutundikwa kwa sababu ya deni lake mpaka alipiwe deni hilo).

Nayo ni kama yafuatavyo:

Haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu; kama vile Zaka, Swaumu, Kafara mbali mbali na Nadhiri: Nazo ni:............................................

..................................................................

Haki za watu: Kwanzia madeni, au nilivyowekeshwa na amana za watu, nazo ni:

Pesa/Amana...................... Mdai ni/Amana............... Anwani yake ni................... Namba yake ya simu ni................... Tarehe ya kulipa, au kutimiza..................

La pili: Kuchukua mali yangu kutoka katika mali zilizo kwa watu kama stahiki zangu, nazo ni kama ifuatavyo:

Pesa..................... Jina la mdaiwa............................. Anwani yake.......................... Namba yake ya simu.............................. Tarehe ya kulipa..............................

La tatu: Kukusanya mali zangu, nazo ni kama ifuatavyo:

(a) Pesa tasilimu zilizotunzwa katika akaunti yangu, na maelezo yake ni kama ifuatavyo:

Benki................. Tawi la.......................... Namba yake......................... Namba ya akaunti ya IBAN........................................... Akaunti imesajiliwa kwa jina la................................... Ni maalumu kwa.............................................

(b) Mali zisizohamishika:

Majengo ninayomiliki yenye maelezo yafuatayo:

Aina ya jengo............................... Namba ya jengo................ Tarehe yake...................... Lilitoka kwa...................... Mji........................... Mtaa.................

La nne: Ninatoa wasia huu katika mali yangu:

Kiasi cha fedha taslimu: (...............................).

Umiliki wa jengo langu, ambalo liko katika miliki yangu iliyoko mtaa wa........................... katika mji wa ............................. na namba ya jengo......................... Tarehe yake.....................

kwa kiwango chake cha asilimia: (..............%).

La tano: Mtu niliyemuusia mali hii niliyousia ni: (........................................) na namba yake ya uraia ni (.....................................). Naye mtu niliyemuusia mali iliyobakia mpaka igawanywe ni: (.......................................) na namba ya kitambulisho chake cha uraia ni (................................................................)

Na mtu niliyemuusia wanangu wenye mapungufu ili awalee malezi mazuri, na azihifadhi mali zao na azizalishe ni: (.......................................) na namba yake ya kitambulisho cha kitaifa ni (................................). Na mtu niliyemuusia kuwaozesha mabinti zangu ni: (...............................................) na namba yake ya kitambulisho cha kitaifa ni (...........................................................)

Na wale wasiokuwa hao, miongoni mwa wale ambao wana vigezo vifuatavyo: Uislamu, upambanuzi, uaminifu, nguvu, uadilifu na wema kwa kadiri itakavyowezekana. Naye ni juu yule nitakayemuachia wasia huu kuchagua mtu wa kumwachia wasia huu badala yake (endapo atahitaji kufanya hivyo), na hivyo hivyo kila aliyeachiwa wasia kwa yule atakayekuwa baada yake.

La sita: Robo ya mali nitakazozitolea wasia zitolewe katika njia za wema na ihisani ikiwemo:

Bajeti maalumu za masuala ya kheri:................................................................................................................................

Ikibakia katika robo hiyo, basi itolewe katika kazi za wema za watu wote (kama vile sekta za elimu, sekta za kijamii na misaada, sekta za kulingania kwa Mwenyezi Mungu, sekta za misikiti, sekta za afya, sekta za matangazo yenye lengo la kufikisha ujumbe (mzuri), na ndugu wa karibu ndio wenye haki zaidi ya kutendewa wema, na ikiwa itatokea haja, basi atangulizwe ndugu wa karibu zaidi.

Na mwisho wa wasia huu, ni matarajio yangu kuwa mtanisamehe kwa yale yaliyojitokeza kwangu, miongoni mwa makosa au mapungufu, na hakuna yeyote aliyesalimika na hilo, na Mwenyezi Mungu pekee ndiye tunayemuomba msaada. Sitasahau kuwausia kuniombea dua nyingi, na ninamuomba Mwenyezi Mungu awabariki ndugu zangu wa karibu, na aufanye mwisho wangu kuwa mwema, na anisamehe mimi na wazazi wangu, na ainyanyue huko Akhera daraja yangu na wazazi wangu na Waislamu wote kwa ujumla, na nimemuidhinisha yeyote atakayeshuhudia hilo, na Mwenyezi Mungu ndiye mbora zaidi wa mashahidi wote.

Wasia huu umeandikwa siku ya............................... sawa na tarehe......./...../143......... Hijria nao umefuta wasia wowote uliokuwa kabla yake.

Na rehema na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad na ali zake na Maswahaba zake.

Bwana/Bibi.................... Jina................................ Tarehe...................... Namba ya kitambulisho cha kitaifa.......................... Sahihi..........................

Mtoa Wasia..............................................

Shahidi wa kwanza............................................................

Shahidi wa Pili............................................................

Tanbihi: Wasia huu ni muhtasari unaowafaa Waislamu wote, na kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana nasi. Kama ambavyo nanyi mnaweza kuandika wasia wenu na kupata ushauri wa bure kutoka katika Kituo cha Waaqif Khubaraa Al-waswaaya Wal-auqaaf kupitia apilikesheni ya wasia.

"Si haki ya mtu Muislamu mwenye jambo analotaka kulitolea wasia alale siku mbili, isipokuwa ahakikishe kwamba anao wasia wake pamoja naye tayari umeshaandikwa." Bukhari - haya yatawekwa katika jalada

Sikuwahi kupitwa na usiku hata mmoja tangu niliposikia maneno haya kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, akisema hivyo, isipokuwa nilikuwa na wasia wangu tayari umekwishaandikwa. Abdallah bin Omari - haya yawekwe katika jalada.

Mwenye furaha zaidi ni yule itakayekatika pumzi yake, lakini matendo yake yasikatike. Ibnu Kudama - haya yawekwe katika rejeo ya mwisho kwenye sehemu ya chini ya ukurasa wa wasia.

Huu ni wasia mwepesi ulioandaliwa kwa ajili ya Waislamu wote - haya yawekwe katika jalada