Skip to content
المَائدة /

Aya 81

5 : 81
المَائدة Aya 120
Sura · المَائدة
Kiswahili · Barawani
5 : 81

وَلَوۡ كَانُواْ يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلنَّبِيِّ وَمَآ أُنزِلَ إِلَيۡهِ مَا ٱتَّخَذُوهُمۡ أَوۡلِيَآءَ وَلَٰكِنَّ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ

Na lau wangeli kuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu, na huyu Nabii, na yaliyo teremshwa kwake, wasingeli wafanya hao marafiki. Lakini wengi katika wao ni wapotofu.

Explanation & meanings · 1
  1. Na lau kuwa itikadi yao ni sawa kama inavyo faa iwe kwa kumuamini Mwenyezi Mungu, na Mtume wake Muhammad s.a.w., na Qur'ani aliyo teremshiwa, basi wasingeli wafanya makafiri kuwa ni wenzao kuwapinga Waumini. Lakini wengi miongoni mwa Wana wa Israili ni maasi, wameacha dini.