3 : 141
وَلِيُمَحِّصَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَيَمۡحَقَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na pia ili Mwenyezi Mungu awasafishe walio amini na awafutilie mbali makafiri.
Explanation & meanings · 1
- Kwa huku kushindwa kwa muda, Mwenyezi Mungu anawasafisha jamaa Waumini, na anawat'ahirisha kutokana na wale wenye nyoyo mbaya na imani dhaifu, na wenye kueneza moyo wa kushindwa na wasiwasi; na kwa hivyo ndio anaung'olea mbali ukafiri na makafiri wenyewe pia.