18 : 74
فَٱنطَلَقَا حَتَّىٰٓ إِذَا لَقِيَا غُلَٰمٗا فَقَتَلَهُۥ قَالَ أَقَتَلۡتَ نَفۡسٗا زَكِيَّةَۢ بِغَيۡرِ نَفۡسٖ لَّقَدۡ جِئۡتَ شَيۡـٔٗا نُّكۡرٗا
Basi wakatoka wawili hao mpaka wakamkuta kijana, akamuuwa. (Musa) akasema: Ala! Umemuuwa mtu asiye na kosa, na wala hakuuwa! Ama hakika umefanya jambo baya kabisa!
Explanation & meanings · 1
- Na baada ya kutoka kwenye jahazi ile wakaingia kuendelea na safari yao. Njiani wakamkuta kijana. Yule mja mwema akamuuwa yule kijana! Musa akasema kwa kuchukia: Unakwenda muuwa mtu asiye na kosa lolote, na wala hakumuuwa mtu yeyote? Hakika umefanya jambo ovu kweli kweli!