Skip to content
المَائدة /

Aya 22

5 : 22
المَائدة Aya 120
Sura · المَائدة
Kiswahili · Barawani
5 : 22

قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِنَّ فِيهَا قَوۡمٗا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدۡخُلَهَا حَتَّىٰ يَخۡرُجُواْ مِنۡهَا فَإِن يَخۡرُجُواْ مِنۡهَا فَإِنَّا دَٰخِلُونَ

Wakasema: Ewe Musa! Huko wako watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka wao watoke humo. Wakitoka humo hapo tutaingia.

Explanation & meanings · 1
  1. Wana wa Israili wakaikhalifu amri ya Mwenyezi Mungu na wakasema: Ewe Musa! Katika nchi hii wamo watu majabari. Sisi hatuna nguvu za kupambana nao. Basi hatutoingia humo maadamu wao wamo. Wakitoka basi tena hapo sisi tutaingia.