10 : 29
فَكَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ إِن كُنَّا عَنۡ عِبَادَتِكُمۡ لَغَٰفِلِينَ
Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni shahidi baina yetu na nyinyi. Hakika sisi tulikuwa hatuna khabari ya ibada yenu.
Explanation & meanings · 1
- Mwenyezi Mungu anatutosheleza kwa ilimu yake na hukumu yake kuwa ni Shahidi wa kutupambanua baina yetu na nyinyi. Sisi tulikuwa mbali nanyi, wala hatukuwa tunafaidika vyovyote kwa huko kutuabudu kwenu.