23 : 77
حَتَّىٰٓ إِذَا فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابٗا ذَا عَذَابٖ شَدِيدٍ إِذَا هُمۡ فِيهِ مُبۡلِسُونَ
Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
Explanation & meanings · 1
- Wanashikilia kupuuza kwao mpaka pale tunapo wapatiliza kwa adhabu kali ya njaa au mauwaji hapa duniani huwa tena wanababaika na kukata tamaa, hawaioni njia ya kuvuka.