5 : 26
قَالَ فَإِنَّهَا مُحَرَّمَةٌ عَلَيۡهِمۡۛ أَرۡبَعِينَ سَنَةٗۛ يَتِيهُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ فَلَا تَأۡسَ عَلَى ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡفَٰسِقِينَ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi nchi hiyo wameharimishiwa muda wa miaka arubaini, watakuwa wakitanga-tanga katika ardhi. Basi wewe usiwasikitikie watu wapotovu.
Explanation & meanings · 1
- Mwenyezi Mungu akamuitikia Musa, akawapigia marfuku hao wakhalifu wasiingie nchi hiyo kwa muda wa miaka arubaini, wakipotea ovyo majangwani hawajui wendako wala watokako. Mwenyezi Mungu akamwambia Musa kama kumuasa: Usisikitike kwa masaibu yaliyo wasibu, kwani hawa ni wapotovu, wameiasi amri ya Mwenyezi Mungu.