42 : 30
وَمَآ أَصَٰبَكُم مِّن مُّصِيبَةٖ فَبِمَا كَسَبَتۡ أَيۡدِيكُمۡ وَيَعۡفُواْ عَن كَثِيرٖ
Na misiba inayo kusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi.
Explanation & meanings · 1
- Na msiba wowote unao kusibuni mnao uchukia ni kwa sababu ya maasi yenu. Na anayo yasamehe Mwenyezi Mungu duniani au akayachukulia ahadi humo, basi Mwenyezi Mungu ni Karimu; hatokuwa tena wa kuadhibu kwa hayo Akhera. Na Kwa hivi ametakasika na dhulma, na amesifika kwa rehema kunjufu.