Skip to content
الإسرَاء /

Aya 64

17 : 64
الإسرَاء Aya 111
Sura · الإسرَاء
Kiswahili · Barawani
17 : 64

وَٱسۡتَفۡزِزۡ مَنِ ٱسۡتَطَعۡتَ مِنۡهُم بِصَوۡتِكَ وَأَجۡلِبۡ عَلَيۡهِم بِخَيۡلِكَ وَرَجِلِكَ وَشَارِكۡهُمۡ فِي ٱلۡأَمۡوَٰلِ وَٱلۡأَوۡلَٰدِ وَعِدۡهُمۡۚ وَمَا يَعِدُهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ إِلَّا غُرُورًا

Na wachochee uwawezao katika wao kwa sauti yako, na wakusanyie jeshi lako la wapandao farasi na waendao kwa miguu. Na shirikiana nao katika mali na wana, na waahidi. Na Shet'ani hawapi ahadi ila ya udanganyifu.

Explanation & meanings · 1
  1. Na wazuge na wavute kwa kuwaita wamuasi Mwenyezi Mungu hao unao waweza miongoni mwao. Na fanya kila juhudi yako ya namna zote za udanganyifu. Na shirikiana nao katika kuchuma mali ya haramu, na kuyatumia kwa haramu, na kuwakufurisha watoto na kuwaghuri wafanye fisadi. Na wape ahadi za uwongo, kama kuwa miungu yao itawaombea, na kuwa watapata utukufu kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu ya nasaba zao. Na Shetani hawaahidi wafwasi wake ila kwa udanganyifu na uficho.