18 : 71
فَٱنطَلَقَا حَتَّىٰٓ إِذَا رَكِبَا فِي ٱلسَّفِينَةِ خَرَقَهَاۖ قَالَ أَخَرَقۡتَهَا لِتُغۡرِقَ أَهۡلَهَا لَقَدۡ جِئۡتَ شَيۡـًٔا إِمۡرٗا
Basi wawili hao wakatoka, hata walipo panda jahazi (yule mtu) akaitoboa. (Musa) akasema: Unaitoboa uwazamishe watu wake? Hakika umefanya jambo baya.
Explanation & meanings · 1
- Wakatoka wakitambaa na mfukwe wa bahari mpaka wakakuta jahazi wakaipanda. Yule mja mwema akaitoboa jahazi ile nayo imo safarini. Musa akapinga kwa kusema: Umeitoboa makusudi upate kuwazamisha watu wake? Ama hakika umefanya jambo ovu!