Skip to content
يُونس /

Aya 72

10 : 72
يُونس Aya 109
Sura · يُونس
Kiswahili · Barawani
10 : 72

فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَمَا سَأَلۡتُكُم مِّنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِۖ وَأُمِرۡتُ أَنۡ أَكُونَ مِنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ

Lakini mkigeuka, basi mimi sikukuombeni ujira. Ujira wangu hauko ila kwa Mwenyezi Mungu. Na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waislamu.

Explanation & meanings · 1
  1. Na ikiwa mtabaki kukataa wito wangu, basi hayo hayatanidhuru mimi kitu. Kwani mimi sikufanya hivyo kwa kutaraji kupokea ujira kwenu ambao naogopa nitaukosa, kwa sababu ya kukataa kwenu! Ujira wangu mimi nautaka kwa Mwenyezi Mungu peke yake. Na Yeye ameniamrisha niwe Muislamu, nimsalimishie Yeye mambo yangu yote.