Skip to content
الإسرَاء /

Aya 4

17 : 4
الإسرَاء Aya 111
Sura · الإسرَاء
Kiswahili · Barawani
17 : 4

وَقَضَيۡنَآ إِلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ فِي ٱلۡكِتَٰبِ لَتُفۡسِدُنَّ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَرَّتَيۡنِ وَلَتَعۡلُنَّ عُلُوّٗا كَبِيرٗا

Na tukawahukumia Wana wa Israili katika Kitabu kwamba: Hakika nyinyi mtafanya fisadi katika nchi mara mbili, na kwa yakini mtapanda kiburi, kiburi kikubwa.

Explanation & meanings · 1
  1. Na tukatekeleza hukumu yetu kwa Wana wa Israili katika tuliyo yaandika katika Lauhun Mahfuudh, Ubao Ulio Hifadhiwa, ya kwamba watafanya ufisadi katika Nyumba Takatifu (Baitul Muqaddas) bila ya shaka yoyote mara mbili. Kila mara katika hizo itakuwa ni udhaalimu na uasi, na kuacha hukumu za Taurati, na kuwauwa Manabii, na mtasaidiana katika madhambi, na kwamba utawala wenu utaenea, na kutukuka na kupanda kichwa na kiburi kwa dhulma zenu.