10 : 76
فَلَمَّا جَآءَهُمُ ٱلۡحَقُّ مِنۡ عِندِنَا قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰذَا لَسِحۡرٞ مُّبِينٞ
Basi ilipo wajia Haki kutoka kwetu walisema: Hakika huu ni uchawi dhaahiri.
Explanation & meanings · 1
- Ilipo dhihiri Haki yetu kwa mkono wa Musa, ule muujiza wa Musa - nao ni fimbo kugeuka nyoka mbele ya macho yao - wao walisema: Hakika huu ni uchawi ulio dhaahiri!