3 : 12
قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ سَتُغۡلَبُونَ وَتُحۡشَرُونَ إِلَىٰ جَهَنَّمَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ
Waambie walio kufuru: Karibuni mtashindwa na mtakusanywa, mtiwe kwenye Jahannam; nako huko ni makao mabaya kabisa.
Explanation & meanings · 1
- Ewe Nabii! Waambie hawa walio kufuru: Bila ya shaka nyinyi mtashindwa hapa duniani, na kesho Akhera mtaadhibiwa. Na Jahannamu ndio itakuwa tandiko lenu la kulalia; na ovu lilioje tandiko hilo!