16 : 87
وَأَلۡقَوۡاْ إِلَى ٱللَّهِ يَوۡمَئِذٍ ٱلسَّلَمَۖ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Na siku hiyo watasalimu amri mbele ya Mwenyezi Mungu, na yatapotea waliyo kuwa wakiyazua.
Explanation & meanings · 1
- Hapo tena wale washirikina walio mshirikisha Mwenyezi Mungu watasalimu amri, waikubali hukumu yake, na yawaondokee yale mawazo yao kwamba walio kuwa wakiwaabudu yatakuja waombea na kuwakinga na adhabu!