13 : 10
سَوَآءٞ مِّنكُم مَّنۡ أَسَرَّ ٱلۡقَوۡلَ وَمَن جَهَرَ بِهِۦ وَمَنۡ هُوَ مُسۡتَخۡفِۭ بِٱلَّيۡلِ وَسَارِبُۢ بِٱلنَّهَارِ
Ni sawa anaye ficha kauli yake kati yenu na anaye idhihirisha, na anaye jibanza usiku na anaye tembea jahara mchana.
Explanation & meanings · 1
- Anazijua hali zenu zote katika maisha yenu, na maneno yenu na vitendo vyenu vyote. Basi anayajua mnayo yaficha na mnayo yatangaza, vitendo na maneno. Na anajua vile mnavyo jificha usiku na kujitokeza mchana. Na yote ni sawa katika ujuzi wake.