5 : 24
قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّا لَن نَّدۡخُلَهَآ أَبَدٗا مَّا دَامُواْ فِيهَا فَٱذۡهَبۡ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَٰتِلَآ إِنَّا هَٰهُنَا قَٰعِدُونَ
Wakasema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako Mlezi mkapigane. Sisi tutakaa hapa hapa.
Explanation & meanings · 1
- Lakini wakakakamia katika ukhalifu wao. Wakasema: Ewe Musa! Sisi bila ya shaka yoyote tumekwisha azimia kuwa hatutaingia nchi hii kabisa, maadamu wamo hao majabari. Basi tuache na yetu; kwani wewe huna madaraka yoyote juu yetu. Nenda wewe na Mola wako Mlezi mkapigane nao hao majabari. Sisi tutakaa hapa hapa hatubanduki.