39 : 43
أَمِ ٱتَّخَذُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ شُفَعَآءَۚ قُلۡ أَوَلَوۡ كَانُواْ لَا يَمۡلِكُونَ شَيۡـٔٗا وَلَا يَعۡقِلُونَ
Au ndio wanachukua waombezi badala ya Mwenyezi Mungu? Sema: Ingawa hawana mamlaka juu ya kitu chochote, wala hawatambui lolote?
Explanation & meanings · 1
- Bali washirikina wakawafanya wengineo badala ya Mwenyezi Mungu kuwa ni waombezi wao wa kuwakurubisha kwake. Waambie, ewe Muhammad: Mnafanya haya ijapo kuwa hawa mnao wafanya "waombezi" hawanacho wanacho kimiliki, wala hawana wanacho kifahamu?