17 : 85
وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلرُّوحِۖ قُلِ ٱلرُّوحُ مِنۡ أَمۡرِ رَبِّي وَمَآ أُوتِيتُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِ إِلَّا قَلِيلٗا
Na wanakuuliza khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu.
Explanation & meanings · 1
- Ewe Muhammad! Watu wako wanakuuliza kwa kutomezwa na Mayahudi: Nini hakika ya Roho? Waambie: Roho ni katika ilimu yake Mwenyewe Mola wangu Mlezi aliyo jikhusisha nayo Yeye. Na nyinyi hamkupewa ilimu ila chache tu ukilinganisha na ilimu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.