39 : 57
أَوۡ تَقُولَ لَوۡ أَنَّ ٱللَّهَ هَدَىٰنِي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُتَّقِينَ
Au ikasema: Ingeli kuwa Mwenyezi Mungu ameniongoa, bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa wenye kumchamngu.
Explanation & meanings · 1
- Au iseme ile nafsi yenye dhambi, kutafuta udhuru: Lau kuwa Mwenyezi Mungu angeli niwezesha kufuata uwongofu bila ya shaka ningeli kuwa duniani katika wale walio jilinda na adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa Imani na vitendo vyema.