Skip to content
الزُّمَر /

Aya 47

39 : 47
الزُّمَر Aya 75
Sura · الزُّمَر
Kiswahili · Barawani
39 : 47

وَلَوۡ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لَٱفۡتَدَوۡاْ بِهِۦ مِن سُوٓءِ ٱلۡعَذَابِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ وَبَدَا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مَا لَمۡ يَكُونُواْ يَحۡتَسِبُونَ

Na lau kuwa walio dhulumu wangeli kuwa na vyote viliomo duniani na pamoja navyo vingine kama hivyo, bila ya shaka wangeli vitoa kujikomboa katika adhabu mbaya hiyo Siku ya Kiyama. Na yatawadhihirikia kwa Mwenyezi Mungu wasiyo kuwa wakiyatarajia.

Explanation & meanings · 1
  1. Na lau kuwa hao walio jidhulumu nafsi zao kwa ushirikina wanamiliki vyote viliomo duniani na mara mbili kama hivyo, bila ya shaka wangeli vitoa kuwa ni fidia ya kujigombolea nafsi zao na adhabu waliyo andaliwa Siku ya Kiyama. Nao watakuja iona adhabu itokayo kwa Mwenyezi Mungu ambayo haikupata kuwapitikia katika mawazo yao.