Skip to content
السَّجدة /

Aya 12

32 : 12
السَّجدة Aya 30
Sura · السَّجدة
Kiswahili · Barawani
32 : 12

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلۡمُجۡرِمُونَ نَاكِسُواْ رُءُوسِهِمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ رَبَّنَآ أَبۡصَرۡنَا وَسَمِعۡنَا فَٱرۡجِعۡنَا نَعۡمَلۡ صَٰلِحًا إِنَّا مُوقِنُونَ

Na ungeli waona wakosefu wanvyo inamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao Mlezi, (wakisema): Mola wetu Mlezi! Tumesha ona, na tumesha sikia. Turejeshe tukatende mema, kwani hakika sisi tumekwisha kuwa na yakini sasa.

Explanation & meanings · 1
  1. Lau kuwa umejaaliwa kuwaona wakosefu kwenye msimamo wa hisabu ungeli ona ajabu. Pale wale wakosefu wenye kujivuna watavyo inamisha vichwa vyao kwa hizaya inayo tokana na Mola wao Mlezi, nao watasema kwa unyonge: Ewe Mola wetu Mlezi! Tumekwisha yaona tuliyo kuwa na upofu nayo, na tumekwisha yasikia tuliyo kuwa na uziwi nayo, basi turejeshe duniani tupate tenda mema ambayo tuliyo kuwa hatuyatendi. Hakika sasa hivi sisi tumeyakinika na walio kuja nayo Mitume wako.