Skip to content
الشُّورى /

Aya 15

42 : 15

Aya 15 of الشُّورى (42 : 15). This page carries the verse in the Uthmani script with a translation of its meaning, at a stable URL that can be cited on its own.

الشُّورى Aya 53
Sura · الشُّورى
Kiswahili · Barawani
42 : 15

فَلِذَٰلِكَ فَٱدۡعُۖ وَٱسۡتَقِمۡ كَمَآ أُمِرۡتَۖ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡۖ وَقُلۡ ءَامَنتُ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ مِن كِتَٰبٖۖ وَأُمِرۡتُ لِأَعۡدِلَ بَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ رَبُّنَا وَرَبُّكُمۡۖ لَنَآ أَعۡمَٰلُنَا وَلَكُمۡ أَعۡمَٰلُكُمۡۖ لَا حُجَّةَ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ يَجۡمَعُ بَيۡنَنَاۖ وَإِلَيۡهِ ٱلۡمَصِيرُ

Basi kwa haya waite! Nawe simama sawa sawa kama ulivyo amrishwa, wala usiyafuate matamanio yao. Na sema: Naamini aliyo teremsha Mwenyezi Mungu katika Vitabu. Na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu. Mwenyezi Mungu ni Mola wetu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Sisi tuna jukumu kwa vitendo vyetu, na nyinyi mna jukumu kwa vitendo vyenu. Hapana kuhojiana baina yetu na nyinyi. Na Mwenyezi Mungu atatukusanya pamoja, na marejeo ni kwake.

Explanation & meanings · 1
  1. Basi kwa ajili ya umoja wa Dini, na kuondoa mtafaruku ndani yake, waite waishike Dini, na shikilia Wito huo kama alivyo kuamrisha Mwenyezi Mungu, wala usitafute kuyaridhi matamanio ya washirikina. Na sema: Mimi naamini Vitabu vyote alivyo wateremshia Mwenyezi Mungu Mitume wake, na Mwenyezi Mungu ameniamrisha nisimamishe uadilifu baina yenu. Na waambie: Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wetu, na ndiye Muumba wenu. Vitendo vyetu ni vyetu sisi, si vyenu. Na vitendo vyenu ni vyenu nyinyi, si vyetu. Hapana la kubishana baina yetu na nyinyi, kwani haki iwazi. Mwenyezi Mungu atatukusanya kwa kutuhukumu kwa uadilifu. Na kwake Yeye peke yake ndio marejeo ya kurejea.